Nadaiwa na microfinance million Tano

Nadaiwa na microfinance million Tano

Uliangalia interest, time na fees unazolipa, tuanzie hapo, weka number zote tukusaidie
Wale jamaahesabu zao sio za level hii. N mikopo yao n dhaman unachukua unaposhikwa kwelikweli hujali. Mkopo wa miezi mitatu riba unakita 50%. Usikute jamaa analipa milion 5 alikopeshwa milion 3 n lki 6.

N hapo kachelewesha mwezi mmoja kila akinipapatua anacjeza mulemule. Yan unskuta anaenda kszin anapata hela anakuja kuwapa wao wamekaa tu, akifanya utani atalipa hiyo milion 5 akaimaliza na kwq sbab ya kujivuta kwa den lile na kulipa kidgo kidogo riba imejiongeza deni limerudi pale pale. Yani unalipa mdpgo mdogo mpaka mlion 5 inaisha ukiliangalia deni lilobakia ni milion 5 ileile.hawaon tabu kupigia riba hata kwa siku wale
 
Mkuu tafuta mkurugenzi wa hiyo office su kampuni kaa nae mezabi mwambie hali halisi na muombe asimamishe ongezeko la riba na mpe ratiba yako namna utakavyopambana kulipa, ofisi wakiwa waelewa watakupa hiyo fursa. Epuka wasije kureport credit bureau itakusumbua huko mbeleni kukopesheka eidha micorofinance au benki.
 
Sijui mtu wa haki na anayemwogopa Mungu anawezaje kufanya biashara ya riba, ni dhulma halali!

Dini za Abraham zinakataza kutoza riba kwa ndugu yako tuu.

Lakini sehemu zingine Riba ni biashara halali kabisa kiimani na kwa Mungu.

Kwa kuongezea, kidini za Abraham kumchukua MTU utumwani ambaye sio ndugu yako sio dhambi na Mungu anabariki.

Waafrika wengi hawafundishwi ukweli wote.
Mzungu na Maurabu au mchina anavyomuona muafrika anajua sio ndugu yake.

Pia wewe kunikopesha Mimi kwaa riba sip dhambi, kwa mujibu wa dini zaa Abraham

Muhimu hapo, aliyekopa ndiye anatatizo kwa sababu hakulazimishwa.

Alafu kanuni ya Dini za Abraham ni kutokukopa. Na ukiona myahudi anakopa ujue hapo ni kwaajili ya investment full stop.

So kusema dhulma haisaidii chochote na haibadili chochote.

Hawapati dhambi popote. Na sio kosa kama Wana leseni kisheria.

Waafrika tunapenda kuvamia mambo bila kuyaelewa kuanzia hayo mambo ya Riba na Dini(dhulma).
 
Jina la ofisi : chidindu wabindindu microfinance

Jina la Mkurugenzi : Msakauzi chidindu

Mahali : Tegeta nyololi

Unakuta mwenye ofisi kaajiriwa na hiyo ofisi kajiajiri kama side hustling. Hapo mtauana bure tu... suluhu mkataba ukaangalwe upya deni lilipwe na mahakama
Sio kweli, kwan kasema shida ni mkataba? Au kafeli marejesho. Note: ile ni biashara na hela uliyopewa ni mtaji, ukikopa kuwa msitrabu kulipa pia.
 
Mkuu tafuta mkurugenzi wa hiyo office su kampuni kaa nae mezabi mwambie hali halisi na muombe asimamishe ongezeko la riba na mpe ratiba yako namna utakavyopambana kulipa, ofisi wakiwa waelewa watakupa hiyo fursa. Epuka wasije kureport credit bureau itakusumbua huko mbeleni kukopesheka eidha micorofinance au benki.

Huyu kashajichanganya.
Hapo njia ni aende mahakamani tuu labda atapata ahueni lakini pesa lazima atoe
 
Sijui mtu wa haki na anayemwogopa Mungu anawezaje kufanya biashara ya riba, ni dhulma halali!
Dhuluma inatoka wapi? Riba ndio faida ya mkopeshaji. Yeye anatafuta hela kwa jasho lake,anakupa ufanyie mambo yake kwa makubaliano riba ni kiasi fulani hela irudi baada ya muda fulani isiporudi hatua atakazochukua ni hizi sasa dhukuma iko wapi? Ulitaka upewe hela bure tu?
Wachuuzi wananunua bidhaa tsh 10 wanauza tsh 20 hio nayo ni dhuluma? Dawa ya deni kulipa. Tatizo wanachukua mikopo na kufanyia mambo yasiyo na faida ikifika wakati wa kulipa wanakuja mitandaoni kujiliza. Mbona wakati anachukua hakuja kuuliza?
 
Hawapati dhambi popote. Na sio kosa kama Wana leseni kisheria.
Hiyo sehemu ya pili ndiyo inayotakiwa ufafanuzi.

Kuwa na "liseni" ya biashara siyo ruhusa ya kufanya biashara inayoumiza walaji wa biashara hiyo.
Biashara hizi za kifedha zina sheria zake zinazowalinda wenye biashara na watumiaji wa biashara hizo. Huko ndiko kunakotakiwa kutazamwa kama masharti ya biashara hiyo yapo ndani ya wigo wa sheria zilizopo.
 
Napambana kulipa, kama juzi nmewalipa million Moja. Lakini wamecalculate riba imenirudisha kwenye ileile million Tano kama sijalipa million.

Am confused nachomokaje. Dhamana ni Mali ya mtu mwingine.
Ndio maana uislamu ulikataza riba
 
Napambana kulipa, kama juzi nmewalipa million Moja. Lakini wamecalculate riba imenirudisha kwenye ileile million Tano kama sijalipa million.

Am confused nachomokaje. Dhamana ni Mali ya mtu mwingine.
Hii huchomoki Mzee.
 
Dhuluma inatoka wapi? Riba ndio faida ya mkopeshaji. Yeye anatafuta hela kwa jasho lake,anakupa ufanyie mambo yake kwa makubaliano riba ni kiasi fulani hela irudi baada ya muda fulani isiporudi hatua atakazochukua ni hizi sasa dhukuma iko wapi? Ulitaka upewe hela bure tu?
Wachuuzi wananunua bidhaa tsh 10 wanauza tsh 20 hio nayo ni dhuluma? Dawa ya deni kulipa. Tatizo wanachukua mikopo na kufanyia mambo yasiyo na faida ikifika wakati wa kulipa wanakuja mitandaoni kujiliza. Mbona wakati anachukua hakuja kuuliza?

Kuelewa kwako ni kidogo, umeandika kama mtoto wa la 2, paragraphs hakuna, komq hakuna, utazani unaandoka barua ya mapenzi? Fool
 
Hapo nilipoona umesema "dhamana ni mali ya mtu mwingine..." wewe una kila dalili ya kulala mbele dhamana iuzwe. Cha kufanya nenda mahakamani ukafungue kesi huelewi mkataba mwisho wa siku mdaiwa hafungwi ila fahamu dawa ya deni ni kulipa tu huna namna...
 
Back
Top Bottom