Nadharia ya miaka 1,000 duniani ni sawa na siku moja mbinguni si sahihi kabisa

View attachment 1125684
Salute..
kuna msemo sijui tulifundishwa au tulisoma wenyewe kwenye vitabu vyetu vya dini (Bibble & Qu'ran) msemo huo unasema kua Miaka elfu moja duniani ni sawa na siku moja mbingu, kiukweli kwa uelewa wangu mdogo wa maswala ya Theologia na Physics nasema huu msemo ni uongo ina wezekana waliotufundisha au tulipousoma kwenye vitabu tuliutafsiri tofauti.
Kwanza kama ulisoma uziwangu wa Time Travel kiasi wadau waliweza kuelezea kadri wajuavyo effect ya Time kwenye Maisha/Uhai wa mwanadamu, nilivutiwa zaidi na mchngowa mkuu BASANORARE kwenye comment hii Time Travel: Je, linaweza kuwa suluhisho la kifo? sikutaka nimjibu pale nikaona nianzishie mada hii kitu labda kila mtu atoa mawazo yake juu huu msemo/Andiko.
.......
Ref kutoka Qu'ran: Surat Hajj 47, allah anasema kuwa siku moja ya Allah ni sawa na miaka elfu moja "1,000".
Ref from Bible: Zaburi 90:4 Kwako miaka elfu moja ni kama siku moja tu, ni kama jana ambayo imekwisha kupita, kwako ni kama mkesha mmoja wa usiku
2Petro 3:8 Lakini, wapenzi, msilisahau neno hili, kwamba kwa Bwana siku moja ni kama miaka elfu, na miaka elfu ni kama siku moja
Haya ndio maandiko ambayo yamefanya kuenea kwa msemo ambao mimi kwa muono wangu naona si kweli kwa jinsi watu wanavyo
yatafsiri, mimii naelewa hivi kuhusu haya maandiko and I hope theseare aint Blasphemy kwani the Almighty hapendi wasiotaka kuhoji...Let's go!

Kwanza kabisa Kiasili Mungu ana sifa kuu ambazo ni Omniscience (Ajuaye yote), Omnipotence (Mwenye uweza na nguvu zote) na Omnipresence (aliyoko kila mahalii).
tunaposema kua kwa Mungu/Mbinguni siku moja sawa na miaka 1000 ya duniani msemo huu unauvunja vipande vipande ile sifa ya Mungu ya kua Ana uwezo wa kila kitu na Hana mwanzo wala mwisho.... Kivipi???????????
duniani sababu kuu ambayo inatufanya twafariki ni kwasababu i)Dhambi ya asili (ii)ili kuweza kubalnce nature na kuruhusu existence ya viumbe vingine duniani (iii)time. Yes tunakufa kwakua kuna muda duniani ambao unatuhesabia siku zetu tunazoishi hapa dunia ..Time is the biggest threat to mankind ndio maana nilisema kwenye mada yangu ya time Travelling kua tukiweza kudhibiti muda basi tunaweza kudhibiti KIFO. Kwa mantiki hiyo nachelea kusema kwamba kama kwa Mungu kuna Muda basi Mungu ana mwanzoo, Mbinguni kuna vifo there is no eternal life at all, Yawezekana basi hakuna Mungu mmoja maana watakua wanapita/wanafariki (God Forgive I feel like I'm going too far).
Kwa mujibu Fundamental physical quantity, the SI-Unit of Time is Second and other si-unit are year,day,month,decade,millisecond,century etc...Hivyo basi kama mbinguni Muda basi Mungu atakua ana muda maalumu aliotokea(ana mwanzo) maana ili muda uweze kuhesabiwa lazima kuwe na jua linalo zunguka, haingii akilini kwamba kila ikifika miaka elfu ya duniani basi Mungu hua analala kwakua jua limezama usiku umeingia haiwezekani.

Ninavyofahamu Mimi kwa Mungu hakuna muda (Timeless) hakuna future wala past kila muda kwake ni present, Mungu hawzi eti kesho nitafanya hivi na hivi big Nope ndio maana malaika hawazeeki wala hawafi maana hakuna Muda waliowekewa unaohesabu miaka yaoo labda technically aliyewaumba anajua umri wao. Sie wandamu tumewekewa muda ili tuweze kupanga malengo yetu, ili tuweze kuishi umri fulani tulipangiwa na Muunmba,,ili siku moja tufe that's all..
Kwa hiyo basi kwa kusema hivo yawezekana msemo huu inawezekana kutokna na ambiguity ya kiswahili chetu wakati unatafsriwa kutaka version ya lugha zingine sie tuliuelewa vibaya. au kwa vyovyote vile ulipokelewa kimakosa kama vitabu vinne vya wakorintho ilivyokua..

Mwisho kabisa niseme kua huu ni muono wangu na sio pie kwamba kila mtu alzima aelewe hivyo..Lakini naamini kwa Mungu ni Timeless
Anybody Concur with me......???????????
~Da'Vinci
Da'Vinci naendelea kukusoma.Unaelekea kumpinga Mungu(sio Shetani,maana kwa wengine hata Shetani ni mungu) in everything.Je wewe ni wa sinagogi la Shetani?I am just thinking loudly.
 
Da'Vinci naendelea kukusoma.Unaelekea kumpinga Mungu(sio Shetani,maana kwa wengine hata Shetani ni mungu) in everything.Je wewe ni wa sinagogi la Shetani?I am just thinking loudly.
Mimi nampinga Mungu kivipi?? Sidhani kuhoji vitu vinavyohusu Mungu ni kupinga uweza wake.

Je wewe unakubaliana kwamba Mbinguni kuna muda?? Au muda upo tu huku kwenye sayari zetu
 
Kama tu kwenye sayari zinatofautiana

Mwaka mmoja wa hapa hauwezi kuwa sawa na kwenye sayari ya jupiter au pluto sikwambii huko mbinguni!

Inawezekana bwna
Naomba msaada mtaalam kwa maswali haya madogo, kutokana na hoja zako za hapo juu:

1. Kwani mbinguni ni wapi?
2. Mungu anapatikana wapi?
3. Je yupo katika miongoni mwa Sayari hizi tunazozijua
4. Ili tupate siku, dunia hulizunguka Jua/Sun (nyota iliyo karibu zaidi na dunia). Mzunguko unapokamilika in 24hrs ndipo hufanya siku 1. Je huko aliko Mungu (kama hapa duniani hatunaye) kifaa alichopo pia hulizunguka hili jua letu?
5. Je si sahihi kusema kuwa Mungu yupo hapa duniani na kila mahali katika Ulimwengu/Universe?
 
Kwani wakati wa uumbaji si Mungu alikuwa akiumba huku akiwa huko huko mbinguni na biblia ikihesabu siku kwa kusema "ikawa jioni, ikawa asubuhi", siku ya pili, ya tatu hadi ya saba? Sasa kudai kwamba miaka elfu moja ya duniani ni sawa na siku moja ya mbinguni si itapelekea madai mengine kwamba uumbaji uliofanyika kwa siku saba za mbinguni zinamaanisha ilitumika miaka 7,000 ya duniani kukamilisha uumbaji? Na hivyo siku ya kupumzika (sabato ya bwana?) inatakiwa iwe kila inapotimia miaka 7,000?
Hii comment inafikirisha sana. Nimeipenda.

1. Yaani je zile siku zilizokuwa zinahesabiwa 1, 2 hadi 7 zilikuwa ni siku zipi hizi za dunia yetu au siku za kule kwake alipo wakati akiumbwa?

2. Je pale panaposema 'Ikawa usiku, ikawa mchana..siku 2 nk., je ilipoingia ule usiku naye akawa gizani hadi kulipopambazuka na kuwa siku mpya?

Kama aliviumbia hivi vitu akiwa huko aliko na hizo siku ni za kwake, basi naona hoja yako ya kuwa dunia na vitu vyote viliumbwa kwa muda sawa na miaka 7, 000 ya duniani na kwamba alipumzika baada ya siku hizo. Ingawa hapa pia kwenye kupumzika kama kulivyotajwa kwenye biblia kuna leta swali Jipya kuwa Je Mungu naye anachoka? Maana kuchoka ni dalili ya kuishiwa nguvu na udhaifu (binafsi naamini Mungu ni muweza wa kila kitu na hajawahi kuchoka wala kulala).

Nyaka-One
Davinci
 
hujaelewa hapo

Iko hv..hebu fikiri
1:mfano mzuri ujenzi wa nyumba hata uwe na matirio yote kwa binadamu huwezi kujenga kwa siku moja nakuhamia siku hiyo hiyo..utatumia muda hata wiki mwezi kama sio miezi.je utatumia miaka mingapi kujenga nyumba za mfano mtaa mmoja tu,àu bara moja tu,au sayari moja tu?

Kisima cha maji pamoja na mitambo yote utachimba wiki au siku kadhaa je.je utatumia muda gani kuchimba,au kutengeneza au kuyafanya maziwa,bahari au mabwawa yaliyopo duniani leo hii.??

Lazima tutatumia miaka na miaka
Lakini kwake hiyo kazi ikikuwa ni simpo tu aliyoifanya kwa kwa siku saba tu. Kama vile wewe unavyoweza kuchakachua kura za jimbo lenu lote na kumtangaza mbunge uliyempanga kuwa ni mshindi ndani ya siku 7 tu.

"Muhudumu naomba Kvant nyingine"
Siku 7 zipi? Maana amesema siku 1 kwake ni sawa na za kwetu 1000. Sasa amehesabu siku 7, huoni hapo ni sawa na miaka 7, 000 ya huku kwetu? Maana hivyo vitu na hizo sayari alitengeneza akiwa huko (kumbuka hivi vitu huku duniani na kwengineko havikuwepo kabla ya hizo siku). Fikilia vizuri hapo.
 
Mambo Ya Rohoni Kuyafasiri Kwa Jinsi Ya Mwilini Ni Ukengeufu Na Uposhaji Wa Maandiko. Mambo Ya Rohoni Yanajulikana Kwa Jinsi Ya Rohoni Tu. Biblia Haisomwi Kama Gazeti Au Kitabu Cha Historia.
Umeamua kujiwekea ukomo wa kufikili. Sasa kama wanaoeleza kwa jinsi ya mwili wamekengeuka, Waeleze wewe basi vizuri maana wewe ni wa rohoni.
 
Yaani kwa maana ya kwamba.

Dunia inatumia mda mwingi kulizunguka jua hivyo kufanya mzunguko uchelewe.

Wakati huo jupita inatumia mda mchache kulizunguka jua hivyo kufanya mzunguko uwahi kukamilika.

Mfano..

Juma anatumia dakika 5 kuzunguka uwanja mita 300.

Wakati huo omari anatumia sekunde 5 kuzunguka uwanja wa mita 300.

Kwa hiyo tunaweza kusema kwamba juma anazunguka uwanja muda mrefu (5dkk) wakati huo omari anazunguka uwanja muda mfupi (secs)

Hivyo ni kwamba

Dakika 5 za juma kuzunguka uwanja wa 300m ni sawa na sekunde 5 za juma kuzunguka uwanja wa 300m.

Kama nimeelewa ndo dunia na jupiter viko hivyo mkuu?

Naomba niendelee kuuliza tena..

Ili kupata siku moja hapa duniani ni kipi kinatokea yaani jua anazunguka dunia ama dunia ndo anamzunguka juaa...?
mzee jupiter inazunguka umbali mrefu zaidi kuliko dunia kwa orbit zao ni tofauti.
 
Kingine kincho sound tofauti masikioni mwangu ni huu msemo kua ili uelewe maandiko ya biblia inabidi roho mtakatifu akushukie kwanza kwakweli mm sidhani kama ni kweli kwamba inambidi ashuke kwanza kisha ndio akufunulie ...noo asee hapana. Kwanini?

Kwa mujibu wa katekismu au mafundisho yoyote yale ya kikristo inafundisha kua Roho mtakatifu hutupatia mapaji yake saba ambapo kati ya hayo mapaji ni Hekima na Elimu. indi tu binaadamu anapozaliwa Mungu humbarikia kila kitu baadhi ya mapaji tunazaliwa nayo japo sio wote, moja ya paji tunalozaliwa nayo ni paji la Hekima, japo kutokana na malezi au mazingira anayokulia mtoto paji hilo laweza kufifia. Hivyo basi katika kutafsiri maandiko ya bible kinachotumika ni Hekima, paji la hekima ndio linalowezesha kuitafakari andiko la biblia, na ukumbuke anayetoa uwezo huo wa kua na hekima Ni Roho mtakatifu.. Hekima hiyo inakuwezesha pindi unaposoma andiko tu kwa mara ya kwanza mojakwamoja unafahamu kua hili andiko lina ujumbe fulani ndani yake, kama vile darasani kuna mtu akiona swali kwa mara ya kwanza tu bila kucherewa haraka anafahamu hili swali lahitaji nini. Hivyo basi kuna watu wanayo hekima hiyo wengine hawana..katika kutafsiri maandiko pia kuna makundi mawili ya watu ambayo ni (i)Watu ambao wakiona andiko wanalielewa na wanaweza kilielezea mbele ya wengine (ii)kuna wengine wakielewa andiko hawawezi kulielezea kwa wengine kutoka na uwezo mdogo wa kuwasilisha hoja mbele za watu {nipo kundi namba mbili}

kwa mantiki hiyo Roho mtakatifu hakushukii ili uweze fafanua andiko ila anakua ashakujalia kipawa chake toka siku wazaliwa...

pia haya ni mawazo yangu

Sitaki kuongelea biblia kwa mifano yako hiyo kwa kuwa biblia ni kitabu kilichojaa mafundisho na maneno ya binadam na hata lugha yake ya asili haipo.

Kuhusu miaka uisemayo kwenye Qur'an imeongelewa ki aina nyingi na kipekee. Sina haja ya kuzirudia ispokuwa fahamu kuwa:

1) Qur'an ipo katika lugha yake ya asili iliyokuja nayo miaka zaidi ya 1,400 nyuma, haijabadilika na wala haitobadilika.

2) Muujiza mmoja wapo wa Qur'an ni kila inapoongelea kitu huongelea kitu hicho kilipotokea au kiongelewacho kwa misamiati (lexicons) ya sehemu na wakati husika (locution).

Kwa maana hizo, ili kuielewa aya au nukuu ya Qur'an ni lazima uielewe misamiati iliyomaanishwa kwa kila lilipoongelewa. Huwezi kuitafsiri 1ur'an neno kwa neno ikaleta maana halisi hata uitafsiri kwa Kiarabu.

Kwa hiyo miaka 1,000 au 50,000 au yoyote itajwapo kwenye Qur'an, kwanza uelewe imeongelea nini hapo Qur'an, ilikuwa inanukuu watu au mtu au onyo au amri au kisa? Na mengineyo mengi. Kama huyajuwi yote hayo hutoweza kuelewa kimekusudiwa nini ilipotajwa hiyo miaka.

Ukitaka kuelewa, weka nukuu ya aya uliyo ikusudia ili kama tunaelewa kimekusidiwa nini, tukupe darsa. Nje ya hapo tutabishana na kunukuu kijinga tu.
 
Kingine kincho sound tofauti masikioni mwangu ni huu msemo kua ili uelewe maandiko ya biblia inabidi roho mtakatifu akushukie kwanza kwakweli mm sidhani kama ni kweli kwamba inambidi ashuke kwanza kisha ndio akufunulie ...noo asee hapana. Kwanini?

Kwa mujibu wa katekismu au mafundisho yoyote yale ya kikristo inafundisha kua Roho mtakatifu hutupatia mapaji yake saba ambapo kati ya hayo mapaji ni Hekima na Elimu. indi tu binaadamu anapozaliwa Mungu humbarikia kila kitu baadhi ya mapaji tunazaliwa nayo japo sio wote, moja ya paji tunalozaliwa nayo ni paji la Hekima, japo kutokana na malezi au mazingira anayokulia mtoto paji hilo laweza kufifia. Hivyo basi katika kutafsiri maandiko ya bible kinachotumika ni Hekima, paji la hekima ndio linalowezesha kuitafakari andiko la biblia, na ukumbuke anayetoa uwezo huo wa kua na hekima Ni Roho mtakatifu.. Hekima hiyo inakuwezesha pindi unaposoma andiko tu kwa mara ya kwanza mojakwamoja unafahamu kua hili andiko lina ujumbe fulani ndani yake, kama vile darasani kuna mtu akiona swali kwa mara ya kwanza tu bila kucherewa haraka anafahamu hili swali lahitaji nini. Hivyo basi kuna watu wanayo hekima hiyo wengine hawana..katika kutafsiri maandiko pia kuna makundi mawili ya watu ambayo ni (i)Watu ambao wakiona andiko wanalielewa na wanaweza kilielezea mbele ya wengine (ii)kuna wengine wakielewa andiko hawawezi kulielezea kwa wengine kutoka na uwezo mdogo wa kuwasilisha hoja mbele za watu {nipo kundi namba mbili}

kwa mantiki hiyo Roho mtakatifu hakushukii ili uweze fafanua andiko ila anakua ashakujalia kipawa chake toka siku wazaliwa...

pia haya ni mawazo yangu
Mwenye hekima na elimu yeyote anaachana na maandiko ya kibinadam kitaka kuujua ujumbe wa Mwenye Mungu.
 
View attachment 1125684
Salute..
kuna msemo sijui tulifundishwa au tulisoma wenyewe kwenye vitabu vyetu vya dini (Bibble & Qu'ran) msemo huo unasema kua Miaka elfu moja duniani ni sawa na siku moja mbingu, kiukweli kwa uelewa wangu mdogo wa maswala ya Theologia na Physics nasema huu msemo ni uongo ina wezekana waliotufundisha au tulipousoma kwenye vitabu tuliutafsiri tofauti.

Kwanza kama ulisoma uziwangu wa Time Travel kiasi wadau waliweza kuelezea kadri wajuavyo effect ya Time kwenye Maisha/Uhai wa mwanadamu, nilivutiwa zaidi na mchngowa mkuu BASANORARE kwenye comment hii Time Travel: Je, linaweza kuwa suluhisho la kifo? sikutaka nimjibu pale nikaona nianzishie mada hii kitu labda kila mtu atoa mawazo yake juu huu msemo/Andiko.

.......
Ref kutoka Qu'ran: Surat Hajj 47, allah anasema kuwa siku moja ya Allah ni sawa na miaka elfu moja "1,000".
Ref from Bible: Zaburi 90:4 Kwako miaka elfu moja ni kama siku moja tu, ni kama jana ambayo imekwisha kupita, kwako ni kama mkesha mmoja wa usiku
2Petro 3:8 Lakini, wapenzi, msilisahau neno hili, kwamba kwa Bwana siku moja ni kama miaka elfu, na miaka elfu ni kama siku moja
Haya ndio maandiko ambayo yamefanya kuenea kwa msemo ambao mimi kwa muono wangu naona si kweli kwa jinsi watu wanavyo
yatafsiri, mimii naelewa hivi kuhusu haya maandiko and I hope theseare aint Blasphemy kwani the Almighty hapendi wasiotaka kuhoji...Let's go!


Kwanza kabisa Kiasili Mungu ana sifa kuu ambazo ni Omniscience (Ajuaye yote), Omnipotence (Mwenye uweza na nguvu zote) na Omnipresence (aliyoko kila mahalii).
tunaposema kua kwa Mungu/Mbinguni siku moja sawa na miaka 1000 ya duniani msemo huu unauvunja vipande vipande ile sifa ya Mungu ya kua Ana uwezo wa kila kitu na Hana mwanzo wala mwisho.... Kivipi???????????
duniani sababu kuu ambayo inatufanya twafariki ni kwasababu i)Dhambi ya asili (ii)ili kuweza kubalnce nature na kuruhusu existence ya viumbe vingine duniani (iii)time. Yes tunakufa kwakua kuna muda duniani ambao unatuhesabia siku zetu tunazoishi hapa dunia ..Time is the biggest threat to mankind ndio maana nilisema kwenye mada yangu ya time Travelling kua tukiweza kudhibiti muda basi tunaweza kudhibiti KIFO. Kwa mantiki hiyo nachelea kusema kwamba kama kwa Mungu kuna Muda basi Mungu ana mwanzoo, Mbinguni kuna vifo there is no eternal life at all, Yawezekana basi hakuna Mungu mmoja maana watakua wanapita/wanafariki (God Forgive I feel like I'm going too far).

Kwa mujibu Fundamental physical quantity, the SI-Unit of Time is Second and other si-unit are year,day,month,decade,millisecond,century etc...Hivyo basi kama mbinguni Muda basi Mungu atakua ana muda maalumu aliotokea(ana mwanzo) maana ili muda uweze kuhesabiwa lazima kuwe na jua linalo zunguka, haingii akilini kwamba kila ikifika miaka elfu ya duniani basi Mungu hua analala kwakua jua limezama usiku umeingia haiwezekani.

Ninavyofahamu Mimi kwa Mungu hakuna muda (Timeless) hakuna future wala past kila muda kwake ni present, Mungu hawzi eti kesho nitafanya hivi na hivi big Nope ndio maana malaika hawazeeki wala hawafi maana hakuna Muda waliowekewa unaohesabu miaka yaoo labda technically aliyewaumba anajua umri wao. Sie wandamu tumewekewa muda ili tuweze kupanga malengo yetu, ili tuweze kuishi umri fulani tulipangiwa na Muunmba,,ili siku moja tufe that's all..

Kwa hiyo basi kwa kusema hivo yawezekana msemo huu inawezekana kutokna na ambiguity ya kiswahili chetu wakati unatafsriwa kutaka version ya lugha zingine sie tuliuelewa vibaya. au kwa vyovyote vile ulipokelewa kimakosa kama vitabu vinne vya wakorintho ilivyokua..

Mwisho kabisa niseme kua huu ni muono wangu na sio pie kwamba kila mtu alzima aelewe hivyo..Lakini naamini kwa Mungu ni Timeless
Anybody Concur with me......???????????
~Da'Vinci
"mbinguni" ndiyo wapi mleta mada?

Maneno yako unayafanya kuwa ya Allah?

Hizo aya ulizoweka sijaona neno "mbingu" wala "mbinguni".

Naona lugha imekupiga chenga ndiyo maana umeshindwa kuelewa.
 
"mbinguni" ndiyo wapi mleta mada?

Maneno yako unayafanya kuwa ya Allah?

Hizo aya ulizoweka sijaona neno "mbingu" wala "mbinguni".

Naona lugha imekupiga chenga ndiyo maana umeshindwa kuelewa.
Kwa hiyo dada utapewa midume rijali mingap manululain
 
Back
Top Bottom