Mzungu ni nani?

Mzungu ni nani?

Paka akiwa mnene ni paka wa kizungu,paka akikondeana ni paka wa kiswahili,

Kuku anayewekwa mahali safi,analindwa,ni kuku wa kizungu ila wale wanaorandaranda wa kienyeji

Mtu akiwa anajali muda msafi ,ana. pesa -yule jamaa mzungu sana hana longolongo kabisa hanaga uswahili kabisa

Lakini mtu muongo,hajali muda ni mswahili-ah yule jamaa mswahili sana maneno mengi,tapeli nk

Mbwa akiwa na mkia mnene,manyoya ni mbwa wa kizungu ila vimbau mbau,wabaya wa kiswahili


Kwenye mabishano au mtu akisifiwa utasikia mimi sini mzungu ,mie siyo mswahili(tapeli tapeli,muongo muongo,hajali muda) kama wewe
umeelezea kizungu zaidi hahahaha
 
Paka akiwa mnene ni paka wa kizungu,paka akikondeana ni paka wa kiswahili,

Kuku anayewekwa mahali safi,analindwa,ni kuku wa kizungu ila wale wanaorandaranda wa kienyeji

Mtu akiwa anajali muda msafi ,ana. pesa -yule jamaa mzungu sana hana longolongo kabisa hanaga uswahili kabisa

Lakini mtu muongo,hajali muda ni mswahili-ah yule jamaa mswahili sana maneno mengi,tapeli nk

Mbwa akiwa na mkia mnene,manyoya ni mbwa wa kizungu ila vimbau mbau,wabaya wa kiswahili


Kwenye mabishano au mtu akisifiwa utasikia mimi sini mzungu ,mie siyo mswahili(tapeli tapeli,muongo muongo,hajali muda) kama wewe
Hahaha umeongea point Kama mzungu
 
Habari za jioni wakuu Nimekuwa nikijiuliza ili swali bila kupata majibu yanayoridhisha, hivi mzungu ni Nani kiasili wazungu ni wakina Nani ili nimuite mzungu awe na viashiria gani... Karibuni sana
 
Uzungu ni ustaarabu wa kimagharibi..unaweza kua mwafrica ukawa umestaarabika kimaghalibi(assimilation).wew ni mzungu tuu
 
Ukishawatambua waafrika, waarab, wahindi, wachina, wajapan na ndugu zao macho madogo wakorea, wavietnam, and the like wanaobaki ndo wazungu.
 
mtu mwenye asili ya ulaya...

mzungu kichaa kwa mfano mzuri
 
Wafuatao ndo wazungu
:1 Waingereza
2: Wafaransa
3: Wajeruman
4: Wamarekani weupe
5:wacanada
6Waaustralia
7.... Wote nchi za Ulaya

Hawa siyo wazungu japo weupe.
Bara Asia
Bara Hindi
Latin America
 
Mzungu ni mtu mwenye asili (asilia) ya ulaya awe anaishi Tanzania, marekani, afrika kusini. Japo kuna wagiriki unaweza kushindwa kuwaita wazungu.

Uzi wa namna hii upo humu JF ulileta dabate refu saana.

katika lugha ukitaka kujua maana ya neno kwanza rudi katika asili ya neno lenyewe.

Kiuhalisia hakuna aliyeweza kutoa uthibitisho wa asili ya neno ila watu wana speculate tu..
1. Wanadai limetokana na neno la kiswahili cha zamani MIZUNGU lenye maana ya kitu cha ajabu, chenye kufanya maajabu. Hivyo kutokana na mambo ya ajabu na ya kutumia akili waliyokuwa wanafanya watu wa ulaya walibatizwa wazungu.

2. Limetokana na kuzunguka. Ikiwa na maana hawa jamaa walikuwa wanapeleleza vitu sana kuzunguka huku na huku..Hivyo ikabidi waitwe wazungu.
 
Wafuatao ndo wazungu
:1 Waingereza
2: Wafaransa
3: Wajeruman
4: Wamarekani weupe
5:wacanada
6Waaustralia
7.... Wote nchi za Ulaya

Hawa siyo wazungu japo weupe.
Bara Asia
Bara Hindi
Latin America
Mrusi?
 
Habari za jioni wakuu Nimekuwa nikijiuliza ili swali bila kupata majibu yanayoridhisha, hivi mzungu ni Nani kiasili wazungu ni wakina Nani ili nimuite mzungu awe na viashiria gani... Karibuni sana
Mzungu ni mnyamwenga
 
Back
Top Bottom