Mzee Yusuph: Walio na nyimbo zangu kwenye simu zao wafute

Anapulizwa Nini huyu mzee maana Kama ameokoka so yeye asilazimishe tuwe wote
 
Huyu muda si mrefu atachanganyikiwa, inaonesha alikosea masharti ya mganga
 
Huyu mzee amefanya dhambi gani inayomtafuna hivyo, pia amejisahau kuwa hizo nyimbo zilikuwa zinauzwa?

Nae pia arudishe mali yote aliyoipata kwa kuuza/kufanya show ya hizo nyimbo
Itakuwa ni ule mtindo wa jaza ujazwe.
 
Yatazungumzwa mengi sana Kuhusu huyu jamaa,lakn Mungu ndy anayetufaham kuliko sisi tunavyojifaham,kwa hyo tusimuhukum kwa Kuwa kama ni dhambi wapo waliotenda dhambi nyingi na kubwa kuliko hizo za kwake,rejea kwa Sauli na Yuda Isikarioti.Mwanadam anapotafuta fedha huamini Kuwa akzipata atakuwa ameyashinda mambo yote lakn ukweli hauko hivyo kwa kuwa fedha huja na mambo yake na kama utakuwa ulizpata kwa namna za ushirkina zinakusumbua sana.Sote tumkumbuke Mfalme Sulemani (Suleiman) baada ya kufanya uchafu wote alisema 'Yote ni ubatili na ni kujilisha upepo' Kwa hyo tusimuandame Mzee Yusuf hayo yalikuwa ni mapito tu ktk historia take ya maisha,tumwache ayafurahie maisha kama wanadam wengine.
 
mzee yusuph yupo sahihi ,ameulizwa kuhusu mziki amejibu kwa kifupi yy amejitoa mbele ya Allah kwahyo km unaendelea sikiliza nyimbo zake ni juu yako na si yy...note mziki kiislam ni haramu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom