Wakubwa wenzangu habarini za weeekend kwangu mimi weekend yangu haiko powaa kabisaa
Mke wangu ni mzuri ana hofu ya mungu ana kazi pia ananipenda ila huwa ana tabia ya kununa hovyo yaani hataki kukosolewa yaani kila nikimkosoa tutakaa siku tatu bila kuongea akiwa kanuna yaani lazma nimuombe msamaha hata kama kanikosea
Pia huwa ana tabia ya kunijaribu sanaa kama kuna kipindi nilimkuta anaongea na mtu usiku nikamwambia SIKUAMINI nakumbuka usiku ule ule alichukua begi lake akaondoka yaaani ndugu zangu nilifikilia sanaa nilipoksea sikupaonaa ila sikukata tamaa nikzidi kumwomba arudi home niliomba msamaha sanaa kisha akakuali akarudi
Kipindi kingine nilipika viazi na nyama nikazidisha mchuzi sikuamini macho yangu yaaani mamaa alikasilika sanaaa akakataa kula akaondoka kwa hasiraa kwenda kulala kwa dadaake kule pia nilitumia nguvu kubwa kumrudisha
Sasa hii ya sasa ndo imenikatisha tamaa yaani niko kikazi tanga mke wangu kuwa anapiga simu mda wote akidai kanimis nikamwambia ntarudi alhamis but nilipata emergrncy mke akakasirika sanaaa huku akisistiza simthamini pia akidai tuachene tuu sasa jana ndio nilirudi home akanipokea vizuri tuu nikamwomba msamaha kwa kumpa feki promis akasema kanismehe kumbe ana yake moyoni
alikataa kuongea na mimi tangu jana bila mimi kujua sababu hadi asubuhi namuaga naenda kazini kumalizia kipolo cha kazi akakasilika zaidi akaondoka pia kazini kwake bila hata kuniaga kitendo kile kimenishangaza sanaaa
Sasa ntaka nifanye mmamuzi magumu naona antaka ajifanye mwanamme ndani ya nyumba ntaka nimpe taraka naombeni ushauri
Aisee hapa nadhani kuna shida sana katikati yako na mkeo, na ninadhani ulikosea kwenye first aproach and treatment kwa mke wako ndio maana kwa sasa unapata shida kumrudisha awe kama mke na mama wa familia kuna mengi sana yanahitajika hapa kutueleza walau washauri tuweze kutafuta suluhu.
Lakini pia hawa biumbe kuna wakati mimba zao zikiwa changa hivi unaweza kutia taraka (baadhi ya wanawake lakin) maana huwa na tabia za ajabu sana kama huna busara unaweza vunja ndoa yako
Ila kama yuko sawa namaanisha hana mimba basi Kuna wakati unatakiwa kuwa mkali na misimamo na kuridhia anacho kitaka ili uweze kupata nin anataka na hapo usubiri chanzo cha ugomvi kiwe yeye, yaan yeye ndio awe mkosaji,
na hata kama atasema anataka kuondoka mwambie nenda na kama umeamua kuondoka usirud hapa tena maana umesha nichosha na tabia hizi ndoa gani imekuwa haina amani kila wakati ni migongano isiyo na tija na kama ataondoka usihangaike naye kabisa na ikiwezekana umblock kabisa ili uweze kupata majibu kama kadhamiria au ni kudeka kwake baada ya kugundua kuwa wewe ni muombaji sana msamaha kwake hata kwa kosa alilo lifanya yeye
Maana umesha mzoesha kuwa akichukia kidogo na kuondoka anajua utamfuata tu, sasa hali hiyo keshaigeuza kama fimbo ya kukuchapia , sasa jaribu kumtilia ngumu na ujikaze hata kama unaona utashidwa kama hanaa nia hiyo ata tafuta namna ya kuupata tu na wewe wala usiwe na presha naye jifanye kama ulisha amua kumuacha iwe zamu yake kukubembeleza, na siku akijishusha na kukubembeleza umsamehe huo ndio utakuwa mwanzo wa nidhamu kurudi. Hawa viumbe ukiona busara imetumika sana sana tena sana na imegonga ukuta tumia udikteta ili mambo yakae sawa.
ANGALIZO: lakin pia katika hili uwe umejiandaa kwamba liwalo na liwe A & B yote yawe majibu sahihi kwako, ila usimpe talaka, kama ni talaka ifuate baada ya hili kukupa majibu.