Naona sasa manabii wa uongo wanaanza kujionyesha. Wewe Luseleko unafikia wapi mpaka umfananishe Nyerere na hawa viongozi wa sasa? Au babu wa loliondo kaanza kukata mirija yako ya kiuchumi ndio unatafuta pa kutokea???
'Mzee wa Upako' ataka Kikwete asisemwe vibaya
Imeandikwa na Shadrack Sagati; Tarehe: 29th March 2011 @ 23:20 Imesomwa na watu: 54; Jumla ya maoni: 0
KIONGOZI wa Kanisa la Maombezi (GRC), Anthony Lusekelo, amewataka Watanzania waache tabia ya kumlaumu au kumsema vibaya Rais Jakaya Kikwete hadharani kwa kuwa vitendo hivyo vinamvunjia heshima kiongozi mkuu wa nchi.
Mchungaji Lusekeko maarufu kama Mzee wa Upako ameshauri viongozi wa dini na wanasiasa wafuate itifaki ya kuzungumza na rais kama ilivyokuwa zamani ili kudumisha utulivu wa nchi.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Dar es Salaam jana, Mchungaji Lusekelo alisema, kitendo cha kumlaumu Rais Kikwete hadharani ni kukosa heshima mbele ya kiongozi huyo na akatolea mfano kuwa dini zote zinakataza kumsuta kiongozi wako hadharani.
Alisema, Rais Kikwete amekuwa mtu wa kulaumiwa tu wakati kuna mengi mazuri anayofanya; lakini Watanzania hawayaoni badala yake wanasubiri siku amekufa ndiyo waanze kutoa sifa zake.
"Tuheshimiane tukiwa hai, tusisubiri kutoa sifa akiwa marehemu…hizi ni fikra za kishetani na hazipaswi kunyamaziwa," alisema Mchungaji Lusekelo.
Alitoa mfano kuwa wakati Mwalimu Julius Nyerere akiwa hai hakuwa na sifa zinazotolewa sasa na watu walisema kuwa wamechoka na unyerere. "Lakini leo hii tunamsifu kwa kila nderemo…watu wamebadilika wanasifu viongozi mpaka wanapotoka ndani ya madaraka," alisema Mchungaji Lusekelo.
"Inakuwaje Rais Kikwete tunayemfahamu aliingia madarakani akiitwa masia na chaguo la Mungu, leo hii ni adui wa kwanza…hivi sasa kukitokea tatizo kama kutonyesha mvua, basi lawama atatupiwa Rais Kikwete."
Mchungaji Lusekelo alisema, imejengeka tabia kuwa sasa ukimsema Rais Kikwete ndiyo unaonekana kuwa jasiri na mzalendo, kitendo alichosema ni utamaduni mbaya kwani hiyo inatokana na uungwana na uhuru alioutoa Rais mwenyewe.
"Uhuru usivuke mipaka hadi tunamvunjia heshima rais wetu," alisema Mzee wa Upako ambaye aliwataka Watanzania kumsaidia na kumtia moyo Rais Kikwete ili awatumikie kwa moyo. Alisema iwapo Watanzania watafanya hivyo Mungu ataendeleza nchi hii na itafika mbali.
Alitoa mfano wa mfumuko wa bei kuwa Watanzania wanamwonea Rais Kikwete kwa kumlaumu kuwa ndiye chanzo cha gharama za maisha kupanda kwani kilichosababisha mfumuko huo wa bei ni kupanda kwa mafuta kwenye soko la dunia.
"Hivi huu utamaduni wa kulaumu viongozi wanaotuongoza ambao unazidi kushamiri utaisha lini? Nchi hii ni sawa na gari, Rais Kikwete akiwa ndiye dereva; hivyo kitendo cha kutoa maneno ya kejeli kwake kinaweza kumchanganya na kujikuta akiliingiza gari katika shimo," alisema kiongozi huyo.
Alisema, wengi wanafikiri kuwa ukiwa Rais basi una moyo wa chuma, kumbe naye ni binadamu anahitaji imani ya Watanzania ili kutekeleza majukumu yake vizuri na yeye ajiridhishe katika kufanya maamuzi yake.
Source: Habari leo
'Mzee wa Upako' ataka Kikwete asisemwe vibaya
Imeandikwa na Shadrack Sagati; Tarehe: 29th March 2011 @ 23:20 Imesomwa na watu: 54; Jumla ya maoni: 0
KIONGOZI wa Kanisa la Maombezi (GRC), Anthony Lusekelo, amewataka Watanzania waache tabia ya kumlaumu au kumsema vibaya Rais Jakaya Kikwete hadharani kwa kuwa vitendo hivyo vinamvunjia heshima kiongozi mkuu wa nchi.
Mchungaji Lusekeko maarufu kama Mzee wa Upako ameshauri viongozi wa dini na wanasiasa wafuate itifaki ya kuzungumza na rais kama ilivyokuwa zamani ili kudumisha utulivu wa nchi.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Dar es Salaam jana, Mchungaji Lusekelo alisema, kitendo cha kumlaumu Rais Kikwete hadharani ni kukosa heshima mbele ya kiongozi huyo na akatolea mfano kuwa dini zote zinakataza kumsuta kiongozi wako hadharani.
Alisema, Rais Kikwete amekuwa mtu wa kulaumiwa tu wakati kuna mengi mazuri anayofanya; lakini Watanzania hawayaoni badala yake wanasubiri siku amekufa ndiyo waanze kutoa sifa zake.
"Tuheshimiane tukiwa hai, tusisubiri kutoa sifa akiwa marehemu…hizi ni fikra za kishetani na hazipaswi kunyamaziwa," alisema Mchungaji Lusekelo.
Alitoa mfano kuwa wakati Mwalimu Julius Nyerere akiwa hai hakuwa na sifa zinazotolewa sasa na watu walisema kuwa wamechoka na unyerere. "Lakini leo hii tunamsifu kwa kila nderemo…watu wamebadilika wanasifu viongozi mpaka wanapotoka ndani ya madaraka," alisema Mchungaji Lusekelo.
"Inakuwaje Rais Kikwete tunayemfahamu aliingia madarakani akiitwa masia na chaguo la Mungu, leo hii ni adui wa kwanza…hivi sasa kukitokea tatizo kama kutonyesha mvua, basi lawama atatupiwa Rais Kikwete."
Mchungaji Lusekelo alisema, imejengeka tabia kuwa sasa ukimsema Rais Kikwete ndiyo unaonekana kuwa jasiri na mzalendo, kitendo alichosema ni utamaduni mbaya kwani hiyo inatokana na uungwana na uhuru alioutoa Rais mwenyewe.
"Uhuru usivuke mipaka hadi tunamvunjia heshima rais wetu," alisema Mzee wa Upako ambaye aliwataka Watanzania kumsaidia na kumtia moyo Rais Kikwete ili awatumikie kwa moyo. Alisema iwapo Watanzania watafanya hivyo Mungu ataendeleza nchi hii na itafika mbali.
Alitoa mfano wa mfumuko wa bei kuwa Watanzania wanamwonea Rais Kikwete kwa kumlaumu kuwa ndiye chanzo cha gharama za maisha kupanda kwani kilichosababisha mfumuko huo wa bei ni kupanda kwa mafuta kwenye soko la dunia.
"Hivi huu utamaduni wa kulaumu viongozi wanaotuongoza ambao unazidi kushamiri utaisha lini? Nchi hii ni sawa na gari, Rais Kikwete akiwa ndiye dereva; hivyo kitendo cha kutoa maneno ya kejeli kwake kinaweza kumchanganya na kujikuta akiliingiza gari katika shimo," alisema kiongozi huyo.
Alisema, wengi wanafikiri kuwa ukiwa Rais basi una moyo wa chuma, kumbe naye ni binadamu anahitaji imani ya Watanzania ili kutekeleza majukumu yake vizuri na yeye ajiridhishe katika kufanya maamuzi yake.
Source: Habari leo