Nahama Aliexpress naenda Ebay

Nahama Aliexpress naenda Ebay

Mshukuru sana MUNGU, Mi juzi juzi tu hapa, walinipiga 130K, nlinunua bidhaa ikaja mbovu, kurudisha kimoja, kila nkiwauliza wana nambia swala langu linashughulikiwa tena hadi wanakua wakari, ipo siku yako we endelea tu.
Chukua tips hii,unavyofungua bidhaa make sure una record process nzima ya ufunguaji..itakusaidia kweny dispute

Sent from my M2101K7AG using JamiiForums mobile app
 
ALIEXPRESS NAVUNJA NAO MKATABA
Tambua kuwa wauzaji toka china pia wapo ebay.

Ila advantage kubwa ya ebay ni katika swala zima la refund, iwapo mzigo haujakufikia kabisa, na tracking inaonyesha hivyo, ila kama umekufikia ni lazima urudishe bidhaa husika ndio utapata fidia.

Swala la msingi ni kumkagua muuzaji husika wa bidhaa kabla ya kununua kwake.
 
Kitu kidogo sana ki circuit flan cha dola mbili uje ulipe sijui kije na nn si hasara hio
Hio free shipping inaweza chukua hata mwaka ama usipate kabisa. Kuna mzigo wangu pia wa mwezi wa 9 upo south Africa bado hata Bongo haujakuja. Kama ni kitu muhimu Lipia tu standard shipping.
 
Pole sana mdau. kama wadau wengine walivyokushauri cha muhimu zingatia haya
  1. Soma reviews za watu walionunua vitu kwa huyo seller uone wana mrate vipi, kama ana reviews chache akili kichwani (ingawa anaweza kuwa ndo ameanza karibuni, ila the rule of thumb ni kwamba reviews chache stay away)
  2. Make sure wakati una search kitu unataka nunua kushoto kwako chagua suppliers ambao ni verified na wanatoa trade assurance hawa ikitokea cha kutokea aidha watakuletea mzigo mwingine ama hela itarudishwa wewe utachagua (nimejaribu kuweka screen shot hapa naona imegoma)
  3. wakati una search bidhaa unayotaka hakikisha pale palipoandikwa sort by unachagua order maana yake ni kwamba watakuletea kwanza suppliers ambao wameuza hiyo bidhaa unayotaka kwa wingi sana ukilinganisha na wengine -yaani bidhaa zao zina ubora/hawana longo longo ndo maana wameweza kuuza kwa wingi ukilinganisha na wengine
  4. kama ni supplier mpya kabisa ni vizuri ukaomba akutumie sample ya bidhaa unayotaka kabla hujaweka hela kununua mzigo mkubwa
  5. ukipata ishu kama hiyo report kwa alibaba/aliexpress mapema waweze mblock huyo seller asiwaumize wengine
binafasi nanunua na kuuza alibaba miaka mingi tu sijapata shida kabisa.pole sana
100%
 
Huwa kitu chochote cha maana sinunui Aliexpress na Ebay pia kuwa makini wauzaji wa aliexpress na ebay wanaweza kuwa hao hao. Make sure seller kauza maelfu ya Bidhaa na ana rating 90+ ili kujua kama sio tapeli.
Dah.. Umenitisha wakati nlitaka kuagiza simu toka south korea kupitia Ebay
 
Nikawaida yangu kuagiza bidhaa mtandaoni na nimeisha pokea order zaidi ya tatu ndani ya muda sahihi Ila hii order ya mwisho ndo ilikuwa matata nimeagiza mzigo wangu LCD Display ya iPhone 6 plus muda umefika nimepokea mzigo wangu kuja kuangalia nakutana na LCD ambayo inaonekana ni used alafu zile lock zake za pembeni zimekatwa Tena zimekatwa kifujo fujo mbaya zaidi kitu chenyewe hakifanyi kazi kiufupi ni dead.

Nime OPEN DISPUTE nikaelezea kila kitu baadae AliExpress wananiambia nirudishe bidhaa ili nirudishiwe pesa zangu na ninavyojua ningumu Posta yetu kutuma vitu nje hasa vitu Kama hivi.

SASA ALIEXPRESS NAVUNJA NAO MKATABA
Nijuavyo mimi usiporidhika na bidhaa wanakupa option 2
1. Wakutumie nyingine
2. Warudishe pesa
Policy ya kurudisha kifaa ndio naisikia kwako
 
Naomba kufahamu namna kupokea mzigo
unapokealea posta au DHL?
Kwa nchi za huku ulaya wanapokea DHL yaani delivery inakuja mpaka mlangoni pako wanagonga wanakupatia mzigo, usipokuepo hme mzigo unapelekwa posta iliokaribu nayo unaachowa kikaratasi kukujuulisha kuwa uwende posta hio kuchukua mzigo wako

Kwa nchi za huko kwetu nafikiri wanakutumia mzigo wako uwende kuupokea posta kwa sababu sisi nchi yetu haina residents address so lazima tuende posta kufuata mzigo, ila kabla ya kununua mzigo nenda posta kwanza kaulizie wakupatie address yao hao posta, thn hio address utaiandika kwenye kwenye sehem ya mzigo wako utakapoupokea yaani ndaani ya huo mtandao wa AliExpress
 
Kwa nchi za huku ulaya wanapokea DHL yaani delivery inakuja mpaka mlangoni pako wanagonga wanakupatia mzigo, usipokuepo hme mzigo unapelekwa posta iliokaribu nayo unaachowa kikaratasi kukujuulisha kuwa uwende posta hio kuchukua mzigo wako

Kwa nchi za huko kwetu nafikiri wanakutumia mzigo wako uwende kuupokea posta kwa sababu sisi nchi yetu haina residents address so lazima tuende posta kufuata mzigo, ila kabla ya kununua mzigo nenda posta kwanza kaulizie wakupatie address yao hao posta, thn hio address utaiandika kwenye kwenye sehem ya mzigo wako utakapoupokea yaani ndaani ya huo mtandao wa AliExpress
Hata Tanzania unaletewa hadi mlangoni, ni vile tu ukinunua vitu online unachagua njia ya Bei rahisi. Tumia Aramex, Dhl etc utaletewa kwako, atleast uwe eneo linafikika kirahisi.
 
Nijuavyo mimi usiporidhika na bidhaa wanakupa option 2
1. Wakutumie nyingine
2. Warudishe pesa
Policy ya kurudisha kifaa ndio naisikia kwako
Nilipewa option moja tu ya kurudisha mzigo ndo nirudishiwe pesa zangu
 
Back
Top Bottom