Ahmet
JF-Expert Member
- Oct 15, 2019
- 1,537
- 3,404
Habari wapendwa,
Kuna hizi theories zinazoelezea chanzo cha Ulimwengu, kwa uelewa wangu hakuna hata moja inayoelezea kikamilifu chanzo cha huu Ulimwengu, bali nyingi zinaelezea modifications na evolution tu ya Ulimwengu ambapo katika kuelezea huko zinaweza zisiwe sahihi pia.
Tuziangalie kwanza nadharia zenyewe na kivipi zimeshindwa kuelezea chanzo Cha Ulimwengu.
1. Big Bang Theory
Hii ni nadharia maarufu miongoni mwetu, lakini si nadharia pekee inayoelezea chanzo cha Ulimwengu. Kwa mujibu wa big bang, Ulimwengu wote ulianza kama punje ndogo (atom), yenye joto sana, ambayo ilikuwa katika mgandamizo mkubwa usiomithirika (infinitely dense). Kisha punje hii akaanza kutanuka na kutengeneza sehemu na wakati (space and time). Kadri Ulimwengu ulivyotanuka basi ukapoa na kufanya baadhi ya sehemu kuwa ni zenye kukalika na viumbe hai kama ilivyo katika Dunia yetu. Wanasayansi wanadai tulio hili la big bang lilotokea takribani miaka bilioni 13.7 iliyopita.
Wanasayansi wanatumia gunduzi mbili za kisayansi kuthibitisha madai haya.
Kwanza, ugunduzi wa Edwin Hubble miaka ya 1920, ambapo Bw. Hubble kwa kutumia telescope, aligundua kuwa bado Ulimwengu unaendelea kutanuka, ambapo alisema kadri galaxies zipokuwa mbalimbali basi ndio zinazidi kukimbiana (Hubble's law).
Pili, ugunduzi wa Cosmic Microwave Background (CMB). Mnamo miaka ya 1960, wanasayansi waligundua mwanga (radiation) ambao ni wa kale na huo mwanga umetawanyika katika sehemu zote za Ulimwengu. Wanasayansi wanaamini kuwa mwanga huu ulitokana na mlipuko wa big bang na umeendelea kuwepo kwa miaka yote hiyo hadi leo. Inaaminika mwanga huu ni kama mwangi au wimbi la mstuko wa big bang ambalo limeendelea kupoa na hatimae kuonekana katika Microwave domain of electromagnetic spectrum.
Udhaifu wa Nadharia Hii
i. Nadharia hii haielezi chanzo cha hiyo punje ndogo. Yaani hii punje ndogo ilitokea wapi, nini kilipelekea kuundwa kwa hii punje ndogo? Hapa pana maswali mengi ambayo sayansi haiwezi kujibu na itaendelea kusemwa tu kuwa "Ulimwengu ulianza kama punje ndogo". Na kama watasema ulitokana na vitu fulani basi watatakiwa kuonyesha pia hivyo vitu vimetokana na nini.
ii. Nadharia hii haielezi nini kilisababisha mlipuko ambao umeunda Ulimwengu huu.
iii. Je hii punje ndogo ilikuwa katika nini? Je Nadharia inasema nini juu ya uwepo wa mazingira fulani ambayo huweza kubeba kitu? Je hiyo punje ilikuwa ipo yenyewe tu? Je inawezekana kitu fulani kisiwepo juu ya kitu chochote? Nadharia bado haijaeleza.
iv. Hivi karibuni Kuna baadhi ya nyota zimegunduliwa kuwa na umri mkubwa kuliko big bang yenyewe. Mfano, Methuselah ni nyota ambayo inakadiriwa kuwa na miaka bilioni 14.45, yaani hii nyota ilikuwepo kabla ya tukio la big bang.
Kutokana na kutokuwa na majibu juu ya maswali haya, Kuna nadharia nyengine zilitungwa, ambazo zilizidi kuzua maswali mengine.
2. Steady-State Theory
Nadharia inasema kuwa Ulimwengu siku zote unatanuka lakini density (tungamo) ikindelea kubaki vilevile ambapo nyota na galaxies mpya huendelea kutengenezwa kwa kiwango sawa na hupoteaji wa nyota na galaxies za zamani ambazo hupotelea kwenda katika Ulimwengu usioonekana. Watafiti wa nadharia hii wanasema kuwa Ulimwengu hauna mwanzo wala mwisho katika muda, na density na mpangilio wa galaxies ni sawa kwa muda wote.
Katika nadharia hii, tunaona moja kwa moja wameshindwa kuonyesha chanzo cha Ulimwengu.
3. The Plasma Cosmology
Nadharia hii inaamini kuwa evolution ya Ulimwengu kwa wakati uliopita inabidi ielezewe kwa kuangalia matukio yanayotokea katika Ulimwengu kwa sasa. Yaani inasema, matukio yanayotokea katika Ulimwengu sasa ndio hayohayo yalitokea katika Ulimwengu wakati uliopita. Nadharia hii pia inakataa kuwa Ulimwengu haujatokana na chochote kama inavyoaminika na watafiti wa big bang. Watafiti wa Plasma Cosmology wanaamini kwamba kwasababu tunaona Ulimwengu unaobadilika, basi huu Ulimwengu ulikuwepo siku zote and utaendelea kuwepo and kubadilika milele. Kama ilivyo Kwa steady state theory, Nadharia hii pia inakataa Ulimwengu kuwa na chanzo.
4. Big Bounce Theory
Big Bounce inasema kuwa Ulimwengu umekuwa ukitanuka na kuanguka mara kadhaa. Yaani Ulimwengu umetanuka mara kadhaa na ku-collapse mara kadhaa. Huu Ulimwengu tulionao ni zao la Ulimwengu ambao uli-collapse na kutanuka tena na wanatabiri kuwa huu Ulimwengu uta-collapse tena na pengine kutanuka tena. Kwahiyo Kuna series ya 'crunches and bangs' ambapo Ulimwengu unatanuka na kuanguka. Bado nadharia hii haionyeshi chanzo cha Ulimwengu bali huonyesha mabadiliko tu. Chanzo cha huo Ulimwengu ambao unacollapse na kutanuka ni kipi? Nini ilikuwa sababu ya kutanuka na ku-collapse? Bado hatupati majibu.
5. The Ekpyrotic Model
Nadharia hii inaamini kuwa big bang ilitokea kwa sababu ya mgongano wa branes mbili ambazo zilikuwa sambamba. Sina tafsiri sahihi ya neno branes, lakini branes inaweza kuelezewa kama any of the spatially extended mathematical objects of zero or more dimensions used in string theory. Watu wa Quantum mechanics na General relativity wanaweza wakanielewa. Katika mazungumzo haya, tuzichukulie hizo branes kwa mfano wa kamba, hivyo basi hizo kamba mbili sambamba zilisuguana na kupelekea moto ambao ndio ukazaa big bang na hatimae kuunda Ulimwengu. Hapa tunapata swali jengine, je hizi branes zilitoka wapi? Nini kilifanya zisuguane? Hapa pia Kuna maswali mengi.
Hitimisho: tumeona kuwa nadharia nyingi hazijaelezea hasa chanzo cha Ulimwengu, baadhi zinasema kabisa Ulimwengu hauna chanza na hautakuwa na mwisho na nyengine zinasema Ulimwengu ulianzia na kitu fulani, lakini haziwezi kuelezea chanzo cha hicho kitu. Yaani nini kilikuwa chanzo cha hicho ambacho wewe unakiona kuwa ndio kimeleta Ulimwengu?
Je, Kuna nadharia nyengine ambazo zina majibu mazuri zaidi?
Je, wale wanaopinga uwepo Mwenyezi Mungu wanategemea nadharia hizi katika kuelezea chanzo cha Ulimwengu?
Kuna hizi theories zinazoelezea chanzo cha Ulimwengu, kwa uelewa wangu hakuna hata moja inayoelezea kikamilifu chanzo cha huu Ulimwengu, bali nyingi zinaelezea modifications na evolution tu ya Ulimwengu ambapo katika kuelezea huko zinaweza zisiwe sahihi pia.
Tuziangalie kwanza nadharia zenyewe na kivipi zimeshindwa kuelezea chanzo Cha Ulimwengu.
1. Big Bang Theory
Hii ni nadharia maarufu miongoni mwetu, lakini si nadharia pekee inayoelezea chanzo cha Ulimwengu. Kwa mujibu wa big bang, Ulimwengu wote ulianza kama punje ndogo (atom), yenye joto sana, ambayo ilikuwa katika mgandamizo mkubwa usiomithirika (infinitely dense). Kisha punje hii akaanza kutanuka na kutengeneza sehemu na wakati (space and time). Kadri Ulimwengu ulivyotanuka basi ukapoa na kufanya baadhi ya sehemu kuwa ni zenye kukalika na viumbe hai kama ilivyo katika Dunia yetu. Wanasayansi wanadai tulio hili la big bang lilotokea takribani miaka bilioni 13.7 iliyopita.
Wanasayansi wanatumia gunduzi mbili za kisayansi kuthibitisha madai haya.
Kwanza, ugunduzi wa Edwin Hubble miaka ya 1920, ambapo Bw. Hubble kwa kutumia telescope, aligundua kuwa bado Ulimwengu unaendelea kutanuka, ambapo alisema kadri galaxies zipokuwa mbalimbali basi ndio zinazidi kukimbiana (Hubble's law).
Pili, ugunduzi wa Cosmic Microwave Background (CMB). Mnamo miaka ya 1960, wanasayansi waligundua mwanga (radiation) ambao ni wa kale na huo mwanga umetawanyika katika sehemu zote za Ulimwengu. Wanasayansi wanaamini kuwa mwanga huu ulitokana na mlipuko wa big bang na umeendelea kuwepo kwa miaka yote hiyo hadi leo. Inaaminika mwanga huu ni kama mwangi au wimbi la mstuko wa big bang ambalo limeendelea kupoa na hatimae kuonekana katika Microwave domain of electromagnetic spectrum.
Udhaifu wa Nadharia Hii
i. Nadharia hii haielezi chanzo cha hiyo punje ndogo. Yaani hii punje ndogo ilitokea wapi, nini kilipelekea kuundwa kwa hii punje ndogo? Hapa pana maswali mengi ambayo sayansi haiwezi kujibu na itaendelea kusemwa tu kuwa "Ulimwengu ulianza kama punje ndogo". Na kama watasema ulitokana na vitu fulani basi watatakiwa kuonyesha pia hivyo vitu vimetokana na nini.
ii. Nadharia hii haielezi nini kilisababisha mlipuko ambao umeunda Ulimwengu huu.
iii. Je hii punje ndogo ilikuwa katika nini? Je Nadharia inasema nini juu ya uwepo wa mazingira fulani ambayo huweza kubeba kitu? Je hiyo punje ilikuwa ipo yenyewe tu? Je inawezekana kitu fulani kisiwepo juu ya kitu chochote? Nadharia bado haijaeleza.
iv. Hivi karibuni Kuna baadhi ya nyota zimegunduliwa kuwa na umri mkubwa kuliko big bang yenyewe. Mfano, Methuselah ni nyota ambayo inakadiriwa kuwa na miaka bilioni 14.45, yaani hii nyota ilikuwepo kabla ya tukio la big bang.
Kutokana na kutokuwa na majibu juu ya maswali haya, Kuna nadharia nyengine zilitungwa, ambazo zilizidi kuzua maswali mengine.
2. Steady-State Theory
Nadharia inasema kuwa Ulimwengu siku zote unatanuka lakini density (tungamo) ikindelea kubaki vilevile ambapo nyota na galaxies mpya huendelea kutengenezwa kwa kiwango sawa na hupoteaji wa nyota na galaxies za zamani ambazo hupotelea kwenda katika Ulimwengu usioonekana. Watafiti wa nadharia hii wanasema kuwa Ulimwengu hauna mwanzo wala mwisho katika muda, na density na mpangilio wa galaxies ni sawa kwa muda wote.
Katika nadharia hii, tunaona moja kwa moja wameshindwa kuonyesha chanzo cha Ulimwengu.
3. The Plasma Cosmology
Nadharia hii inaamini kuwa evolution ya Ulimwengu kwa wakati uliopita inabidi ielezewe kwa kuangalia matukio yanayotokea katika Ulimwengu kwa sasa. Yaani inasema, matukio yanayotokea katika Ulimwengu sasa ndio hayohayo yalitokea katika Ulimwengu wakati uliopita. Nadharia hii pia inakataa kuwa Ulimwengu haujatokana na chochote kama inavyoaminika na watafiti wa big bang. Watafiti wa Plasma Cosmology wanaamini kwamba kwasababu tunaona Ulimwengu unaobadilika, basi huu Ulimwengu ulikuwepo siku zote and utaendelea kuwepo and kubadilika milele. Kama ilivyo Kwa steady state theory, Nadharia hii pia inakataa Ulimwengu kuwa na chanzo.
4. Big Bounce Theory
Big Bounce inasema kuwa Ulimwengu umekuwa ukitanuka na kuanguka mara kadhaa. Yaani Ulimwengu umetanuka mara kadhaa na ku-collapse mara kadhaa. Huu Ulimwengu tulionao ni zao la Ulimwengu ambao uli-collapse na kutanuka tena na wanatabiri kuwa huu Ulimwengu uta-collapse tena na pengine kutanuka tena. Kwahiyo Kuna series ya 'crunches and bangs' ambapo Ulimwengu unatanuka na kuanguka. Bado nadharia hii haionyeshi chanzo cha Ulimwengu bali huonyesha mabadiliko tu. Chanzo cha huo Ulimwengu ambao unacollapse na kutanuka ni kipi? Nini ilikuwa sababu ya kutanuka na ku-collapse? Bado hatupati majibu.
5. The Ekpyrotic Model
Nadharia hii inaamini kuwa big bang ilitokea kwa sababu ya mgongano wa branes mbili ambazo zilikuwa sambamba. Sina tafsiri sahihi ya neno branes, lakini branes inaweza kuelezewa kama any of the spatially extended mathematical objects of zero or more dimensions used in string theory. Watu wa Quantum mechanics na General relativity wanaweza wakanielewa. Katika mazungumzo haya, tuzichukulie hizo branes kwa mfano wa kamba, hivyo basi hizo kamba mbili sambamba zilisuguana na kupelekea moto ambao ndio ukazaa big bang na hatimae kuunda Ulimwengu. Hapa tunapata swali jengine, je hizi branes zilitoka wapi? Nini kilifanya zisuguane? Hapa pia Kuna maswali mengi.
Hitimisho: tumeona kuwa nadharia nyingi hazijaelezea hasa chanzo cha Ulimwengu, baadhi zinasema kabisa Ulimwengu hauna chanza na hautakuwa na mwisho na nyengine zinasema Ulimwengu ulianzia na kitu fulani, lakini haziwezi kuelezea chanzo cha hicho kitu. Yaani nini kilikuwa chanzo cha hicho ambacho wewe unakiona kuwa ndio kimeleta Ulimwengu?
Je, Kuna nadharia nyengine ambazo zina majibu mazuri zaidi?
Je, wale wanaopinga uwepo Mwenyezi Mungu wanategemea nadharia hizi katika kuelezea chanzo cha Ulimwengu?