Nahitaji majibu kuhusu kirusi cha HIV

Nahitaji majibu kuhusu kirusi cha HIV

Sun is Sun

JF-Expert Member
Joined
Mar 13, 2024
Posts
1,153
Reaction score
1,699
Habari za wakati huu Ndugu zangu Wana-jamiiforums. Nina maswali kadhaa kuhusu kirusi kinachosababisha HIV.

1. Kwanini ni vigumu kirusi kinachosababisha HIV kufa hata kikiwa nje ya mfumo wa mwili wa binadamu? Mfano( Mtu mwenye maambukizi anashona viatu ila bahati mbaya sindano inamchoma, Anachukua sindano anaihifadhi sehemu, Baada ya mda kama miezi minne mtu asiyekuwa na maambukizi Anachukua ile sindano ila na yeye kwa bahati mbaya inamdunga, Baada ya muda anaanza kuonesha dalili na baada ya vipimo anaonesha yupo +tive. Hii ina maana kwamba kwa mda wa miezi minne virusi vilikuwa vina-survive kwenye sindano bila kula chochote.

2. Kwanini kuna baadhi ya watu wachache ambao kirusi cha HIV hakiwezi kuwaletea madhara.
Kuna watu hata ukiwaongezea damu yenye kirusi bado hawatapata HIV na hata vipimo haviwezi kuonesha kama wana maambukizi, Ingawa wana uwezo wa kuambukiza wengine. Kwanini hii hutokea?

3. Kwanini kirusi cha HIV kinaleta madhara kwa Wanadamu tu?
Kirusi cha HIV hakileti madhara kwa nyani, kuku, mbwa, nyoka, punda, ng'ombe, simba n.k, Kwanini wataalam?

4.Kwanini mwenye virusi vya HIV akiacha kutumia dawa virusi vinakuwa sugu?

5. Mwisho. Kirusi cha HIV kiligunduliwa na nani? Na species yake ilitolewa wapi Kwa manufaa gani?.

Wataalam karibuni tujadili hili.
Asanteni.
 
. Kwanini kuna baadhi ya watu wachache ambao kirusi cha HIV hakiwezi kuwaletea madhara.
Kuna watu hata ukiwaongezea damu yenye kirusi bado hawatapata HIV na hata vipimo haviwezi kuonesha kama wana maambukizi, Ingawa wana uwezo wa kuambukiza wengine. Kwanini hii hutokea?
Hili lilishaelezewa humu na DR Mambo Jambo na mimi ni mmoja ya hao watu au nikwambie kiufupi tu ni kwamba virus vinapoingia mwilini kuna mambo mawili yanatokea Seli Hai Nyeupe ndio zinazoulinda mwili na kitu kingine chochote kisichohusiana na mwili kwa ikitokea kuna intruders Seli Hai Nyeupe zinakua km Jeshi la Mwili wako maana yake vitashuka Vikosi kuwahi Bukoba mara moja Vikapambane na Nduli anaetaka kuichukua Ardhi ya Tanzania, sasa ikitokea Virus vimeingia kisha Seli Hali Nyeupe ikaviona km Sehemu ya Mwili basi Virus havitopigana na Seli Hai Nyeupe na hapo mtu hatougua Ukimwi ila atakua anaishi na Virusi vya Ukimwi na hatougua maana Virusi vinaishi mwilini ila havipigani na kuua Seli Hai Nyeupe na kumfanya mtu apoteze Kinga ya Mwili na hii hutokea tupo wachache sana
 
Kwanini mwenye virusi vya HIV akiacha kutumia dawa virusi vinakuwa sugu?
Hii inaeleweka anadukua formula ya dawa ni sawa na wewe uwekwe mazingira ambayo mvua na baridi inanyesha muda wote halafu upewe siku 2 au 3 za bila mvua na baridi hizo siku 2/3 lazima uzitumie kutafuta mbinu za kukabiliana na mvua na baridi na mvua maisha yako yote yaan lazima uwahi miavuli na makoti na masweta mazito na majaketi haraka hata baridi na mvua vikija vinakukuta ushajikoki, sasa Virus navyo vina hio tabia
 
Maswali yako ni mazito na yanaangazia vipengele muhimu kuhusu virusi vya HIV. Hebu tujadili moja baada ya jingine:

1. Kwanini ni vigumu kirusi cha HIV kufa hata nje ya mwili wa binadamu?

Kwa kweli, virusi vya HIV haviwezi kuishi kwa muda mrefu nje ya mwili wa binadamu. HIV ni dhaifu nje ya mazingira ya mwili na hawezi kustahimili hali ya hewa kali, jua, au ukavu. Kwa mfano:

Damu ikiwa imetoka mwilini na kukaushwa, HIV huweza kufa ndani ya muda mfupi (dakika au saa kadhaa).

Katika sindano, ikiwa kuna kiasi cha damu kilichokwama ndani, virusi vinaweza kuishi kwa muda fulani ikiwa mazingira ni ya unyevunyevu. Lakini kwa miezi minne, uwezekano wa virusi kubaki hai ni mdogo sana.

Uambukizo wa HIV kwa njia ya sindano hutokea mara nyingi kwa watu wanaoshirikiana sindano safi za kudunga madawa ya kulevya, ambapo damu inaingia moja kwa moja mwilini bila kukauka.

Kwa hivyo, tukio ulilotaja ni nadra sana kutokea kwa muda huo mrefu.

2. Kwanini kuna watu wachache ambao kirusi cha HIV hakiwezi kuwaletea madhara?

Hii ni kwa sababu ya tofauti za kijenetiki katika baadhi ya watu. Kuna watu wenye mabadiliko (mutation) kwenye jeni iitwayo CCR5-Δ32. Jeni hii inahusika na mapokezi ya HIV kwenye chembechembe za kinga (CD4).

Watu wenye nakala mbili za CCR5-Δ32 hawawezi kupata maambukizi ya HIV kwa njia ya kawaida, kwani virusi haviwezi kuingia kwenye chembechembe za mwili wao.

Wale wenye nakala moja wanaweza kuambukizwa, lakini HIV inashambulia mwili wao polepole sana.

Hii ndio msingi wa matibabu ya "Berlin patient" na "London patient" ambao walipona HIV baada ya kupokea upandikizaji wa uboho kutoka kwa wafadhili waliokuwa na jeni hii.

3. Kwanini HIV huleta madhara kwa wanadamu pekee?

HIV ni sehemu ya kundi la virusi vinavyoitwa lentiviruses, ambavyo vinaathiri mamalia tofauti.

HIV asili yake ni kwa nyani, lakini kwao huitwa SIV (Simian Immunodeficiency Virus) na haileti madhara makubwa kwao kwa sababu wameishi nayo kwa maelfu ya miaka na miili yao imezoea.

Wanyama wengine kama mbwa, ng'ombe, na ndege hawana vipokezi maalum vya HIV kwenye chembechembe zao za kinga, hivyo hawawezi kuambukizwa wala kudhuriwa na virusi hivyo.

4. Kwanini mwenye HIV akiacha kutumia dawa virusi vinakuwa sugu?

Dawa za ARVs (Antiretroviral Therapy) hufanya kazi kwa kudhibiti virusi visizaliane.

HIV huwa na kasi kubwa ya kubadilika kijenetiki (mutation), na kama mtu akiacha kutumia dawa, virusi vilivyobaki vinaweza kubadilika na kuwa sugu kwa dawa hizo.

Hii inafanya iwe vigumu kuzuia kuzaliana kwao tena, na kusababisha kinga ya mwili kuharibika haraka zaidi.

5. Kirusi cha HIV kiligunduliwa na nani, na species yake ilitoka wapi?

HIV kiligunduliwa kwa mara ya kwanza mwaka 1983 na wanasayansi wawili kwa nyakati tofauti:

Luc Montagnier wa Pasteur Institute, Ufaransa

Robert Gallo wa Marekani

HIV inaaminika kuwa ilitokana na SIV kutoka kwa nyani wa Afrika, hususan jamii ya chimpanzi (Pan troglodytes). Inaaminika kuwa virusi hivi vilihamia kwa wanadamu kupitia uwindaji wa nyani kwa chakula, ambapo damu yenye virusi iliingia mwilini mwa wawindaji.

HIV-1 (iliyotawala duniani) ilitoka kwa chimpanzi, wakati HIV
 
Mwisho. Kirusi cha HIV kiligunduliwa na nani? Na species yake ilitolewa wapi Kwa manufaa gani?.
Hiki kirusi kiligunduliwa na madaktari, chanzo ni nyani alifanyiwa utafiti huko Misitu ya Congo DRC wanapogombea Ardhi yenye Madini sasa km unavyojua Wazungu wakafanya mapenzi na Nyani hapo balaa ndipo lilipoanzia, hakuna manufaa ni udadisi tu wa madaktari ku-test magonjwa, lakini nikwambie tu mambo mengi hususani magonjwa unayaona chanzo chake ni masuala ya ki-vita na masuala ya kijeshi zaidi hata hii HFC connection inayokuwezesha kutumia Smartphone leo ni military made, virusi vipo kibao huko maabara za duniani vinauzwa tu hata wewe ukitaka unaweza kwenda kuvinunua ila gharama yake sio ndogo
 
Hili lilishaelezewa humu na DR Mambo Jambo na mimi ni mmoja ya hao watu au nikwambie kiufupi tu ni kwamba virus vinapoingia mwilini kuna mambo mawili yanatokea Seli Hai Nyeupe ndio zinazoulinda mwili na kitu kingine chochote kisichohusiana na mwili kwa ikitokea kuna intruders Seli Hai Nyeupe zinakua km Jeshi la Mwili wako maana yake vitashuka Vikosi kuwahi Bukoba mara moja Vikapambane na Nduli anaetaka kuichukua Ardhi ya Tanzania, sasa ikitokea Virus vimeingia kisha Seli Hali Nyeupe ikaviona km Sehemu ya Mwili basi Virus havitopigana na Seli Hai Nyeupe na hapo mtu hatougua Ukimwi ila atakua anaishi na Virusi vya Ukimwi na hatougua maana Virusi vinaishi mwilini ila havipigani na kuua Seli Hai Nyeupe na kumfanya mtu apoteze Kinga ya Mwili na hii hutokea tupo wachache sana
Kwahiyo wewe ni HIV+?

Cc: mzabzab
 
Hiki kirusi kiligunduliwa na madaktari, chanzo ni nyani alifanyiwa utafiti huko Misitu ya Congo DRC wanapogombea Ardhi yenye Madini sasa km unavyojua Wazungu wakafanya mapenzi na Nyani hapo balaa ndipo lilipoanzia, hakuna manufaa ni udadisi tu wa madaktari ku-test magonjwa, lakini nikwambie tu mambo mengi hususani magonjwa unayaona chanzo chake ni masuala ya ki-vita na masuala ya kijeshi zaidi hata hii HFC connection inayokuwezesha kutumia Smartphone leo ni military made, virusi vipo kibao huko maabara za duniani vinauzwa tu hata wewe ukitaka unaweza kwenda kuvinunua ila gharama yake sio ndogo
Kwahiyo CPA makala yupo sahihi?
 
Kwahiyo wewe ni HIV+?

Cc: mzabzab
Hujanielewa mkuu soma tena sijasema ni +ve mimi ni -ve yaan mashine inasoma -ve sababu ni sehemu ya mwili havipigani na Seli Hai Nyeupe na kufanya CD4 ishuke kiasi cha kuonyesha una Ukimwi Upungufu wa Kinga Mwilini, hapo inabidi utulie ili unielewe mfano wewe hapo Mwilini unaishi na bacteria Mwilini wapo wazuri na wapo wabaya ila wabaya wanapozidi wanaanza kudhoofisha kinga ya mwili kwa hio utahitaji dawa utumie ili upunguze idadi ya bacteria mwilini unapotumia dawa sio kwamba unaua bacteria wote ila unapunguza idadi isiweze kusumbua kinga ya mwili pia una virusi ndani ya mwili wako ambavyo havipigani na kinga ya mwili ila vikianza kupigana ndio unaona unaanza na mafua mafua kichwa kuuma juu huko ndani kuna vita kubwa sana inaendelea
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom