Mohamed Said ni mwanaharakati na mwandishi wa habari. Habari zake nyingi ni kumponda Nyerere namna alivyowatelekeza wazee waislamu wa kariakoo baada ya Uhuru akidai kuwa hao wazee ndio waliodai Uhuru wa Tanganyika akina Sykes.
Hata siku moja sijaona makala yake namna ambavyo JOHN OKELLO alivyoongoza kikosi cha mapinduzi kule Zanzibar wakati hayati Karume yuko Dar es salaam usiku huo. John Okello baada ya kumpindua Muarabu akatangaza baraza la mapinduzi na kumtangaza Karume kama rais wa Zanzibar kupitia vyombo vya habari.
Siku moja baadae akampokea Karume pamoja na Abdulrahman Babu kutoka Tanganyika walikokuwa wamefichwa na Nyerere.
Mganda Mkristo John Okello huwezi kukuta ametajwa kwenye waasisi wa mapinduzi.
Mzee Mohamed Said mbona huandiki mambo haya? Kila siku wewe ni Nyerere na wazee wa kariakoo tu?
Hata siku moja sijaona makala yake namna ambavyo JOHN OKELLO alivyoongoza kikosi cha mapinduzi kule Zanzibar wakati hayati Karume yuko Dar es salaam usiku huo. John Okello baada ya kumpindua Muarabu akatangaza baraza la mapinduzi na kumtangaza Karume kama rais wa Zanzibar kupitia vyombo vya habari.
Siku moja baadae akampokea Karume pamoja na Abdulrahman Babu kutoka Tanganyika walikokuwa wamefichwa na Nyerere.
Mganda Mkristo John Okello huwezi kukuta ametajwa kwenye waasisi wa mapinduzi.
Mzee Mohamed Said mbona huandiki mambo haya? Kila siku wewe ni Nyerere na wazee wa kariakoo tu?