GeniSys101
JF-Expert Member
- Aug 10, 2015
- 1,229
- 1,468
Pole sana mdau. kama wadau wengine walivyokushauri cha muhimu zingatia haya
- Soma reviews za watu walionunua vitu kwa huyo seller uone wana mrate vipi, kama ana reviews chache akili kichwani (ingawa anaweza kuwa ndo ameanza karibuni, ila the rule of thumb ni kwamba reviews chache stay away)
- Make sure wakati una search kitu unataka nunua kushoto kwako chagua suppliers ambao ni verified na wanatoa trade assurance hawa ikitokea cha kutokea aidha watakuletea mzigo mwingine ama hela itarudishwa wewe utachagua (nimejaribu kuweka screen shot hapa naona imegoma)
- wakati una search bidhaa unayotaka hakikisha pale palipoandikwa sort by unachagua order maana yake ni kwamba watakuletea kwanza suppliers ambao wameuza hiyo bidhaa unayotaka kwa wingi sana ukilinganisha na wengine -yaani bidhaa zao zina ubora/hawana longo longo ndo maana wameweza kuuza kwa wingi ukilinganisha na wengine
- kama ni supplier mpya kabisa ni vizuri ukaomba akutumie sample ya bidhaa unayotaka kabla hujaweka hela kununua mzigo mkubwa
- ukipata ishu kama hiyo report kwa alibaba/aliexpress mapema waweze mblock huyo seller asiwaumize wengine