My week end is super crazy

Afadhali imekupa uzoefu mpya na kujifunza mambo mapya hasa namna bora ya kumlea kijana awe tayari kuishi mazingira tofauti tofauti.
Kabisa.
Tena bora siku hizi anatoka hata kucheza nje๐Ÿ˜€
Zamani ilikua ni ndani tu.
Kipindi cha likizo alikua mpweke.
Siku ya kwanza katoka nje jirani alinipigia eti mmesahau kufunga geti fulani katoroka ๐Ÿ˜€๐Ÿ˜€ namuona huku nje๐Ÿ˜€
 

Alinifanya nitafakari mambo mengi sana. Tukamwambia, sio mara zote tunakua na pesa, ndio maana tunanunua vitu vya kutosha mwezi mzima. Tukamuuliza, ukitoka shule ukafika nyumbani ukaambiwa chakula kimeisha hatujanunua itakuaje? Akasema si Dada atawapigia simu bodaboda akanunue vitu? Tukamwambia bodaboda anataka pesa, na kama hatuna wakati huo itakuaje? Akasema, mbona kila siku hua kuna pesa kwenye pochi ya Mama? Tukamwambia zina matumizi mengine.

Ila cha ajabu, ukirudi na vitu nyumbani anavyokupokea atasema thank you Daddy for us buying stuffs, kumbe kichwani hua ana maswali yake.

Ana maswali mengi sana kuliko Dada yake mkubwa.
 
Wala usijali sana yawezekana nina ma tv mengi ila na wewe una kitu hata nikiuza hizo tv zote siwezi kukipata.

Pia maisha ni furaha.
Kuwa na ma tv mengi haimaanishi mtu ana furaha.
Kama una furaha ushayapatia maisha.
Aaah Pridah acha kunipanga basi๐Ÿคฃ๐Ÿคฃ๐Ÿคฃ๐Ÿคฃ
 
Huyo hela yake itatoka baada ya kufanyiwa uhakiki wa kutosha.
 
What is week end? Hebu tafsiri kwa kiswahili ili nielewe.
 
Watu wananunua TV kama unavyonunua chumvi.
Halafu huwezi amini zilivyofungwa tu na interest ya kuangalia cartoon imeisha.
Nahisi ile kugombania remote na kupigana pigana ni starehe kwao
 
Halafu huwezi amini zilivyofungwa tu na interest ya kuangalia cartoon imeisha.
Nahisi ile kugombania remote na kupigana pigana ni starehe kwao
Ndo hivyo.

Kuna dogo alikuwa analilia sana game kila ikitoka lazima apate, tena apate mapema kabla ya wenzake.

Lakini akishaipata anacheza hata wiki haifiki anaitupa pembeni kashaisahau.

Anashughulika na mambo mengine.

Lakini asipopata sasa, huo muziki wake ๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚
 
Hela za LG 4 kwa mkupuo natolea wapi mtumishi?๐Ÿ˜€

Kina Junior acha wapambane na solarmax macho yao bado hayajaona mengi hayawezi kuharibika.

Mimi na wewe tushaona mengi haya macho tukizembea kidogo tu tunaanza kuona ukungu๐Ÿ˜€๐Ÿ˜€
๐Ÿคฃ๐Ÿคฃ๐ŸคฃWewe naona unatakq kuua urafiki na hao nduguzo wakitoka huko majuu wakute unawatazamisha kina junya solarmax
 
๐Ÿ˜€๐Ÿ˜€๐Ÿ˜€
Ila watoto wana visa jamani๐Ÿ˜€
Nimempigia picha huyo dogo nimejikuta nacheka๐Ÿ˜€

Ila pamoja na hekaheka zao zote huwa wanaburudisha sana.

Wana uwezo wa kukukera mpaka ukatamani kumtupa dirishani hlf ndani ya dakika akakufanya utabasamu na usahau yote๐Ÿ˜€
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn moreโ€ฆ