kavulata
JF-Expert Member
- Aug 2, 2012
- 16,247
- 16,169
Mzee Warioba mimi namuona kama Mzee mnafiki mkubwa anaetaka kurekebisha makosa yake kupitia Samia, Rais mwanamke mzanzibari. Kuna wakati namuona kama mzee ambae watu fulani wanamtumia vibaya kutaka kufanikisha agenda zao.
Mzee Warioba anaonekana amepiga U-turn kutoka kwenye mrengo wa Ujamaa wa nchi za mashariki kwenda kwenye mrengo wa ubepari wa nchi za magharibi. Hapendi tena demokrasia za China, Urusi, Cuba, Hungary na Korea Kaskazini bali anataka demokrasia za Magharibi sawa na akina Lissu na Kambona Oscar.
Mwaka 1977 wakati katiba hii inaandikwa yeye alikuwa wapi?
Wakati Nyerere anaitumia Katiba hii ya kijamaa na yeye kuwa Waziri Mkuu hakuiona hii Katiba?
Nyerere na Warioba walikuwepo wakati Rais Mwinyi na Mkapa wanatumia katiba hii mbona wote hawakushauri iandikwe katiba mpya ili kuingiza hayo anayotaka yawemo kenye Katiba?
Warioba alikuwepo wakati wa utawala wa Kikwete na Magufuli mbona hakuwalazimisha waandike Katiba mpya?.
Rais Magufuli alitamka wazi kuwa hataandika katiba mpya kwakuwa hakuahidi kuandika Katiba mpya wakati wa kampeni zake za urais, alimfanya nini?.
Angekuwa mimi ndiye Rais Samia ningeacha kuandika Katiba mpya kama vile walivyoshindwa/walivyoacha kuiandika akina Nyerere, Mwinyi, Mkapa, Kikwete na Maguli. Sababu kubwa zilizowafanya Nyerere, Mwinyi, Mkapa, Kikwete na magufuli kuacha kuandika katiba mpya ni moja tu, nayo ni hofu ya kuuvunja Muungano. Mama Samia asiipuuze hofu hii pia, ni kubwa na ipo dhahiri. Huyu Warioba tofauti na Nyerere, yeye anataka serikali tatu. Aliogopa kumshauri Nyerere, Mkapa na Magufuli lakini sasa anaona kuwa ni rahisi sana kwa Samia.
Aogopwe kama ukoma.
Mzee Warioba anaonekana amepiga U-turn kutoka kwenye mrengo wa Ujamaa wa nchi za mashariki kwenda kwenye mrengo wa ubepari wa nchi za magharibi. Hapendi tena demokrasia za China, Urusi, Cuba, Hungary na Korea Kaskazini bali anataka demokrasia za Magharibi sawa na akina Lissu na Kambona Oscar.
Mwaka 1977 wakati katiba hii inaandikwa yeye alikuwa wapi?
Wakati Nyerere anaitumia Katiba hii ya kijamaa na yeye kuwa Waziri Mkuu hakuiona hii Katiba?
Nyerere na Warioba walikuwepo wakati Rais Mwinyi na Mkapa wanatumia katiba hii mbona wote hawakushauri iandikwe katiba mpya ili kuingiza hayo anayotaka yawemo kenye Katiba?
Warioba alikuwepo wakati wa utawala wa Kikwete na Magufuli mbona hakuwalazimisha waandike Katiba mpya?.
Rais Magufuli alitamka wazi kuwa hataandika katiba mpya kwakuwa hakuahidi kuandika Katiba mpya wakati wa kampeni zake za urais, alimfanya nini?.
Angekuwa mimi ndiye Rais Samia ningeacha kuandika Katiba mpya kama vile walivyoshindwa/walivyoacha kuiandika akina Nyerere, Mwinyi, Mkapa, Kikwete na Maguli. Sababu kubwa zilizowafanya Nyerere, Mwinyi, Mkapa, Kikwete na magufuli kuacha kuandika katiba mpya ni moja tu, nayo ni hofu ya kuuvunja Muungano. Mama Samia asiipuuze hofu hii pia, ni kubwa na ipo dhahiri. Huyu Warioba tofauti na Nyerere, yeye anataka serikali tatu. Aliogopa kumshauri Nyerere, Mkapa na Magufuli lakini sasa anaona kuwa ni rahisi sana kwa Samia.
Aogopwe kama ukoma.