Mzee Mwanakijiji vs Waziri Abadallah Kigoda.

Mzee Mwanakijiji vs Waziri Abadallah Kigoda.

Gadizooooo!!! sijui hisia zangu zikoje kuweza kutajwa kwenye mstari mmoja na mtu ambaye amehusika sana ubinafsishaji wa raslimali zetu na ambaye amerudishwa tena kusimamia sekta hiyo hiyo - watu wakiamini kuwa anaweza kubadili msimamo wake. Upande mwingine mimi na Kigoda tumejenga urafiki mkubwa sana ambao wengi hawaujui na kwa wanaokumbuka tulishirikiana kufanikisha jambo moja la kifamilia kule Handeni - bila msaada wa Kigoda nisingeweza kufanikiwa kabisa kuunganisha ile familia.

Lakini, ni ulinganisho wa pande mbili - mimi kwama mtu wa kawaida, mwenye kudhauralika, na ambaye jamii inaniona mshamba - hence 'mwanakijiji' na wale ambao jamii inawaona ndio wenye nchi na wenye kustahili zaidi. Japo wengine wameona ni ulinganisha wa kazi ya mwandishi binafsi naona ni ulinganisho wa mchango wa kila mmoja wetu. Mada nzima ninavyoiona mimi ni kuwa wapo watu wengi wanaotoa mchango katika jamii yetu kwa nafasi walizonao na labda wakati mwingine wanaonekana kujitolea zaidi kufanya mambo hayo kuliko wale ambao waliomba kazi na kuajiriwa kulipwa mshahara kufanya kazi hizo!! this to me is the paradox. Iweje mtu aliyeomba kazi (akachaguliwa au kuteuliawa) anapewa posho, na mishahara minono aonekane anafanya madudu na mtu mwingine anayejitolea anaonekana ana uchungu zaidi na kazi hiyo?

Tumeona kina mama na vijana, wake kwa waume wakifanya mambo mbalimbali katika jamii zao na wengine wakiendeleza harakati za mabadiliko. Wapo ambao ni mashujaa wasiotajwa ambao huko maofisini wameona madudu na wakayaibua na sifa ikawaendea wana siasa wa kuchaguliwa. Jibu laweza pia kuwa rahisi - hawa wanaojitolea hawastahili kudai lolote (iwe fidia au tuzo) kwani wanafanya kutoka kwenye mioyo yao; bila kuombwa au kulazimishwa. Hili ndilo pia tishio kubwa dhidi yao - mtu ambaye anafanya kazi kwa kujitolea utamkataza vipi wakati hujamuajiri, humlipi na wala humgharimii kwa vyovyote? Well, mtu huyo ANAKUWA NA NGUVU kuliko wale wanaolipwa na kuajiriwa kufanya mambo kwani hawa wanafanya mambo wakifikiria matokeo yake. Siyo kwamba hawawezi kufanya wanayofanya "kina mwanakijiji" bali wanafikiria wakifanya zaidi wataitwa na kukaripiwa, watatishiwa ajira zao na labda watanyanyaswa kwa namna moja au nyingine...

Inafikirisha sana....

Mzee mwenzangu mwanakijiji naomba nikupe mfano huu, "mtoto analelewa na wazazi na walezi wengine lakini huyo mtoto akiharibu atanyooshewa kidole mzazi mara hili mara lile, vivyovivyo na akitenda baya, sababu mzazi ndio decision maker wake hata kama yule mzazi alikuwa anamuongoza vibaya na majirani wakamrekebisha mtoto akawa na tabia njema sifa itarudi kwa mzazi"

Narudi kwako Mzee mwenzangu ukitaka posho na heshima za kiuwaziri nenda jimboni kwako gombea wakuchague sisi tulio majimbo mengine tupambane na changamoto kwa pamoja ndio uiano huo utakuwepo.

Kumbuka ukiwa icon mabaya yako na mazuri yako yote yataonekana, tutakupima kwahilo zaidi ya hapo embu jifananishe na watumia kalamu wenzako muone kwanini Michuzi ni maarufu au anamarupurupu zaidi yako wakati yeye ni std7 with camera professional na leo yuko Ikulu. Heshima mkuu na jamani wale wenzangu karibuni kesho Jangwani
 
Sijaelewa hapa. Yani unataka Mwanakijiji, mwandishi wa kujitegemea alipwe sawa na waziri? Ivi unajua maana ya kuwa waziri wewe? Wewe unaona kabisa kazi zao zinalingana? kazi kweli kweli! Mwisho mtadai mbeba matofali katika ujenzi alipwe sawa na mchora ramani ya jengo hilo linalojengwa!
 
Je, kutoa posho kwa waandishi lazima iwe hongo? Jibu ni Hapana. Waandishi kama watu wengine nao wana mahitaji ya kawaida kama wanasiasa. Nchi hii ni yetu sote.
Mkuu Aweda, suala la posho kwa waandishi ni suala tete, mimi nimeshalipigania sana humu kuwa kama washiriki wa mkutano, warsha, semina, vikao au makongamano, wanastahili sitting allowance, lunch na transport na huwa zinalipwa, why not waandishi wasilipwe?!.

Kwa waandishi rushwa ni pale anapopokea chochote ili aandike, au kufungwa mdomo ili asiandike!.

Maoni ya waandishi kwenye katiba mpya yatapokelewa kama maoni ya wananchi wengine wowote, nothing special kuhusu maoni ya waandishi habari.
 
kumbe tunaongea na mafyatu,unajisifia et?....mlala heri!...una nin?....sikusikii vizuri hvyo vyeti vyako vichafu vya kununu vya IT ndio unajiona maisha umeyamaliza!we dogo jiangalie sana wewe,huwa na kutahadhalisha sana,jiangalie we dogo.....ohooo!!

Nimesoma IT kabla haijaitwa IT, way back in 1982, ulikuwa umeshazaliwa?
 
Mkuu Aweda, suala la posho kwa waandishi ni suala tete, mimi nimeshalipigania sana humu kuwa kama washiriki wa mkutano, warsha, semina, vikao au makongamano, wanastahili sitting allowance, lunch na transport na huwa zinalipwa, why not waandishi wasilipwe?!.

Kwa waandishi rushwa ni pale anapopokea chochote ili aandike, au kufungwa mdomo ili asiandike!.

Maoni ya waandishi kwenye katiba mpya yatapokelewa kama maoni ya wananchi wengine wowote, nothing special kuhusu maoni ya waandishi habari.

Wamezowea vibahasha. Kama unabisha muulize Pasco wa JF.
 
mada ni nzuri ila sijaona uwiano wa kuwafananisha hawa watu wawili. Ninachoona hapa ni kiwa mleta mada anadhani mwanakijiji ni muanzilishi wa jf. Sio hivyo. Kadhalika sijaona kwa nini kigoda aingie hapa. Hata kama ni mifano kuna taratibu zake. Mada ni jema sana tu
 
Mchukulie mzee mwanakijiji kama mwandishi makini na msomi anayetumia akili yake aliyojaliwa na mwenyenzi Mungu kufikiri juu ya nchi yake na kuziandika fikra hizo ktk mitandao ya kijamii na magazetini. Mwanakijiji ni mwakilishi wa waandishi wote wazuri wa habari akiwepo wewe wa JF. Mchukulie waziri Abdallah Kigoda, waziri wa viwanda na biashara kama mwakilshi wa mawaziri na watumishi wote wa Serikali.

Wote hawa ( Mwanakijiji na Kigoda) ni watanzania na wana haki sawa, wote wanawatumikia watanzania kwa nia njema ya kusukuma guruduma la maendeleo mbele. Mmoja analipwa mshahara, posho, gari, mkopo wa mil 90 ( kama mbunge nk ) mwingine (mwanakijiji) hana vyote hivyo. Kwanini? jibu, ndivyo ilivyo.

Wote wawili wanatumia akili, wote wawili wanawatumikia watz, wote wanatumia muda wao kufanya kazi moja ya kujenga nyumba moja TZ, Wote wamesomeshwa na kodi zetu na wote ni watanzania. Tafauti za nini kati yao? Jibu ndivyo ilivyo.

Kati yao hakuna mwenye haki ya uraia zaidi ya mwingine na kazi zao zina tija sawa. Pengine mwanakijiji anaweza kuwa bora kuliko baadhi ya mawaziri ambao hata watz waliowengi hawawajui hata kwa majina. Kwa nini tofauti kwenye masilahi baina yao? Jibu, ndivyo ilivyo.

Kwanini inapofika kwenye maslahi (Mishahara, posho, mikopo na magari) tunabaguana? Je, kwa nini michango ya hawa watz wawili inaheshima tofauti sana mbele ya Serikali? ndivyo ilivyo.

Au Je, kwa kuwa mmoja cheo chake kinatangazwa redioni na kwenye vyombo vya habari na Rais ndio sababu ya kuwa na maslahi zaidi? Je, waziri wa habari naye angepewa Jukumu la kutangaza waandishi wa habari wenye vigezo fulani elimu nk, wangeweza kuwa na sifa ya kupata hayo maslahi ya watumishi wengine? Au je, tija ya waandishi ni ndogo sana kuliko hawa mawaziri wanaopata maslahi? Je, ni watu wanagapi wanasoma makala za mwanakijiji na kufunguka? Kwa nini imekuwa hivi?

Kwenye nchi za wenzetu, vyombo vya habari inakaribia kuwa mhimili wa nne wa dola, kwetu sisi hata shukrani hamna. Kwanini? ndivyo ilivyo.

Je, hii ni sawa? Je, tunawezaje kuliweka jambo hili vizuri ktk katiba mpya? Hivi huyu mtanzania aliyetumia akili yake kuanzisha JF ambayo imekuwa msaada sana hakustahili maslahi hayo anayopata Abadallah Kigoda?

Jibu la wengi ni, hivyo ndivyo ilivyo. Kwa maoni yangu si kila jambo lilivyo, ndivyo inavyopaswa kuwa, mengine NDIVYO ILIVYO LAKINI SIVYO INAVYOTAKIWA KUWA. Inawezekana Kinyume chake pia ni nzuri zaidi.


Kwa maoni yangu bado unafikiria kimaskini na kimaslahi zaidi. Wewe kam mwandishi ingekuwa vyema kama hoja yako ingelenga maendeleo ya nchi kwa ujumla, kwa maana ya kupunguza tofauti za umaskini wa walio wengi (Gin coeficient). Kuto kunagalia kwa upana mfumo wa maendeleo ya Tz kumeondoa uhalisia wa mada yako kwa mtanzania.

Asilimia 80 ya wtz tuko vijijini tunahangaika ila kupata mavuno mengi nakusali/kuomba dua mvua zije za kutosha ili mavuno yamwe mazuri. Mavuno yakija mengi utasikia usiuze nje ya wilaya/mkoa/nchi hivyo kufanya bei ya mazo ya mkulima kuwa ya chini. Wakati huo bei za bidhaa nyingine zinapanda bila mipaka je hii ni sawa. Nadhani ili kuweka usawa wakulima pia waruhusiwe kuuza mazo yao wanakopenda.

So please hoja yako mimi naona inajikita zaidi kwenye ubinafsi wa sekta yako. Halafu maendeleo hayaji kwa posho.
 
Nimesoma IT kabla haijaitwa IT, way back in 1982, ulikuwa umeshazaliwa?
Kwenye IT hamna experiance wewe Pambaf!!!!!! Aliyesoma Windows NT server na aliyesoma windows 2008 server aliye juu ni huyu wa 2008 sasa wewe ni outdated vibaya mno Pambaf mkubwa wewe nilikuwa nakuamini kumbe wewe gamba kuliko Mzee wa gombe
 
Mkuu Aweda, suala la posho kwa waandishi ni suala tete, mimi nimeshalipigania sana humu kuwa kama washiriki wa mkutano, warsha, semina, vikao au makongamano, wanastahili sitting allowance, lunch na transport na huwa zinalipwa, why not waandishi wasilipwe?!.

Kwa waandishi rushwa ni pale anapopokea chochote ili aandike, au kufungwa mdomo ili asiandike!.

Maoni ya waandishi kwenye katiba mpya yatapokelewa kama maoni ya wananchi wengine wowote, nothing special kuhusu maoni ya waandishi habari.

pasco kwa bahasha humtoi.!
 
Mkuu Michael unataka waandishi walipwe na serikali? Hii huoni itakuwa hatari kwa uhuru wao? Hivi unadhani Dailynews na Habari leo hakuna waandishi mahiri? Mimi najua kwamba kuna waandishi mahiri akina Kulangwa lakini unaona wanachokiandika? Unakikubali?

Katika nchi yoyote lazima hawa watu kama akina Mwanakijiji wawepo wakiwa wanafany kazi bila kulipwa na serikali ili wawe huru kutoa mawazo yao. Hawa huitwa wanaharakati.
 
aweda,

huwezi fananisha nanasi na ndizi.

Mwanakijiji kumfananisha na abdallah kigoda ni kama kufananisha mbingu na ardhi.

nini cha maana na cha akili alichofanya mwanakijiji zaidi ya majungu na fitna za mitandaoni?

Abdallah kigoda on the other hand, ni mmoja katika watu mahiri sana na "he is a born leader".

khaaa!! We jamaa kweli akili zako ndembendembe
 
mada ni nzuri ila sijaona uwiano wa kuwafananisha hawa watu wawili. Ninachoona hapa ni kiwa mleta mada anadhani mwanakijiji ni muanzilishi wa jf. Sio hivyo. Kadhalika sijaona kwa nini kigoda aingie hapa. Hata kama ni mifano kuna taratibu zake. Mada ni jema sana tu


umeongea point mno
Kigoda sio opposite ya Mwanakijiji
Kigoda ni mtu makini.mchapakazi hata kama sio perfect
kumuweka katika article hii sio kumtendea haki
 
Mie kigoda namfagilia sana, hasa pale aliponing'olea ekelege. Big up mgoshi!
 
Kama inawezekana na kama tunakubaliana kuwa Kigoda na mwanakijiji wanatoa mchango kwa wananchi basi walipwe wote. Kama haiwezekani kuwalipa wote basi hata kutambua mchango wa huyo ambaye tumeshindwa kumlipa ni muhimu. Tatizo ni kwamba waandishi hawalipwi na hawaheshimiki wakati ni fani muhimu sana. Ikumbukwe hapa tunajadili zaidi ya mwanakjijij na Kigoda.
Na swali la pili ni je, kwa kuwa tunaandika katiba mpya, je kuna haja ya kutambua mchango wa hao waandishi wa habari? Je, kama taifa hatuwezi?

Kama ni hivyo ungembambanisha MM na Waziri wa habari, nadhani ingeleta maana zaidi na uelewa pia. Mtu aweza kuuliza kwa nini umemchagua A Kigoda?
 
umeongea point mno
Kigoda sio opposite ya Mwanakijiji
Kigoda ni mtu makini.mchapakazi hata kama sio perfect
kumuweka katika article hii sio kumtendea haki

Hakika, angalau kama angemtumia Waziri wa Habari Ingefana zaidi.
 
Wamezowea vibahasha. Kama unabisha muulize Pasco wa JF.
Kwa vile nilikuwa mwandishi wa habari nikifanya kazi newsroom for 10 good years hivyo nafahamu plight ya waandishi wa habari.

Bahasha ninazozitetea mimi ni zile za stahili zao!. Kwa taarifa yako mpaka Ikulu wanakata bahasha!. Tena sisi ni umasikini tuu wa serikali yetu, Ikulu ilitakiwa kuwa na waandishi wafuatao.
1. Press Secretary wa rais/ Presidential Spokes person. ( Salva)
2. Ass. PS (Premmy)
3. Presidential Producer ( hatuna)
4. Presidential Reporter (Hatuna)
5. Presidential Photographer(Michuzi/Maro)
6. Presidential Videographer (hatuna)
7. Presidential Sondman ( hatuna)
9. Presidential Presenter (hatuna)
10Presidential Editor (hatuna)

Kila rais akisafiri lazima asafiri na watu hao na kwa vile kwenye timu ya rais hatuna hao watu, Ikulu inalazimika kutoa bahasha nene kuwaazima watu hao toka vyombo vya habari vya umma na binafsi!.

Kuna mada nilisema sio kila bahasha za waandishi ni rushwa!. Bahasha nyingine ni za logistic na facilitation na ndizo ninazozitetea mpaka mwisho!.

Jee mnaijua ni nchi gani inachukia sana rushwa kuliko nchi nyingine yoyote?. Ni China!. Ukishikwa na rushwa, unanyongwa!. Jee mnajua ni shirika gani la habari ambalo ni kubwa kuliko yote duniani?. Ni Xhinua la China limepeleka waandishi wake nchi zote duniani!. Kwa nini mashirika mengine hayana waandishi nchi zote?. Ni mambo tuu ya bahasha!. Hii inamaanisha China ndio nchi inayoongoza kwa kukata bahasha za waandishi!. Bahasha zote za waandishi zingekuwa ni rushwa, basi China isingekata!.

Hivi wangapi wanaelewa haki ya kupata habari ni haki yao ya msingi?. Jee mnafahamu kila kitongoji, kila kijiji, kila wilaya, kila mkoa, kila taasisi ilipaswa kuwa na ofisa habari mwenye jukumu la kutoa habari ili kuwapatia Watanzania haki yao ya msingi ya right to information. Jee ni kwa nini watu hawa hawapo?, ni mambo ya bahasha, hawana bahasha za kuwalipa!.

Nachukia rushwa kwa moyo wangu wote lakini natetea bahasha ambazo sio rushwa kwa nguvu zangu zote!.

Pasco
 
pasco kwa bahasha humtoi.!
Idawa ni kweli kwa asilimia 100% mimi Pasco wa jf kwa bahasha stahiki, hunitoi!. Nimeshazivuta sana nilipokuwa reporter na sasa mimi ndio msambazaji wa bahasha hizo kama mwezeshaji!.
 
Muongozo Mbovu. Rasimu mbovu. Itazalisha katiba iliyojaa matapishi na mbovu kuliko zote hapa duniani.
 
Suala la mfumo wa utawala hutegemea pai utamaduni wa wananchi juu ya kuihoji serikaliyao. Mfano USA vyombo vya habari vipo juu ya rais, na mahakama ipo juu ya rais. Nadhani kuna umuhimu wa kuliweka kwenye katiba


Ng'wanakidiku hapa umeongeza maneno na kubadilisha maana nzima ya uchangiaji. Kwa msaada zaidi, Marekani na kwingineko kwenye demokrasia iliyopevuka mihimili mikuu ya nchi (serikali, bunge, mahakama) utendaji wake hauingiliwi katika maamuzi yake kisheria. Vyombo vya habari haviko juu ya rais, bali uhamasisho(influence) wake kwa jamii ni mkubwa ambapo Raisi inabidi avitegemee sana katika utendaji wake ili ujumbe wake uiwifikie jamii katika hali chanya.
 
Back
Top Bottom