Mzalendo asiyependa kukaguliwa....

Mzalendo asiyependa kukaguliwa....

jibu hoja ?,CAG kaitwa ikulu au bungeni?

Bunge linamhitaji CAG hata kwa pingu!? Acha utani boss. Inawezekana siku CDF akilituhumu bunge aitwe na Spika tena akikataa afungwe pingu? Msituone sisi ni wajinga wa hivyo. Kuna ripoti ya 1.5t mpaka leo haijajadiliwa na bunge na spika ndio kikwazo. Je CAG naye aagize spika aitwe kwenye ofisi ya CAG kuonyesha ni kwanini hiyo ripoti haijadiliwi? Jiwe ndio Kampa kiburi spika, na nia ni kumtisha CAG kuhusu 1.5t.
 
Hawamuwezi CAG...


Ndiyo maana hata nanilii kipindi kile alimlazimisha CAG mbele ya hadhara aseme kama hizo pesa 1.5trillion ni kweli hazijulikani zilizpo kibabe sana...


Cc: mahondaw
 
Bunge linamhitaji CAG hata kwa pingu!? Acha utani boss. Inawezekana siku CDF akilituhumu bunge aitwe na Spika tena akikataa afungwe pingu? Msituone sisi ni wajinga wa hivyo. Kuna ripoti ya 1.5t mpaka leo haijajadiliwa na bunge na spika ndio kikwazo. Je CAG naye aagize spika aitwe kwenye ofisi ya CAG kuonyesha ni kwanini hiyo ripoti haijadiliwi? Jiwe ndio Kampa kiburi spika, na nia ni kumtisha CAG kuhusu 1.5t.
CAG aliwahi kukataa hiyo 1.5 tena mbele ya rais
 
jibu hoja ?,CAG kaitwa ikulu au bungeni?
Kwani Ndugai cheo chake ni kipi hasa?
tapatalk_1541058442974.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
CAG aliwahi kukataa hiyo 1.5 tena mbele ya rais

Majibu ya hesabu yanatolewa hadharani? Siku ile alienda na vitabu pale? Pale yale majibu aliyompa yaliendana na hadhira na hakuhitaji malumbano maana sio mtu wa malumbano ya kisiasa. Ripoti yake ilionyesha kuna 1.5t isiyo na maelezo mujarabu, mpaka leo kamati ya PAC wamewahi kuitoa bungeni kama inavyopaswa? Hiyo nguvu na jazba ya spika ni kutaka kuficha hayo matumizi mabovu ya pesa ya umma fullstop.
 
Hii awamu ilijipambanua kwamba inapigana na ufisadi lakini kumbe ni usanii mtupu. CAG kawaumbua
WaTz tuna ugonjwa mmoja wa kusahau pindi tulabinshwapo sukari kidogo! CCM na UFISADI - iwe ni ya Nkapa, iwe ya Kikwete, au iwe ya Jiwe - ni kama Samaki na Maji. Samaki hawezi kuishi zaidi ya masaa matatu nje ya maji. Vivyo hivyo, CCm haiwezi ku-survive bila ufisadi (ni utamaduni umejengwa. unaweza kuja kwa majina na kwa namna mbalimbali, lakini ni wizi wa kimfumo). Utamaduni huu hauwezi kutoweka bila CCM kufa kwanza (yaani ikaondolewa madarakani hata kwa muhula mmoja) na pengine ikazaliwa upya huko mbeleni. Ushahidi ni Jiwe, mbali ya kutotaka kukaguliwa (tena kwa mujibu wa Katiba aliyoapa kuilinda) hata kabla ya kuwa rais ameacha stori nyingi huko mawizarani ambazo huibua maswali mengi badala ya majibu - lakini ndiye anyeonekana na kushangiliwa kuwa MZALENDO nambari wani! Kama uzalendo ndio huu, nime-declare sitataka kuwa mzalendo hata siku moja.Acha niwe wakala wa mabeberu.
 
Majibu ya hesabu yanatolewa hadharani? Siku ile alienda na vitabu pale? Pale yale majibu aliyompa yaliendana na hadhira na hakuhitaji malumbano maana sio mtu wa malumbano ya kisiasa. Ripoti yake ilionyesha kuna 1.5t isiyo na maelezo mujarabu, mpaka leo kamati ya PAC wamewahi kuitoa bungeni kama inavyopaswa? Hiyo nguvu na jazba ya spika ni kutaka kuficha hayo matumizi mabovu ya pesa ya umma fullstop.
Hizo nguvu wanazitumia kishamba sana kiasi kwamba kila mtu anajua nini wanataka kuficha, kile kitendo cha spika kumuita CAG kwa pingu ndio ushamba wenyewe wa madaraka.
 
huyu jamaa figisu atazofanyiwa ndani na nje ya nchi harudi 2020.

mwisho wa hii movie ni dhahiri steringi kwishnei!!
 
Majibu ya hesabu yanatolewa hadharani? Siku ile alienda na vitabu pale? Pale yale majibu aliyompa yaliendana na hadhira na hakuhitaji malumbano maana sio mtu wa malumbano ya kisiasa. Ripoti yake ilionyesha kuna 1.5t isiyo na maelezo mujarabu, mpaka leo kamati ya PAC wamewahi kuitoa bungeni kama inavyopaswa? Hiyo nguvu na jazba ya spika ni kutaka kuficha hayo matumizi mabovu ya pesa ya umma fullstop.
ahhhh hahahh,hizo propaganda tu,hii nchi ikipigwa 1.5 kuna watu hawatalipwa mshahara miezi miwili
 
Kama uzalendo ndio huu, nime-declare sitataka kuwa mzalendo hata siku moja.Acha niwe wakala wa mabeberu.
Mkuu hii statement yako imenifikirisha sana, wengine tunajitahidi kazini tusidokoe hata senti kuonyesha uzalendo kesho unasikia watu wamepiga 1.5T halafu wanapata na watu wa kuwashangilia, mwisho wa siku unajiona fala.

Uzalendo ulienda na Nyerere.
 
ahhhh hahahh,hizo propaganda tu,hii nchi ikipigwa 1.5 kuna watu hawatalipwa mshahara miezi miwili

Unaweza usiipige 1.5t uweke mfukoni yote, lakini unaweza kufanya miradi ya upendeleo na katika hiyo miradi ukala 10% yako. Mfano halisi wa hizo hela ni mradi wa Chattle airport. Tunasema hivi, tunataka kujua 1.5t zilitumika kwenye nini na ruhusa ya nani fullstop. Kitisho cha pingu hakiwatoi. Huyo spika aliyejigeuza PS wa jiwe hana bahati safari hii.
 
Unaweza usiipige 1.5t uweke mfukoni yote, lakini unaweza kufanya miradi ya upendeleo na katika hiyo miradi ukala 10% yako. Mfano halisi wa hizo hela ni mradi wa Chattle airport. Tunasema hivi, tunataka kujua 1.5t zilitumika kwenye nini na ruhusa ya nani fullstop. Kitisho cha pingu hakiwatoi. Huyo spika aliyejigeuza PS wa jiwe hana bahati safari hii.
mbona Polepole aliwaeleza kila kitu
 
Back
Top Bottom