Na mimi ni banker yamenikuta

Na mimi ni banker yamenikuta

Banker ametoweka yuko na habipt,mrejesho akitoa hela hata confess Jf
 
Tena achana kabisa na huo ujinga. Jenga maisha yako, usikurupukie mambo hayo. Badirisha mtizamo wako kabisa, rudi kwa mola wako utakwisha!
 
Habari wana JF,

Waswahili wanasema ukiona mwenzako ananyolewa tia maji nywele zako. Kuna mdau mmoja (banker) aliwahi leta topic kuhusu masikitiko yake jinsi alivyotendwa na bint wa IFM pale Kilimanjaro Hotel.

Wadau nami yamenikuta, nami pia ni banker tena junior officer tu hapa jijini Mwanza. Hii ni ajira yangu ya kwanza na ni miezi michache tu imepita tangu nipate hiki kibarua. Here is my story.

Mimi ni mtulivu na nisiye na makuu na ni mwezi mmoja sasa tangu nifahamiane na bint mmoja mwenye asili ya bara la Asia. Amenivutia naye anaonekana kuvutiwa nami.

Kwa kuwa nimetengana na aliyekuwa mwandani wangu mwezi May nikaona sasa ni muda muafaka wa kupata mbadala wake. Tofauti na yule mdau mwingine ambaye alikua anachepuka, mimi nilikua single mpaka nilipokutana na huyo binti.

Jumamosi iliyopita yani tarehe 1 August, nilimuita Mayi Hotel nikamwaga sera zangu. Kiukweli nimempenda. Ni mpole, na ana aibu na bashasha fulani hivi ya kike. Akaniambia nisiwe na wasi wa
 
Very good! una akil kama ndengu kuota na kuiva wakat wa kpind cha kiangaz! hivo ndo kukomesha viranguz wa mjin.
 
tafuta mtu wa saiv yako mkuu,inaonekana hivyo viatu unavitamani ila kwako ni oversize,we mtu anakuomba 250k unadondosha simu, wakati watu wanahonga murrano na usipoangalia presha itakuondoa,tangu lini mke ukamtolea dar?kwa kazi yako hiyo tafuta banker mwenzio mtaendana.





Habari wana JF,

Waswahili wanasema ukiona mwenzako ananyolewa tia maji nywele zako. Kuna mdau mmoja (banker) aliwahi leta topic kuhusu masikitiko yake jinsi alivyotendwa na bint wa IFM pale Kilimanjaro Hotel.

Wadau nami yamenikuta, nami pia ni banker tena junior officer tu hapa jijini Mwanza. Hii ni ajira yangu ya kwanza na ni miezi michache tu imepita tangu nipate hiki kibarua. Here is my story.

Mimi ni mtulivu na nisiye na makuu na ni mwezi mmoja sasa tangu nifahamiane na bint mmoja mwenye asili ya bara la Asia. Amenivutia naye anaonekana kuvutiwa nami.

Kwa kuwa nimetengana na aliyekuwa mwandani wangu mwezi May nikaona sasa ni muda muafaka wa kupata mbadala wake. Tofauti na yule mdau mwingine ambaye alikua anachepuka, mimi nilikua single mpaka nilipokutana na huyo binti.

Jumamosi iliyopita yani tarehe 1 August, nilimuita Mayi Hotel nikamwaga sera zangu. Kiukweli nimempenda. Ni mpole, na ana aibu na bashasha fulani hivi ya kike. Akaniambia nisiwe na wasi wasi kama Mungu amepanga tuwe pamoja basi itakuwa.

Leo tarehe 7, nikiwa kwenye morning meeting pale job nikapokea msg ya salam mapema isivyo kawaida. Mazungumzo yakafikia baby nina shida ya pesa.Nikauliza kiasi gani, to my surprise "laki 2 na nusu". Haki ya Mungu nilihis mikono yanitetemeka na smu nikaidondosha kwenye kiti.

Hata branch manager alihisi kitu uso wangu ulivyobadlka ghafla maana tulikaa opposite na nilikua nasoma kinyemela. Nikahs labda kakosea huyu.

Anyway, 250k sometimes can not be a big deal, but within 7 days of relationship na maisha yetu yenyewe haya? Vijana wenzangu hapa mmh, hii kali.

Sikujibu mpaka kikao kilipoisha nikajitetea nilikua kikaoni. Hata hivyo niliruka hicho kibom. Nikaulizwa sasa ntatoa ngapi, to be honest niliruka tena mara ya pili. Akajifanya kunielewa.

Mpaka sasa najiuliza, hivi hawa wadada wanadhani sisi bankers tunalipwa mamilioni kama ya Escrow? Anyway, hivi ndani ya wiki moja unanipiga mzinga mkubwa hivyo? Aah kuweni fair bwana, msione bankers wana vigari, ni vya mkopo hivyo.

Nikitazama geto langu halijapendeza kiasi nipendavyo, namna hii si tunarudishana nyuma. Nitaanzisha biashara zangu kweli, ntafikia plan zangu za kutokua mwajiriwa miaka kadhaa ijayo?

Cha ajabu huyu Muasia wangu anauza duka ambalo anadai wanamiliki yeye na dada yake. Kiasi fulani ni miss independent, lakin kwanini vibom hivi. Au ndio kujaribiwa huku?

Mpaka usiku huu hatujawasiliana, tulikua na appointment kuonana jioni ya leo imefail nilibanwa na majukum lakini hata hivyo simu yangu pendwa ilipata majanga siku nzima.

Worse enough namba yangu nyingine hana nami namba zake sijakariri. Nimekuta msg zake kadhaa za hasira akijua labda ndio nimepotea mazima tangu niruke vibom vyake. Akiamka asubuhi sijui itakuaje?

Mmmh! Naomba asubuhi ifike haraka nijue mwisho wa sinema yetu. Ila kama tutawasiliana vizuri asubuhi nimepanga nimuite nimweleze hali halisi ya life langu na mambo yangu kiujumla, lazima tudefine life-mbivu na mbichi.

Nijue moja kama amekuja kwangu kuchuma bora ajitoe kabisa nami nikae chonjo. Na kama kweli ananipenda she has to agree with reality. Siwezi kuishi maisha ya kuigiza kisa mwanamke, huo ndio msimamo wangu.

Sijui kapata wapi akili za kujaribiana wakati mimi sijawahi kufanya show offs za aina yoyote kwake.
 
Mbona papuchi huwa mnawahi kuomba hata ukiwa kwenye masaa tu ya relationship...

Ukome nyie wafanyakazi wa benk huwa mnajionaga mnazo sana.
 
Keep that shit in your pants! You don't even know your status!? What a douchebag! If dont have money why board a train by its head!!?? And you are telling us this shit!?? Watu wanahonga passo umeomba elf 250 and you piss your pants! Tatol wreckage!!!

Tatizo ni nini muugwana? Kwani binadamu wote ni sawa? Mfano Bw. Mengi anaweza kuhonga kiwanda (Bonite) lakini si kuhonga IPP yote, vivyo hivyo wewe unaweza kuhonga Passo lakini si kiwanda. Huyu jamaa naye anaweza kuhonga sh.10,000 lakini si 250,000. Kila mtu na level yake. Hata angelalamika kuombwa 10,000 kama ndio level yake mimi naona ni sawa tu.
Huu utofauti wa kipato ndio unaifanya dunia isonge (balance). Hatuwezi wote kuwa matajiri. Never, ever. Ni vema ukaheshimu maono ya kila mmoja hapa.
 
Back
Top Bottom