Mzee Butiku: Tukubali tunaye Rais

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
4,393
Reaction score
14,499
Mkurugenzi Mtendaji na Rais wa Taasisi ya Mwalimu Julius Nyerere, Joseph Butiku, amewataka Watanzania kukubaliana na uhalisia kwamba nchi tayari ina Rais aliye tayari kwa maridhiano.

Butiku ametoa kauli hiyo leo Machi 4, 2026, wakati wa maadhimisho ya Siku ya Maridhiano (Maridhiano Day) yaliyofanyika katika ukumbi wa Kwa Tunza, wilayani Ilemela, mkoani Mwanza.

Akizungumza katika hafla hiyo, amesema kuwa tume iliyoundwa na Rais Samia Suluhu Hassan imeongezewa muda hadi mwezi Aprili, na kuwataka wananchi kuwa na subira.

“Nimesikia tume iliyoundwa na Rais Samia imeongezewa muda mpaka mwezi wa nne (Aprili). Tukubali tusubiri aje atuambie jambo na lije litusaidie kwenye mazungumzo,” amesema Butiku.

Aidha, amewataka viongozi wa dini nchini kuendelea kuhimiza haki na amani kwa wakati mmoja, akisisitiza kuwa hakuna amani ya kweli bila haki.

Your browser is not able to display this video.

 
Huyu hakuchanganyikiwa; huyu ni mtu anayefanya jambo analojuwa mwenyewe kuwa siyo sahihi.

Anazungumzia HAKI na AMANI, na kusisitiza; wakati huo huo anapiga chenga kuzungumzia kinyume cha alichozungumzia mwanzo.

Hii ni 'strategy' (mkakati) ambao wameamua hawa w waovu kuchanganya akili za watu.
Mwovu ambaye kaamua kuvuruga HAKI, utamsafisha vipi ili akidhi kuwa Rais? Mtu asiyependa HAKI; unahimiza watu wamtambue kuwa halali!

Mzee Butiku anafanya kazi anayojuwa inamwondolea heshima zote. Hiyo Taasisi ya Mwalimu ingekuwa ni taasisi huru ingemwondoa huyu mshenzi aliyeamua kulidhalilisha jina la Mwalimu Nyerere kwa sababu zake azijuazo mwenyewe.

Mzee Butiku haitendei HAKI taasisi ya Mwalimu Nyerere. Anaifedhehesha.
 
well done, well said mzee Joseph Butiku
 

Msilazimishe Watanzania kukubali uongo hakukuwa na Chaguzi Tanzania. Mnaongelea Mungu wakati mnaongelea uongo Mungu hapendi uongo
 
https://www.facebook.com/
View: https://www.facebook.com/share/v/1SuugJZWog/
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…