Nadaiwa na microfinance million Tano

Nadaiwa na microfinance million Tano

Napambana kulipa, kama juzi nmewalipa million Moja. Lakini wamecalculate riba imenirudisha kwenye ileile million Tano kama sijalipa million.

Am confused nachomokaje. Dhamana ni Mali ya mtu mwingine.
Uliingia mkataba wa mkopo kwa hiyari yako mwenyewe, kwa hiyo basi unawajibika kulipa deni lako lote kama vile ambavyo limeainishwa kimkataba.

Ebu dadavua zaidi kuhusu deni lako la msingi, yaani principal amount, riba yaani interest, loan tenure, pamoja na masharti mengine ikiwamo adhabu ya ucheleweshaji wa malipo ya mkopo, ili upewe ushauri mzuri. wa kuweza kukusaidia.
 
Hiyo sehemu ya pili ndiyo inayotakiwa ufafanuzi.

Kuwa na "liseni" ya biashara siyo ruhusa ya kufanya biashara inayoumiza walaji wa biashara hiyo.
Biashara hizi za kifedha zina sheria zake zinazowalinda wenye biashara na watumiaji wa biashara hizo. Huko ndiko kunakotakiwa kutazamwa kama masharti ya biashara hiyo yapo ndani ya wigo wa sheria zilizopo.

Hakuna Sheria za dunia zisizoumiza tabaka la chini.

Njia pekee ni kutokopa. Lakini ukishakopa jua kabisa Sheria haiwezi kumfavour mkopaji.
Riba ipo kumnufaisha anayekukopesha sio mkopaji.
 
Napambana kulipa, kama juzi nmewalipa million Moja. Lakini wamecalculate riba imenirudisha kwenye ileile million Tano kama sijalipa million.

Am confused nachomokaje. Dhamana ni Mali ya mtu mwingine.
Kimbia
 
Rejea masharti ya mkataba wao mliokubaliana, je yamebadilika au ni Yale Yale au wewe ndio tatizo mkuu
Watu uwa wananishangaza sana, wanakuja kulalamika eti wanaonewa wakati hawakusoma makubaliano au mkataba kabla ya kupewa pesa.
 
Kwa kuongezea, kidini za Abraham kumchukua MTU utumwani ambaye sio ndugu yako sio dhambi na Mungu anabariki.
UONGO.


Utumwa kwenye BIBLIA.


Utumwa kwenye Biblia sio utumwa huu tunaojua wa kukandamiza na kuonea watu.

Utumwa kwenye Biblia hauna tofauti na ajira leo hii, ndomaana mnaitwa Watumishi.


1) Mtu hakupaswa kuchukuliwa kinguvu na kufanywa mtumwa. Adhabu ya mtu anayefanya hivi ni kifo. Kwahiyo mpaka hapa tuna uhakika MUNGU hakuunga mkono utumwa tunaoujua.

"Yeyote anayemteka nyara mwingine akamuuza au akamweka kwake, akikamatwa ni lazima auawe."
Kutoka.21.16.NENO



2)
MUNGU alikataza kuonea na kudhulumu watu, hata wageni / watumwa.

i) "Usimwonee mtu maskini na mhitaji ambaye umemwajiri, akiwa ni nduguyo Mwisraeli au mgeni anayeishi katika mojawapo ya miji yenu.

Mlipe ujira wake kila siku kabla ya jua kutua, kwa sababu yeye ni maskini na anautegemea ujira huo. La sivyo, anaweza kumlilia Bwana dhidi yako, nawe ukapata hatia ya dhambi."

Kumbukumbu.24.14-15.NENO


ii) "Usimtendee mgeni vibaya au kumdhulumu, kwa kuwa nanyi mlikuwa wageni huko Misri.

“Usimdhulumu mjane wala yatima.


Ukifanya hivyo nao wakinililia, hakika nitasikia kilio chao.

Hasira yangu itawaka, nami nitawaua kwa upanga, wake zenu watakuwa wajane na watoto wenu watakuwa yatima."

Kutoka.22.21-24.NENO



3)
Utumwa ulikuwa makubaliano, hasa ili kulipa deni.

Watumwa wa kiyahudi wamepewa muongozo kabisa wa muda wa kazi. Watumwa wa kigeni ni wazi ingekuwa makubaliano yao na mabosi zao maana ni kosa kuwalazimisha.

i) “Ukimnunua mtumwa Mwebrania, atakutumikia kwa miaka sita. Lakini katika mwaka wa saba, atakuwa huru naye ataenda zake pasipo kulipa chochote."
Kutoka.21.2-3.NENO

ii) "Kama Mwebrania mwenzako, mwanaume au mwanamke, akijiuza kwako na kukutumikia miaka sita, katika mwaka wa saba ni lazima umwache aende zake akiwa huru.

Nawe wakati utakapomwachia usimwache aende mikono mitupu."

Kumbukumbu.15.12-13.NENO



4) Watumwa waliokimbia kutoka nchi zingine walipaswa kupokelewa vuzuri na waisraeli. Labda walikuwa wanateswa huko. Wakija Israeli wanakuja nyumbani.

"Ikiwa mtumwa amekimbilia kwako, usimrudishe kwa bwana wake.

Mwache aishi miongoni mwenu mahali popote anapopapenda na katika mji wowote anaochagua. Usimdhulumu."

Kumbukumbu.23.15-16.NENO



5) Atakayempiga akamuumiza mtumwa, mtumwa anakuwa huru kutoka hapo hata kama muda wa kuondoka haujafika.

“Mtu akimpiga mtumwa wa kiume au wa kike kwenye jicho na kuliharibu, ni lazima amwache huru yule mtumwa kama fidia ya hilo jicho.

Akimvunja jino mtumwa wa kiume au wa kike, ni lazima amwache huru huyo mtumwa kwa kufidia hilo jino."

Kutoka. 21.26-27.NENO



6) Atakayeua mtumwa wake ataadhibiwa. Damu kwa kwa damu. Mtumwa asipokufa hatoadhibiwa, lakini tumeona mtumwa anakuwa huru kuondoka akitaka.

"Mtu akimpiga mtumwa wake wa kiume au wa kike kwa fimbo na mtumwa huyo akafa papo hapo, ni lazima aadhibiwe,

lakini ikiwa mtumwa ataamka baada ya siku moja au mbili, hataadhibiwa, kwa sababu yule mtumwa ni mali yake."

Kutoka.21.20-21.NENO



7) Mabosi wakristo wanaagizwa watendee watumwa wao / wafanyakazi wao / watumishi kwa haki.

"Ninyi mabwana, watendeeni watumwa wenu yaliyo haki na yanayostahili, mkitambua kwamba ninyi pia mnaye Bwana mbinguni."
Wakolosai.4.1.NENO



8) Utumwa kwenye biblia hauna ubaguzi wa rangi, taifa, kabila. Wote waisraeli na wasio wasiraeli walikuwa watumwa. Utumwa wa kutesa tunaojua ulikuwa ni ubaguzi kwa binadamu wengine.



 
Wanakubalijr dhamani ya mtu mwingine?? Sepa wapambane na mwenye mali!
 
Dhuluma inatoka wapi? Riba ndio faida ya mkopeshaji. Yeye anatafuta hela kwa jasho lake,anakupa ufanyie mambo yake kwa makubaliano riba ni kiasi fulani hela irudi baada ya muda fulani isiporudi hatua atakazochukua ni hizi sasa dhukuma iko wapi? Ulitaka upewe hela bure tu?
Wachuuzi wananunua bidhaa tsh 10 wanauza tsh 20 hio nayo ni dhuluma? Dawa ya deni kulipa. Tatizo wanachukua mikopo na kufanyia mambo yasiyo na faida ikifika wakati wa kulipa wanakuja mitandaoni kujiliza. Mbona wakati anachukua hakuja kuuliza?
Mkuu, sisi watanzania tunapenda sana kukopa lakini inapofika wakati wa kulipa hatuishi kulalama. Ndiyo maana huwa nasema KATU usimkopeshe mtanzania fedha au kama ni kukopesha uwe tayari kusamehe. Kwa mfano kuna ile imani potofu kuwa eti ukinunua nyumba ya mtu aliyeweka kama dhamana benki halafu akashindwa kulipa, utapata balaa kwa kuishi kwenye hiyo nyumba. Yaani tishio la huu ujinga lengo lake ni kuwa benki zishindwe kuuza nyumba za wateja walioshindwa kulipa... Mimi nadhani tungedai kuwa na uwazi zaidi kwenye kuonyesha mpangilio wa malipo na riba yake. Kwa mfano kuna nchi moja niliona, ukikopa eg sh milioni 10, na ukasema utalipa kwa miaka mitatu... unapewa kabsa mchanganuo wa malipo kwa kila mwezi. Kwa mfano wetu wa milioni 10 kwa miaka mitatu, utapewa invoice ya malipo inayoonyesha kila mwezi unalipa 360,000 x 36 = 12,960,000. Hii unaonyeshwa na kupewa siku ya kuomba mkopo, kwa hiyo unajua kabisa ni nini kipo mbele yako.
 
Njia zilizokatazwa kutumiwa kutengeneza pesa kwenye Biblia, according to Ryan Moroney:

1) Get rich quick schemes (Utajiri wa harakaharaka)
"Mali ya harakaharaka hutoweka, lakini akusanyaye kidogokidogo ataiongeza."
Methali.13.11.BHND



2) Usury (Kausha damu, ni utumwa wa kifedha)

"Aongezaye mali yake kwa riba na kutoza faida anamkusanyia mwingine mwenye kuwahurumia maskini."
Methali.28.8.BHND

(Huyu anasema kuwekeza kwenye soko la hisa si kosa kwenye Biblia, na inapendekezwa. Hajataja maandiko.

"Jishughulishe na biashara hata kama kwa kubahatisha; yawezekana baadaye ukapata chochote kile."
Mhubiri.11.1.BHND

“Tena, ufalme wa mbinguni ni kama mtu aliyetaka kusafiri, naye akawaita watumishi wake na kuweka mali yake kwenye uangalizi wao.

Mmoja akampa talanta tano, mwingine talanta mbili, na mwingine talanta moja. Kila mmoja alipewa kadiri ya uwezo wake. Kisha yeye akasafiri.

Yule aliyepewa talanta tano akaenda mara moja akafanya nazo biashara akapata talanta nyingine tano zaidi.

Yule aliyepewa talanta mbili akafanya vivyo hivyo, akapata nyingine mbili zaidi.

Lakini yule mtumishi aliyekuwa amepokea talanta moja, alienda akachimba shimo ardhini na kuificha ile talanta ya bwana wake
.

Mathayo.25.14-18.NENO




3) Hustle culture (kufanya kazi ili uwe tajiri kuwa ndo kipaumbele kikuu maishani, ukiiacha imani na familia nyuma.

"Usijitaabishe ili kuupata utajiri, uwe na hekima kuonesha kujizuia."
methali.23.4.NENO




View: https://www.instagram.com/reel/DTbBO3MEnCt/?igsh=M3prN2c2Mng0c2cx
 
Hakuna Sheria za dunia zisizoumiza tabaka la chini.

Njia pekee ni kutokopa. Lakini ukishakopa jua kabisa Sheria haiwezi kumfavour mkopaji.
Riba ipo kumnufaisha anayekukopesha sio mkopaji.
Mimi sijui hiyo dunia unayoishi wewe; kwa hiyo usitake nishirikishwe kwenye dunia ya namna hiyo; yenye sheria zinazokusudwia kuumiza baadhi ya watu katika jamii.
Njia pekee ni kutokopa. Lakini ukishakopa jua kabisa Sheria haiwezi kumfavour mkopaji.
Riba ipo kumnufaisha anayekukopesha sio mkopaji.
Utakuwa una akili ya kipekee sana kuwa na fikra za aina hii. Bila shaka unaishi pangtoni.
 
Mimi sijui hiyo dunia unayoishi wewe; kwa hiyo usitake nishirikishwe kwenye dunia ya namna hiyo; yenye sheria zinazokusudwia kuumiza baadhi ya watu katika jamii.

Utakuwa una akili ya kipekee sana kuwa na fikra za aina hii. Bila shaka unaishi pangtoni.

Huwezi nielewa.

Nikuambie tuu hata anayekukopesha hawezi kukukopesha kama hanufaiki na hakuumizi.
Sasa utachagua akuumize Sana au kidogo.
Ila kuumizwa lazima uumizwe.

Ukishachagua maumivu kazi kwako. Yakikushinda tafuta wanasheria
 
Huwezi nielewa.

Nikuambie tuu hata anayekukopesha hawezi kukukopesha kama hanufaiki na hakuumizi.
Sasa utachagua akuumize Sana au kidogo.
Ila kuumizwa lazima uumizwe.

Ukishachagua maumivu kazi kwako. Yakikushinda tafuta wanasheria
Kwani wewe ni nani usieleweke?
Hata ukiandika takataka kama unavyofanya mara kadhaa humu zitaeleweka kuwa ni takataka.

Haya unayoandika hapa ni upuuzi.
 
JIULIZE katika 5m principle ni sh ngapi? Interest ni ngapi? Je upo nje ya Muda penalty mpk sasahiv ni. Sh ngapi?
 
Kwani wewe ni nani usieleweke?
Hata ukiandika takataka kama unavyofanya mara kadhaa humu zitaeleweka kuwa ni takataka.

Haya unayoandika hapa ni upuuzi.

Kwa hiyo wewe ni mzoa takataka? Maana Mimi nimeziweka hapa. Wewe unakuja kuzizoa
 
Amua utakavyo mwenyewe. Nimekwisha malizana na wewe.
Muda wa kupoteza kuzungushana na akili za aina hii sina.

Ulipoona mawazo ya wenzako takataka ulifikiri mzoataka atakuwa nani kama sio Wewe?😂😂

By the way ni KAZI uliyoamua kuichagua mwenyewe. Na ipo halali kisheria. So usijisikie vibaya
 
Ulipoona mawazo ya wenzako takataka ulifikiri mzoataka atakuwa nani kama sio Wewe?😂😂

By the way ni KAZI uliyoamua kuichagua mwenyewe. Na ipo halali kisheria. So usijisikie vibaya
Basi, nitatafuta siku maalum tuyazungumze yote hayo.
 
Basi, nitatafuta siku maalum tuyazungumze yote hayo.

Haina shida. Muhimu tuu ni kujua kutumia lugha vizuri hata kama umeona mawazo ya wenzako ni low quality, au yanapotosha, au yakijinga.
Hiyo ndio Akili, na hekima na ukomavu kama mtu mzima.

Lakini kuanza kusema ooh takataka, sijui mavimavi, unajishushia brand, nyota na kwa vile utakuwa chini sio ajabu ukajibiwa kwa viwango vya chini bila heshima.
Ni Bora kukaa kimya.
 
Haina shida. Muhimu tuu ni kujua kutumia lugha vizuri hata kama umeona mawazo ya wenzako ni low quality, au yanapotosha, au yakijinga.
Hiyo ndio Akili, na hekima na ukomavu kama mtu mzima.

Lakini kuanza kusema ooh takataka, sijui mavimavi, unajishushia brand, nyota na kwa vile utakuwa chini sio ajabu ukajibiwa kwa viwango vya chini bila heshima.
Ni Bora kukaa kimya.
Nishakupa ahadi mkuu, tafuta tu siku nzuri kwako, yote hayo tutayajadili kwa kiwango chochote utakachotaka mwenyewe.
Huwa sina fungu maalum ninalolazimika kujifunga; hata hilo la uzoa takataka naliweza sana.
 
Back
Top Bottom