DuaZaMama
JF-Expert Member
- Jun 2, 2025
- 1,882
- 4,129
Msanii na mtengeneza maudhui ya mtandaoni (Digital Content Creator) Bw. Clemence Mwandambo amefika katika ofisi za Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Mbeya tarehe 17 Novemba 2025 kwa ajili ya kujisajili na kupata Namba ya Utambulisho wa Mlipa Kodi (TIN). Hatua hiyo inalenga kumwezesha kukadiriwa rasmi kama mfanyabiashara wa mtandaoni na kuendesha shughuli zake kwa kufuata matakwa ya kisheria.