Nahitaji Msaada Kuchagua Vyombo vya Muziki

Ramthods

JF-Expert Member
Jun 2, 2009
515
186
Ndugu wana JF,

Mama yangu anafanya semina mara kwa mara, na pia ni mtoa mada mzuri sana katika mambo mbali mbali ya kijamii. Ameanzisha ministry ambayo hualika watoto yatima, na wana ndoa, wajane n.k kwa ajili ya mafunzo mbali mbali ... that's it.

Nilimuahidi kuwa ningemnunulia vyombo vya muziki - speakers, mixer, amplifier n.k ili wapunguze gharama wanazotumia kukodisha hivi vyombo.

Pia, nadhani vitamsaidia sana maana yeye hutoa pia mada kwenye kitchen parties, send off na harusi.

Binafsi, sina utaalamu kabisa na hivyi vyombo - jambo ambalo limenipa shida sana kujua "Quality ya vyombo, price, na wapi naweza kuvipata"

Nimejaribu kuzunguka maduka tofauti tofauti mjini, na pia kuulizia watu wanaofanya shughuli kama hizi - lakini bado sijapata ushauri wa kueleweka.

Naomba kama unafahamu, una utaalamu wowote kuhusu vyombo vya muziki utoe mchango wako kwenye hii thread.

Vyombo vinavyohitajika vinatakiwa viwe na uwezo wa kupiga muziki, na kutangazia kwenye ukumbi wa kawaida (watu 300 hadi 600). Kama vile tunavyoviona kwenye sherehe mbalimbali za maharusi au send off.

Natanguliza shukrani!
 
Ndugu wana JF,

Mama yangu anafanya semina mara kwa mara, na pia ni mtoa mada mzuri sana katika mambo mbali mbali ya kijamii. Ameanzisha ministry ambayo hualika watoto yatima, na wana ndoa, wajane n.k kwa ajili ya mafunzo mbali mbali ... that's it.

Nilimuahidi kuwa ningemnunulia vyombo vya muziki - speakers, mixer, amplifier n.k ili wapunguze gharama wanazotumia kukodisha hivi vyombo.

Pia, nadhani vitamsaidia sana maana yeye hutoa pia mada kwenye kitchen parties, send off na harusi.

Binafsi, sina utaalamu kabisa na hivyi vyombo - jambo ambalo limenipa shida sana kujua "Quality ya vyombo, price, na wapi naweza kuvipata"

Nimejaribu kuzunguka maduka tofauti tofauti mjini, na pia kuulizia watu wanaofanya shughuli kama hizi - lakini bado sijapata ushauri wa kueleweka.

Naomba kama unafahamu, una utaalamu wowote kuhusu vyombo vya muziki utoe mchango wako kwenye hii thread.

Vyombo vinavyohitajika vinatakiwa viwe na uwezo wa kupiga muziki, na kutangazia kwenye ukumbi wa kawaida (watu 300 hadi 600). Kama vile tunavyoviona kwenye sherehe mbalimbali za maharusi au send off.

Natanguliza shukrani!

Mkuu,
Naomba unipatie maelezo zaidi kwa kunitumia kwenye email SIKONGE@GMAIL.COM. Naomba unipe maelezo zaidi uko mji gani na kiasi gani cha pesa uko tayari ku-spend. Hii itakuwa rahisi kujua wapi nikuelekeze au wapi uagize na vyombo gani vinaweza kukufaa.

Pia muandikie email (PM) ndugu MTANZANIA wa humuhumu Jamiiforums ambaye kama sikosei atakuwa na vyombo kama hivyo hivyo au hata zaidi.
Kwa sasa sokoni kuna mashine za aina nyingi sana na ni bei yako tu. Kuna Microphone kama za shure zinazouzwa hadi zaidi ya dola 1000 moja na nyingine hata dola 10 moja. Mixer zipo zikiwa intergrated na amplifier na nyingine tofauti. Spiker ndiyo usiseme huko kuna za kitoto na heavy duty za bei mbaya kama za JBL. Na zipo ambazo ni ACTIVE (huhitaji amplifier) au za kawaida. Ndiyo maana nasema ukitoa bei gani wataka ku-spend itakuwa rahisi zaidi kukupa msaada uanzie wapi. Kumbuka quality ya sauti ina-cost saana. Hasa hizo Hzs zinaposhuka chini zaidi (sauti kubwa na nzuri ya BASS) huwa inabidi fedha nyingi zitoke. Ndiyo maana ukikuta spiker kubwa hasa sub-woofer zinazopiga kuanzia 20Hzs, bei yake huwa si ya kuvutia kwa watu masikini. Ila kwa wenye pesa zao, mhhhh...
Nilishasikia Mzungu mmoja kajenga jumba lake na kwenye basement akaweka mziki wake wa nguvu na huwa anashuka huko ili kusikiliza miziki yake ya Jazz na Blues. Spiker peke yake alilipa $100,000/- Hivyo hapa Mkuu, ulingo ni Mpana sana, ila Mungu bariki kila mfuko una kisehemu chake.
 
Mkuu,
Naomba unipatie maelezo zaidi kwa kunitumia kwenye email SIKONGE@GMAIL.COM. Naomba unipe maelezo zaidi uko mji gani na kiasi gani cha pesa uko tayari ku-spend. Hii itakuwa rahisi kujua wapi nikuelekeze au wapi uagize na vyombo gani vinaweza kukufaa.

Pia muandikie email (PM) ndugu MTANZANIA wa humuhumu Jamiiforums ambaye kama sikosei atakuwa na vyombo kama hivyo hivyo au hata zaidi.
Kwa sasa sokoni kuna mashine za aina nyingi sana na ni bei yako tu. Kuna Microphone kama za shure zinazouzwa hadi zaidi ya dola 1000 moja na nyingine hata dola 10 moja. Mixer zipo zikiwa intergrated na amplifier na nyingine tofauti. Spiker ndiyo usiseme huko kuna za kitoto na heavy duty za bei mbaya kama za JBL. Na zipo ambazo ni ACTIVE (huhitaji amplifier) au za kawaida. Ndiyo maana nasema ukitoa bei gani wataka ku-spend itakuwa rahisi zaidi kukupa msaada uanzie wapi. Kumbuka quality ya sauti ina-cost saana. Hasa hizo Hzs zinaposhuka chini zaidi (sauti kubwa na nzuri ya BASS) huwa inabidi fedha nyingi zitoke. Ndiyo maana ukikuta spiker kubwa hasa sub-woofer zinazopiga kuanzia 20Hzs, bei yake huwa si ya kuvutia kwa watu masikini. Ila kwa wenye pesa zao, mhhhh...
Nilishasikia Mzungu mmoja kajenga jumba lake na kwenye basement akaweka mziki wake wa nguvu na huwa anashuka huko ili kusikiliza miziki yake ya Jazz na Blues. Spiker peke yake alilipa $100,000/- Hivyo hapa Mkuu, ulingo ni Mpana sana, ila Mungu bariki kila mfuko una kisehemu chake.

Asante sana mkuu kwa maelezo yako.

Binafsi, I was planning to spend up to around 8Mil. Sina uhakika sana kama hizi zinatosha, lakini pia nilikua na plan labda niagize nje, may be naweza nika save costs kidogo.

Mimi nipo Dar, hapa kwetu bongo.

Pia, mambo kama quality and capacity - hapo kidogo utaalam unapiga chenga. But, nachohitaji ni sawa na zile zinazotumika kwenye kumbi za sherehe za kawaida - siyo ya quality ya hali ya juu ya kutumika pale Diamond Jubilee!
 
Sikonge

Hata mimi nimejifunza kitu hapo, kumbe hata U-DJ unauweza! ila usitake 10% kwa huyu jamaaa!
 
Sikonge

Hata mimi nimejifunza kitu hapo, kumbe hata U-DJ unauweza! ila usitake 10% kwa huyu jamaaa!

Masanilo,
Nilikuwa kwanza nataka nifahamu jamaa yuko wapi. Mie sintaweza kumsaidia kununua maana huku Sikonge, vyombo upate wapi? Nitamuelekeza ni wapi na vipi anaweza kuvinunua. Kwa muono wangu wa haraka haraka, ni heri awasiliane na Mtanzania na kwa kuwa yeye alishanunua na kuvipeleka hadi Kyela, anaweza kumsaidia jamaa ili na yeye pia anunue. Uzuri wa UK, kuna jamaa wanauza package nzima na hapo wanapunguza bei. Hivi vyombo duniani havipishani sana bei ingawa China/Hong Kong ni rahisi ila huko unaweza kuletewa vyombo feki. Hivyo mkuu mie sintachukua hata 1%.

Masa, mie ni mpenzi mkubwa sana wa hivi vifaa vya Electronics. Kwa mfano nafahamu kuwa Michuzi anatumia Canon EOS 5D na bei lake liko zaidi ya $2,000 bila Zoom zoom. Kubwa lake linaitwa Mark II kwa sasa na hili lina bei chafu sana.
Kama wataka kuwa DJ, basi kwa sasa kuna kitu inaitwa SERATO. Sema bei lake kubwa sana. Hili inabidi uwe na computer aina ya MAC (wanasema hazifi ikiwa kazini???) na hapo unaunganisha computer kwenye gramaphones au Cd players na kwa kupitia hicho chombo cha SERATO na Mixer. Wanadai kuwa faida yake ni kwamba, huhitaji CDs. Miziki yote unakuwa nayo kwenye MP3 ndani ya LAPUTOPU (hii Mwakalinga hakupi maana ni aghali) na hapo unarahisisha maisha.
Kwa sasa nataka nimuagiza Mtanzania hii camera mpya ya Canon SX1. Ina zoom yake kubwa optical zoom 20 x) na inapiga video HD na sound ni stereo. Ila sema nalo bei yake ni kubwa na zito (linatumia battery 4, AA).

Ukitaka kununua Camera, basi ingia hapa upate shule: http://www.dcresource.com/reviews/cameraList.php

Hivi vingine waweza kuviona ndani ya EBAY.COM na kwa Uk ni ebay.co.uk. Humo utakuta maduka na ukiyafuatilia watakudirect kwenye site yao.

Zinaniuwa ni hizi zimekaa kama caves. Unakuta wanaziunga na zinaleta picha kama KIMPIRA. Kama sikosei The rolling stones walianza kwa kutesa nazo sana maana ukiangalia juu unaona kimpira ila kinatema cheche hadi unachanganyikiwa, hasa mzee Mick Jagger anapoanza ule wimbo wake wa Kishoga "start me up" au there big hit "Satisfaction".
Hebu zione mwenyewe: http://www.jblpro.com/products/Tour/index.html

NB: Kwa pesa hiyo ni rahisi kuagiza nje na utapata vizuri sana kwa bei kama nusu huku ukiweka nusu nyingine kwa usafiri. na kulipia ushuru kama ikibidi. Jaribu kumwandikia Mtanzania PM uone kwa kiasi gani ataweza kukusaidia. Uaminifu wake naweza kusema ni kama asilimia 99.50. Hiyo 0.5 % naiacha maana na yeye ni binadamu tu kama wengine. UK wapo wauzaji wengi na package kibao. Ukivuta subira ikipita X-Mas wanashusha kidogo bei na wapo waweza kuvipata kwa bei nafuu.
 
Last edited:
Mkuu, utaalamu wako ni wa hali ya juu, nashukuru sana. Nimependa sana mambo ya Camera hapo. Mimi pia napenda sana photography - ila mambo hayajakaa safi bado. Siku nikipata mshiko kidogo, nadhani nitatoka na Super Zoom.

Nime m PM Mtanzania, hope he will come back with positive thing.

I can wait - hapa bongo naona bei zao zipo juu, hazipishani sana na za Land Cruiser used ... teh teh teh - just kidding lol!
 
Sikonge

Tuache utani mazee uko vizuri kwenye hayo madude. Mimi nina Yashica 45, zile za zamani unachungulia na kurudisha mkanda manually, Radio nina ya bend 3 ya mkulima, ilianguka toka darini nimeifunga na kamba za katani inakula mzigo tu!
 
Sikonge

Tuache utani mazee uko vizuri kwenye hayo madude. Mimi nina Yashica 45, zile za zamani unachungulia na kurudisha mkanda manually, Radio nina ya bend 3 ya mkulima, ilianguka toka darini nimeifunga na kamba za katani inakula mzigo tu!

Haya, na LAPUTOPU yako ni ya lini? Wewe nawe kwa kamba?

Nimeona makala moja juu ya Mariah Carey na Mumwe Nick Cannon, na nikasoma kuwa jamaa alikuwa ni DJ. Nakuwekea hapa LINK uone. Kama nilivyosema, hata yeye ana Apple Computer. Naona jamaa wamepata soko zuri sana kwa ma DJ. Hii yangu mie ni ASUS, ovyo kabisa. Huwa natakani wakati mwingine nilitupe dirishani. Haya nakupa video angalia mwenyewe.

Ukiangalia utaona maneno SERATO LIVE, ndiyo hicho chombo homeboy (hapo kwenye picha ya chini). Hiyo Laptop nafikiri itakuwa pia MAC. Unaweza kumix Video Clips au Audio peke yake. Masa nunua hicho kifaa, totoz zote zitapanga mstari ziwe zako.

http://www.hollyscoop.com/video/mariah-carey-nick-cannon-1st-wedding-anniversary_1001173.aspx

SERATO.jpg





sslsetup.gif
 
Sikonge

Tuache utani mazee uko vizuri kwenye hayo madude. Mimi nina Yashica 45, zile za zamani unachungulia na kurudisha mkanda manually, Radio nina ya bend 3 ya mkulima, ilianguka toka darini nimeifunga na kamba za katani inakula mzigo tu!

Lakini Masa, hii Radio yako bado ipo poa kabisa. Wengi wangelitamani wawe nayo kama hii. Mwenzio nilitesa sana miaka hiyo na hii nikiwa Dj wa hapa Wilaya ya Sikonge. Miziki yetu wakati ule ndiyo inatesa ni Salongo, Baruti(veve), Shikashika, Super Mazembe, Lipua Lipua, Tabora Jazz, Nyanyembe, na Kiko Kids na watoto wa Nyumbani wa Sikonge, Sukasuka Jazz Band ikiongozwa na Mwalimu Borafya akipiga Solo, wewe acha mchezo bwana. Sukasuka walikuwa wakiimba "sukasuka polepole, usimcheke mchinja mbwa, wazimu utakurudia...." Sijui ilikuwa na maana gani yarabi..... But Life was Good.

Radio_Cassette_Recorder.jpg
 
Mkuu nitafute nikupe bei nzuri
 

Attachments

  • 1401347180272.jpg
    1401347180272.jpg
    41.4 KB · Views: 617
  • 1401347243096.jpg
    1401347243096.jpg
    43.7 KB · Views: 485
  • 1401347324817.jpg
    1401347324817.jpg
    52.2 KB · Views: 767
Back
Top Bottom