NAJYUZ
JF-Expert Member
- May 10, 2021
- 1,883
- 3,217
Ni vitu gani vitakavyo kufanya ufukuzwe chuoni Monduli TMA..?unajua kulikuwa na wa aina mbili kule monduli
1. ni wale ambao walishapiga kozi rts wana vyeo kuanzia private wakaenda munduli kupiga kozi ya uafisa ,hao ni pamoja na wale millitary science ambao wanapiga kozi rts halafu hufanya tena usahili wa kwenda monduli. hao sasa wakirudishwa wanarudi vikosini mwao kuendelea na majukumu yao ya vikosini.
2.
ni wale walio chukuliwa vyuoni wenye fani ya udaktari na mainjinia ambao walifanyiwa usahili pale makutupora halafu wakapiga kozi ya jkt, baada ya kumaliza wakafanya usahili wa kwenda monduli walioshindwa wakaenda msata waliofaulu ndio wakaenda monduli moja kwa moja wakiwa bado hawajapitia mafunzo ya awali ya kijeshi,, sasa ndo hao ambao wakishindwa kule wanarudi kama raia tuu wakaambiwa wasubiri wapige kozi tena ya awali ya kijeshi rts ili wawe maprivate .sasa wengine wanaona jau kozi ya monduli ilivo ngumu halafu unarudi tena kuwa kiruta wa rts sio poa japo kuna watu wanakomaa tuu
Sent using Jamii Forums mobile app