Mmekuja kwa staili hii ee! Ccm CCm! my Ass wala mcimtetee bwana enu! wenye akili wanaelewa wanaohusika na drugs traffickng& business kuwa ni wakubwa wa nchi hii na wenye kuheshimiwa ktk jamii, hapa namaanisha wanasiasa, wachungaji kama fulani, wasanii, na mamluki wengine, ni kondoo wa dad pekee wanaopingana na ukweli.
Kila siku Gwajima anatukana serikali je ni nani anamlinda??
Unaweza Kuona akina Mama Rwakatare na madawa ya kulevya wapo CCM na siku zote wana sifia Serikali Ukoo Wa Bwiga upo huko una sifia serikali ankina Prof Kapuya: Anaglia hapa ujue vizuri:
MAKOSA YA PROF. JUMA KAPUYA.
Bila kuathiri sharia ya Ubakaji, Prof Kapuya anaonekana na muogopa Binti huyo na kuashiria kuwa ni mzazi mwenzie na yapo mambo mazito ambayo Binti huyo anayajua dhidi ya KAPUYA. Wametajwa watu wengi kuwa wametapeliwa na Bint huyo lakini watu wote hao hakuna hata mmoja anayemouogopa Binti huyo kama anavyofanya Kapuya.Taarifa za Mitandao zinaonyesha kuwa Kapuya ametuma Zaidi ya Tshs 3,000,000 kwa kificho kwa madai kuwa anamsaidia ada mtoto huyo huku yeye Mwenyewe Kapuya anasema kuwa Mtoto huyo ni tapeli .Sasa hapa Kapuya anajichanganya. Ni kwa vipi mtoto huyo Kapuya aseme kuwa Mkubwa na mama mzima kabisa wa miaka 21 ,lakini wakati anatoa msaada wake anasema alikuwa anamulipia ada ya Shule sasa ni lini KAPUYA aligundua kuwa anatapeliwa??Ni lini Kapuya aligundua kuwa huyo ni mtu mzima sasa angesitisha malipo hayo??? Ni kwa nini Kapuya akubali kulipa pesa hiyo kwa Mkono badala ya kulipa moja kwa moja Shuleni ?? Ni kwa vipi waziri wa ulinzi anatapeliwa na Kahaba na kuuza utu na nchi??
(A) USHAHIDI YA MALIPO YA M-PESA KUTOKA SIMU YA KAPUYA (0755993930):
(1)
R93NY448 ImethibitishwaUmepokea Tsh505,000 kutoka kwa
JUMA KAPUYATarehe 21/6/13 saa 11:07 AM Salio lako la M-PESA ni Tsh 505,000
(2)
U26UG365. Imethibitishwa Umepokea Tsh 300,000 kutoka kwa JUMA KAPUYA
Tarehe 31/8/13 saa 3:28 PM Salio lako la M-PESA ni Tsh 300,000
(3) V04EU470 Imethibitishwa Umepokea Tsh 400,000kutoka kwa JUMA KAPUYA
Tarehe 24/9/13 saa 2:38 PM Salio lako la M-PESA ni Tsh 400,040
Malipo ya mwisho ya KAPUYA yamefanyika hadi tarehe 24/9/2013 wakati yeye mwenyewe Kapuya anasema kuwa amegundua kuwa Binti huyo ni mtu mzima na tapeli sasa ni kwa nini alikuwa analipa pesa kwa tapeli???
(B) UJUMBE WA VITISHO KUTOKA SIMU YA KAPUYA.
Simu 0784 993930 mali ya JUMA KAPUYA imekuwa ikitoa vitisho hasa baada ya mgogoro huu kufika kwenye media.
(i) Hata hivyo kufikia mwezi Februari mwaka huu 2013 , mtu asiyefahamika alienda nyumbani na kutelekeza gari aina ya T.199 BGY Mercedes Benzi ya Blue wakati wanafunzi hao wakiwa shuleni, kisha kuacha ufunguo kwa jirani yao kwa maelekezo kuwa wakifika awapatie.
Na Kapuya aliwapigia simu kuwaarifu kuwa amempa zawadi ya gari kwa ajili ya matumizi ila yeye na dada yake wanaruhusiwa kuuza ili wapate pesa kwa ajili ya mahitaji yake siku zilizosalia, kwani muda sio mrefu baada ya uchguzi mkuu 2015, Kapuya atakuwa Waziri Mkuu, hivyo itakuwa ngumu yeye kumtumia huyo binti pesa kama alivyoelekezwa na jeshi la polisi kituo cha Oysterbay.
Baada ya mwanafunzi huyo na dada yake ambaye ana umri wa miaka 20, kupewa gari walishindwa kulitumia hivyo kutoa taarifa polisi kwani kwa kupokea gari hilo ilikuwa ni kuwatelekeza kwani yeye hana hata hela ya kuweka mafuta ya gari, hivyo walienda polisi ili kesi ipelekwe mahakamani kumshtaki kapuya.
Polisi wa Oysterbay walikubali kulipeleka tatizo hilo kwa Katibu wa Bunge, ambaye alimwita mwanafunzi huyo na mdogo wake waende Dodoma kukutana na Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge ingawa walipofika Dodoma walikaa na kamati ya hiyo kwa maelezo kuwa Kapuya hakuwepo hadi Bunge lilipoisha walirejeshwa Dar es Salaam.
Mtoto huyo na dada yake alitoka ofisi za CCM lakini akiwa anaelekea kituo cha basi alithadharishwa na mwanafunzi mwingine kwa haraka kuwa akimbie kwa kuwa atamwagiwa tindikali na watu waliokuwa wanamfuata nyuma, alikimbilia katika mtaa wa Hoteli ya Star light kisha aliomba msaada baada ya kupotea njia na hivyo alisaidiwa na mama mmoja kufikishwa chumba cha habari cha Channel Ten. Mmoja wa watoto hao, alidai kuwa miongoni mwa vijana waliokuwa wanawatisha juzi walikuwa katika gari T170 BGY, Benz, Cream Metalic, ambayo inamilikiwa na KAPUYA.
Hapa inajieleza wazi kuwa vyombo vya dola kwa maana ya polisi wanafahamu jambo hili na kwamba sehemu ya polisi hawa wapo katika mfuko wa KAPUYA na hawa uwezo juu ya suala hili.
(ii) Alfajiri saa 11:21 kupitia simu yake ya mkononi yenye namba
0784993930, Profesa Kapuya alituma ujumbe ufuatao kwa mtoto huyo
: "chagueni kunisubiri tuje tuongee au mnataka kufa?"
Baadaye saa 1:07 asubuhi, alituma ujumbe mwingine kutoka simu hiyo hiyo kwenda kwa mtoto huyo, ukisema
: "Mkiuawa, itakuwa nzuri, itawapunguzia gharama za kuishi. Usitake kugombana na serikali, mtoto mdogo kama wewe. Sisi ndo wenye nchi yetu.
"
Mwambieni Mbowe mwenye hilo gazeti awape nyumba ya kuishi. Si mmemuingizia hela leo? Mnatumika bure watu wanaingiza hela nyingi, mmenitibua lazima niwauwe wiki hiii haitaisha, nitapanga kambi popote.
"
Jana si wamekuficha? Tuone kama utalindwa milele. Kazi ya kulindwa imeisha, maana wameshatengeneza hela. Lazima mvae sanda. Hilo sio ombi, ni wajibu wenu. Mnajitia mafia watoto sio? Watoto wetu wanauza unga, nani anawakamata? Nani atapigana nasi?"Ujumbe mwingine uliotumwa kwa mtoto huyo saa 11:2 3 ulisema:
"nimwakosea sana, acha nife mie nakunywa sumu nijiue, na nyie mje mnizike.", saa 5:17 usiku wa kuamkia jana alituma ujumbe usemao: "Si mpo Bilz? Sasa tupo pamoja na nyie mpaka usiku."Baadaye saa 5:31 alituma ujumbe huu: "Hivi hamkubali kushindwa? Leo ulifuata nini ofisi ya CCM?"
(iii) Huku akiendeleza vitisho vya kuwaua ikiwa binti huyo hatakubali, katika moja ya ujumbe wake, Kapuya alisema
: "Najua kesi ni watu wawili, sasa kwanini hamkubali? Hivi hela nitakayompa mtu akuue si bora nikupe uanze maisha?
"Wakili nimempa hela nyingi, magazeti pia nimewapa, naumia jamani, unaweza kukanusha taarifa hii na kufuta ushahidi halafu mimi nikupe hela uende popote, bungeni sifiki na nitafukuzwa, nyie mtapata nini?
"Nakupa masaa mpaka saa sita nitakuwa nimeshatuma hela, unachukua passport unasepa na hakuna kurudi, ukikaidi roho itakwenda kupumzika, unataka kufa kibudu? Jiangalie.
"Ukienda kwa DPP mwambie kuwa hutaki kesi, mimi niitwe, usipokubali nitakuua, yaani siku si nyingi, na hakuna wa kunifanya lolote, umeshasikia vifo vingapi, unataka kufa wakati huu au kwa ahadi ya Mungu?" alimwandikia ujumbe binti huyo.
Kapuya alizidi kumbembeleza binti huyo akimwomba afikirie namna alivyowasaidia kiasi cha kuwapa gari aina ya Benz, na kwamba hata kama amemwambukiza ukimwi, lakini atambue kuwa maisha hayana spea.
"Sikiliza nawaambieni, kwanini mnatumiwa, maana yake ni kuwa hao watu wa haki za binadamu hawawezi kuwapa hela…hebu tafakari nimetoa Benz, nimekupa ukimwi sawa, maisha hayana spea, mimi nitafungwa, wewe utapata nini? Mimi nina miaka 69 hata nikifa leo, nakubali kwenda popote hata kwa DPP tukae meza moja, najua nitafungwa tu."
Kwa mujibu wa mawasiliano yaliyonaswa na Tanzania Daima Jumatano, Kapuya hata hivyo ameendelea kutishia kumtoa roho binti huyo hasa baada ya kuona ushauri wake unagonga mwamba. Moja ya ujumbe uliotumwa kutoka katika namba hiyo unasomeka hivi
: "Nitakuua tu huwezi kukimbia milele, si hutaki kunisikiliza, kwani kesi ya Mahita ilikuwaje? Mbona anahudumia na hakuna wa kumfanya lolote, kuwa kimya uone, hujachelewa, kama hutaki lazima mimi na Hamis tukuue."
(iv) Uchunguzi wetu umebaini kuwa mara baada ya taarifa ya gazeti hili jana kuandika mwendelezo wa kashfa hiyo, huku likimkariri Waziri wa Ushirikiano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), Samuel Sitta, akihoji ukimya wa serikali katika kashfa hiyo, Profesa Kapuya alituma ujumbe mwingine wa kutishia kumuua binti huyo. Ujumbe huo kutoka simu namba 0784993930 inayomilikiwa na Kapuya kwenda kwa namba inayomilikiwa na binti huyo, unasomeka hivi:
"
Ni lazima nitakuua wewe na ndugu yako na atakaetaka kuwasaidia, huyo Samweli Sitta asijiingize kwenu, yaani nitakuua tena sijui leo mtalala wapi! We unadhani nani atakayenifunga? Ndo nishakupa ukimwi, sasa nakutaka uache mara moja kuongea na mtu, nitakuwinda popote tuone!"
MGOGONGANO WA POLISI JUU YA KESI YA KAPUYA.
Profesa Kapuya ambaye amewahi kushika nyadhifa kadhaa za uwaziri katika Serikali ya Awamu ya Tatu na Nne, tayari amefunguliwa jalada namba
OB/RB/21124/13 katika Kituo cha Polisi Oysterbay jijini Dar es Salaam, tangu Novemba 24 mwaka huu.Jalada hilo lilifunguliwa na mwanafunzi anayedai kubakwa na kutishiwa kuuawa, lakini Jeshi la Polisi limekuwa likishughulikia suala hilo katika namna ya kumlinda mtuhumiwa. Taarifa zinaonyesha kuwa polisi wamemfungulia
jalada la uchunguzi ambalo kwa kawaida hufunguliwa kama mtoa taarifa huwa ni msiri ili suala husika liweze kuchunguzwa na kupelelezwa kuthibitishwa kama ni la kweli au la ndipo malalamiko yapelekwe kwa Mkurungezi wa Mashtaka (DPP).
Kwa upande mwingine, jalada la malalamiko hufunguliwa kama mlalamikaji yupo na kinachohitajika ni polisi kuandika maelezo wakiyapeleka kwa DPP, ajiridhishe ili walalamikaji waweze kufika kutoa ushahidi wao mahakamani.Taarifa zimethibitisha kuwa Kapuya amefunguliwa jalada la uchunguzi ambapo kwa mujibu wa taratibu za kipolisi, wanaweza kusema wamechunguza na wamebaini kuwa suala husika halina ukweli wowote hivyo jalada laweza kutupiliwa mbali bila hata ya kulifikisha kwa DPP.Pia szipo taarifa kuwa kuna mawasiliano baina ya maofisa wa jeshi hilo kuanza kutofautiana huku wengine wakionya kuwa ikiwa suala hilo litachukuliwa kwa wepesi ili kumwepusha Kapuya asifikishwe mahakamani, laweza kuhamasisha raia kuichukia serikali na kuliona Jeshi la Polisi kuwa linalinda wahalifu hasa viongozi.Polisi walimwita msichana (Mwanafunzi) anayemlalamikia Kapuya na kumhoji awataje mashahidi watakaotoa ushahidi katika suala hilo endapo polisi wataamua kulipeleka suala hilo mahakamani jambo ambalo ni kinyume na taratibu za polisi.
MTOTO WA KAPUYA KATIKA TUHUMA ZA KUUA AMELINWA NA POLISI.
MTOTO wa Prof Kapuya aitwaye Baraka kapuya , anadaiwa kumuua mwanafunzi wa kiume kwa kumfyatulia risasi wakigombea msichana .
Habari za uhakika kutoka Tabora, zinasema kuwa tukio hilo lilitokea Novemba 28 ,2009 wakati wa Sikukuu ya Idd el Hajj katika ukumbi wa
starehe uliopo Kaliua, Tabora.
Taarifa zilionyesha kuwa tukio hilo lilitokea baada ya mtoto huyo wa waziri Kapuya kumkuta mwanafunzi huyo akiwa na msichana, ambaye pia ni mtoto wa shule, wakamgombania.
Katika tafrani hiyo ndipo Baraka Kapuya alipotoa bastola na kumfyatulia mwanafunzi huyo na kumuua hapo hapo.
Tarehe 22/12/2009 JESHI la Polisi limemsafisha
BARAKA KAPUYA (33) ambaye ni mtoto wa Waziri wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana, Profesa Juma Kapuya aliyedaiwa kuhusika na tuhuma za mauaji ya mwanafunzi wa kidato cha pili
, Majuto Luchamila (17) aliyeuawa kwa kupigwa risasi shingoni.Akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa habari kuhusu tukio hilo lililotokea mkoani Tabora hivi karibuni, Msemaji wa Jeshi la Polisi, Abdallah Mssika alisema uchunguzi uliofanywa na jeshi hilo umebaini kuwa mwanafunzi huyo aliuawa kwa kupigwa risasi shingoni na
mlinzi Mea Kajumulo (27) wa Kampuni ya Salu yenye makao makuu yake mkoani Shinyanga.
Mssika alisema wakati wa sherehe za Idd el Fitri Septemba 21, mwaka huu saa 7.30 usiku, kwenye ukumbi wa disko wa Hoteli ya Millenium, Kajumulo ambaye ni mlinzi wa jengo la hoteli hiyo alifyatua risasi na kisha kumjeruhi shingoni mwanafunzi huyo na baadae kufariki dunia. "Jeshi la Polisi tunatoa ufafanuzi kuhusu kifo cha kusikitisha kilichotokea mkoani Tabora cha mwanafunzi wa kidato cha pili katika Shule ya Sekondari ya Ushokora ya Kaliua wilayani Urambo kuwa mwanafunzi huyo hakupigwa risasi na Baraka Kapuya bali na mlinzi wa jengo hilo," alisema Mssika.
Alisema jengo hilo linamilikiwa na Profesa Kapuya ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Urambo Magharibi na kwamba hoteli hiyo inasimamiwa na Baraka ambaye ni mtoto wa waziri huyo.
Kwa mujibu wa Mssika, uchunguzi wa awali wa tukio hilo lilitokea wakati wa sikukuu ya Idd umebaini kuwa katika ukumbi huo kulikuwa na disko ndipo ilipotokea vurugu kati ya kundi la vijana waliokuwa wakimtaka binti mmoja ambaye hakujulikana jina lake, kurejesha fedha zao sh 20,000 ambazo ni gharama walizotumia wakati wa burudani hiyo pamoja naye.
Alisema vijana hao walifikia hatua ya kumtaka msichana huyo awarudishie kiasi hicho walichotumia kwa kuwa hakuwakubalia walipokuwa wakimtaka kimapenzi.
Mssika alisema wakati vijana hao wakimdai binti huyo fedha, ndipo alipoamua kukimbilia kwa mlinzi wa ukumbi huo kama njia ya kusalimisha maisha yake, lakini bado kundi la vijana hao liliendelea kumfuata na kumzonga na baadaye kumvamia mlinzi huyo kwenye lindo lake huku wakiwa katika hali ya vurugu.
Alisema mlinzi huyo alijaribu kuwazuia, lakini waliendelea kumzonga na katika purukushani hizo vijana hao walianza kumpora mlinzi silaha aliyokuwa nayo na kwa bahati mbaya risasi moja ilifyatuka na kumpiga mwanafunzi huyo shingoni na baadaye kupoteza maisha.
"Kwa taarifa za awali za uchunguzi zinaeleza kuwa mlinzi alijitahidi kuwazuia, lakini vijana hao hawakuelewa na kwamba mwanafunzi huyo alikuwa miongoni mwa vijana waliomvamia mlinzi siku ya tukio," alisema Mssika.
Katika ufafanuzi wake alisema mara tu baada ya tukio hilo, mlinzi huyo alibaini kufanya makosa na madhara yaliyotokea alikimbia kuondoka sehemu ya tukio na alikwenda nyumbani kwa mlinzi mwenzake ambaye hakuwa zamu siku hiyo na kumkabidhi silaha kabla ya yeye kutoroka.
Hata hivyo, alisema Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na polisi mkoani Shinyanga na mmiliki ya Kampuni ya ulinzi ya Salu walifanikiwa kumkamata na kumfikisha Polisi Tabora ambako alikiri kuhusika katika mauaji hayo na tayari alifikishwa mahakamani Septemba 28, mwaka huu.
Mssika alisema siku ya tukio kulitokea kundi kubwa la wananchi ambao waliamua kumtafuta Baraka kwa lengo la kutaka kulipiza kisasi, lakini hata hivyo baada ya kumkosa waliamua kuvunja vioo vya madirisha, milango, vyombo vya muziki na kupora mali mbalimbali zikiwemo baiskeli zaidi ya 50 zilizokuwa zimeegeshwa nje ya jengo hilo.
Vurugu hizo zilitulizwa na polisi wa kituo kidogo cha Kaliua walioomba msaada kutoka Urambo.Vile vile aliongeza kuwa uchunguzi wa Jeshi la Polisi haujapata ushahidi unaoonyesha ugomvi wa kimapenzi kati ya pande hizo mbili na kueleza kuwa silaha hiyo iliyotumika ipo mikononi mwa polisi.
Desemba 14 mwaka huu gazeti hili liliandika habari yenye kichwa cha habari ‘Mtoto wa waziri aua mwanafunzi' wakigombea msichana.
Vyanzo vya habari viliiambia Tanzania Daima kuwa tukio hilo lilitokea baada ya mtoto huyo wa waziri kumkuta mwanafunzi huyo akiwa na msichana, ambaye pia ni mtoto wa shule, wakamgombania.Katika tafrani hiyo, ndipo mtoto wa kigogo huyo alipotoa bastola na kumfyatulia mwanafunzi huyo na kumuua.Vyanzo hivyo vinasema kwamba ndugu wa marehemu, kwa kumwogopa waziri au kwa ushawishi wa ajabu wa mtoto wa waziri, waliamua kufanya mazishi kimya kimya bila ya kutoa taarifa polisi.
Aidha, inaelezwa kuwa msichana huyo kwa sasa ametoroshwa na kupelekwa kusikojulikana ili kuficha ukweli wa tukio hilo ambalo linaonekana kufanywa siri nzito.