Mzalendo asiyependa kukaguliwa....

Mzalendo asiyependa kukaguliwa....

Kitendo cha Spika kumdhalilisha Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za serikali CAG, ni dalili za wazi kabisa kuwa serikali kupitia kwa Spika ina jambo inalificha haitaki lijulikane.

Mbona watangulizi wake walikuwa wanakaguliwa wakati mwingine walikuwa wanakutwa na madudu makubwa lkn serikali zilikuwa zinakuja na majibu, ingawa mengine yalikuwa si ya kuridhisha lkn walijibu.

Kuna wanaojiuliza, inawezekana ni 1.5T alizohoji CAG, au kuna ufisadi mkubwa unafanyika kupitia miradi mikubwa ya Stieglars Gorge, ujenzi wa SGR, ununuzi wa ndege nk.

Ina maana serikali hii haina watu wenye akili ya kupangua hoja 'professionally' hadi wafunike wizi kishamba namna hii, mbona kwenye EPA walikuja na majibu, Tegeta Escrow walijibu kisomi ingawa hatukuridhika lkn walijibu.

Kwanini isiwe sasa kuna nini wanaficha? Ni uzalendo gani huo sasa wa kutataa kukaguliwa. Kama hamtaki taasisi za serikali zikaguliwe hiyo vita ya UFISADI ni kiini macho tu.

Huu ni mtazamo finyu na hatari sana! na ni wa hovyo…ni kama unajitekenya mwenyewe afu unacheka…ukiambiwa jizi sijui utakataa!? Hivi Magu amewakosea nini huyu baba wa wa watu ambaye wakati wote yuko busy akiibuwa mambo yanaoikwamua nchi yetu pendwa tz? Kila muda mnajaribu kumchokonoa na kumtupia kila upuuzi wa kashfa zisizo na maana yoyote. yaani kwangu mie hata kama ingekuwa kweli amechukua hayo ma 1.5T ningeenda kulala kitandani kwangu kwa amani nikijua ataibuka na jambo lenye maslahi mapana ya nchi yangu ya Tz lenye matumizi sawia ya 1.5T! Nyie wenye mawazo ya kumhisihisi vibaya ndio wenye nia ovu, na mshindwe na kulegea!
 
Huu ni mtazamo finyu na hatari sana! na ni wa hovyo…ni kama unajitekenya mwenyewe afu unacheka…ukiambiwa jizi sijui utakataa!? Hivi Magu amewakosea nini huyu baba wa wa watu ambaye wakati wote yuko busy akiibuwa mambo yanaoikwamua nchi yetu pendwa tz? Kila muda mnajaribu kumchokonoa na kumtupia kila upuuzi wa kashfa zisizo na maana yoyote. yaani kwangu mie hata kama ingekuwa kweli amechukua hayo ma 1.5T ningeenda kulala kitandani kwangu kwa amani nikijua ataibuka na jambo lenye maslahi mapana ya nchi yangu ya Tz lenye matumizi sawia ya 1.5T! Nyie wenye mawazo ya kumhisihisi vibaya ndio wenye nia ovu, na mshindwe na kulegea!
Unavyowaza kuwa hata angechukua hizo 1.57T wengine nao wanawaza tofauti heshimu mawazo yao.
 
Unavyowaza kuwa hata angechukua hizo 1.57T wengine nao wanawaza tofauti heshimu mawazo yao.
Rais wetu mpendwa JJPM anahitaji kutiwa moyo sio upuuzi huu wa banyamlenge ambao kucha kuchwa wanatafuta mbinu za kumhujumu! Inanikera mie…basi tu! Eh Mwenyezi Mungu tunaomba uzidi kumtia nguvu na kumuongoza rais wetu mpendwa Dr. JJPM na serikali yake! Mungu tunaomba uzidi ibariki nchi yetu tanzania!
 
Ndungai ni fimbo ya ikulu, yaani ikulu inamchapa CAG kwa fimbo, inayoitwa Ndungai ambaye ni speaker wa bunge, na yeye kwa kuwatisha wabunge wenzake wa ccm atawaambia msipokubaliana na hoja husika rais atavunja bunge.

Sasa kada mwenzangu wa lumumba sijui umesahau jinsi tunavyoendesha inchi na chama chetu kinafiki.
jibu hoja ?,CAG kaitwa ikulu au bungeni?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
self proclaiming mzalendo, bila shaka alikaa na mtoto wa shangazi wakapanga matumizi ya kodi za wananchi kanakwamba ni hela walizozipata baada ya kuuza ng'ombe wao. Umefika wakati wa kukaguliwa anafura kwa hasira na kuanza kumtumia yule matonya kumtisha mkaguzi. 2020 wapinzani watamchafua sana na asivyojua kujibu hoja anaweza kufa kwa presha.
Hahahaha

2020 John Walker out
 
CAG aliwahi kukataa hiyo 1.5 tena mbele ya rais
We mtoto acha kupotosha,raisi wako aliuliza kama pesa hizo zimeibwa ndipo CAG akakataa.
.
.
Kwenye ripoti ya cag hakusema zimeibwa bali hazijulikani zilipo kwani hakuna mahali zimeainishwa matumizi yake,
so swali aliloulizwa si juu ya kutoonekana bali kuibwa na jibu alilotoa ni sahihi.

Cha kujiuliza raisi kwanini aulize swali tofauti na ambalo lingefaa kuuliza? MWIZI.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
jibu hoja ?,CAG kaitwa ikulu au bungeni?
Kaitwa Bungeni.......

Lakini kwa kuwa serikali hii namna inavyofanya kazi kati ya Bunge na serikali, kama chanda na pete, itakuwa ameitwa "indirect" Ikulu kwenda jibu mashitaka
 
CAG aliwahi kukataa hiyo 1.5 tena mbele ya rais
Pale sio mahali pake kubishana na jiwe mwenye mamlaka yaliyopitiliza, CAG amefanya ukaguzi maalum kuhusu 1.5T, ss kabla hajatoa amri ya kumkamata kwa pingu cag, apeleke hiyo ripoti pac ili matukio yaende first come first served!
 
Back
Top Bottom