Nahitaji msaada wenu hali yangu ni mbaya

Nahitaji msaada wenu hali yangu ni mbaya

Nitalala hata chini lakini sio kwenda kumuongezea mzigo mama yangu aliyenilea kwa tabu hatahivyo sikatai hali ikiwa mbaya zaidi nitarudi wacha nipambane kwanza. Asanteni kwa wote mnaonishauri na kunipa pole
 
Kwani unafamilia au una mke anakutegemea mana kama upo mwenyew mimi sioni kama kuna tatizo lolote dili zipo kibao kitaani endelea kufany uku ukiendekea kutafuta ajira nyingine
 
pole! unasema ulikuwa mwajiriwa siyo napenda kujua pensheni yako vipi, fuatilia nadhani utapata mwanzo ujiajiri!
sikuhizi kazi hakuna na ukipata ni stress tupu!
kaa chini ujipange huo ndio ukubwa na si lazima ukae dar tu
 
Mkuu nilishaapa sitakuja kuingia darasani tena baada ya kuhitimu haka kadegree niliko fanikiwa kukapata!
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] najua sana ndo maana nilikuchokoza tu,vipi kwa sasa unapanga foleni atm au bado upo na bahasha ya kaki
 
Vijana wengi wanapoajiriwa hawajiongezi kufungua vitegauchumi vya kuongeza kipato, hawaweki akiba ya kuwakomboa kujiajiri siku kibarua kikiota nyasi.

Wengine wakipata ajira ni bata batani mpaka manyoya wanakula....

Sasa huyu ili apate msaada wa ushauri ni vyema atuambie ana nini ili tumpe mwangaza. Achilia mbali vitu vilivyoibiwa.....
Haya makosa Mungu aniepushe nayo kwa kweli. Mwaka huu naomba sana Mungu aniwezeshe kukamilisha mabanda nianze ufugaji wa kuku, mbuzi na ng'ombe. Kuajiriwa taabu sana. Ee Mwenyezi Mungu nisaidie mja wako!
 
Habari ndugu zangu natumaini mambo yanakwenda kama yalivyopangwa na mwenyezi Mungu. Niende kwenye point moja kwa moja, kazi niliyokuwa nafanya ile kampuni imefunga business na inarudi nchini kwao maana hapa upepo wa biashara sio mzuri(hawapati faida na wanatumia gharama kubwa kwenye expenses kama mishahara na kadhalika) hivyo imepelekea kupunguza wafanyakazi zaidi ya robo tatu hadi sasa.

Hivi sasa nipo mtaani nahangaika kutafuta kibarua kingine. Nilipokuwa nimepanga ambapo nilijitahidi kununua vitu kadhaa vya ndani, mwezi uliopita walinivunjia nikiwa sipo na kuiba vitu karibu vyote na kesi ipo polisi, hivi sana nakaa kwa ndugu hapahapa Dar.

Tatizo kubwa ni hapa ninapokaa kila siku huyu ndugu analalamika na nikikosea kitu hata kwa bahati mbaya anasema niondoke na ni mzigo kwake, yeye ameolewa na ana watoto.

Kiukweli inafika sehemu naona maisha magumu sana na mzazi wangu mmoja aliyebaki(mama) ni mzee hafanyi shughuli yoyote ya mimi kumtegemea yeye zaidi ananitegemea pia.

Elimu yangu ni degree ya maswala ya IT na uzoefu ninao wa kutosha, nisaidieni nipate sehemu ya kujishkiza kwa muda wakati ninaendelea kupambana kwani naamini muda si mrefu nitafanikiwa na nitarudisha chochote nitakachosaidiwa.

Naweza kufanya kazi nje ya kazi za IT na pia hata mikoani naweza kwenda, ninajua lugha 3 Kiswahili, English na French.

Asanteni, naombeni maswali mengine nitayajbu PM au mnipe mawasiliano zaidi.
Mkuu, nimepata suluhisho la kinacho kusibu. Na nilikua ninamsimulia jamaa flani kisa chako hapa bar.... Naomba kesho asubuhi unitumie namba yako ya simu kwa pm, then nitakuunganisha na mkuu aone vyenye atakusaidia kazi ya kufanya kwa shirika lao, ngawa mshara ameniambia utakua ni kati ya 500/700 elfu.
Naomba sana unitumie nambayako mapema ili tuone namna ya kuibaka hiyo nafasi yaku volunteer.
Nami nitakutwangia kilongalonga ili nijue kila kitakachojiri.
 
Mkuu, nimepata suluhisho la kinacho kusibu. Na nilikua ninamsimulia jamaa flani kisa chako hapa bar.... Naomba kesho asubuhi unitumie namba yako ya simu kwa pm, then nitakuunganisha na mkuu aone vyenye atakusaidia kazi ya kufanya kwa shirika lao, ngawa mshara ameniambia utakua ni kati ya 500/700 elfu.
Naomba sana unitumie nambayako mapema ili tuone namna ya kuibaka hiyo nafasi yaku volunteer.
Nami nitakutwangia kilongalonga ili nijue kila kitakachojiri.
Bazazi@work
 
Me nataka kujua tu je unatafuta kazi ya ofisini peke yake au kazi yoyote ambayo utaweza kuingiza kipato na upo tayari kupokea kiasi gani kwa mwezi??kuna sehemu zongine inabidi kuweka degree na uzoefu pembeni then unaangalia namna ya kufight kimapato ni muhimu sana nadhani.....shamba je unaweza kukaa na kuangalia mifugo??
 
Back
Top Bottom