Mzee Timothy Apiyo Afariki Dunia

Mzee Timothy Apiyo Afariki Dunia

Utashangaa sasa watu wanaenda kuuza sura kwake wakati walishindwa kumsaidia akiwa hai licha ya kuwa kiongozi mwandamizi mstaafu wa serikali. anyway labda Familia itaambulia angalau rambirambi.
 
The Boss, hicho ni kipindi cha nyuma sana. Serikali miaka mingi imempatia gari na msaidizi wa kudumu na kumsaidia katika matibabu. Hata gharama za matibabu ni serikali imekuwa ikimpatia. Last year or so alipewa gari nyingine mpya Discovery 4.

Kama mapungufu yapo ni ya kawaida.

Baada ya uhuru hatukuwa na mpango kamambe wa pensheni kwa wazee wetu. Lakini pia hakukuwa na utaratibu maalum wa kuwahudumia viongozi hao baada ya kusitaafu kwa maana ya utaratibu unaoongozwa na sheria za nchi. Ni busara tu za viongozi wa sasa kutoa msaada kwani hauko kwenye sheria.

Wengi walikuwa wazalendo na waadilifu wa hali ya juu, walitupenda na kuipenda nchi yao. Tunahitaji kujifunza kutokana na matukio haya na kuyaandaa maisha yetu na pia kutengeneza mpango mkakati wa kuleta mageuzi ya namna ya kuwahudumia wazee wetu waliolitumikia taifa letu zaidi ya nusu ya maisha yao wakiwa duniani.
 
Kulikuwa na madai ya Mzee Apiyo kutofautiana na Mwinyi mwaka hasa kuhusu teuzi mbalimbali alizokuwa akizifanya Mwinyi ambapo marehemu Mzee alikuwa anawasiliana na Mwalimu kabla ya uteuzi kuwa rasmi. Wapo waliodai kuwa hata Mwinyi alifikia kususa Ikulu na kurudi Zanzibar mpaka marehemu Mzee Thabit Kombo na Nyerere walipoingilia kati na Mzee Apiyo kustaafu rasmi.......in came Paul Rupia
 
NAKUMBUKA Mwalimu Nyerere alijengewa nyumba na Jeshi la wananchi kule butiama wakati wa ALLY HASSAN MWINYI. Hii ni ishara kwamba Wazee hawa walipigania uhuru ili sisi wa baadaye tuje tuishi vizuri zaidi. Kimsingi, kama MWINYI angeacha kumjengea Nyerere nyumba hiyo nadhani Nyerere ndiye angekuwa rais wa kwanza mstaafu Afrika anayeishi kwenye ile nyumba yake mbovu mithili ya tembe ( mviringo) iliyopo kijijini Butiama. Kama nakumbuka vema ina vyumba viwili tu na muonekano wa kale.

Wengi wanaotembelea butiama wakiambiwa kwamba ile ndiyo nyumba ya mwalimu baada ya kustaafu na kukaa Ikulu kwa miaka 23 wanatoa machozi na kushindwa kuamini.

WATANZANIA WENZANGU KUFA MASIKINI KWA VIONGOZI WETU HAO KUNATUPA FUNZO ZURI KWAMBA UONGOZI NI DHAMANA. JAMBO LA MSINGI TUWAENZI KWA JINSI WALIVYOJITOLEA BURE KUITUMIKIA NCHI YETU.

HATA TUNGEWAPA NYUMBA WANGEZIACHA DUNIANI LAKINI HISTORIA YAO ITABAKI NA SISI DAIMA KWA KAZI KUBWA WALIOFANYA.
 
APIYO ni mtu wa Musoma kwa Nyerere tulitegemea ndiye angefaidi zaidi matunda ya Nyerere wa kabila lake ( kwa maana ya kutoka mkoa mmoja).

Tunajifunza kuwa wenzetu walitanguliza mbele utanzania wetu kuliko ukabila, udini na hata ubaguzi wa rangi.

Kutoka Musoma kwake (APIYO) haikuwa tiketi ya kuishi maisha ya peponi bali kuitumikia nchi. Mwalimu yeyote mzuri anatakiwa kuishi maisha ya wanafunzi wake. Hawa wazee wameonyesha njia ya namna ya kujitolea kwa ajili ya nchi yetu bila kudai fidia au fadhila ama shukrani.
 
The Boss, hicho ni kipindi cha nyuma sana. Serikali miaka mingi imempatia gari na msaidizi wa kudumu na kumsaidia katika matibabu. Hata gharama za matibabu ni serikali imekuwa ikimpatia. Last year or so alipewa gari nyingine mpya Discovery 4.

Kama mapungufu yapo ni ya kawaida.

Kiongozi!

Naona imetoa PROMO ya kutosha katika hilo. Wewe ndio upo jikoni nini? R.I.P. Apiyo.
 
Last time nilisikia huyu mzee analalamika kutelekezwa na serikali
maisha yalikuwa magumu mno kwake...

Nakumbuka alikuwa anaongea kwenye redio anaelezea ni jinsi gani serikali imemtelekeza na mafao yake alikuwa anayapata kimgogorogogoro, nadhani baada ya yale malalamiko serikali ili respond better.
 
Sijawahi kumsoma kwenye kitabu chochote cha historia, si primary wala sekondari.

Historia ili iwe historia sio mpaka ipite kitabuni. kuna watu wanamfahamu Nelson Mandela ingawa hawajawahi kumsoma popote au kwenye darasa lolote bali ni kupitia masimulizi ya mdomo. Tujifunze kwamba historia ya kutukuka haiwezi kufa eti tu kwa sababu haikuandikwa popote. Hapo zamani za kale hapakuwepo na vitabu lakini kupitia simulizi kuwa binadamu wa kale tunawakumbuka hadi leo kutokana na kazi kubwa walioifanyia dunia. Kwa mantiki hii haina maana kuwa tusiandike historia la hasha ni njia nzuri zaidi ya kutunza kumbukumbu ingawa si njia pekee ya kufanya mtu akumbukwe kwa mema aliyowaachia binadamu wenzake.
 
NAKUMBUKA Mwalimu Nyerere alijengewa nyumba na Jeshi la wananchi kule butiama wakati wa ALLY HASSAN MWINYI. Hii ni ishara kwamba Wazee hawa walipigania uhuru ili sisi wa baadaye tuje tuishi vizuri zaidi. Kimsingi, kama MWINYI angeacha kumjengea Nyerere nyumba hiyo nadhani Nyerere ndiye angekuwa rais wa kwanza mstaafu Afrika anayeishi kwenye ile nyumba yake mbovu mithili ya tembe ( mviringo) iliyopo kijijini Butiama. Kama nakumbuka vema ina vyumba viwili tu na muonekano wa kale.

Wengi wanaotembelea butiama wakiambiwa kwamba ile ndiyo nyumba ya mwalimu baada ya kustaafu na kukaa Ikulu kwa miaka 23 wanatoa machozi na kushindwa kuamini.

WATANZANIA WENZANGU KUFA MASIKINI KWA VIONGOZI WETU HAO KUNATUPA FUNZO ZURI KWAMBA UONGOZI NI DHAMANA. JAMBO LA MSINGI TUWAENZI KWA JINSI WALIVYOJITOLEA BURE KUITUMIKIA NCHI YETU.

HATA TUNGEWAPA NYUMBA WANGEZIACHA DUNIANI LAKINI HISTORIA YAO ITABAKI NA SISI DAIMA KWA KAZI KUBWA WALIOFANYA.

Sasa ukitaka kujua hawa wa leo ni viongozi wa sampuli gani; tafadhali temebelea hapo Regent estate utakuta kasili la mkulu na baada ya hapo nenda kijijini Msoga huko Chalinze ukaone estate ya Vasco Dagama!!! Sina shaka utajua kuwa hawa wa leo sio viongozi wazalendo bali viongozi wezi!!!
 
Kiongozi!

Naona imetoa PROMO ya kutosha katika hilo. Wewe ndio upo jikoni nini? R.I.P. Apiyo.

Mkuu Selungo; ni wajibu wangu kama mtoa taarifa kufafanua lile ninalolifahamu kwa uwezo wangu. Namfahamu mzee na baadhi ya wanafamilia kwa kiasi fulani, japo si sana.
 
Last edited by a moderator:
Sasa ukitaka kujua hawa wa leo ni viongozi wa sampuli gani; tafadhali temebelea hapo Regent estate utakuta kasili la mkulu na baada ya hapo nenda kijijini Msoga huko Chalinze ukaone estate ya Vasco Dagama!!! Sina shaka utajua kuwa hawa wa leo sio viongozi wazalendo bali viongozi wezi!!!
.

Hitimisho la wizi linaweza kuhojiwa kwani ulimwengu wa sasa duniani pote viongozi hulipwa vizuri na wamewekewa utaratibu maalum wa kisheria wa maisha yao baada ya kustaafu ( upo kikatiba) na wawapo kazini. Wizi ni jambo moja baya na marupurupu kwa viongozi wengine ni jambo lingine kwani yanatosha kufanya mambo makubwa bila kuiba. ENZI ZA MWALIMU HAKUKUWA NA MPANGO HUU bali LENGO Ilikuwa ni kuweka misingi BORA ya kuijenga nchi kuelekea maisha bora kwa watakaofuata.
 
Wenzake wa umri huo wana majumba masaki , mikocheni na Mbezi beach...
Ukonga alifuata nini kama sio kukumbuka shuka asubuhi??????
01_11_0hte6m.jpg


IMG_9141.JPG


Apiyo.JPG

Ndugu zangu

Mzee Timoth Apiyo amefariki dunia usiku wa jana akiwa katika matibabu South Africa katika Hospitali ya Mill Park South Africa.

Serikali ikishirikiana kwa karibu na ubalozi wetu South Africa unafanya mipango ya kusafirisha mwili kuuleta Tanzania.

Msiba upo nyumbani kwake Sitaki Shari.

Poleni sana wafiwa; Clay; Slyvia pamoja na wanafamilia wote.

Bwana alitoa na Bwana ametwaa.

Rest in Peace Mzee Apiyo. You lived your life kwa uadilifu wa juu.
 
Ni habari ya huzuni. Taifa letu linapungukiwa na wazee waadilifu, waliotumikia/kuwajali watu na wachapakazi. Eeh Mungu uilaze roho yake pahala pema peponi. Ameni.
 
Back
Top Bottom