Bushmamy
JF-Expert Member
- Aug 18, 2019
- 8,848
- 15,253
Tarehe 25 Mwezi April ni kumbukizi ya Nabii Mkuu Mh Dokta GeorDavie kukumbuka siku yake ya kuzaliwa ambapo Maelfu ya waumini wa huduma ya Ngurumo ya Upako walisherekea kwa pamoja huku wageni kutoka nchi mbali mbali kutoka nchini Congo, South Africa, Kenya na maeneo mbali mbali ya pembezoni ya dunia walikuwepo katika siku hii muhimu kwa Nabii Mkuu.
Awali akizungumzia siku hiyo muhimu kwake Mh Nabii Geordavie Mkuu amesema kwamba siku hiyo ilikuwa ifanyike tarehe 25 mwezi April lakini kutokana na siku hiyo kuangukia siku ya kazi na sio siku ya huduma, hivyo kupelekea kufanyika siku ya juma pili ya tarehe 23 kwa lengo la wana Ngurumo kupata fursa ya kusherekea pamoja na Nabii Mkuu Mh Dokta GeorDavie .
Nabii Mkuu Mh Dokta GeorDavie amesema wakati anakumbuka siku yake ya kuzaliwa anashukuru Mungu amefanikiwa kusaidia jamii katika kutoa misaada mbali mbali ikiwemo mitaji kwa vijana wanawake wazee na rika mbali mbali ambapo mpaka kufikia mwaka huu wa 2023 amesha tumia kiasi cha shilingi Milioni 400 kugusa jamii katika kutoa mitaji kugawa piki piki bajaji vifaa vya studio kwa wasanii , mitaji kwa wafanya biashara wa soko la Samunge jijini Arusha na wengine wengi kutoka mikoani pamoja na nje ya nchi ambapo Nabii Mkuu Mh Dokta GeorDavie amegusa jamii kwa mahitaji muhimu .