Mzee baba, pakacha limeanza kuvuja ujue...

Mzee baba, pakacha limeanza kuvuja ujue...

Asilimia kubwa ya wasukuma hawana ujanja kwa akina "Cheupe Dawa" . Naota kuna babu Seya mwingine atakula mvua. Labda tu kama mwenye cheupe dawa awe mwoga,,ila akianza kufuatilia tu,,mtamsikia.
Kuna watu mnawaza mpaka mnaacha watu waonekane vichaa kwa kucheka, nimewaza hiyo kauli yako ya Babu Seya nikawaza hadithi ya "Nani amfunge paka kengele"
 
Watu wameamua kulianzisha mdogo mdogo dhidi ya ASIYEJARIBIWA maana hawa WAKUJA wamewaudhi sana. Haingii akilini kufanya upuuzi mkubwa kama huu wa kuwaingiza walipa kodi mabilioni ya hasara eti kwa kumuunga mkono uchwara.

Kumbe nanyi mlielewa vivyo hivyo
Hii ngoma karibu inapasuka mwisho wake hahahhhh ni haya
Hahaaaha mshana jr una akili wewe
BAK angalia body language ya kujitetea kwao utagundua jambo
 
Tuhuma ni tuhuma tuu... Lakini kwangu tuhuma zisizothibitika wala kuthibitishwa zinabaki kuwa uzushi.... Na mimi sina kaliba na uzushi.... Sijui nini kilinipelekea kukumbuka riwaya ya Ngoswe... PENZI KITOVU CHA UZEMBE... Dah nikayakumbuka ya kudamka alfajiri na mapema kwenda kule kilimani kumuona cheupe dawa... Si adhabu hii jamani... Mateso bila chuki... Kiroho safi kabisa... Hongera mzee baba... Hongera cheupe....

Kuna wale wazee na kawimbo kao kalikokosa udhamini wa kuingia studio... Naambiwa singo yao ile haikidhi vigezo... Kale kawimbo ka MATEMBELE NI MATAMU.... Kweli Ngoswe aliona mbali... Na mtunzi wa MATEMBELE aliona karibu....

mzee baba huku kwenye chama la wana hali si shwari... Wanachonga waziwazi sasa hivi... Hawana shukrani na hawana upendo kwa wageni.. Kwao wao mgeni ni siku ya kwanza tuu... Sasa wnalalamikia uwingi wa wageni... Wenyewe wanawaita wakuja.. Wanawaita mizigo... Wanawaita wadekaji.... Hali si shwari sana pakacha limeanza kuvuja....

Mkubwa mpya wa usalama wetu Barabarani naye kaharibu... Japo ndio kutenda kwa weledi... Anapingana na dhana ya kukusanya mapato yetu ili kibubu kitune... Wanakaya wamemfurahia sana... Hakuna tena kutoza faini za kijinga... Kwahiyo hapa hakuna tena viwango elekezi vya kukusanya kwa siku wiki hata mwezi... Wanakaya wamepata mkombozi hatimaye... Mungu naye hujibu maombi kwa wakati wake....!!!!... Ila zile mbwembwe za jeshi la polisi kujivunia kuwa mwezi huu wamekusanya billion ngapi zitakoma.. Wao sio kitengo cha mamlaka ya mapato.. Faini za uonevu kwishney....

Mzee baba pakacha limeanza kuvuja... Wameanza kupambana na wewe... Mbwa anataka kula mbwa... Filamu ya half ray imedoda... Ile ya viongozi 20... Filamu ya nabii Tito imechacha.. Wanakung'ong'a.. Kikulacho ki nguoni mwako... Wasikupake mafuta kwa mgongo wa chupa..... Ni wanafique

Uliyasikia ya Benedict ? Yule mtia nia?
Uliyasikia ya Nnauye Jr?
Uliyasikia ya bwana Ole ?
Umeyasikia ya Riz moko?
Wote wametoa ya moyoni halafu wakakana lakini neno likitoka limetoka ni kama risasi haina rivasi.... Basi ndio hivyo mzee baba... Hao wote ni kiwakilishi cha wengi ndani ya chama la wana...pakacha limeanza kuvuja... Naamini halijasababishwa na Ngoswe.... Inatosha tu kusema.... MATEMBELE ni MATAMU....!!!!
Umesahau kauli ya Mkuu wa watenda haki kuhusu wanasiasa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom