Mzee Mwanakijiji vs Waziri Abadallah Kigoda.

Usitegemee, wala usitarajia kuwa itaandikwa katiba itakayotoa usawa kati ya watawala na watawaliwa, never...
MKUU katiba ya Kenya ni nzuri sana, Usikate tamaa we still have the chance.
 
mwanakijiji anaitaji pongezi .pöngezi zetu za kutoka moyoni ni fadhila tosha zaidi ya hongo wanayopewa mawaziri wetu.

Je, kutoa posho kwa waandishi lazima iwe hongo? Jibu ni Hapana. Waandishi kama watu wengine nao wana mahitaji ya kawaida kama wanasiasa. Nchi hii ni yetu sote.
 
Pole sana Comrade kumbe hata kwenye mwanga huu wa jua bado upo gizani kwa nini huiishi kuwatumikia watu badirika ndugu yangu utatumwa mpaka lini huuni ufahari wa wewe nawe kuwatuma watu:
Niko tayari

Hapo nilipokuwekea nyekundu badilisha, inaonesha kuwa Kiswahili chako ni cha manati.

Nashkuru Mungu kukufahamisha kuwa sijawahi kuwa mlala hoi wala mlala hai nimezaliwa nikiwa mlala heri na mpaka leo ni mlala heri. Naajiri toka nimezaliwa AlhamduliLllah.
 
Suala la mfumo wa utawala hutegemea pai utamaduni wa wananchi juu ya kuihoji serikaliyao. Mfano USA vyombo vya habari vipo juu ya rais, na mahakama ipo juu ya rais. Nadhani kuna umuhimu wa kuliweka kwenye katiba

Mkuu tuko pamoja.
Baadhi ya tamaduni zetu nzuri lazima tuzilinde na kuziendeleza. Jambo la muhimu hapa ni kuwa si kila utamaduni wetu ni mzuri.
Utamaduni wetu kuhusu waandishi ndivyo ulivyo ( waandishi wa habari hawalipwi) Je, ndivyo tunavyotakiwa tuendelee kuwa?
 
Kwa maoni yangu kuna haja ya kuliangalia hili la tasnia ya habari,isichukuliwe kama sehemu ya kuanzdika umbea wa fulani kafumania au kufumaniwa,na nikienda specifically kazi za mwanakijiji zinanifanya nifikiri sana in parteining alichokileta Aweda.
na kwa wale mnaolinganisha mbingu na ardhi kati ya Mwanakijiji na anaofanana nao katika kuelimisha umma,ku-impart knowledge vichwani mwa watu,kuwa-emancipate watu kifikra,sina budi kusema Mwanakijiji yuko juu zaidi ya Kigoda Abdala.
you people think twice!
 
Jamani hapa tusikae kishabiki bila mantiki, wekeni CV ya mwanakijiji na ya Kigoda ndo tujadili. Alafu huyu mwanakijiji ninani hasa na je anajulikana na wangapi? Embu tujadili kiakili tutoe itikadi zetu, maana nyie mnaomtetea inawezekana mnamjua tangia zamani lakini sisi wengine tumemuonea JF. Na angekuwa anajitambua na kujiheshimu angeachana na nickname akaweka jina kamili. Kwakweli hapa namfananisha na msanii maana ili atoke kwakutojiamini anatumia jina lenye swaga kibao.
 
Mchukulie mzee mwanakijiji kama mwandishi makini na msomi anayetumia akili yake aliyojaliwa na mwenyenzi Mungu kufikiri juu ya nchi yake na kuziandika fikra hizo ktk mitandao ya kijamii na magazetini. Mwanakijiji ni mwakilishi wa waandishi wote wazuri wa habari akiwepo wewe wa JF. Mchukulie waziri Abdallah Kigoda, waziri wa viwanda na biashara kama mwakilshi wa mawaziri na watumishi wote wa Serikali.

Wote hawa ( Mwanakijiji na Kigoda) ni watanzania na wana haki sawa, wote wanawatumikia watanzania kwa nia njema ya kusukuma guruduma la maendeleo mbele. Mmoja analipwa mshahara, posho, gari, mkopo wa mil 90 ( kama mbunge nk ) mwingine (mwanakijiji) hana vyote hivyo. Kwanini? jibu, ndivyo ilivyo.

Wote wawili wanatumia akili, wote wawili wanawatumikia watz, wote wanatumia muda wao kufanya kazi moja ya kujenga nyumba moja TZ, Wote wamesomeshwa na kodi zetu na wote ni watanzania. Tafauti za nini kati yao? Jibu ndivyo ilivyo.

Kati yao hakuna mwenye haki ya uraia zaidi ya mwingine na kazi zao zina tija sawa. Pengine mwanakijiji anaweza kuwa bora kuliko baadhi ya mawaziri ambao hata watz waliowengi hawawajui hata kwa majina. Kwa nini tofauti kwenye masilahi baina yao? Jibu, ndivyo ilivyo.

Kwanini inapofika kwenye maslahi (Mishahara, posho, mikopo na magari) tunabaguana? Je, kwa nini michango ya hawa watz wawili inaheshima tofauti sana mbele ya Serikali? ndivyo ilivyo.

Au Je, kwa kuwa mmoja cheo chake kinatangazwa redioni na kwenye vyombo vya habari na Rais ndio sababu ya kuwa na maslahi zaidi? Je, waziri wa habari naye angepewa Jukumu la kutangaza waandishi wa habari wenye vigezo fulani elimu nk, wangeweza kuwa na sifa ya kupata hayo maslahi ya watumishi wengine? Au je, tija ya waandishi ni ndogo sana kuliko hawa mawaziri wanaopata maslahi? Je, ni watu wanagapi wanasoma makala za mwanakijiji na kufunguka? Kwa nini imekuwa hivi?

Kwenye nchi za wenzetu, vyombo vya habari inakaribia kuwa mhimili wa nne wa dola, kwetu sisi hata shukrani hamna. Kwanini? ndivyo ilivyo.

Je, hii ni sawa? Je, tunawezaje kuliweka jambo hili vizuri ktk katiba mpya? Hivi huyu mtanzania aliyetumia akili yake kuanzisha JF ambayo imekuwa msaada sana hakustahili maslahi hayo anayopata Abadallah Kigoda?

Jibu la wengi ni, hivyo ndivyo ilivyo. Kwa maoni yangu si kila jambo lilivyo, ndivyo inavyopaswa kuwa, mengine NDIVYO ILIVYO LAKINI SIVYO INAVYOTAKIWA KUWA. Inawezekana Kinyume chake pia ni nzuri zaidi.
Mkuu we una wivu,majungu na unafiki.samahani lakini kwa maneno hayo.Hivi tangu lini watu wakafanana kimaisha au kipato?yaani umefananisha vitu viwili tofauti nafikiri hapo ungefananisha huyo Mzee Mwanakijiji na Mh.Mbowe na Dr.Slaa lakini ufananisho wako ni wa majungu na chuki binafsi.Nina hakika we una tofauti kubwa ya kipato,posho na mengineyo na katibu kata wako wa chama chako hilo hujaliona.Ni kweli Mzee mwanakijiji ana mchango mkubwa wa kimawazo ktk jamii tena inaonesha ni mahiri katika fani yake lakini ni wangapi wanamfahamu au kufaidika na mawazo yake ambayo mara nyingi yapo kwenye magazeti na mitandao? Mara nyingi makala zake zipo biased anapendelea sana CDM na ndiyo maana we umepata msukumo wa kumsifu hapa.Tafakari kwanza then utoe vitu vinavyofanana uzito.Hivyo ndivyo ilivyo mkuu.
 
Mkuu we una wivu,majungu na unafiki.samahani lakini kwa maneno hayo.Hivi tangu lini watu wakafanana kimaisha au kipato?yaani umefananisha vitu viwili tofauti nafikiri hapo ungefananisha huyo Mzee Mwanakijiji na Mh.Mbowe na Dr.Slaa lakini ufananisho wako ni wa majungu na chuki binafsi.Nina hakika we una tofauti kubwa ya kipato,posho na mengineyo na katibu kata wako wa chama chako hilo hujaliona.Ni kweli Mzee mwanakijiji ana mchango mkubwa wa kimawazo ktk jamii tena inaonesha ni mahiri katika fani yake lakini ni wangapi wanamfahamu au kufaidika na mawazo yake ambayo mara nyingi yapo kwenye magazeti na mitandao? Mara nyingi makala zake zipo biased anapendelea sana CDM na ndiyo maana we umepata msukumo wa kumsifu hapa.Tafakari kwanza then utoe vitu vinavyofanana uzito.Hivyo ndivyo ilivyo mkuu.

Wakurogwa,
Nadhani hujanielewa hata kidogo. Mimi sijasema kwamba Mwanakijiji au waandishi wa habari walipwe mishahara na posho sawa sawa na wabunge, mikopo mil 90 nk. Hapana. Inafahamika kuwa ktk nchi hii kila mtu analipwa mshahara kulingana na kazi anayofanya na ngazi aliyopo. mwl mkuu wa shule na mfanya usafi hawalipwi sawa. Swali ni je, ngazi ya waandishi wa habari kwa ujumla wao ndani ya nchi iko wapi? Na je, waandishi wa habari hawana mchango ktk taifa hili? kama wabunge, walimu na madaktari tunawalipa vipi kuhusu wao?
 
Kama issue ni kuwatetea wanahabari embu tuanze na mtiririko wa background ya huyo mwanahabari. Alipomaliza form 4 akaenda wapi au kipi kilifuata maana kuna house made aliona wife wa bosi wake kanunuliwa nguo nzuri na yeye akaletewa ya kawaida akaanza kunong'ona eti mimi naamka saa kumi nafanya kazi zote yeye anaamka saa tatu hana analolifanya ndo anapata kizuri. Jamani unapokuwa ngazi ya juu wewe ni decision maker, siye wachini tutatumika mpaka position ndio itakayokuokoa. Naomba tufunge mjadala maana tutachukiana bure ingawa ndo ukweli wenyewe
 
Jamani hapa tusikae kishabiki bila mantiki, wekeni CV ya mwanakijiji na ya Kigoda ndo tujadili. Alafu huyu mwanakijiji ninani hasa na je anajulikana na wangapi? Embu tujadili kiakili tutoe itikadi zetu, maana nyie mnaomtetea inawezekana mnamjua tangia zamani lakini sisi wengine tumemuonea JF. Na angekuwa anajitambua na kujiheshimu angeachana na nickname akaweka jina kamili. Kwakweli hapa namfananisha na msanii maana ili atoke kwakutojiamini anatumia jina lenye swaga kibao.

Mkuu wewe unaitwa nani? pwito? Mbona hujaweka majina yako yote matatu kikamilifu?
Kama wewe unataka tujadili maoni yako wakati hutumii majina yako halisi kwa nini unataka tusiheshimu maoni ya huyu mpambanaji mwakijiji? Hoja ni hoja aliyotoa wala siyo sura yake AU kimo chake.
 
Aweda,

Huwezi fananisha nanasi na ndizi.

Mwanakijiji kumfananisha na Abdallah Kigoda ni kama kufananisha Mbingu na Ardhi.

Nini cha maana na cha akili alichofanya Mwanakijiji zaidi ya majungu na fitna za mitandaoni?

Abdallah Kigoda on the other hand, ni mmoja katika watu mahiri sana na "he is a born leader".

Jamani ni nini kilichopo kwenye vichwa vya hawa jamaa?... Hata kusoma na kuelewa makala hii fupi imekuwa taabu mpaka unakuja na jazba za namna hii?... Au Aweda amegusa maslahi ya huyu jamaa? Au umeelewa vibaya habari?

Message anayoituma Aweda ni kwamba kuna watu wanamchango mkubwa sana kwenye jamii lakini wamesahaulika au wanapuuzwa na serikali lakini kuna Mchwa na Kupe wako hadi vijijini wanauza Ardhi za WaTZ kinyemela wanakumbatiwa na Serikali hii ya CCM.
 
Mkuu wewe unaitwa nani? pwito? Mbona hujaweka majina yako yote matatu kikamilifu?
Kama wewe unataka tujadili maoni yako wakati hutumii majina yako halisi kwa nini unataka tusiheshimu maoni ya huyu mpambanaji mwakijiji? Hoja ni hoja aliyotoa wala siyo sura yake AU kimo chake.

Ndomaana nasema tunaandika tusiyoyaelewa sasa unamjadili mwanakijiji na Kigoda unataka majina yangu mimi kwani nimekwambia nataka nilipwe sawa na Kigoda au mwanakijiji? Wewe kama umeleta mada tuijadili subiri uulizwe maswali ya nyongeeza ili tuchangie kwa haki jamani. Sio chuki tu sababu Kigoda yuko CCM. Tafakari unganisha nukta na ufunguke
 
Ningeshangaa kama jina Abdallah lingepita bila kutetewa na mdini mkuu wa JF ambaye ameamua kubadili ID!
Back to the topic ni vizuri kuwatambua waandishi wazuri na kazi zao na mchango wao kwa maendeleo ya taifa ukaheshimika na kukumbukwa na hata na vizazi vijavyo.Kiukweli mkuu mwanakijiji anafanya kazi kubwa sana kuliko inayofanywa na the so called "vigogo" wengi.Lakini sio waandishi wote wanafanya kazi ya kusimamia ukweli na maslahi kwa taifa.Wengi wanajulikana kwa jinsi walivyo cheap na kutumikia matumbo yao.Hata mawaziri na hao wengine wanaotambuliwa na katiba ya sasa sio wote hawana utaifa.Inawezekana hata wawili kati yao wapo genuine.Kwahiyo tukubaliane katiba mpya itambue na kuheshimu michango wa watanzania kwenye taifa lao.Kuna waalimu,wauguzi,wanasheria,wakulima,wafanyabiashara,wanamichezo na wengine wengi ambao mchango wao kwa taifa ni mkubwa lakini wanatengwa na mfumo wa katiba hii inayojali vyeo na sio michango.Tuwe na katiba ambayo ita'appreciate' michango mbalimbali ya kila mwananchi kwa taifa lake.Tubadili mfumo huu 'rigid' wa kujali vyeo vilevile bila kujali vinatupa mchango gani kama taifa.
 
Kama issue ni kuwatetea wanahabari embu tuanze na mtiririko wa background ya huyo mwanahabari. Alipomaliza form 4 akaenda wapi au kipi kilifuata maana kuna house made aliona wife wa bosi wake kanunuliwa nguo nzuri na yeye akaletewa ya kawaida akaanza kunong'ona eti mimi naamka saa kumi nafanya kazi zote yeye anaamka saa tatu hana analolifanya ndo anapata kizuri. Jamani unapokuwa ngazi ya juu wewe ni decision maker, siye wachini tutatumika mpaka position ndio itakayokuokoa. Naomba tufunge mjadala maana tutachukiana bure ingawa ndo ukweli wenyewe

Pwito now you talking.
Nani aliyesema kuwa waandishi wa habari ni house made hivyo hawastahili kulipwa? Ni nani huyo aliyesema nafasi ya uwaziri house wife hivyo wanastahili maslahi makubwa? Je alitumia vigezo gani kufikia uamuzi huo? Je, wakati tunapohama toka karne ya Viwanda na kuingia information age hivyo vigezo bado vina tija?
 
Mwanakijiji (na wengineo) avute subira kidogo. anaweza kuwa karibu kidogo na Kigoda kimaslahi na mambo mengine. wameanza kutoa ma DC kutoka miongoni mwao (wana habari).

ila wasi wasi wangu ni kuwa M.M. anasema ukweli mno na kuonekana mpinzani, cjui kama atapewa u DC.
NDIVYO ILIVYO!

Na kwa kuwa ccm wanapenda sana vibaraka itakuwa ngumu sana kw M/M kuwa miongoni mwao.watasema kuwa huyu siyo mwenzetu.kisa hawapendi kuelezwa ukweli.Na yote hiyo wamesahau kuwa mara zote ukweli unafanya watu wawe huru lakini kwao ni sumu kuelezwa kweli.
 
Kama inawezekana na kama tunakubaliana kuwa Kigoda na mwanakijiji wanatoa mchango kwa wananchi basi walipwe wote. Kama haiwezekani kuwalipa wote basi hata kutambua mchango wa huyo ambaye tumeshindwa kumlipa ni muhimu. Tatizo ni kwamba waandishi hawalipwi na hawaheshimiki wakati ni fani muhimu sana. Ikumbukwe hapa tunajadili zaidi ya mwanakjijij na Kigoda.
Na swali la pili ni je, kwa kuwa tunaandika katiba mpya, je kuna haja ya kutambua mchango wa hao waandishi wa habari? Je, kama taifa hatuwezi?

Ok. Nimekuelewa. Kumbe unataka waandishi wa habari wapate heshima wanayostahili. Naunga mkono, lakini... Mimi ni mwanasheria, wakili wa kujitegemea, na kwa bahati mbaya/nzuri sijaajiriwa serikalini. Naomba nitambuliwe kwa ni natoa mchango mkubwa kutetea haki za wananchi
Mimi ni daktari, sijaajiriwa serikalini, lakini nina hospitali yangu. Naomba nitambuliwe kwa sababu ninatoa mchango kwa jamii.
Mimi ni dereva wa daladala, naendesha mamia ya watu kila siku kutoka temeke hadi muhimbili. Kwa bahati mbaya sikuajiriwa serikalini. Naomba nilipwe na serikali kwa sababu natoa mchango mkubwa sana kwa jamii...

Bwana Mikael P Aweda naomba unitetee popote utakapoweza nami niatmbuliwe...

Kuhusu kuyaingiza hayo kwenye katiba bwana Mkaili, nilishakwambia; Katiba ni document ya kuwalinda na kuwatetea watawala dhidi ya watawaliwa... Kama unataka waandishi wa habari wawe watawala sawa...
 
Aweda,

Huwezi fananisha nanasi na ndizi.

Mwanakijiji kumfananisha na Abdallah Kigoda ni kama kufananisha Mbingu na Ardhi.

Nini cha maana na cha akili alichofanya Mwanakijiji zaidi ya majungu na fitna za mitandaoni?

Abdallah Kigoda on the other hand, ni mmoja katika watu mahiri sana na "he is a born leader".

Wewe ndugu yangu humfahamu Mzee mwanakijiji, ila ipo siku utamfahamu! hata mimi wakati flani nilikuwa kama wewe lakini leo nimefunguka kifikra!hope wengi wamefunguka pia
 
Thx, fursa ya katiba mpya ni lazima tuitumie vizuri. Turekebishe kila tatizo.

Hakuna kitu hapo.Hata nchi zilizo endelea waandishi wa habari vs mawaziri hawawezi kulingana kimaslahi na ki vyeo, japokuwa kila mmoja anamtumikia mwananchi. Na mbona umechukua mwandishi wa habari tu, je madaktari, walimu, nk au kwa vile mwanakijiji ni jamaa na rafiki yako ?,punguza fikra chache, kuwa na fikra pana zaidi.
 
Wewe ndugu yangu humfahamu Mzee mwanakijiji, ila ipo siku utamfahamu! hata mimi wakati flani nilikuwa kama wewe lakini leo nimefunguka kifikra!hope wengi wamefunguka pia

Mwanakijiji makala sake nyingi ni za uchonganishi na uzushi, he is not credible person at all never ever, labda kwa watu wachache wenye fikra chache
 
15 Reactions
Reply
Back
Top Bottom