Nahitaji msaada wenu hali yangu ni mbaya

geek01

Senior Member
Jul 11, 2017
143
267
Habari ndugu zangu natumaini mambo yanakwenda kama yalivyopangwa na mwenyezi Mungu. Niende kwenye point moja kwa moja, kazi niliyokuwa nafanya ile kampuni imefunga business na inarudi nchini kwao maana hapa upepo wa biashara sio mzuri(hawapati faida na wanatumia gharama kubwa kwenye expenses kama mishahara na kadhalika) hivyo imepelekea kupunguza wafanyakazi zaidi ya robo tatu hadi sasa.

Hivi sasa nipo mtaani nahangaika kutafuta kibarua kingine. Nilipokuwa nimepanga ambapo nilijitahidi kununua vitu kadhaa vya ndani, mwezi uliopita walinivunjia nikiwa sipo na kuiba vitu karibu vyote na kesi ipo polisi, hivi sana nakaa kwa ndugu hapahapa Dar.

Tatizo kubwa ni hapa ninapokaa kila siku huyu ndugu analalamika na nikikosea kitu hata kwa bahati mbaya anasema niondoke na ni mzigo kwake, yeye ameolewa na ana watoto.

Kiukweli inafika sehemu naona maisha magumu sana na mzazi wangu mmoja aliyebaki(mama) ni mgonjwa na mzee hafanyi shughuli yoyote ya mimi kumtegemea yeye zaidi ananitegemea pia.

Elimu yangu ni degree ya maswala ya IT na uzoefu ninao wa kutosha, nisaidieni nipate sehemu ya kujishkiza kwa muda wakati ninaendelea kupambana kwani naamini muda si mrefu nitafanikiwa na nitarudisha chochote nitakachosaidiwa.

Naweza kufanya kazi nje ya kazi za IT na pia hata mikoani naweza kwenda, ninajua lugha 3 Kiswahili, English na French.

Asanteni, naombeni maswali mengine nitayajbu PM au mnipe mawasiliano zaidi.


Naweza kufanya kazi kama;
-mauzo(Sales)
-Kusimamia biashara
-kazi za site
-data entry and data management
-na kadhalika
Hata ya kulala hapohapo itakuwa vyema zaidi.
 
Pole kwa yanayo kusibu mkuu.
Naomba nikuulize maswali tafadhali, ili tujirishishe na haya ulio yasema.
 
Endelea kukomaa,ila pole sana,hayo ni ya kidunia,usikate tamaa,mtumainie Mungu atakuwekea wepesi...
 
Pole kwa yanayo kusibu mkuu.
Naomba nikuulize maswali tafadhali, ili tujirishishe na haya ulio yasema.
Karibu ndugu ukiona nachelewa kujibu ni kwasababu nashindwa kuingia humu muda wote.
 
Binafsi naona unachangamoto ndogo sana na sio matatizo.
Unaweza kukutana na mtu hana hata cha kuanzia na ukisema umsaidie unashindwa uanzie wapi? ila wewe una Skills na angalau Degree ya kuweza kujipigania.

Hauko peke yako mkuu usife moyo , kikubwa Pambana unavyoweza (hata vibarua vya kujenga)

Mwenye nia njema hakati tamaa.
 
Wakati unafanya kazi ulijiwekea akiba kiasi gani ili tukuoneshe pa kuanzia?
 
kazi niliyokuwa nafanya ile kampuni imefunga business na inarudi nchini kwao maana hapa upepo wa biashara sio mzuri(hawapati faida na wanatumia gharama kubwa kwenye expenses kama mishahara na kadhalika) hivyo imepelekea kupunguza wafanyakazi zaidi ya robo tatu hadi sasa.

.
kaka si wewe tu, baadhi ya makampuni ya Madini na NGO's zimenyimwa leseni za kuoperate hapa nchini zimefunga, watu wanahaha kutafuta kazi nyingine, tatizo sasa ukiwa abave 40 ni sheshe mno kupata kazi - Umri.
Pia mishahara ya Makampuni ya Madini na NGO's huwa ni mikubwa, sasa interviewer unamwambia nilikuwa nakula 4.2m kwa mwezi; Jamaa wanabakia mdomo wazi - kuna kazi hapo.

ni hali tete sana, ila komaa mwanangu.. ila kama una familia na watoto wanasoma hizi shule zetu za acaemia na bado umepanga hapo ndipo huwa patamu kidogo...pole mkuu.
 
Habari ndugu zangu natumaini mambo yanakwenda kama yalivyopangwa na mwenyezi Mungu. Niende kwenye point moja kwa moja, kazi niliyokuwa nafanya ile kampuni imefunga business na inarudi nchini kwao maana hapa upepo wa biashara sio mzuri(hawapati faida na wanatumia gharama kubwa kwenye expenses kama mishahara na kadhalika) hivyo imepelekea kupunguza wafanyakazi zaidi ya robo tatu hadi sasa.

Hivi sasa nipo mtaani nahangaika kutafuta kibarua kingine. Nilipokuwa nimepanga ambapo nilijitahidi kununua vitu kadhaa vya ndani, mwezi uliopita walinivunjia nikiwa sipo na kuiba vitu karibu vyote na kesi ipo polisi, hivi sana nakaa kwa ndugu hapahapa Dar.

Tatizo kubwa ni hapa ninapokaa kila siku huyu ndugu analalamika na nikikosea kitu hata kwa bahati mbaya anasema niondoke na ni mzigo kwake, yeye ameolewa na ana watoto.

Kiukweli inafika sehemu naona maisha magumu sana na mzazi wangu mmoja aliyebaki(mama) ni mzee hafanyi shughuli yoyote ya mimi kumtegemea yeye zaidi ananitegemea pia.

Elimu yangu ni degree ya maswala ya IT na uzoefu ninao wa kutosha, nisaidieni nipate sehemu ya kujishkiza kwa muda wakati ninaendelea kupambana kwani naamini muda si mrefu nitafanikiwa na nitarudisha chochote nitakachosaidiwa.

Naweza kufanya kazi nje ya kazi za IT na pia hata mikoani naweza kwenda, ninajua lugha 3 Kiswahili, English na French.

Asanteni, naombeni maswali mengine nitayajbu PM au mnipe mawasiliano zaidi.
kwa uandishi wako wewe ni jinsi ya kike..
 
Habari ndugu zangu natumaini mambo yanakwenda kama yalivyopangwa na mwenyezi Mungu. Niende kwenye point moja kwa moja, kazi niliyokuwa nafanya ile kampuni imefunga business na inarudi nchini kwao maana hapa upepo wa biashara sio mzuri(hawapati faida na wanatumia gharama kubwa kwenye expenses kama mishahara na kadhalika) hivyo imepelekea kupunguza wafanyakazi zaidi ya robo tatu hadi sasa.

Hivi sasa nipo mtaani nahangaika kutafuta kibarua kingine. Nilipokuwa nimepanga ambapo nilijitahidi kununua vitu kadhaa vya ndani, mwezi uliopita walinivunjia nikiwa sipo na kuiba vitu karibu vyote na kesi ipo polisi, hivi sana nakaa kwa ndugu hapahapa Dar.

Tatizo kubwa ni hapa ninapokaa kila siku huyu ndugu analalamika na nikikosea kitu hata kwa bahati mbaya anasema niondoke na ni mzigo kwake, yeye ameolewa na ana watoto.

Kiukweli inafika sehemu naona maisha magumu sana na mzazi wangu mmoja aliyebaki(mama) ni mzee hafanyi shughuli yoyote ya mimi kumtegemea yeye zaidi ananitegemea pia.

Elimu yangu ni degree ya maswala ya IT na uzoefu ninao wa kutosha, nisaidieni nipate sehemu ya kujishkiza kwa muda wakati ninaendelea kupambana kwani naamini muda si mrefu nitafanikiwa na nitarudisha chochote nitakachosaidiwa.

Naweza kufanya kazi nje ya kazi za IT na pia hata mikoani naweza kwenda, ninajua lugha 3 Kiswahili, English na French.

Asanteni, naombeni maswali mengine nitayajbu PM au mnipe mawasiliano zaidi.
Kujua lugha tatu haina faida kwa kazi ya IT, labda ungesema unajua programming language 3. OK kwa kweli maisha ya sasa yamechafuka, enzi zetu mtu akiwa na certificate ya IT tena toka chuo uchwara cha mtaani anakuwa na soko kuajiriwa hata kujiajiri lakini sasa hivi mtu na digirii yake tena ukute toka chuo kinachotambuliwa lakini hawezi kuajiriwa wala kujiajiri.
 
Hili Swali sikia tu ameulizwa mwenzio!
Swali gumu sana
Vijana wengi wanapoajiriwa hawajiongezi kufungua vitegauchumi vya kuongeza kipato, hawaweki akiba ya kuwakomboa kujiajiri siku kibarua kikiota nyasi.

Wengine wakipata ajira ni bata batani mpaka manyoya wanakula....

Sasa huyu ili apate msaada wa ushauri ni vyema atuambie ana nini ili tumpe mwangaza. Achilia mbali vitu vilivyoibiwa.....
 
Back
Top Bottom