Nadharia ya miaka 1,000 duniani ni sawa na siku moja mbinguni si sahihi kabisa

Ngoja na mimi nijaribu kuwaza kwa sauti na kuchangia;

Nadhani hiyo phrase na context zilipotumika zinazidi kuelezea na kuthibitisha "umilele" wa Mungu
Kwanza kwenye zaburi, mtunga zaburi anaomba na ku-acknowledge that things we see taking a long time to us as humans can be done in a very short time by God. Angalia anazungumzia perishing in the para. Hii ya kusema miaka elfu ni sawa na siku moja mimi nadhani mwandishi amewaza 1000 years (millenium) kuwa kipindi kikubwa cha kulinganisha na siku moja. So unaweza kujua kwa mfano kwenye zaburi hiyo hiyo anapoendelea kuzungumzia 70 to 80 years ya uhai wa binadamu ingekuwa ni miaka mingapi. Meaning to God what we think as long time is a very short moment and what we think can be done in long term (1000 years in this case) can be done in almost instant moment by God

Kwenye kitabu cha Peter, mwandishi anajaribu kuwakumbusha na kutukumbusha sisi sote kutoishi kwenye dhambi kwa vile eti Bwana aliahidi angerudi then watu wanaona amekawia so waka-assume hatarudi.
He is bringing in this concept of time to remimd them kwamba wasiweke ukomo kwa lini Bwana atarudi au wasiache kuenenda kwenye njia sahihi just because time has passed and the Lord has not come back.

Hizi phrase actually zinatuambia tusiweke ukomo kwenye existence na acting ya Mungu kwa sababu God is eternal and we should not think kwamba the action is time barred. To us ni miaka 1000 lakini kwa Mungu ni kama one day (kwamba we think wa have waited for so long, but hii inatuambia tuwe wavumilivu kwani what we think as 1000 years (too long), Mungu anaitazama kama siku moja ( very short period)
 
Siri za uumbaji wa hii dunia hakuna mwanadamu anazijua, manabii walitoa chache na nyingi ni ngumu kuzielewa.

Kwa mfano hakuna mwanadamu ajuaye dunia hii imekuwepo kwa miaka mingapi tangu uumbaji...

Shetani alipotupwa duniani alitoa baadbi ya siri Hasa wanazotumia watu kwenda kuzimu; namna ya kutenganisha mwili na nafsi nk

Yesu kristo alitoa mafundisho tu lakini hakusema kule mbinguni nini kilifanyika kabla ya uumbaji na baada ya uumbaji, mamlaka yaliyokuwepo nk.. Kulikuwa na limitation kwake kwa sababu naye alizaliwa kama binadamu wa kawaida ili kupitia kwake tuamini.
 
Kwa uelewa wangu"Miaka 1000 = 1day" ni lugha ya picha ambayo ina tafsiri yake so hutakiwi kuichukulia kama ilivo. Vitabu vyetu vya Imani vimetumia lugha ya moja kwa moja(direct) na ya picha/ mafumbo (indirect).

UELEWA WANGU KATIKA HILI.
Ni kwamba vitu ambavyo vinaweza kufanyika kwa miaka 1000 hapa duniani kwa Mungu huweza kufanyika siku moja tu/. Mambo ambayo binadamu tunayaona ni magumu kwa Mungu ni rahisi sana.
 
Basi na iwe tu hiyo hiyo miaka 1,000. Maana tumejikuta tupo tu na hatuna uwezo wa kuipunguza. Vyovyote tutapokea.
 
Ili tuhesabu siku ni lazima vitu viwili vitokee
1.Mchana kuuvua usiku
2. Usiku kuuvua mchana
Kama vitu hivi kwa Mungu huko alipo hakuna basi , utakuwa umesema kweli
 
Kwa uelewa mdogo tu, siku huhesabiwa kwa kuzama kwa jua na kutokeza, this results due to earth rotation. Sasa je, huko kwa Mungu kuna dunia inazunguka jua?

Hii nadharia ya Mungu inachanganya sana!
Kwani wakati wa uumbaji si Mungu alikuwa akiumba huku akiwa huko huko mbinguni na biblia ikihesabu siku kwa kusema "ikawa jioni, ikawa asubuhi", siku ya pili, ya tatu hadi ya saba? Sasa kudai kwamba miaka elfu moja ya duniani ni sawa na siku moja ya mbinguni si itapelekea madai mengine kwamba uumbaji uliofanyika kwa siku saba za mbinguni zinamaanisha ilitumika miaka 7,000 ya duniani kukamilisha uumbaji?

Na hivyo siku ya kupumzika (sabato ya bwana?) inatakiwa iwe kila inapotimia miaka 7,000?
 
Kwani wakati wa uumbaji si Mungu alikuwa akiumba huku akiwa huko huko mbinguni na biblia ikihesabu siku kwa kusema "ikawa jioni, ikawa asubuhi", siku ya pili, ya tatu hadi ya saba? Sasa kudai kwamba miaka elfu moja ya duniani ni sawa na siku moja ya mbinguni si itapelekea madai mengine kwamba uumbaji uliofanyika kwa siku saba za mbinguni zinamaanisha ilitumika miaka 7,000 ya duniani kukamilisha uumbaji? Na hivyo siku ya kupumzika (sabato ya bwana?) inatakiwa iwe kila inapotimia miaka 7,000?
hujaelewa hapo

Iko hv..hebu fikiri
1:mfano mzuri ujenzi wa nyumba hata uwe na matirio yote kwa binadamu huwezi kujenga kwa siku moja nakuhamia siku hiyo hiyo..utatumia muda hata wiki mwezi kama sio miezi.je utatumia miaka mingapi kujenga nyumba za mfano mtaa mmoja tu,àu bara moja tu,au sayari moja tu?

Kisima cha maji pamoja na mitambo yote utachimba wiki au siku kadhaa je.je utatumia muda gani kuchimba,au kutengeneza au kuyafanya maziwa,bahari au mabwawa yaliyopo duniani leo hii.??

Lazima tutatumia miaka na miaka
Lakini kwake hiyo kazi ikikuwa ni simpo tu aliyoifanya kwa kwa siku saba tu. Kama vile wewe unavyoweza kuchakachua kura za jimbo lenu lote na kumtangaza mbunge uliyempanga kuwa ni mshindi ndani ya siku 7 tu.

"Muhudumu naomba Kvant nyingine"
 
View attachment 1125684
Salute..
kuna msemo sijui tulifundishwa au tulisoma wenyewe kwenye vitabu vyetu vya dini (Bibble & Qu'ran) msemo huo unasema kua Miaka elfu moja duniani ni sawa na siku moja mbingu, kiukweli kwa uelewa wangu mdogo wa maswala ya Theologia na Physics nasema huu msemo ni uongo ina wezekana waliotufundisha au tulipousoma kwenye vitabu tuliutafsiri tofauti.
Kwanza kama ulisoma uziwangu wa Time Travel kiasi wadau waliweza kuelezea kadri wajuavyo effect ya Time kwenye Maisha/Uhai wa mwanadamu, nilivutiwa zaidi na mchngowa mkuu BASANORARE kwenye comment hii https://www.jamiiforums.com/threads...-kuwa-suluhisho-la-kifo.1585916/post-31526494 sikutaka nimjibu pale nikaona nianzishie mada hii kitu labda kila mtu atoa mawazo yake juu huu msemo/Andiko.
.......
Ref kutoka Qu'ran: Surat Hajj 47, allah anasema kuwa siku moja ya Allah ni sawa na miaka elfu moja "1,000".
Ref from Bible: Zaburi 90:4 Kwako miaka elfu moja ni kama siku moja tu, ni kama jana ambayo imekwisha kupita, kwako ni kama mkesha mmoja wa usiku
2Petro 3:8 Lakini, wapenzi, msilisahau neno hili, kwamba kwa Bwana siku moja ni kama miaka elfu, na miaka elfu ni kama siku moja
Haya ndio maandiko ambayo yamefanya kuenea kwa msemo ambao mimi kwa muono wangu naona si kweli kwa jinsi watu wanavyo
yatafsiri, mimii naelewa hivi kuhusu haya maandiko and I hope theseare aint Blasphemy kwani the Almighty hapendi wasiotaka kuhoji...Let's go!

Kwanza kabisa Kiasili Mungu ana sifa kuu ambazo ni Omniscience (Ajuaye yote), Omnipotence (Mwenye uweza na nguvu zote) na Omnipresence (aliyoko kila mahalii).
tunaposema kua kwa Mungu/Mbinguni siku moja sawa na miaka 1000 ya duniani msemo huu unauvunja vipande vipande ile sifa ya Mungu ya kua Ana uwezo wa kila kitu na Hana mwanzo wala mwisho.... Kivipi???????????
duniani sababu kuu ambayo inatufanya twafariki ni kwasababu i)Dhambi ya asili (ii)ili kuweza kubalnce nature na kuruhusu existence ya viumbe vingine duniani (iii)time. Yes tunakufa kwakua kuna muda duniani ambao unatuhesabia siku zetu tunazoishi hapa dunia ..Time is the biggest threat to mankind ndio maana nilisema kwenye mada yangu ya time Travelling kua tukiweza kudhibiti muda basi tunaweza kudhibiti KIFO. Kwa mantiki hiyo nachelea kusema kwamba kama kwa Mungu kuna Muda basi Mungu ana mwanzoo, Mbinguni kuna vifo there is no eternal life at all, Yawezekana basi hakuna Mungu mmoja maana watakua wanapita/wanafariki (God Forgive I feel like I'm going too far).
Kwa mujibu Fundamental physical quantity, the SI-Unit of Time is Second and other si-unit are year,day,month,decade,millisecond,century etc...Hivyo basi kama mbinguni Muda basi Mungu atakua ana muda maalumu aliotokea(ana mwanzo) maana ili muda uweze kuhesabiwa lazima kuwe na jua linalo zunguka, haingii akilini kwamba kila ikifika miaka elfu ya duniani basi Mungu hua analala kwakua jua limezama usiku umeingia haiwezekani.

Ninavyofahamu Mimi kwa Mungu hakuna muda (Timeless) hakuna future wala past kila muda kwake ni present, Mungu hawzi eti kesho nitafanya hivi na hivi big Nope ndio maana malaika hawazeeki wala hawafi maana hakuna Muda waliowekewa unaohesabu miaka yaoo labda technically aliyewaumba anajua umri wao. Sie wandamu tumewekewa muda ili tuweze kupanga malengo yetu, ili tuweze kuishi umri fulani tulipangiwa na Muunmba,,ili siku moja tufe that's all..
Kwa hiyo basi kwa kusema hivo yawezekana msemo huu inawezekana kutokna na ambiguity ya kiswahili chetu wakati unatafsriwa kutaka version ya lugha zingine sie tuliuelewa vibaya. au kwa vyovyote vile ulipokelewa kimakosa kama vitabu vinne vya wakorintho ilivyokua..

Mwisho kabisa niseme kua huu ni muono wangu na sio pie kwamba kila mtu alzima aelewe hivyo..Lakini naamini kwa Mungu ni Timeless
Anybody Concur with me......???????????
~Da'Vinci
 
Nikubaliane na mleta post kwa hoja yake ya Mungu kutokuwa na kipindi cha wakati yaani yeye ni wa eternally hana mwanzo wala mwisho. Nino hili la kiswahilili "milele" linapotumika ndani ya maandiko matakatifu limeonyesha kuwa ni kupindi cha wakati maalumu. Kama utaielewa lugha ya biblia mwanzo ambao ni ilipoanzia nyakati ni baada ya anguko la Adamu. Kabla ya hapo kulikua na umilele. Sasa baada ya anguko kukawa na kupungukiwa na utukufu wa Mungu kwa mamkind. Huu upungufu umetuwekea veil . Kiasi kwamba mapana ya ulimwengu wa roho ulio mbali sana na huu wa mwili umepotea kwa mamkind unless otherwise.

Kwa watu waliojaliwa mfano wa manabii wamepewa uwezo wa kuona ambayo watu wengi wa kawaida hawaoni wala kufahamu kwayo.

Ili Mungu kuchukuana na watu wa stara(pazia) imebidi itumike lugha ya mfano. Na hasa akitolea mifano vitu vinavyofahamika katika mazingira yetu wanadamu. Kwa suala la hii miaka imetumiwa lugha ya 'kama' sii halisi. "Mwaka mmoja ni kama miaka elfu".

No wonder Bwana Yesu aliwaambia wanafunzi wake hasa wale tenashara "Kama ikiwa naongea na ninyi yaliyo ya kidunia hamuelewi itakuwa vipi nikiwazungumzia ya mbinguni?"
Hata hivyo sii kwamba mtabaki vipofu kwa ya uhaibuni bali "Yafaa mimi niondoke ili yule msaidizi niliyewaambia habari yake kutoka kwa Baba aje naye ni Roho mtakatifu"
Ndio kusema kuna kuachana mbali kati ya hekima ya kibinadamu na hekima ya Mungu.
 
Ngoja kwanza

Kwa nini sasa sir God anataka tufe

Hafu pia kwani kati yetu sisi na malaika nani ni bora kwake ?

Kwa nn na sisi asingetufanya kama malaika ?!
 
Ngoja kwanza

Kwa nini sasa sir God anataka tufe

Hafu pia kwani kati yetu sisi na malaika nani ni bora kwake ?

Kwa nn na sisi asingetufanya kama malaika ?!
Mkuu umeuliza kwa nini sir god anataka tufe...

Sijajua umeuliza kwa mujibu wa kitabu gani mkuu bibilia ama Qurani..mana naweza kukujibu kwa mujibu wa Quran hilo swali kumbe wewe umeuliza kwa mujibu wa bibilia..



Mimi naomba nikujibu kwa mujibu wa Qurani vipi mkuu uko tayari ?
 
Nilichoelewa mimi na akili yangu ya KVANT KUBWA ni


Wanaposema miaka 1000 kwake ni sawa na siku 1.anatumbusha viumbe wake kuwa yeye hapotezi KUMBUKUMBU.

Kwa binadamu ni rahisi na kawaida kukumbuka ratiba na mizunguko yake yote aliyoifanya jana (tarehe na mwezi wa jana mwaka huu) lakini asikumbuke route au mizunguko,ratiba yake aliyoifanya tarehe na mwezi wa jana ya (mwaka uliopita)..

Mfano wakati una miaka mitatu uliwahi kuiba andazi sokoni(hiyo ni dhambi ulifanya). Lakini leo hii hukumbuki chochote na unaweza ukajiona huna dhambi duniani..kisa ni muda mrefu umepita...lakini kwa Mungu hatasahau atalikumbuka tukio lako lote kama vile limefanyika muda mfupi uliopita(saa au siku moja iliyopita)
Hivo utakumbushwa na kuhukumiwa vile vile...asante ngoja niendele kunywa KVANT yangu
Dah hii KVANT yako ya Leo Si mchezo, Post moja inarudiwa mara 4, Hongera kwa kupata KVant
 
Back
Top Bottom