Mzee Jumbe ausia asizikwe Kiserikali

Mzee Jumbe ausia asizikwe Kiserikali

Nani kasema patawekwa bendera yoyote? Mbona mnapenda sena kukurupuka!!
Kama hawakumhitaji akiwa hai hawawezi kumhitaji akiwa mfu. Kamaliza kazi yake, tumuombee dua akapumzike kwani 'kufa kila mtu ni lazima, mkamia kifo nani?' Aliuliza S. A. Kandoro
 
Nyie lumumba mlitaka mmmzike kiserikali mpate sifa.....eti ktk barua toka magogo inasema tmeshtushwa SANA ,what @ f

Ovaa
Mh!! Mjomba hata msiba nao siasa??

Kweli hii dunia kuna watu wa ajabu na maajabu...
Msibani napo ligi???
 
Mh!! Mjomba hata msiba nao siasa??

Kweli hii dunia kuna watu wa ajabu na maajabu...
Msibani napo ligi???
Wosia wake aliyeutoa si umeusoma....
Hataki mazishi ya kiserikali ...alishajua wanafki watasogea

Ova
 
'Aliagiza kuwepo na utabaka katika kubeba jeneza na kufukia kaburi'. Waislamu tusaidieni ufafanuzi katika hili kwa sababu siyo kila wosia unakubalika katika uislamu.
Kinyume chake ndivyo wasia unavyotaka, "kusiwepo", hiyo ni mwendelezo wa sentensi ya ukanusho inayoanza hapo mwanzo. Yaani AMEKATAA matabaka/makundi katika mazishi yake, watu wote wawe na lengo moja tu nalo kuzika. Hapa alikuwa na lengo la kutoingiza siasa katika maziko yake kama kwa kawaida wanavyofanyiwa wanasiasa wengi.
 
Jumbe+pic.jpg

Rais wa Pili wa Zanzibar, Aboud Jumbe Mwinyi amefariki dunia mbele ya familia yake, akiwa ameacha ujumbe unaokataza mazishi yake kuhusisha taratibu zinazokiuka mafundisho ya dini ya Kiislamu.

Jumbe, ambaye alivuliwa nyadhifa zote serikalini na ndani ya CCM kutokana na kutofautiana na chama hicho katika suala la muundo wa Muungano, alishika nafasi ya urais mwaka 1972 baada ya muasisi wa Zanzibar, Abeid Amaan Karume kuuawa katika jaribio la mapinduzi.

Akizungumzia kifo hicho, mtoto wa Jumbe Mustafa Jumbe amesema sababu ya kifo cha baba yake ni umri mkubwa ambao ni miaka 96.

Amesema kabla ya kuzikwa leo mwili, utaswaliwa katika msikiti wa Mwembeshauri na kuzikwa nyumbani kwake Migombani, Zanzibar.

“Marehemu ameacha wake wawili, watoto 14 na wajukuu zaidi ya 30,” amesema Mustafa.

Akataa kuzikwa kifahari
Mazishi ya kiongozi huyo aliyekaa madarakani kwa miaka 12 ikiwa ni muda mrefu kuliko marais wengine wa Zanzibar, yanaweza kutoshirikisha taratibu za kiserikali kutokana na wosia alioandika kabla ya kifo chake.

“Sitaki katika maziko yangu kutumbuizwa chochote kiendacho hata kidogo kinyume na mafundisho ya Islamu,” anaandika katika wosia huo.

“Sitaki beni (bendi), sitaki mizinga, sitaki maombolezo wala lolote jingine lenye hata chembe ya kufuru. Sitaki hivyo nikiwa hai, nitakapoondoka katika dunia. Mwenyezi Mungu anatosha kuwa shahidi wangu, duniani na akhera.”

Kwa kawaida kiongozi wa kada yake anapofariki, hupigiwa mizingi 21 na kusubiri taratibu za kiserikali ambazo wakati mwingine huchukua muda kukamilika tofauti na sheria za dini hiyo.
 

Attachments

  • upload_2016-8-15_8-7-15.png
    upload_2016-8-15_8-7-15.png
    4.7 KB · Views: 46
Akataa kuzikwa kifahari

Kila mtu na imani yake.Hataki kuzikwa kifahari lakini maiti yake inasafirishwa kifahari kwa ndege ya kifahari,waombolezaji wakisafiri kwa ndege na magari ya kifahari kwenda kwenye hayo mazishi na maiti yake inaagwa kwenye nyumba zake binafsi za kifahari zilizoko nchi mbili ya Tanzania bara iliyoko dar es salaam,kigamboni na na ile ya Zanzibar iliyoko migombani ,Maiti yenyewe inasindikizwa kifahari kwa ving`ora na mapikipiki na vyakula vinavyoliwa ni vya kifahari mwisho wa siku unaambiwa hakuzikwa kifahari.Haya sawa.

Unaambiwa aliiishi kifari halafu hakuzikwa kifahari .Haya.
 
CCM wanafiki sana. Katika miaka 32 ya maisha yake nje ya Uongozi wamemshirikisha katika lipi hasa.
 
Imani ndio inasema azikwe kiserekali au jeneza lifunikwe na bendera ya ccm? Shirikisha ubongo kabla ujatanua mdomo
Alilazimishwa kuachia ngazi hivyo akitoka kwenye Serikali kwa sababu ya tofauti ya mawazo yake.Akanyang'anywa kadi ya CCM hivyo Hakuna sababu ya kuvikwa Bendera ya CCM. pole
 
CCM wanafiki sana. Katika miaka 32 ya maisha yake nje ya Uongozi wamemshirikisha katika lipi hasa.

Walimnyang'anya kadi na kumfuta uanachana hivyo hawana haki hata ya kumwita Mwanachama wa CCM.
 
Back
Top Bottom