Nahitaji msaada wenu hali yangu ni mbaya

Nahitaji msaada wenu hali yangu ni mbaya

Asanteni mnaonipa moyo, bado nahitaji msaada
 
Habari ndugu zangu natumaini mambo yanakwenda kama yalivyopangwa na mwenyezi Mungu. Niende kwenye point moja kwa moja, kazi niliyokuwa nafanya ile kampuni imefunga business na inarudi nchini kwao maana hapa upepo wa biashara sio mzuri(hawapati faida na wanatumia gharama kubwa kwenye expenses kama mishahara na kadhalika) hivyo imepelekea kupunguza wafanyakazi zaidi ya robo tatu hadi sasa.

Hivi sasa nipo mtaani nahangaika kutafuta kibarua kingine. Nilipokuwa nimepanga ambapo nilijitahidi kununua vitu kadhaa vya ndani, mwezi uliopita walinivunjia nikiwa sipo na kuiba vitu karibu vyote na kesi ipo polisi, hivi sana nakaa kwa ndugu hapahapa Dar.

Tatizo kubwa ni hapa ninapokaa kila siku huyu ndugu analalamika na nikikosea kitu hata kwa bahati mbaya anasema niondoke na ni mzigo kwake, yeye ameolewa na ana watoto.

Kiukweli inafika sehemu naona maisha magumu sana na mzazi wangu mmoja aliyebaki(mama) ni mgonjwa na mzee hafanyi shughuli yoyote ya mimi kumtegemea yeye zaidi ananitegemea pia.

Elimu yangu ni degree ya maswala ya IT na uzoefu ninao wa kutosha, nisaidieni nipate sehemu ya kujishkiza kwa muda wakati ninaendelea kupambana kwani naamini muda si mrefu nitafanikiwa na nitarudisha chochote nitakachosaidiwa.

Naweza kufanya kazi nje ya kazi za IT na pia hata mikoani naweza kwenda, ninajua lugha 3 Kiswahili, English na French.

Asanteni, naombeni maswali mengine nitayajbu PM au mnipe mawasiliano zaidi.
Mbona wewe ni asset, tuliza akili ingia kwenye mitandao ya UN, EAC HQ, African Court HQ Ars.
Apply on line wala usiogope, fanya maombi pia utafanikiwa!!
 
Naona kazi inakuja ila nikushauri kitu kimoja Sikuhukumu lakini kwa kuwa hujaelezea kwa undani nikuope ushauri kwani mpapa mtu atake kukufukuza kunaweza kuwa na kitu fulani. Nakueleza ujue kukaa kwa mtu mwingine yoyote zaidi ya mama yako mazazi inabidi uwe extra careful. Mfano kama unalala sitting room hutakiwi kulala mpaka saa tatu. Jitakidi kadri unavyoweza kufuata principal za ile nyumba. Labda wao wameozoea saa mbili wanakula wewe unataka kuwekewa chakula uje ugonge mlango mlango saa sita. I am just saying kwa vile kuna uwezekano wa kupata kazi karibuni basi jitahidi kuendeana na maisha ya host wako ili uje uondoke kwa vizuri. Baada ya kupata kazi nusu mshahara wako wa kwanza mpelekee Mama yako mzazi. Then jijenge na maisha huku ukiendelea kumtunza mama yako mzazi!
 
Habari ndugu zangu natumaini mambo yanakwenda kama yalivyopangwa na mwenyezi Mungu. Niende kwenye point moja kwa moja, kazi niliyokuwa nafanya ile kampuni imefunga business na inarudi nchini kwao maana hapa upepo wa biashara sio mzuri(hawapati faida na wanatumia gharama kubwa kwenye expenses kama mishahara na kadhalika) hivyo imepelekea kupunguza wafanyakazi zaidi ya robo tatu hadi sasa.

Hivi sasa nipo mtaani nahangaika kutafuta kibarua kingine. Nilipokuwa nimepanga ambapo nilijitahidi kununua vitu kadhaa vya ndani, mwezi uliopita walinivunjia nikiwa sipo na kuiba vitu karibu vyote na kesi ipo polisi, hivi sana nakaa kwa ndugu hapahapa Dar.

Tatizo kubwa ni hapa ninapokaa kila siku huyu ndugu analalamika na nikikosea kitu hata kwa bahati mbaya anasema niondoke na ni mzigo kwake, yeye ameolewa na ana watoto.

Kiukweli inafika sehemu naona maisha magumu sana na mzazi wangu mmoja aliyebaki(mama) ni mgonjwa na mzee hafanyi shughuli yoyote ya mimi kumtegemea yeye zaidi ananitegemea pia.

Elimu yangu ni degree ya maswala ya IT na uzoefu ninao wa kutosha, nisaidieni nipate sehemu ya kujishkiza kwa muda wakati ninaendelea kupambana kwani naamini muda si mrefu nitafanikiwa na nitarudisha chochote nitakachosaidiwa.

Naweza kufanya kazi nje ya kazi za IT na pia hata mikoani naweza kwenda, ninajua lugha 3 Kiswahili, English na French.

Asanteni, naombeni maswali mengine nitayajbu PM au mnipe mawasiliano zaidi.


Naweza kufanya kazi kama;
-mauzo(Sales)
-Kusimamia biashara
-kazi za site
-na kadhalika
Hata ya kulala hapohapo itakuwa vyema zaidi.
Njoo ufanye kazi nasi
 
Mwana unachosema kinakaribiana kabisa na hali halisi iliyopo hapa, muda mwingine hata kula inakuwa ni ishu na kulalamika siwezi. Ila bado naamini ipo siku tu.
 
Ni kama vile unataka kuajiriwa tu huwazi kitu kingine. Kuajiriwa ni kitu kizuri..lakini wakati unatafuta ajira fikiria na kitu kingine.
Huna hobby yoyote? Siku hizi hobby yako inaweza kukulea kipato. Ingia youtube check jinsi ya kutengeneza kitu chochote. DIYs zipo za kutosha na ni simple sana.
Ukifikiria kuajiriwa peke yake utadata.
 
Pole sana mkuu, mola wako mlezi atakupa mpaka uridhike
 
Ni kama vile unataka kuajiriwa tu huwazi kitu kingine. Kuajiriwa ni kitu kizuri..lakini wakati unatafuta ajira fikiria na kitu kingine.
Huna hobby yoyote? Siku hizi hobby yako inaweza kukulea kipato. Ingia youtube check jinsi ya kutengeneza kitu chochote. DIYs zipo za kutosha na ni simple sana.
Ukifikiria kuajiriwa peke yake utadata.
Mkuu yeye amesema siku nyingine hata pesa ya kula ni shida, ungemsaidia angalau pesa ya kuingia huko YouTube ili ajifunze hicho unachomwambia.
 
Mkuu yeye amesema siku nyingine hata pesa ya kula ni shida, ungemsaidia angalau pesa ya kuingia huko YouTube ili ajifunze hicho unachomwambia.
Baadhi ya vifurushi vya siku hizi vina YOUTUBE bure.
 
Pole
Mwana unachosema kinakaribiana kabisa na hali halisi iliyopo hapa, muda mwingine hata kula inakuwa ni ishu na kulalamika siwezi. Ila bado naamini ipo siku tu.
Pole nimeona michango naamini umefanikiwa tayari! Ukitoka mkumbuke Mama yako Mzazi upate baraka zaidi.
 
Pole

Pole nimeona michango naamini umefanikiwa tayari! Ukitoka mkumbuke Mama yako Mzazi upate baraka zaidi.
Asante mkuu ila bado sijafanikiwa, nitaleta mrejesho kwa lolote nitakalopata
 
Michango yenu inanipa moyo sana japo bado sijapata ila naamini nitafanikiwa kupata hata kibarua soon.
 
Dah magufuli damu zitamdai hizi,,watu wana degree? Ok all in all pole mkuu.
 
Uza hata maji barabarani, ujue kuna mda karatasi AKA vyeti inabidi uviweke pembeni uanze kupambana kiume
 
Back
Top Bottom