Mtangazaji: Sina hakika mie nakufahamu kama wewe ni wanachama wa CCM lakini kwa nini wanachama wa wenzako wa ccm wanakushambulia kwa kiasiwakati maoni haya ni ya wananchi?
Warioba:Aaa wanasema ni sera ya chama
Mtangazaji: chama chenu lakini wewe ni wanachama ?
Warioba:Mimi niliwambia wala sikuwambia ccm nilisema na taifa zima.Tulichaguliwa wajumbe 34 tulikuwa kwenye tume,wajumbe 32 kutoka makundi mbalimbali ,katibu na naibu katibu.Kwenye tume kama nilivyosema nilivyokuwa natoa taarifa nilipoteuliwa kuwa mwenyekiti na kuona kundi nilikuwa nalo nikaona hapa siamini kama tutatoka na kundi litakoundanisha watanzania kulikuwemo wawakilshi wa yama vya siasa kwa hivyo tulikaa na kukubaliana huyo ametoka ccm,mwingine chadema,cuf,nssr na mkundi mengine tukibaki na misimamo ya vyama hatutafanya lolote.kwa hiyo sisi kama watanzania tumepewa kazi ya taifa na tutakuwa waaminifu na tutakwenda kuwasikiliza watanzania tupendekeze kama wanavyotaka wanachi na si vinginevyo.
Sasa chama change baada ya kutoka ile na ni kweli wote wananitukana ni kutoka chama change sasa nashangaa kwa sababu wananifahamu kama ni muumimi muundo wa muungano mie ni mmoja wao yaani nimetumia nchi hii kama unajua 1994 nilifika nikakata tama nikasema tujaribu seriakli mbili kuelekea moja.
Mtangazaji:Nani aliwapa hii kazi?
Warioba: Kwanza Nashangaa Yule mama aliyetoa taarifa kamati number moja anasema hatukuwatuma kwenda kufanya hii ,sisi tumefanya kazi kwa mujibu wa sheria na tumefanya kazi kwa kuangalia sheria popote tulikukuwa ilikuwa jambo ambalo la kuzingatia ni uwepo wa muungano na sheria haikusema tuzingatie muundo wa serikali mbili bali uwepo wa muungano na wanachi ndo walizungumzia muundo wa muungano na tukaangalia hoja zilizpo na uhalisia wa utulivu wengi walipendekeza serikali tatu kwa hoja zilizpo na matitizo tukiendela na muundo wa serikali mbili mambo yatakuwa mabaya
Mtangazaji:Wanasema hamkuzingatia hadidu za rejea mkaenda kivenuvenu tu?
Warioba:Katika taarifa tulizotoa kuna vitabu vingi moja ya ile ripoti imeeleza mzhakato wote ,imeeleza historia unajua wakati mwingine wanavyoongea inafikiwa wakati mtu unaoana hawajasoma hizo taarifa
Mtangazaji:Jaji kutoka rohoni mwako unajuta kuwa mwenyekiti katika mchakato huu?
Warioba :Hapana ilikuwa ni hekima tuweze kushughulika kutengeneza katiba hii kwangu ni kwa kweli naona faraja ni heshima kubwa nimepewa kutengeeza katiba kwa mara ya kwanza kutoka wanachi wa kawida nimetumia wakati kutoka utumishi ulitukuka kwa sio sisi wanaotusema wala haina shida ila tunjivunia kwa mara ya kwanza tumetoa utumishi uliotukuka
Mtangazaji:Na unazungumzajehija hii ukuifufua Tanganyika tanznia itakufa
Warioba:Mie nawashangaa watu waliokuwa mstari wa mbele kusema Tanganyika ndo inayofaidika sasa ndo wanaosema ukifufua utavunja Tanzania siwaelewi wanasema Tanganyika ipo na ndo inafaidi.
Tulikwenda Zanzibar wakati tunapata maoni ya wananchi tuakaona tupate na maoni ya taasisi.Hawa sasa wanaosema kwamba ukifufua Tanganyika muungano utakuafa ndio walikuwa wanalalamika jinsi mawaziri wazanzibar wanavyonyayaswa kuapata mikopo na serikali ya muungano inayohudumia Tanganyika.
Mtangazaji:Unazungumzaje kuhusu mwendendo wa bunge la katiba
Warioba:Tatizo ni vyama vyoa kwa hyo unakuta ccm imemua kwamba sisi tujaribu ya kwetu na ndio wengi.wale wenine kwa kuwa hawna wingi kwa kupitisha maamuzi ndo maana wazazuia ili wasipitishe