Nahitaji msaada wa kisaikolojia niache tabia ya ulevi

ndege JOHN

JF-Expert Member
Aug 5, 2015
19,569
44,791
Inasikitisha sana sijui ni kwanini hata nimejikuta nimekwisha tumbukia kwenye ulevi wa kutisha kwa hali niliyofikia ni hatari kwani nakunywa pombe karibu kila siku bila ya kupumzika.

Nimeshakunywa za kienyeji karibu zote, pombe kali zote na kwa sasa nimezamia kwenye bia yaani speed yangu kwa kweli sio nzuri.

Nikinywa nikalewa naanza kujisemesha kuwa Mimi siogopi cha Ukimwi wala kansa nakunywa bia nikalale sitaki mwanamke nawaachia wanywa soda.

Kiukweli naogopa kifo kinachosababishwa na unywaji wa pombe kibaya zaidi nahisi ulevi umenisababishia niwe mbali na Mungu wetu imani imeshuka sana sipati tena muda wa kumkumbuka Yesu.

Nahitaji kubadilika lakini mwenyewe nimeshindwa ndugu wameshaongea mpaka wamechoka wameamua kuniacha tu mwenyewe nifanye ninalotaka nikipata kansa au bawasili au maradhi ya pombe nipambane nayo mwenyewe.

Naomba mtaalam wa saikolojia/kiroho wa kujitolea kunisaidia anisaidie mbinu mbadala, natambua ya kwamba maamuzi ya mwisho yananihitaji Mimi binafsi nijikane lakini kama nilivyosema imekuwa ngumu NASHINDWA.
 
Pole sana kuna wakati tuluenda vema mpaka ukaacha kabisa! Ninini kimekusibu tena? Kumbuka ulevi wa kila siku huchosha sana figo na hupunguza kws kiwango kikubwa uwezo wa kujamiiana...

Kama bado una tumaini la kuwa fulani positively huko mbeleni basi una nafasi nzuri ya kuilinda afya yako kwasasa!
 
Hapo kwny bawasiri nimecheka Sana mzee 😄😄😄,kwani unatumia choo Cha kukaa?

Pole Sana brother,kila mlevi/mnywaji Mara nyingi anapitia situation Kama yako(regrets) pale hangover inapokua imechachamaa lkn baadae anarudia Kule Kule.

Najua hakuna kitu nimeshauri Cha maana mpk hapo,lkn jua situation yako watu wengi wanaipitia kuanzia wanyonge,mawaziri,wanyabiashara etc.Don't give up bro.
 
Inasikitisha sana sijui ni kwanini hata nimejikuta nimekwisha tumbukia kwenye ulevi wa kutisha kwa hali niliyofikia ni hatari kwani nakunywa pombe karibu kila siku bila ya kupumzika.

Nimeshakunywa za kienyeji karibu zote, pombe kali zote na kwa sasa nimezamia kwenye bia yaani speed yangu kwa kweli sio nzuri.

Nikinywa nikalewa naanza kujisemesha kuwa Mimi siogopi cha Ukimwi wala kansa nakunywa bia nikalale sitaki mwanamke nawaachia wanywa soda.

Kiukweli naogopa kifo kinachosababishwa na unywaji wa pombe kibaya zaidi nahisi ulevi umenisababishia niwe mbali na Mungu wetu imani imeshuka sana sipati tena muda wa kumkumbuka Yesu.

Nahitaji kubadilika lakini mwenyewe nimeshindwa ndugu wameshaongea mpaka wamechoka wameamua kuniacha tu mwenyewe nifanye ninalotaka nikipata kansa au bawasili au maradhi ya pombe nipambane nayo mwenyewe.

Naomba mtaalam wa saikolojia/kiroho wa kujitolea kunisaidia anisaidie mbinu mbadala, natambua ya kwamba maamuzi ya mwisho yananihitaji Mimi binafsi nijikane lakini kama nilivyosema imekuwa ngumu NASHINDWA.
Kama uliweza kusimama imara na Guru Mshana Jr, na ulipo muacha ukarudi nyuma kimaadili, rudi tena kwa Mentor wako, a.k.a RABI Master Mshana Jr
 
Inasikitisha sana sijui ni kwanini hata nimejikuta nimekwisha tumbukia kwenye ulevi wa kutisha kwa hali niliyofikia ni hatari kwani nakunywa pombe karibu kila siku bila ya kupumzika.

Nimeshakunywa za kienyeji karibu zote, pombe kali zote na kwa sasa nimezamia kwenye bia yaani speed yangu kwa kweli sio nzuri.

Nikinywa nikalewa naanza kujisemesha kuwa Mimi siogopi cha Ukimwi wala kansa nakunywa bia nikalale sitaki mwanamke nawaachia wanywa soda.

Kiukweli naogopa kifo kinachosababishwa na unywaji wa pombe kibaya zaidi nahisi ulevi umenisababishia niwe mbali na Mungu wetu imani imeshuka sana sipati tena muda wa kumkumbuka Yesu.

Nahitaji kubadilika lakini mwenyewe nimeshindwa ndugu wameshaongea mpaka wamechoka wameamua kuniacha tu mwenyewe nifanye ninalotaka nikipata kansa au bawasili au maradhi ya pombe nipambane nayo mwenyewe.

Naomba mtaalam wa saikolojia/kiroho wa kujitolea kunisaidia anisaidie mbinu mbadala, natambua ya kwamba maamuzi ya mwisho yananihitaji Mimi binafsi nijikane lakini kama nilivyosema imekuwa ngumu NASHINDWA.
Tushajiuliza hizi sredi unazoletaga mfululizo za ovyo zinachochewa na nini? Leo jibu limepatikana
 
Mkuu karibu Mwanza tuna kituo cha kulea wanaopitia urahibu. Ni mafunzo ya mwaka moja.
Kunakuwa na huduma ya maombi na mind transformation kozi. Kituo kiko chini ya Kanisa TAG.BMCC mwanza. Tuko malimbe karibu na chuo kikuu cha SAUT. Kwa msaada wa Mungu utaacha.
 
Inasikitisha sana sijui ni kwanini hata nimejikuta nimekwisha tumbukia kwenye ulevi wa kutisha kwa hali niliyofikia ni hatari kwani nakunywa pombe karibu kila siku bila ya kupumzika.

Nimeshakunywa za kienyeji karibu zote, pombe kali zote na kwa sasa nimezamia kwenye bia yaani speed yangu kwa kweli sio nzuri.

Nikinywa nikalewa naanza kujisemesha kuwa Mimi siogopi cha Ukimwi wala kansa nakunywa bia nikalale sitaki mwanamke nawaachia wanywa soda.

Kiukweli naogopa kifo kinachosababishwa na unywaji wa pombe kibaya zaidi nahisi ulevi umenisababishia niwe mbali na Mungu wetu imani imeshuka sana sipati tena muda wa kumkumbuka Yesu.

Nahitaji kubadilika lakini mwenyewe nimeshindwa ndugu wameshaongea mpaka wamechoka wameamua kuniacha tu mwenyewe nifanye ninalotaka nikipata kansa au bawasili au maradhi ya pombe nipambane nayo mwenyewe.

Naomba mtaalam wa saikolojia/kiroho wa kujitolea kunisaidia anisaidie mbinu mbadala, natambua ya kwamba maamuzi ya mwisho yananihitaji Mimi binafsi nijikane lakini kama nilivyosema imekuwa ngumu NASHINDWA.
Jikite na bangi wewe ..... Sasa naenda mwezi wa3 nakunywa lakini jumamosi tu na kwenye masherehe.
 
Mkuu kabla ya kuamua kuacha kunywa pombe kuna maswali ya awali ya kujiuliza.

1. Kwanini unataka kuacha kunywa pombe? Watu wanaacha kwa sababu mbalimbali kama ukata etc.

2. Mambo gani mazuri yanatokana na wewe kunywa pombe? Muhimu kujua ili kutafuta njia mbadala baada ya kuacha.

3. Mambo gani mabaya yanayotokana na wewe kunywa pombe?

4. Mambo gani mazuri unayategemea baada ya kuacha kunywa pombe?

5. Mambo gani mabaya yanayoweza kutokana na wewe kuacha kunywa pombe?

Kutokana na majibu ya maswali hapo juu, hizi ni baadhi ya hatua unazoweza kuchukua. Zipo nyingi. Hizi ni baadhi tuu:

1. Kama ni mnywaji sana ongea kwanza na daktari wako. Kuacha pombe ghafla kunaweza kukuletea madhara hasa kama ni mnywaji sana. Kuacha ghafla unaweza ku-suffer from panic attacks, anxiety, shakes, mapigo ya moyo kwenda mbio, au hata mwili kupungua. Kwa hiyo, kunaweza kuwa na umuhimu wa kupata ushauri wa kitaalamu kwanza jinsi ya kuacha.

2. Badilisha attitude yako juu ya pombe. Kumbuka hakuna anayekulazimisha kuacha pombe (rafiki yako mkubwa ambae amekuwa na wewe kwa muda mrefu). Panga tarehe za kuacha. Be ambitious but reasonable. Kama ni mnywaji sana punguza kidogo kidogo. Ukiacha gafla unawezapatwa na symptoms. Ndio maana wanasizitiza kupata ushauri wa daktari ili aweze kukupangia kitaalamu jinsi ya kuacha pombe.

3. Kama una pombe nyumbani, get rid all of them. Unaweza kusema itabidi uache pombe kidogo kwa ajili ya wageni. Lakini it is perfectly fine kumpa mgeni chai, soda au hata maji. Kama ni mgeni aliyezoea kuja kwako na kunywa pombe ukimwambia kuwa huna pombe ndani kwa sababu una mkakati wa kuacha kunywa, nadhani atakuelewa vyema.

4. Rudi back to your feelings. Ukijiskia unataka kulia, then lia. Laugh when you can. Kula ukiwa na njaa. Lala ukiwa umechoka. Usitumie ule muda uliokuwa unautumia kunywa pombe kwa kwenda kulala. It won't help. Mwanzoni itaonekana ni weird but embrace it. Kuna uwezekano kwa sababu ya pombe hujawahi kujua hisia zako kwa muda mrefu. So, you will have to learn to curve.

5. Usifanye kitu ambacho hauko tayari kukifanya. Kama unaenda kwenye sherehe na kuna pombe usinywe pombe kwa sababu wengine wanakunywa. Mwanzoni inaweza kuwa ngumu lakini you will need to rain check. Protecting your sobriety should be your first priority.

6. Kuna uwezekano mkubwa wa kuachana kwa muda na baadhi ya marafiki zako ambao ulikuwa unakunywa nao. Baadae utakuja kushangaa kuwa in fact marafiki ambao ulikuwa unakunywa nao walikuwa wanakunywa only occasionally, tena bia mbili tuu wakati wewe ulikuwa ulikuwa unakata bia tano.

7. Kama nyumbani unatumia viungo vya kupikia ambavyo vinalazimisha kuwepo kwa bia au wine, then achana navyo. Pia kuna wale wanaosema nyamba choma haiendi bila bia. Itakubidi ukae mabli na nyama choma kwa muda. Wapo ambao wanachoma nyama na kuichanganya na bia wakati inachomwa. Itabidi uache kama unafanya hivyo.

8. Tafuta kibox kidogo cha mbao cha kuhifadhia fedha. Kila unapofikiria kununua pombe, chukua hizo pesa na tumbukiza huko. Baadae utakujashangaa kiasi cha fedha ambazo ulikuwa unapotezea kwenye pombe. Ikishindikana basi tumia hizo fedha kupunguza stress kama kupata massage au jiunge na gym.

9. Nununua ring ya bei rahisi na ivae kila wakati kama kielelezo kuwa haugusi tena pombe. Kama wewe ni Mkatoliki unaweza kuvaa Rozari kama kielelezo kuwa hutakunywa pombe wakati ukiwa umeivaa. Ukisikia hamu ya pombe tuu look at the ring.

10. Kunywa maji kwa wingi. Hata kama ni kutembea na chupa za maji barabarani usiogope.

11. Omba support kutoka kwa ndugu mme/mke kuhusu what you are going through and nini unachotaka ku-achieve.

12. Kama kuna chama chochote cha watu wanaotaka kuacha pombe, jiunge nacho. Kama ukikuta chama chenyewe hakina mshiko, don't feel guilty. Its not your fault.

13. Baada ya siku 90 ya kuwa sober, your whole outlook itabadilika na mwili wako utakuwa in full recovery mode. Utakuwa mtu tofauti na ulivyokuwa na kuna uwezekano weight yako ikapungua pia. Don't worry.

14. Tengeneza list ya vitu ambavyo umefanya by using alcohol without alcohol, then celebrate maana list itakuwa ndefu.

15. Furahia how it feel unapokwenda kulala jioni bila kupoteza network.

16. Usijaribu kuwaelezea watu kuhusu kuacha kwako pombe. Watu wengi hawanywi pombe kama walivyokuwa wanakinywa zamani. Hawapo kama wewe na hawataweza kukuelewa kuwa una tatizo la kunywa pombe. Of course, wako ambao wana hilo tatizo. Either way kuna uwezekano wakakuambia huna tatizo. Mtu akitaka kukukaribisha pombe mwambie asante lakini nitakunywa soda; najaribu kupunguza weight. Kama ni watu wa karibu ipo siku watajua kweli wata-appreciate kwa wewe kuamua kuachana na pombe.

17. Kubali na kumbuka kuwa pombe sio kitu muhimu maishani mwako kupita vyote.

18. Kuwa na sababu nzuri ya kuacha pombe. Ni muhimu sana kuwa na sababu tena iwe ya msingi. Kama sababu ni pesa imepungua, kuna uwezakano ukarudia tena pombe kama pesa ikiongezeka. So ni bora kuwa na strong and valid reason.

18. Usikwepe kwenda sehmu ambazo utakunywa pombe, kama kwenye sherehe, n.k. Badala yake nenda kwenye hizo sehemu ukiwa na attitude nzuri na kumbuka kuwa na good time bila hata kunywa pombe. You can have a good time bila kunywa pombe. Yes, you can. Tena utashangaa jinsi watu na heshima zao wanavyo-behave baada ya kulewa. Kwangu hii ndio sababu pekee iliyonifanya nisinywe pombe.

19. Memorise a prayer, shairi, nk then rudia kulisema pale unapokuwa katika hatihati za ku-loose your control. It will keep your heard together. Kwa mfabo mtu ambaye anataka kuacha kuchukua rushwa anaweza ku-memorise baadhi ya sentensi kwenye speeches za Mwalimu Nyerere kama "Rushwa ni adui wa haki." Tafuta misemo ambayo inahusina na ulevi.

20. Jipe mwenyewe zawadi kila siku au kila saa kwa kutokunywa. Sio lazima iwe zawadi kubwa. Just a simple treat kujipongeza.

21. Nasistiza tena. Ongea na daktari wako. Kuacha pombe gafla kunaweza kukuletea madhara makubwa hasa kama ni mnywaji wa kupindukia.

22. Fanya mazoezi. Mazoezi yatakufanya u-deal the stress na pia yatasaidia kutuliza ubongo wako na kuboresha afya yako kwa ujumla.

23. Kulingana na ushauri wa daktari, meza vitamin B supplements kila siku kwa wiki ya kwanza ya kuacha pombe. Pombe inaadhiri uwezo wa mwili wako ku-absorb these. Upungufu wa Vitamin B unaweza kusababisha severe cognitive impairment. So, ongea na daktari wako juu ya hili na hasa kama unatumia medication nyingine.

24. Kama ni mlevi sana jaribu ku-visualize jinsi unaakavyokuwa wakati ukiwa umelewa na jiulize kama unataka kuendelea kuwa vile.

25. Kama unatoka kazini na kwenda moja kwa moja bar kunywa, jaribu kubadilisha routine kwa kufanya shughuli nyingine kama kutembelea ndugu na jamaa, kwenda gym au kanisani/msikitini. Ikishindikana kabisa then, jikite JF. JF is never boring na utafaidika zaidi ya kunywa pombe. Ni heri uwe mlevi ya JF kuliko mlevi wa pombe.

26. Kula kwanza kabla ya kunywa. Hii itapunguza interest ya kutaka kunywa.

27. Siku za mwanzoni punguza kiasi cha pombe unayokunywa. Halafu jaribu ku-imagine kutokana na kunywa mno jinsi unvyopoteza network, unavyojitapikia, kichwa kinauma, unachelewa kazini, nk.

28. Don't give up. Wapo wanaosema wamekuwa wakinywa kwa muda mrefu sana kwa hiyo hawawezi kuacha, sijui wamejaribu kuacha mara nyingi lakini nimeshindwa, n.k. Hakuna age limit ya kuacha kunywa pombe. Unaweza kuacha katika umri wowote. It is never too late to quit drinking.

29. Kama wewe ni mtu wa club sana, kuna strategy alikuwa anatumia rafiki yangu na ilimsadia. Kuwa yeye atakuwa dereva kila tukienda out. Kwa hiyo hatagusa pombe kabisa ili aturudishe nyumani salama. Ilimsaidia sana kutokunywa.

29. Kumbuka kuacha kunywa pombe kutakuongezea urefu wa maisha yako hapa duniani. Pamoja na magojwa yanayosababishwa directly na unywaji wa pombe kupita kiasi, ukiwa mlevi kupindukia unaweza kufanya mmabo ya ajabu na kusabisha sio kifo chako tuu bali vifo kwa watu wengine pia kama ku-drive wakati umelewa.

30. Don't let guilty affect you. Unaweza kuji-feel mshamba au guilty kwa kutokunywa pombe lakini usilaumu mwenyewe au mtu mwingine. Hakuna kitu muhimu kama wewe. You are of no use to anyone kama ukifa na magonjwa yanayosabishwa na ulevi. You must overthrow the oppressive rule of alcohol and start afresh, just as any country in revolution. Jiulize Libya waliweza kuachana na Gadaffi wewe kweli utashindwa kuachana na pombe? It will be hard and you must learn from the past, lakini kumbuka kuwa umenganywa na pombe kwa muda mrefu. Sasa ni muda wa kuanza kuyaishi maisha yako. Those around you will appreciate it too.

Goodluck.
 
Inasikitisha sana sijui ni kwanini hata nimejikuta nimekwisha tumbukia kwenye ulevi wa kutisha kwa hali niliyofikia ni hatari kwani nakunywa pombe karibu kila siku bila ya kupumzika.

Nimeshakunywa za kienyeji karibu zote, pombe kali zote na kwa sasa nimezamia kwenye bia yaani speed yangu kwa kweli sio nzuri.

Nikinywa nikalewa naanza kujisemesha kuwa Mimi siogopi cha Ukimwi wala kansa nakunywa bia nikalale sitaki mwanamke nawaachia wanywa soda.

Kiukweli naogopa kifo kinachosababishwa na unywaji wa pombe kibaya zaidi nahisi ulevi umenisababishia niwe mbali na Mungu wetu imani imeshuka sana sipati tena muda wa kumkumbuka Yesu.

Nahitaji kubadilika lakini mwenyewe nimeshindwa ndugu wameshaongea mpaka wamechoka wameamua kuniacha tu mwenyewe nifanye ninalotaka nikipata kansa au bawasili au maradhi ya pombe nipambane nayo mwenyewe.

Naomba mtaalam wa saikolojia/kiroho wa kujitolea kunisaidia anisaidie mbinu mbadala, natambua ya kwamba maamuzi ya mwisho yananihitaji Mimi binafsi nijikane lakini kama nilivyosema imekuwa ngumu NASHINDWA.

PITIA HAPA BRO
Utangulizi:

Ulevi wa pombe limekuwa ni janga linaloitafuna sana jamii yetu kutokana na kusababisha matatizo mengine mengi zaidi ikiwemo umaskini, migogoro kwenye ndoa, ugomvi na hata mauwaji, watu kufukuzwa kazi , matatizo ya kiafya na mengineyo mengi.

Pamoja na matatizo yote hayo lakini bado walevi wanaongezeka kila uchao, Pengine ni kutokana na serikali na jamii nzima kutolitilia maanani suala hili na au ni wahusika kutojua wafanye nini ili kujinasua na janga hili.

Hivyo katika makala haya nitajadili chazo cha watu wengi kuwa walevi wa pome,mbinu unazoweza kuzitumia ili kuacha pombe na faida za kuacha tabia hiyo.

Nini Chanzo Cha watu wengi kuwa walevi wa pombe?

Watu wengi huingia katika ulevi wa pombe kutokana na sababu nyingi zikiwemo za kiuchumi, kimazingira na kijamii, kama ifuatavyo:-

Kupoteza kazi, kuporomoka au kufilisika kiuchumi:

Uchuguzi unaonyesha kuwa sehemu kubwa ya watu waliojiingiza katika ulevi wakiwamo wasomi na watu wa makundi mbalimbali huwa ni kutetereka kwa hali zao za kiuchumi kama vile kufilisika mitaji yao ya biashara au kupoteza kazi au vyeo vikubwa maofisini.

Hali hizi zote huwatokea watu katika namna ya bila wao kutarajia au kujiandaa na hivyo kukosa uwezo wa kuhimili mtikisiko huo bila kukumbwa na msongo wa mawazo.

Wengi wao huwa si wepesi wa kuipokea hali hiyo na kuacha maisha mapya yaendelee bali hukumbwa na msongo mkubwa wa mawazo kila wakati.

Hivyo ili kujaribu kuepuka mawazo mengi zaidi mtu huamua kuanza kunywa pombe kama njia ya kumfanya ayasahau masahibu yaliyomsibu.

Mfarakano wa kifamilia au kupoteza ndoa:

Migogoro na mifarakano katika familia zetu hutufikisha mahala tukajikuta tunaanzisha tabia ambazo mtu hukuwahi kuwa nazo wala kufikiri kuja kuwa nazo.

Mathalani mtu aliyepoteza ndoa katika mazingira ya kutatanisha hujikuta akikosa mwelekeo na kubaki kuwa na msongo wa mawazo kila wakati, matokeo yake huamua kujiingiza kwenye ulevi wa pombe kama njia ya mkato ya kumfanya ayasahau madhila yaliyompata.

Kupewa majukumu makubwa ya kiofisi au kitaasisi:

Watu wengi wanapopewa majukumu makubwa ya kiofisi hujikuta katika wakati mgumu wa kuandamwa na mawazo mengi ya kila wakati wakijaribu kuwaza jinsi gani wafanye ili taasisi iweze kukuwa na kustawi kukidhi matarajio waliyojiwekea.

Mathalani taasisi zinazojiendesha kibiashara matarajio yake huwa ni kukuza mtaji kwa kufanya biashara na huduma zinazoiletea taasisi faida kubwa. Katika mazingira haya mkuu wa taasisi anatakiwa kuwaza na kubuni mbinu na mikakati ya kuiwezesha taasisi yake kufikia malengo hayo.

Hali kama hii humfanya mhusika ajikute anaanza kutumia pombe kama njia ya kupunguza msongo wa mawazo kichwani akijaribu kujiepusha na hatari ya magonjwa yasiyoambukiza kama vile ugonjwa wa moyo, kisukari na mengineyo hasa kama taasisi husika haifanyi vizuri.

Kujiweka jirani muda mwingi na walevi wa pombe:

Kuna watu wengi wamejikuta wanajiingiza katika unywaji wa pombe kutokana na kuzungukwa na washirika wake wa kazini au katika biashara ambao ni walevi wa pombe.

Kutokana kuwa na mazingira ya ukaribu na watu wa aina hii, mtu hujikuta akishawishika au kushawishiwa kuanza tabia ya ulevi wa pombe.

Kuiga au kufuata mkumbo:

Vijana wengi a hasa wanafunzi wa shule na vyuo huona fahari sana wanapojiona wamelewa pombe, Hujiona kama vile ni watu wanaofanya mambo ya kikubwa na hivyo kujiona kama vile wao ni wakubwa sana kuliko wenzao ambao sio walevi.

Kutokana na mtazamo huu baadhi ya wanafunzi nao hujiingiza kwenye vitendo vya ulevi ili nao waweze kusifiwa na kuonekana mbele ya jamii ya wanafunzi wenzao kuwa nao ni wakubwa au ni mafahari.

Kufanya sana shughuli zinazohusiana na pombe:

Kuna wakati mtu hujikuta akianguka katika ulevi wa pombe kutokana na kujishughulisha za utengenezaji ama uuzaji wa pombe.

Mathalani, watu wanaofanya kazi katika viwanda vinavyozalisha pombe hulazimika kuonja pombe yao mara baada ya kuizalisha kabla ya kuipakia katika chupa /vifungashio ili kujiridhisha na ubora wa bidhaa yao. Hivyo kwa wafanyakazi wa mazingira kama haya ulevi wa pombe kwao huwa ni kawaida.

Kurithi tabia kutoka kwa wazazi:

Kuna baadhi ya wazazi ambao ni walevi wa pombe nao pia hurithisha tabia hizi kwa watoto wao. Hali hii hutokana na wazazi hawa kufanya vitendo hivi vya ulevi mbele za watoto wao bila kukumbuka kuwa vina athiri watoto kisaikolojia na kitabia, Hivyo watoto nao hujikuta wanakuwa wepesi wa kuanza kufanya vitendo hivyo wakijiona kamakwamba wana baraka za wazazi wao.

Mbinu za kuachana na ulevi wa pombe:.

Mbinu zifuatazo zinaweza kumsaidia mtu yeyote katika mazingira yoyote kuacha ulevi wa pombe na akabaki salama kama ifuatavyo;-

Kujiweka bize muda wote na shughuli au mazowezi:

Kujiweka bize muda wote na shughuli au mazowezi huifanya akili yako ijikite zaidi na kile unachokuwa unakifanyia kazi kwa muda huo badala ya kukumbuka vile vya nyuma.

Mbinu hii husaidia sana kupunguza msongo wa mawazo kwa watu waliokumbwa na madhila mbalimbali kama vile kupotezakazi, ndoa au kufilisika mtaji wa biashara na mengineyo.

Jambo la kufanya ni kupanga ratiba yako ya shughuli katika mtiririko utakaokufanya usipate muda wa kukaa bila shughuli. Ikitokea huna shughuli , unga ratiba ya kufanya mazoezi mepesi ya viungo kila wakati.

Ukipewa majukumu makubwa shirikisha wataalamu kupata matokeo mazuri:

Kwa wale wanaokumbwa na msongo wa mawazo kutokana na majukumu makubwa ya kitaasisi, huna haja ya kuitumia pombe kama suluhisho, bali shirikisha wataalamu walio katika fani husika, mfano wataalamu wa miradi, wataalamu wa masoko n.k.

Wape malengo na waeleze unataka kupata matokeo gani katika mradi au huduma za biashara ya taasisi yako, na unata wao washughulike na kitu gani? Kisha wawezeshe kwa vitendea kazi na mazingira bora.

Uwapo nyumbani tumia sehemu ya muda wako kuzungumza na mwenzi wako , watoto wako na kufanya mazowezi ili kuuweka mwili bize na usitowe nafasi ya kukaa na kuzubaa kuanza kufikirisha kichwa kupita kiasi.

Epuka habari au mazingira yanayoshawishi ulevi:

Iwapo katika ofisi yako au biashara zako unaona unazungukwa na watu wengi ambao ni walevi wa pombe, basi, kama ni ofisini nyanyua sheria na kama ni kwenye biashara basi tafuta washirika wengine. Ukibaki na msimamo huo siku zote hata wao watakosa hamu ya kuleta habari za ulevi mbele yako.

Jiwekee malengo binafsi na jisimamie wewe mwenyewe:

Mara nyingi watu wanaojiingiza katika ulevi wa pombe kwa kufuata mkumbo huwa ni watu wasiokuwa na malengo binafsi na hivyo wanayumbishwa kirahisi na tabia za watu wengine.

Ili kuvuka vyema katika wimbi hili ni muhimu hasa kwa vijana kujiepusha na makundi ya watu wenye tabia zisizofaa.

Fanya shughuli zako kitaalamu achana na mazoea:

Kwa wale wafanyakazi wa viwanda vya kutengeneza pombe, bado wanayo nafasi ya kuacha kunywa pombe kwa lego la kupima uora na adala yake watumie vifaa maalumu.

Hivi sasa kuna uvumbuzi wa vifaa vya kisayansi vinavyoweza kutumika kupimia ubora wa pombe ikiwemo kiwango cha kilevi na uwiano wa vile ulivyochanganya kutengeneza hiyo pombe na ukapata majibu sahihi bila kunywa hiyo pombe mdomoni.

Nini faida za kuacha kunywa pombe?

Huimarisha afya ya mwili na akili:


Utafiti unaonyesha kuwa, mlevi yeyote wa pombe yuko katika hatari ya kuugua aina 40 za magonjwa, ikiwemo saratani, magonjwa ya moyo,Figo,Ini, akili na mengineyo yasiyoambukiza. Hivyo uamuzi wa kuacha ulevi wa pome unakuweka mbali kabisa a hatari hizi.

Huimarisha uchumi na kuwezesha kufanya miradi ya maendeleo:

Watu wengi wanaojihusisha na ulevi wa pombe huelekeza fedha zao nyingi kwenye kugharamia pombe kila siku , hivyo basi hatua ya kuacha pombe husaidia kubana bajeti na kuongeza ziada ya fedha ambayo husaidia kufanya mambo mengine ya maendeleo.

Huongeza uwezo wa kufikiri kwa utulivu na kuamua mambo kwa busara:

Pombe kwa kawaida huathiri zaidi ubongo na uwezo wa binadamu kujitambua anapokuwa akifanya jambo flani.

Hivyo basi kuacha kunywa pombe huwezesha akili ya mtu kutulia na kufanya kazi sawasawa muda wote.

Hupunguza mifarakano na kuleta amani katika jamii:

Ulevi wa pombe ndio husababisha ugomvi na kuleta mifarakano katika familia, Hivyo hatua ya kuacha kunywa pombe husaidaia sana kuimarisha amani na upendo katika familia zetu.

Huimarisha nidhamu na utendaji kazi nyumbani na maofisini:

Ulevi wa pombe huchangia sana kumfanya muhanga kushindwa kufanya shughuli zake kwa utulivu na badala yake muda wote huwaza kunywa pombe na hivyo hushindwa kutimiza vema majukumu yake ya kila siku.

Matokeo yake huwa ni kupoteza kazi na kubakia akihangaika mitaani. Hivyo kuacha ulevi wa pombe ni hatua moja muhimu sana katika kulinda pia ajira ya muhusika.

Hupunguza uchakavu wa mwili na kuongeza uimara na unadhifu:

Mbali na madhara ya ndani ya kiafya, pombe pia huchakaza na kulegeza uimara wa mwili wa mhanga, kwani walevi wengi hula chakula kidogo sana bila kujali mahtaji ya mwili.

Hivyo basi hatua ya kuacha ulevi wa pombe husaidia kuimarisha mwili na kupunguza uchakavu unaomfanya mhanga kuonekana kuwa na sura na umbile lisilowiana na umri wake halisi.



Hitimisho:

Kwakua madhara ya ulevi wa pome yamekuwa yakiathiri jamii yetu nzima ya Watanzania wote wakiwemo wasiokunywa wala kutengeneza pome hiyo, hivyo ni jukumu letu sote kama taifa kujenga mazingira rafiki yatakayosaidia kupunguza ulevi na kundi la walevi katika jamii yetu.

Nyenzo muhimu katika kufanikisha hili ni kutoa elimu kwa walevi wote itakayowahamasisha kuachana na tabia hizo hasa kwa kutambua hasara za ulevi wa pombe na faida za kuachana na utamaduni huo.
 
Inasikitisha sana sijui ni kwanini hata nimejikuta nimekwisha tumbukia kwenye ulevi wa kutisha kwa hali niliyofikia ni hatari kwani nakunywa pombe karibu kila siku bila ya kupumzika.

Nimeshakunywa za kienyeji karibu zote, pombe kali zote na kwa sasa nimezamia kwenye bia yaani speed yangu kwa kweli sio nzuri.

Nikinywa nikalewa naanza kujisemesha kuwa Mimi siogopi cha Ukimwi wala kansa nakunywa bia nikalale sitaki mwanamke nawaachia wanywa soda.

Kiukweli naogopa kifo kinachosababishwa na unywaji wa pombe kibaya zaidi nahisi ulevi umenisababishia niwe mbali na Mungu wetu imani imeshuka sana sipati tena muda wa kumkumbuka Yesu.

Nahitaji kubadilika lakini mwenyewe nimeshindwa ndugu wameshaongea mpaka wamechoka wameamua kuniacha tu mwenyewe nifanye ninalotaka nikipata kansa au bawasili au maradhi ya pombe nipambane nayo mwenyewe.

Naomba mtaalam wa saikolojia/kiroho wa kujitolea kunisaidia anisaidie mbinu mbadala, natambua ya kwamba maamuzi ya mwisho yananihitaji Mimi binafsi nijikane lakini kama nilivyosema imekuwa ngumu NASHINDWA.
Baada ya kuacha pombe utafanya nini umewahi kujiuliza ilo,tafuta mbadala ndio ikupe nguvu ya kujitenga na pombe na pia badili marafiki
 
Soma hiki kitabu-kinaweza kukusaidia kuna mada za jinsi ya kuacha sigara,pombe,madawa ya kulevya na jinsi unavyoweza kujitibu magonjwa na matatizo mbalimbali ya kiafya. 0756625286.
IMG-20211203-WA0000.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom