Bibi Titi Mohamed Shujaa Mwongoza Njia

Mohamed Said

JF-Expert Member
Nov 2, 2008
20,925
30,273
SIKU YA MWANAMKE DUNIANI

Gazeti la Mwananchi la leo limechapa makala ambayo walinitembelea Maktaba nami nikawazungusha katika mitaa ambayo wanawawake wa Tanganyika walikuwa hawapunguia katika harakati zao za kupigania uhuru.

Naanza na kipande hicho hapo chini kinachomjulisha Bibi Titi miaka ya mwanzo ya TANU.

Baadae In Shaa Allah tutawatembelea wanawake wengine waliopita katika mlango aliofungua Bibi Titi.

Mikutano ya TANU ya siku za mwanzo ilikuwa ikifanyika kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja mbele ya Princess Hotel.

Kwenye jukwaa lililojengwa kwa miti walikuwa wakikaa wale viongozi wa mstari wa mbele ndani ya TANU - Nyerere rais wa TANU, Sheikh Suleiman Takadir, Mwenyekiti wa Baraza la Wazee wa TANU, Bibi Titi Mohamed, John Rupia na Clement Mtamila.

Sahani ya santuri ilikuwa ikipigwa katika gramafoni kupitia kipaaza sauti.

Mwimbo uliokuwa ukipigwa ulikuwa wa Frank Humplink. Frank alikuwa kijana wa Kichagga kutoka Moshi.

Baba yake alikuwa Mzungu.

Humplink alikuwa mwimbaji na mpiga gitaa maarufu sana wakati ule akipiga muziki wake na dada zake wawili Maria na Regina Humplink.

Wimbo uliopendwa sana na TANU na ndiyo uliokuwa ukipigwa katika mikutano yake yote na uliosisimua wananchi ulikuwa na mashairi yafuatayo, ‘’Uganda nayo iende, Tanganyika ikichangamka, Kenya na Nyasa zitaumana.’’

Mwimbo huu ulikuwa na ujumbe wa kisiasa kwa Waafrika wa Tanganyika.

Ujumbe katika wimbo huo ulikuwa kuwa, Tanganyika itakapoamka, kutakuwa vilevile na mapambano nchini Uganda, Kenya na Nyasaland.

Wimbo huu ulikuwa ukivuma toka kwenye vipaza sauti mfululizo kabla ya mkutano huku watu wakikusanyika viwanjani.

Haikupita muda mrefu serikali ya kikoloni ilipata maana halisi ya wimbo huo. Mara moja mwimbo huo ukapigwa marufuku na serikali.

Serikali ya kikoloni iliamuru kwamba mashairi ya wimbo huo yalikuwa watu kuasi.

Lakini kabla ya wimbo huo kupigwa marufuku ulipendwa sana na ulikuwa ukiombwa na wasikilizaji na kupigwa katika kituo cha radio Sauti ya Dar es Salaam.

Baada ya amri ya serikali kituo hicho kiliacha kupiga wimbo huo.

Huenda huu ulikuwa wimbo wa kwanza kupigwa marufuku katika historia ya utangazaji Tanganyika.

Kwa muda mrefu sana wimbo huu ulikuwa kama wimbo rasmi wa TANU.
(Kutoka kitabu cha Abdul Sykes)

Katika gazeti hili hapo chini mwandishi Imani Makongoro kaeleza kutokana na mazungumzo yetu historia ya wanawake wazalendo waliopigania uhuru wa Tanganyika lakini hawafahamiki na mchango wao bado kutambulika.:

1709705888739.png

1709706254995.jpeg

Amina Kinabo
1709706323421.png

Halima Selengia
1709706376874.png

Halima Khamis
1709706596034.png

Shariffa bint Mzee
1709724473961.png

Nyange bint Chande
1709724526571.png

Zarula bint Abdulrahman
1709724857268.jpg

Tatu bint Mzee
 

Attachments

  • 1709706207143.jpeg
    1709706207143.jpeg
    66 KB · Views: 3
SIKU YA MWANAMKE DUNIANI

Gazeti la Mwananchi la leo limechapa makala ambayo walinitembelea Maktaba nami nikawazungusha katika mitaa ambayo wanawawake wa Tanganyika walikuwa hawapunguia katika harakati zao za kupigania uhuru.

Naanza na kipande hicho hapo chini kinachomjulisha Bibi Titi miaka ya mwanzo ya TANU.

Baadae In Shaa Allah tutawatembelea wanawake wengine waliopita katika mlango aliofungua Bibi Titi.

Mikutano ya TANU ya siku za mwanzo ilikuwa ikifanyika kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja mbele ya Princess Hotel.

Kwenye jukwaa lililojengwa kwa miti walikuwa wakikaa wale viongozi wa mstari wa mbele ndani ya TANU - Nyerere rais wa TANU, Sheikh Suleiman Takadir, Mwenyekiti wa Baraza la Wazee wa TANU, Bibi Titi Mohamed, John Rupia na Clement Mtamila.

Sahani ya santuri ilikuwa ikipigwa katika gramafoni kupitia kipaaza sauti.

Mwimbo uliokuwa ukipigwa ulikuwa wa Frank Humplink. Frank alikuwa kijana wa Kichagga kutoka Moshi.

Baba yake alikuwa Mzungu.

Humplink alikuwa mwimbaji na mpiga gitaa maarufu sana wakati ule akipiga muziki wake na dada zake wawili Maria na Regina Humplink.

Wimbo uliopendwa sana na TANU na ndiyo uliokuwa ukipigwa katika mikutano yake yote na uliosisimua wananchi ulikuwa na mashairi yafuatayo, ‘’Uganda nayo iende, Tanganyika ikichangamka, Kenya na Nyasa zitaumana.’’

Mwimbo huu ulikuwa na ujumbe wa kisiasa kwa Waafrika wa Tanganyika.

Ujumbe katika wimbo huo ulikuwa kuwa, Tanganyika itakapoamka, kutakuwa vilevile na mapambano nchini Uganda, Kenya na Nyasaland.

Wimbo huu ulikuwa ukivuma toka kwenye vipaza sauti mfululizo kabla ya mkutano huku watu wakikusanyika viwanjani.

Haikupita muda mrefu serikali ya kikoloni ilipata maana halisi ya wimbo huo. Mara moja mwimbo huo ukapigwa marufuku na serikali.

Serikali ya kikoloni iliamuru kwamba mashairi ya wimbo huo yalikuwa watu kuasi.

Lakini kabla ya wimbo huo kupigwa marufuku ulipendwa sana na ulikuwa ukiombwa na wasikilizaji na kupigwa katika kituo cha radio Sauti ya Dar es Salaam.

Baada ya amri ya serikali kituo hicho kiliacha kupiga wimbo huo.

Huenda huu ulikuwa wimbo wa kwanza kupigwa marufuku katika historia ya utangazaji Tanganyika.

Kwa muda mrefu sana wimbo huu ulikuwa kama wimbo rasmi wa TANU.
(Kutoka kitabu cha Abdul Sykes)

Katika gazeti hili hapo chini mwandishi Imani Makongoro kaeleza kutokana na mazungumzo yetu historia ya wanawake wazalendo waliopigania uhuru wa Tanganyika lakini hawafahamiki na mchango wao bado kutambulika.:

View attachment 2925765
View attachment 2925771
Amina Kinabo
View attachment 2925775
Halima Selengia
View attachment 2925778
Halima Khamis
View attachment 2925786
Shariffa bint Mzee
View attachment 2926020
Nyange bint Chande
View attachment 2926021
Zarula bint Abdulrahman
View attachment 2926032
Tatu bint Mzee
Bibi Titi hakuwahi kuwa shujaha,wala hana mchango wa maana katika siasa za Tanganyika.

Bibi Titi anakuzwa kwasababu za kidini zaidi.Bibi hakuwa msomi Mwl Nyerere alimbeba kwakuwa hawakuwepo Wanawake wengi wasomi enzi hizo.

Ukipipitia mchango wa Bibi Titi ndani ya Bunge la wakati huo ambapo lugha ya Kiingereza ilikuwa ikitumika "Bibi Titi" alikuwa kichekesho.
 
Back
Top Bottom