Mzazi wewe ndio unayekuza kijana shapu au goi goi

Mzazi wewe ndio unayekuza kijana shapu au goi goi

ERTUGRUL BEY

JF-Expert Member
Joined
Aug 6, 2020
Posts
11,529
Reaction score
21,530
Screenshot_20260120-144516_Google.jpg


My people,​

Unapomuacha mtoto wako aache sahani mezani baada ya kula sio tu kwamba unamfanya awe na tabia mbaya bali unamtengenezea mazingira ya kuwa na future mbaya huko ukubwani.

Mtoto anapomaliza kula na kisha mzazi ukamuondolea sahani yake,hii inamjenga mtoto akilini kwake kwamba kuna mtu siku zote atakuwa around kumfanyia mambo yake,kwahiyo hana haja ya kuwa na mashaka na baadhi ya mambo kwani siku zote kuna mtu yupo pale kwa ajili yake

Hii imenikumbusha Prince William baada ya kukabidhiwa rasmi ufalme,akiwa pale mezani ana Saini nyaraka,peni haikuwa mbali na yeye ni swala la kunyoosha kidogo tu mkono na kuichukua lakini aliashiria msaidizi wake amsogezee,wale walio ona hiyo clip watakubaliana na mimi kwamba ule ndio ubaya wa malezi ya kufanyiwa kila kitu.

Haya wale ni familia ya kifalme je vipi watoto wako na wangu tunawatengenezea mazingira gani katika future yao?

Watoto wa namna hii huwa wanashindwa kuwajibika wanapokuwa watu wazima,kwasababu wameshazoea kufanyiwa kila kitu,na pale wanapoingia kwenye mazingira ambayo yanawalazimisha wawajibike na kuchakalika,wanaanza kulaumu kazi kwamba ni ngumu,au kulaumu boss mkali au hata kulaumu system nzima ya mpangalio wa kazi pale kwenye maeneo yao ya kazi

Kwahiyo tangu wakiwa wadogo wafundishe wajue kwamba hapo nyumbani sio hotelini kwamba kuna mtu atawafanyia au kuwahudumia ,bali hapo ni home wana kila sababu ya kuwa na jukumu la kushirikiana kufanya kazi,wakifika umri wa kufua nguo basi wafue nguo zao,hata kama una washing mashine,siku moja moja hakikisha wanafua kwa mikono yao,wafagie hapo nyumbani,hii itawajenga wawe watu wanao jua kuwajibika na watathamini kile ambacho wanakifanyia kazi

Kumbuka vijana wengi ambao leo hii hawawajibiki,hawataki kufanya kazi au hawajitumi,msingi mkubwa wa tabia zao hizi zilianzia nyumbani,kuna nyumba moja ya wapangaji ipo karibu na home,mazingira yake machafu,matakataka yapo hapo,majani hayaja limwa na wao wala hawana habari.

Hapo moja kwa moja unajua tu kwamba wamekutana watu ambao sio responsible, watu ambao ni goi goi na hawajitumi kusafisha mazingira yao,unaweza kabisa kujaji kuwa mazingira ya ukuaji wao haya kuwafunza kuwa responsible adults

Lau mie ningekuwa mmoja wa wapangaji pale,basi ama ningefanya usafi mwenyewe au kuwahamasisha wenzangu nao wajitume kusafisha mazingira yao

Kwahiyo kuwaacha watoto bila kuwajibika hapo home sio kwamba unawapenda bali unawatengeneza kuwa kizazi cha hovyo sana huko mbele ya safari

Kuwapenda watoto ni kuwaelekeza mapema kabisa kwamba wanatakiwa wajifunze kufanya shughuli mbali mbali hapo nyumbani na wakiwa wakubwa watakushukuru sana,nililima bustani,nilichunga ng'ombe na kukamua,nilifanya usafi wa mazingira,leo hii ni mtu wa kujituma sana kwasababu wazazi wallinifundisha toka awali kabisa kuwa a responsible man.

Ni hayo tu
 
Tuna watoto vishoia sana Tena sana wakiona hata mende utadhan wameona nyoka
Kuua mdudu anayetambaa ni shida kuoga yenyewe mpaka wasimamiwe kufua ndo huwaon wao wanajua kula tv games na michezo kazi zingine dada au mama
Kama na wake au mama wa baadaye hichi kizaz hawatoboi kama ni baba wa kesho ndo hakuna kitu nyie mababuna mabibi ndo mtalea familia zao
 
Mitoto hiihii inayolelewa na house girl ya kila kitu dadaa njaa, dadaa mmaa, dadaa duduu, dadaa washa tivuu, dadaa peleke chooni, dadaa vichee kiatu, hebu tuache masikhara kwa kweli.
Kweli kabisa ni mtihani sana kwakweli, dada wa Kazi hana time ya kuwapa malezi elekezi,na hata akiwapa utakuta mitoto inakuja kuko Mplain dada anatutuma tufanye hivi au vile
 
Tuna watoto vishoia sana Tena sana wakiona hata mende utadhan wameona nyoka
Kuua mdudu anayetambaa ni shida kuoga yenyewe mpaka wasimamiwe kufua ndo huwaon wao wanajua kula tv games na michezo kazi zingine dada au mama
Kama na wake au mama wa baadaye hichi kizaz hawatoboi kama ni baba wa kesho ndo hakuna kitu nyie mababuna mabibi ndo mtalea familia zao
Kweli kabisa kuna shida mingi Sana kizazi hiki ni game na tv ndio mpango mzima
 
Tuna watoto vishoia sana Tena sana wakiona hata mende utadhan wameona nyoka
Kuua mdudu anayetambaa ni shida kuoga yenyewe mpaka wasimamiwe kufua ndo huwaon wao wanajua kula tv games na michezo kazi zingine dada au mama
Kama na wake au mama wa baadaye hichi kizaz hawatoboi kama ni baba wa kesho ndo hakuna kitu nyie mababuna mabibi ndo mtalea familia zao
Vishoia😂😂😂 ukaona ni kiswahili 😅
 
Back
Top Bottom