Hivi ni kweli wateule wa Kristo watakaa mbinguni na kujifunza hukumu ya wenye dhambi kwa miaka elfu moja (1,000) pekee yake?

Nyaka-One

JF-Expert Member
Oct 27, 2013
4,318
5,990
Leo nimekaa na kujiuliza. Kwa wakristo tunaambiwa baada ya Yesu kurudi na kuwachukua wateule wake hao wateule watakaa mbinguni kwa miaka 1,000 wakijifunza hukumu ya wenye dhambi. Hiyo miaka 1,000 ni sawa na masaa 8,760,000. Na katika kujifunza hiyo hukumu hao wateule watakuwa wanaangalia "video" ya matendo ya kidhambi kwa kila mwanadamu ikiwa ni moja ya kazi kubwa watakazofanya wakiwa huko mbinguni. Hoja yangu ipo kwenye kuangalia hizo "video" za dhambi walizotenda watu.

Kwa sasa watu tulio hai duniani ni wastani wa watu 8,000,000,000. Hiyo idadi ni bila kuhesabu waliokwisha kufa miaka yote nenda rudi huko nyuma. Tukikadiria walio hai na waliokwisha kufa jumla wawe mara mbili ya tuliopo leo hii jumla tunakuwa 16,000,000,000 (bilioni 16). Ukisema dhambi za kila mmoja zionyeshwe japo kwa saa moja tu itahitaji masaa bilioni 16 ambazo ni sawa na miaka 1,826,484! Ukisema hizo dhambi za kila mmoja zionyeshe japo ndani ya dakika moja tu bado itachukua miaka 30,441 kuangalia video za hao watu wote.

Kumbuka hiyo hesabu niliyoandika hapo juu ni kwamba muda wote, kila siku kwa miaka yote hiyo ni watu kukaa macho na kuangalia video tu bila kazi nyingine kama kuimba/kumsifu Mungu, watu kuuliza maswali kwa yale mapya na ya kustaajabisha watakayokutana nayo huko mbinguni, kuongea na wapendwa wao ambao walikufa duniani na kuagana kwa maneno kama "R.I.P.", "tutaonana baadae", n.k. ambayo kwa pamoja ukiyajumlisha ni wazi itachukua miaka mingi zaidi ya ile niliyotaja awali ambayo ni zaidi ya miaka 1,000 iliyotajwa kwenye biblia.

Kwa mwenye uelewa zaidi naomba ufafanuzi wake.
 
Aisee!

Huu uongo...

Mi najua wateule tutapumnzika baada ya taabu zetu zote...
 
Miaka 1000 duniani wanasema sawa na siku moja mbinguni ..so piga hesabu zako hapo uone na mwaka moja Dunia ni sawa na millisecond mbinguni
 
kama ni ivo kweli kitakachofanyika hapo hao wateule watarishwa data kwenye bongo zao kama ilivyo robot alie tengenezwa leo anadata za miaka ya nyuma BC uko kwaio watakuwa na uelewa mkubwa ambao wao wenyewe hawajui wameutoa wap
 
Leo nimekaa na kujiuliza. Kwa wakristo tunaambiwa baada ya Yesu kurudi na kuwachukua wateule wake hao wateule watakaa mbinguni kwa miaka 1,000 wakijifunza hukumu ya wenye dhambi...

Mkuu naona leo nitetee hapo maana nimekuwa nikipinga baadhi ya vitu lakini leo naomba kutetea..

Japo idadi ya watakaofanya hivyo sio wote..

Hili swala linawezekana nitakutolea mfano mdogo tu.

Nitaanza na mfano Halisi baadae nitaamia kwenye biblia.

Kwenye dunia Ya kiroho hakuna Muda wala saa wala nyakati.

Imagine unaweza kulala ndani ya Nusu saa ukaota story ambayo unaweza kuisimulia kila angale kwa muda wa Masaa zaidi ya Matatu na ukiweka ndoto hiyo kwenye muvi inawwza kuchukua Masaa zaidi ya manne..
Lakini kiufupu ndoto hiyo umeiota kwa nusu saa au dakika 15 tu uliyoota.


Sasa narudi kwenye Biblia Unakumbuka kuwa story ya kuumbwa kwa ulimwengu mpaka Story za Yakobo na story ya watu wote wa mwanzo including torati nzima na hadithi zote na watu wote alipewa Musa Kwa siku moja lakini unaweza ukahadithia story moja tu ya Ibrahimu ukatumia sku zaidi ya tatu...

Unafahamu kuwa Ufunuo wa Yohana alifunuliwa yohana kwa siku moja akiwa patmo...
Sasa niambie unaweza kuyaangalia matukio hayo na kuyachambua kwa muda gani?
 
Weka kifungu cha Biblia sio porojo
Mama mchungaji na wewe umekuwa Thomaso?
Umesahau kuna mauti mbili, na ufufuo mbili..

Ufufuo wa kwanza kwa ajili ya wema na ufufuo wa pili kwa waovu...

Screenshot_20231107-192355.png
 
Mkuu, sijasahau, ila hilo la kujifunza hukumu kwa miaka 1000...

Sijaliona kwa neno
Kujifunza hukumu Hiyo sio fungu l biblia ila ni Kitabu cha Ellen G Whites..Mafunzo ya wasabato hayo...,😅😅
Nahisi itakuwa kwenye Tumaini la Vizazi vyote
 
Back
Top Bottom