Nahisi Mungu ni mbinafsi

Nahisi Mungu ni mbinafsi

Eti chuo cha Tandabui kinatoa kozi gani wadau?
 
Ngoja nikusaidie japo kidogo kwa mfano hoja yako ya nne kuwa wanawake wanakandamizwa na Mungu ndio maana hawakuwa hata viongozi wala hawana haki ya mirathi vitu vya uongo kabisa

Maandiko yanataja viongozi wengi wanawake nitakutajia wawili mmoja ni dada yake Musa ambaye alikuwa nabii Miriamu mbali ya kuwa nabii alikuwa kiongozi pia wa pili anaitwa Deborah huyu mpk vita aliwaongoza waisraeli baada ya mwanaume kusoma pia alikuwa nabii na wengine wengi

Habari ya mirathi nao ni uongo mwingine wanawake walikuwa na haki ya kurithi pitia hapa

Yoshua 17 : 3 - Lakini Selofehadi, mwana wa Heferi, mwana wa Gileadi, mwana wa Makiri, mwana wa Manase, hakuwa na wana waume ila binti; na majina ya hao binti zake walikuwa wakiitwa Mala, na Noa, na Hogla, na Milka, na Tirsa.

Yoshua 17 : 4 - Nao wakakaribia mbele ya Eleazari, kuhani, na mbele ya Yoshua, mwana wa Nuni, na mbele ya mashehe, wakasema, Bwana alimwamuru Musa kutupa sisi urithi kati ya ndugu zetu; basi kwa kuiandama hiyo amri ya Bwana akawapa urithi kati ya ndugu za baba yao.
 
Mungu no Mbinafsi kweli..

Kwani anajitosheleza na kila kitu/jambo...

Haitaji KAMPANI (Has a ya Mwanaadamu) kufanya Mambo/Maamuzi yake....

MUNGU NI MBINAFSI...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hapana ,, wapo wanaokesha nyumba, za ibada lakini hawafanikiwi lakini wengine wasioabudu wanafanikiwa
Nini maana ya kufanikiwa. Uzima wa mtu haupo katika wingi wa vitu au Mali. Asikudanganye mtu yoyote, maisha bila Yesu ni bure. Haijalishi mtu ana Mali nyingi kiasi. Kuna faida mtu, kuupata ulimwengu wote na kuishia jehanamu ya milele kwenye moto? Baraka za Mungu siku zote hazina majuto. Ukimtegemea Mungu atakupa baraka ambazo fedha haiwezi kununua. Afya njema ni baraka ya Mungu, furaha ni baraka za Mungu nk. Yoyote anayemtegemea Mungu, hawezi kupungukia na kitu. Kumbuka kuna needs na wants. Siku zote Mungu atahakikisha ukimtegemea unapata the needs. Halafu ukizidi, kumtegemea, atakupandisha kidogo kidogo. Kumbuka utajari na baraka zidumuzo hutoka kW Mungu tu.

Of course, kuna watu wamefanikiwa kwa njia zisizo halali, kuua ,kudhulumu etc. Pia mafanikio yanatokana na principles of life, kama working hard. Sasa uwe mpagani au la, usipofuata kanuni hizi huwezi kufanikiwa. Kusali ni muhimu, but bidii pia ni muhimu. Ukiwa na Yesu, ukatia na bidii kufanikiwa ni lazima. Yaani lazima utafanikuwa tu.

La muhimu zaidi, ni kutokufa katika dhambi. Haitasaidia ukifanikiwa kama trump na kuishia jehanamu ya moto
 
Kama kuna watu wanaweza kumpinga Mungu,ina maana Magu yeye ni zaidi ya Mungu?
 
Nahisi Mungu ni mbinafsi kwa sababu zifuatazo

1)humpa amtakaye, Mungu kupitia vitabu vya dini amekuwa akisema mara kwa mara kwamba yeye humpa neema na humfanikishia mahitaji mja amtakaye, hapa moja kwa moja ana dhihirisha sifa ya ubinafsi kwa maana kama hakupendi hata umuombe namna gani hutofanikiwa abadani asilani.


2)humuongoa au humuepusha na maasi mtu amtakaye , hapa pia ana dhihirisha ubinafsi wake, kwa kuwa kama mja fulani anatenda dhambi Mungu atafanya juu chini kumuepusha hata kama huyo mtu hakuwa mtu wa ibada, lakini wakati huo huo wengine wakitenda maovu anawaacha wateketee na hawapi msaada wowote, hapa inaonesha kwa kiasi gani ana ubinafsi.

3)kuna mwengine hata afanye mema kiasi gani, malipo atakayopewa ni madogo sana, lakini mwingine akifanya mema kidogo ana shushiwa lundo la thawabu.

4)Ana waonea sana wanawake, hataki wawe viongozi, kwenye umiliki wa mali hasa Mirathi anataka wanaume tu ndio wapewe vipaumbele vya kumiliki.

5)kuna wengine tangu anazaliwa mpaka anafariki hajawahi kuonja raha yoyote ya dunia na wala hajui dunia ikoje, kwa sababu utakuta amezaliwa kipofu na maradhi tele mwilini na hajawahi kupata nafuu kuanzia ana zaliwa mpaka anafariki.
Ulikofika siyo kuzuri

Kwa we siyo mbinafsi hebu fikiria baada ya deki dekio unatunza wapi baada ya kufagia mfagio unatunza wapi

Viatu vinakupa dhamani kubwa sana kwa nini usiviweke kwenye kochi
Badala yake unaviwekwa kwenye nanillliiiii

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni kweli kabisa mkuu haiwezekani mungu atuache wengine tunadhini na kufanya mazambi hili atusubiri kutuhukumu wakati remote control ya binadamu anayo yeye
 
Nini maana ya kufanikiwa. Uzima wa mtu haupo katika wingi wa vitu au Mali. Asikudanganye mtu yoyote, maisha bila Yesu ni bure. Haijalishi mtu ana Mali nyingi kiasi. Kuna faida mtu, kuupata ulimwengu wote na kuishia jehanamu ya milele kwenye moto? Baraka za Mungu siku zote hazina majuto. Ukimtegemea Mungu atakupa baraka ambazo fedha haiwezi kununua. Afya njema ni baraka ya Mungu, furaha ni baraka za Mungu nk. Yoyote anayemtegemea Mungu, hawezi kupungukia na kitu. Kumbuka kuna needs na wants. Siku zote Mungu atahakikisha ukimtegemea unapata the needs. Halafu ukizidi, kumtegemea, atakupandisha kidogo kidogo. Kumbuka utajari na baraka zidumuzo hutoka kW Mungu tu.

Of course, kuna watu wamefanikiwa kwa njia zisizo halali, kuua ,kudhulumu etc. Pia mafanikio yanatokana na principles of life, kama working hard. Sasa uwe mpagani au la, usipofuata kanuni hizi huwezi kufanikiwa. Kusali ni muhimu, but bidii pia ni muhimu. Ukiwa na Yesu, ukatia na bidii kufanikiwa ni lazima. Yaani lazima utafanikuwa tu.

La muhimu zaidi, ni kutokufa katika dhambi. Haitasaidia ukifanikiwa kama trump na kuishia jehanamu ya moto

Je wote Wanaoamini juu ya yesu au Mungu hakuna asiyekuwa na afya njema au furaha? Wapo wengine hawana imani juu ya Yesu na wanaishi vyema tu. Mfano waislamu na mabaniani hawaamini katika kumuabudu yesu lakini wapo wenye afya njema tu na pia yupo mkristo umwambii kitu kwa yesu lakini bado ana maisha yenye changamoto kibao.

Na swala la pili nikuulize je ulimwengu unaongozwa na miungu mingapi? Kwamfano Kama Mungu wa wakristo ndio sahihi kwanini waislamu, mabudha, wabaniani, n.k. wanapoomba kwa imani zao nao wanajibiwa maombi yao? Kwanini huyo yesu asioneshe uwezo wake kwa kutokuteleza mahitaji ya mtu anayeomba kinyume chake? Fikiria mtu ana amini ng'ombe ndiye Mungu wake na akiomba kwa imani yake kwa ng'ombe anasaidiwa pia.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Je wote Wanaoamini juu ya yesu au Mungu hakuna asiyekuwa na afya njema au furaha? Wapo wengine hawana imani juu ya Yesu na wanaishi vyema tu. Mfano waislamu na mabaniani hawaamini katika kumuabudu yesu lakini wapo wenye afya njema tu na pia yupo mkristo umwambii kitu kwa yesu lakini bado ana maisha yenye changamoto kibao.

Na swala la pili nikuulize je ulimwengu unaongozwa na miungu mingapi? Kwamfano Kama Mungu wa wakristo ndio sahihi kwanini waislamu, mabudha, wabaniani, n.k. wanapoomba kwa imani zao nao wanajibiwa maombi yao? Kwanini huyo yesu asioneshe uwezo wake kwa kutokuteleza mahitaji ya mtu anayeomba kinyume chake? Fikiria mtu ana amini ng'ombe ndiye Mungu wake na akiomba kwa imani yake kwa ng'ombe anasaidiwa pia.


Sent using Jamii Forums mobile app
Iko hivi, ukweli ni kwamba walio na Yesu wanatumaini. Hata wakipitia changamoto, Yesu Kristo hufanya huwasadia. Changamoto zipo kwa kila mtu, ila walio na Yesu, wanashinda zaidi ya kushindwa. Wakiugua hospital zikishindwa, bado wana msaada wa Mungu alio hai. Hiyo ndio tofauti.

Kingine, kila kitu chema chatoka kwa Mungu. Mungu ana penda watu wote ndio maana mvua na jua huwapatia wema na waovu. Kwa hiyo vyote walivyonavyo wema na waovu vyatoka kwa Mungu pekee.

Cha muhimu zaidi, walio na Yesu, wanatumaini hata baada ya kufa. Hii ni kwasababu wanae Yesu ambaye ni ufufuo na uzima. Hata wakifa, wataishi milele na Yesu mbinguni. Wasio na Yesu, hata wakiwa na mali nyingi kiasi gani, mwisho wa mtu bila Yesu, ni kilio na kusaga meno. Ni hukumu ya kutisha na moto was milele.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom