Mzee Jaji Warioba ndani ya Dk 45 ITV

Mzee Jaji Warioba ndani ya Dk 45 ITV

Huyu mzee ana hekima sana! Anafafanua kuhusu uzanzibar na Tanganyika akikumbushia G55 ya 1994. Pia ameeleza kisa cha Steven Wassira kuhamia upinzani enzi zile, amemshangaa Dr. H. Kigwangala kusema uongo bungeni eti Warioba alikuwa tume zakina Nyalali
 
'namshangaa daktari mzima (Kigwangala) kusema uongo' Jaji Walioba.
 
Wajumbe wa katiba badala ya kutazama mambo kw amtazamo wa kitaifa wanajadili kwa kuangalia mwaka kesho 2015 .... jaji Warioba
 
Aneleza kuwa tume ya katiba ilifuta misingi na itikadi za kivyama hiyo ndiyo iliyopelekea wao kuimarisha umoja wao na kupatikana kwa rasimu zote mbili.
 
Transparency and accountability ni msingi mkubwa sana wa Utawala Bora,.... Jaji Warioba
 
Anagusia kuwa kipengele cha maadili nacho kitakuwa kigumu kwa wajumbe hasa walioko wenye mfumo wa kimamlaka yaani kutoka c.c.m ambao wataguswa na mambo ya ufisadi ni wizi wa mali za umma.
 
Wananchi walitaka Rais achaguliwe na watu, Matokeo ya Uchaguzi wa Raisi yahojiwe Bungeni, Madaraka ya Raisi yapunguzwe,,,,, Wajumbe la Wabunge Maalum la Katiba wamepinga ..... By Warioba
 
Bado anawasiwasi na sura zingine hasa sura zinazozungumzia maadili na miiko ya uongozi itapuuziwa na baadhi ya viongozi.
 
Katiba iliyopo ina msingi wa Chama Kimoja, sasa tunatengeneza katiba mpya yenye mtazamo wa vyama vingi, katika katiba ya zamani madaraka ya uongozi yalikuwa mikononi mwa mtu mmoja ambaye ni kiongozi wa chama ambaye pia alikuwa ni Rais.
 
Jamani mwenzunu naogopa wasijemuuwa huyu mzee warioba manake masisiem miye siwaamini hata kidogo
 
Mh. Jaji ameulizwa kama kuna sura zingine zitaleta mvutano kama sura ya 1 na 6, anasema kuna sura ambazo anaona kabisa jinsi hawa jamaa walivyojipanga watayaondoa tu!
 
Tusipokuwa na katiba mpya tunaweza kupoteza utulivu uliopo, viongozi wabadirishe mitizamo yao wajadili maoni yanayotokana na mapendekezo ya wananchi .... Jaji Joseph Sinde Warioba
 
Mwalimu alikuwa na mtazamo wa serikali mbili kwenda serikali moja ambapo yeye warioba anasaema kuwa akiwa katibu wa ulinzi na usalama wa chama.
-anawaasa watanzania kutokukata tamaa na anawaomba watanzania kuwa na moyo wa kuipata katiba bora.
Ana waomba viongozi wa serkali kutokwamisha mchakato mzima wa upatikanaji wa katiba mpya.
Anamalizia
'mti wenye matunda ndio hupigwa mawe'.
Viva shujaa j.s warioba.
Viva e.buhohela.
Go!go itv go!
 
Bila maridhiano kupata theruthi mbili kwa upande wowote ule kwa Zanzibar itakuw ani ngumu, kama viongozi wetu hawataonyesha njia ya sisi kuwa wamoja kwa hoja moja kupatikana kwa theruthi mbili aidha za kuunga mkono S#3 au S#2 haitawezekana.
 
Back
Top Bottom