Nahisi Mungu ni mbinafsi

Nahisi Mungu ni mbinafsi

Mmhh sijui umefikilia nini lakini acha yabaki kuwa mawazo yako tu
 
Iko hivi, ukweli ni kwamba walio na Yesu wanatumaini. Hata wakipitia changamoto, Yesu Kristo hufanya huwasadia. Changamoto zipo kwa kila mtu, ila walio na Yesu, wanashinda zaidi ya kushindwa. Wakiugua hospital zikishindwa, bado wana msaada wa Mungu alio hai. Hiyo ndio tofauti.

Kingine, kila kitu chema chatoka kwa Mungu. Mungu ana penda watu wote ndio maana mvua na jua huwapatia wema na waovu. Kwa hiyo vyote walivyonavyo wema na waovu vyatoka kwa Mungu pekee.

Cha muhimu zaidi, walio na Yesu, wanatumaini hata baada ya kufa. Hii ni kwasababu wanae Yesu ambaye ni ufufuo na uzima. Hata wakifa, wataishi milele na Yesu mbinguni. Wasio na Yesu, hata wakiwa na mali nyingi kiasi gani, mwisho wa mtu bila Yesu, ni kilio na kusaga meno. Ni hukumu ya kutisha na moto was milele.

Umejibu pasipo kutafakari zaidi kusudio langu. Cha kwanza utambue ya kwamba hata Kama unamtegemea yesu na akakusaidia kwa imani yako hiyo haimaanishi ya kwamba unachokiabudu ndicho sahihi na ndio maana nimekupa mfano wa mtu anayeabudu ng'ombe na akaomba kwa ng'ombe na akafanikiwa hitaji lake au mfano pia kwa waislamu wanaabudu Mungu tofauti na yesu na wanaomba na wakatimiziwa hitaji Lao hizo zote ni imani tu. Hizi dini wengi wamezirithi, wewe ungekuta wazazi wako kwenye dini tofauti na ya ukristo nawewe ungefuata dini walizonazo na ungejiona upo sahihi katika imani yako.

Halafu kuhusu kutoa hukumu ya kutisha, Mungu yupi huyo katili atoe hukumu kwa binadamu wakati asilimia kubwa ya matatizo ya binadamu ameyasababisha yeye mwenyewe? Kwanini amuumbe binadamu mwenye mapungufu halafu amwachie shetani awachezee viumbe vyake wakati anajua kuwa binadamu ni dhaifu?

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom