Mzee Timothy Apiyo Afariki Dunia

Kulikuwa na madai ya Mzee Apiyo kutofautiana na Mwinyi mwaka hasa kuhusu teuzi mbalimbali alizokuwa akizifanya Mwinyi ambapo marehemu Mzee alikuwa anawasiliana na Mwalimu kabla ya uteuzi kuwa rasmi. Wapo waliodai kuwa hata Mwinyi alifikia kususa Ikulu na kurudi Zanzibar mpaka marehemu Mzee Thabit Kombo na Nyerere walipoingilia kati na Mzee Apiyo kustaafu rasmi.......in came Paul Rupia

Wengine watasema hizi hata kama si tetesi hapa si mahala pake, hususan wakati huu wa msiba.

Wengine watasema ukweli ni muhimu zaidi ya yote, na obituary nzuri ya uongo ni kumtusi marehemu zaidi ya obituary mbaya ya ukweli .

Kwa wanaosema la kwanza nitawaomba samahani, ukweli utabaki Mzee Apiyo was a Nyerere man and this showdown did actually happen, and what Safari described is accurate, according to various reputable Ikulu insiders.

Pichani naona Pinda kaenda kumuona Mzee wake waliyefanya naye kazi Ikulu ya Nyerere zamani, na Mzee Apiyo kaweka heshima mbele kwa Waziri Mkuu wake.
 
Update 3: 14th June 2013


  1. Mwili utawasili leo saa moja jioni
  2. Utapelekwa nyumbani Sitakishari
  3. Kesho Jumamosi saa 2 last respect nyumbani kwake
  4. baada ya hapo utapelekwa karimjee Hall kwa last respect ya kitaifa. Public.
  5. Baada ya hapo mwili utasafirishwa kwa ndege kwende Musoma kwa maziko siku ya Jumapili.
 
RIP Timoth Apiyo au Baba IKU.

Hakika nimepata mshtuko mkubwa kusikia kifo cha Mzee wetu Apiyo. Kwa wengine ambaye tulifanyakazi naye kwa ukaribu sana tunamkumbuka namna alivyokuwa mchungu na mwenye uzalendo wa hali ya juu sana.

Nakumbuka mwanzoni mwa miaka ya 80's akiwa kule Majumba sita (Sitakashari njia ya kwenda Segerea Seminari) akiwa na majirani zake Mzee Brown Ngwirurupi (aliyekuwa Meneja mkuu Sigara TCC), Mzee Simbila aliyekuwa mmoja kati ya wakuu wa magereza, Balozi Mwasakafyuka, Mzee Timoth Apiyo (au wengi tulizoea kumwita baba IKU), Meneja wa TZ Fishernet Mzee Mwakipesile (aliyekuwa mkuu wa mkoa Mbeya na Mbunge wa Kyera), na kakaye Wasira. Hilo ndio eneo alilokuwa anaishi wakti huoo bila shaka sasa litakuwa limeendelea zaidi.

RIP baba IKU ( Mzee T Apiyo.
 
Back
Top Bottom