My cup runeth over ~ Na Kikombe changu kinafurika

My cup runeth over ~ Na Kikombe changu kinafurika

A. TEAM HAPPINESS

Patric kichwa mzungu mkuti, haja plan kupata mtoto mwengine, akamchungua Maringo wake wakarudi nyumbani, anampikia, anamfulia, Rasheeda anaulizia alipo haambiwi hajibiwi simu hazipokelewi, kesho yake akaenda kumwombea ruhusa ofisini ya bed rest miezi 4 akaambiwa azifanyie kazi from home! Maringo akafurahi alihusi kibarua kimeota nyasi!

Patric akaajiri maid wa kampuni 2, mmoja wa mazingira ndani na nje ya nyumba mwengine wa kupika na kufua

Mrembo akaenda kulipiwa mahari na Musa kwao, process zikaenda vizuri kabisa, kurudi nyumbani baada ya sherehe Mrembo anatapika, kupelekwa hospital ana kibendi miezi 3 Muss oya oya nyiiimgi kafurahi anakuwa baba

Selina in Dubai, ameshazoea therapy akili imekaa sawa, akapewa assignment kwenda kushop nguo za watoto, akaweza akafaulu halii tena, akaambiwa aka shop nguo ya wedding akaenda akawa anaskia uchungu akarudi akafeli test akaendelea na therapy kwa muda wa wiki 3 akaambiwa arudi tena kushop nguo za watoto na harusi, kwa watoto akapitaa kwa harusi akapitaa
Kesho yake akarudishwa kushop kwa nguo za wajawazito, hakulia akaambiwa amepona test ya mwisho kwenda kufunga ndoa church, akapewa test ya madhabahuni akiwa amevaa gauni la harusi akatembea kwenda madhabahuni anasubiriwa na mumewe hakuskia uchungu, akafaulu test, therapy ikaisha ada imetendewa haki
Akampigia simu Drogba aje, baada ya siku 5 akaja, anamshangaa selina amenenepa, anashangaa ana furaha, ana amani, kapendeza, ana imani, wakazuruuuura dubai huku wanapigana mechi, siku moja akamwambia Drogba kwanini mimi na wewe tusifunge ndoa hapa hapa, mapenzi ni ya wawili sherehe kubwa itafanyika kwenu Lagos, Drogba akasita kwanza akampiga mechi, kamkolezaaa weee, Drogba aka give up, wakaenda kanisani Dubai wakaoana, Selina anafuraha wakaenda honeymoon wanapigana mechi, siku ya kuondoka kurudi Lusaka wako airport, Selina akatapika Bwaaah, eh vipi mke wangu
Selina: hata sijui labda malaria. Wakasafiri salama kufika nyumbani Lusaka Selina akatapika tena, Drogba akampeleka hospital, kucheki anamimba changa ya wiki 2. Drogba akafurahi na Selina akaona Mungu kamkumbuka! Drogba akaharakisha sherehe ya harusi kwaooo Lagos!



Neema ameshakuwa bingwaa anasafiri anaenda kijijini anapewa mechi, anarudi lusaka Masoud nae kakolea wanapigana mechi anarudi kijijini, siku wanapeana mapenz, Neema akatapika kamtapikia Masoud, Masoud bado yupo ndani ya Neema, uuuwi wakaachana akaenda kutapikia bafuni, baadae wamekaa wanakunywa chai anazidi kutapika, wakapelekana hospital kama kumbikumbi, kupimwa anamimba ya miezi 2
Masoud akafurahi sio kitoto, mke wangu si nikuoe tu me sipendi kuzaa nje, Neema anacheka tu sawa mume wangu

Pastor waki na Mary siku wamelala ndani Dereva akaingia, tobaa Mary kalala na Pastor huo ugomvi haukuwa mdogo, dereva katukana na wewe, matusi matusi Mary katukanwa mpaka Pastor kaingilia kati, wakaanza kupigana ngumi nanwewe Pastor kapigwa mpaka kazimia, Mary akamzoazoa pale mpaka hospital, wanaingia hospital akina Neema na Masoud wanatoka, Neema kumwona anashangaa imekuwaje, wakarudi ndani kufuatilia, Mary haongei baadae dokta anasema Pastor amepata nafuu lakini tunamlaza, Mary akapumua, Dokta akamwuliza kuna nini, kabla Mary hajajieleza Dereva akajibu nimempiga mimi ananichukulia mke wangu, nimemfumania, Neema akasema kweli mfuska ni mfuska huku anacheka bora me niliondoka kwenye maisha yake ningekufa na ukimwi buree wakaondoka na Masoud, Mary anashangaa statement ya Neema ana ukumwi?! Akachoka na kuchoka akakaa chini sakafuni

Itaendelea saa 10 Jioni
 
A. TEAM HAPPINESS

Baada ya siku 1 kupita dokta akaja na majibu ya Pastor, tobaa roho yangu Pastor ameadhirika ana ukimwi! Dadeki!
Mary akalowa hana hali, network imekata kichwani, dokta tafadhali pima tena, yakarudiwa virus zipo pale pale tobaaa roho yangu! Ina maana na mie ninao, akalazwa kwa presha akaja Patric kumcheki, maana alimtafuta akamkosa alitaka kuona watoto, dokta akampa cd yote! OMG akamdanganya dokta me mumewe naomba mpime kila kitu, Mary hajui hili wala lile majibu yameletwa na yeye ameathirika! Patrix akaweka mikono kichwani, WTF?! Aids?! OMG! Akacheeeeeka dokta akamwuliza unacheka nini?! Apatric: akamjibu how about that, cash me outside!
Doctor haelewi akahisi Patric ameloose network, wakampima na yeye kiiila kitu! Wakakuta yupo vizuri jamaa hana Aids wakasubiri ametulia wakampa majibu akashukuru hakuamini, dah akashukuru mazima, akauliza mkewake Mary amepataje ukimwi akaambiwa ametoa kwa Pastor! Akajisemea tu maombi ya alfajiri kwa Pastor yamejibu!

Njiani anajiambia mke wangu atakufa tu na watoto watakuja kwangu akawa anajichekea akaondoka kwenda kwa Rasheeda akampa ubuyu, inabidi na wewe ukaicheki afya yako maana me sina Rasheeda akaibua ugomvi, tobaaa bonge la gomvi na siendi walaa nini Patric akaona hapakaliki hapa akaondoka kwenda kwa Maringo akakuta amani tele akakaa hakuongea kitu,
Maringo best rest anaifurahia, working from home msahara unaingia kama kawa, anaskia raha asijue Patric kaponea kwenye mdomo wa mamba

Dereva kurudi akadai ajue afya ya Mary, dokta akasema mumewe ameshapewa kila kitu na tumempima nae pia yupo salama
Dereva: mmempima nini?!
Dokta: afya yake maana alizimia
Dereva: afya ya Mary ipo vipi?!
Dokta: siruhusiwi kusema kaka wewe ni nani wake?
Dereva: me mpenzi wake
Dokta: akaangalia tu chini maana ilo picha ni hatarious!
Dereva akalazimisha apewe majibu Mary akiwa amelala akashtuka mnagombania nini, Dereva akafunguka, Mary akamwambia Dokta me nipo divorced na huyu ni mume wangu mtarajiwa, naomba tu usome matokeo hapa hapa mbele yake
Dokta akafanya yake, wishes za mgonjwa ni command kwake
Akasoma matokea ya Pastor kuwa ana ukimwi, akasoma ya Mary kuwa ana ukimwi!
Lahaulaaaa! Akajisemea Dereva! Akaaa chini kabisaa maana alikuwa amesimama! Akamwambia dokta soma vizuri tafadhali, Dokta akarudia! Dah Mary akajilalia usingizi huku analia
Dokta akampooza Dereva usilie tafadhali maana unamfanya mgonjwa azidiwe kwani wewe hauna ukimwi kama unataka ku prove inabidi upime!
Dereva akakataa akaondoka zake nyumbani anamlaumu Mary, we ndio umeniua mnyama mkuwa, Mary akamjibu wakati unanikamatia kamatia haukusema nakuua sasa hivi ndio nakuua?! Utajiju tukutane ahera kama sio Paradiso!

Masoud akamwambia Neema inabidi tukacheki afya zetu kabla hatunafunga ndoa, wakaenda kupima hawana mawaya, Masoud akamwambia Neema inabidi nikutie out kesho tafuta nguo yako nzuuuri tunaenda vacation pakakucha wakavaa wakakodi taxi mara wanaona wanaenda mahakamani, kufika Masoud ameshaandaa kiiila kitu ameshalipia wakafungiwa ndoa! Neema akafurahi na mimba yake ya miezi 2, officially Mrs Masoud, kweli wabongo ni wazuri basi tu mpenz msomaji hautaki kukubali, Mbongo anaweza olewa mara 3 hata 5 akamzidi Kim Kardashian. Wakaingia honeymoon zao Dubaaaaaiii, Neema anajiambia ningefia kanisani mie kama sio kuthubutu ningefikaje Dubai, kha! Akajilia zake raha na mimba yake nene!

Luwi na Evelyne wamerudi toka honeymoon maisha yanaendelea Luwi akarudi mzigoni na Evelyne akarudi mzigoni
Baada ya miezi 2 eve aka concive! Kucheki ana mimba ya mieiz 3, akampigia wifi yake maringo akamweleza, Maringo akampa hongera akamwambia me nina mwezi tu hapa nijifungue, Eve anashangaa me sina habari wifi yangu nitakuja kukuona usikonde!

Rasheeda akawa hawasiliani tena na Patric wamenuniana tangu aambiwe akapime ni muda sasa na hela zinaanza kukata za matumizi, akaamua kijisalimisha kwa pilato akaenda kupima akakutwa hana, akamtumia sms Patric ukimwi me sina nani alikudanganya, usiku wake Patric akaja kuhakikisha akakuta ni kweli! Akaamua kumwomba msamaha kwa kumpooza!

Alfajiri maringo akamkumbuka mama yake akampigia simu Mama sijakusikia muda miezi 2 sasa, wakaongea palee akamweleza mamake kuwa anamwitaji aje akae pale maana ana mwezi tu ajifungue, mama akafurahi akamwamsha Patric, Maringo kusikia Patric yupo pale akakata simu na kuizima kabisaa!

Manoa na Kungwi wameshazoeana kwanza kungwi mwenyewe ameshapigwa chini na Masoud akamfuata nyumbani kwake kungwi ameficha pete ya ndoa wakaenda kucheza mieleka palee Manoa akapropose Kungwi anashangaa! Kha! Akakubali ombi la Manoa!
Asubuhi akapigiwa simu na Rasheeda akapewa umbea toka kwa mke wa Dereva mumewe amepata ukimwi, akamtania Kungwi me mwenyewe nimeenda kupina huku, na wewe ukacheki afya haya mambo ya Bubaa hatuyawezi asee, me nipo safi mweupee kama malaika, kungwi akamwambia me nipo safi maana hapa nimeshakuwa Proposed na ex wako manoa, Rasheeda akampa hongera sana all the best jamani nawatakia maisha mema me nipo nitashughulika mia mia, Kungwi akaliweka akilini la ukimwi, siku akaamua aende kujichekia tu afya!
Tobaaa roho yakeee! Kupimwa amejaza miukimwi sio kitoto! Akaliiiiiiaaaaaaaa aliliiiiiaaaaaa hakujua ameupatia wapi ule waya, aliliiiaaa mpaka akakaribia kuchanganyikiwa akalazwa na dokta kwa kuchomwa sindano za usingizi, akapigiwa simu Manoa akaambiwa mkewe amelazwa, akaja fasta kusikia majibu akawa mdogo kama nukta, wakaona wamcheki Afya Manoa akakimbia kabisaa hakutaka kuangaliwa, aliogopa sana, akaamua akimbia aache marehemu mtarajiwa kwa hospital bed!
Kungwi akaulizws hauna mtu mwengine wa karivu akamwambia nina mwanangu anaitwa Pendo mpigie, akapigiwa wakaja na Joseph wakaambiwa mama yao ni mwathirika kwahiyo wajue jinsi ya kuishi nae! Wakachoka, basi wakamtia moyo pale na nini, wakaruhusiwa aondoke nae wakaamua kumchukua akaishi nao

Harusi ya Selina aikafanyika lagos Nigeria, ebwana ee bonge la dude bonge la sherehe bonge la mipedeshee! Anamwagiwa tu mi dolari! Rain money kwa wiiingii! OGA anamkaziiiia Selina kwanza haamini ana mimba ya miezi 2 akaona ana fekisha. Didie anamfurahia shemeji yake na pacha wake kuoa. Dance dance dance mpaka alfajiri, wakaenda zao honeymoon Mrs Drogba on fleekest!



Kungwi anawaza kazoa wapi miwaya, akawa anakumbuka ramani zoote alizochepuka! Akamkumbuka Drogba laba kale katoto kana miwaya nini?! Anawaza hamalizi labda Ismail labda maswali anajiuliza mwenyewe anajijibu mwemyewe haelewi!
Akawa anasononeka pale akaja Caroline, anamwongelesha kidhungu anataka wakacheze nae, bibi mtu anakataa amechoka, Caroline anamlaumu kiila siku unaumwa tu jaman twende tukachezee, Kungwi hataki, Caroline akamwambia mbona umekuwa weird skuhizi au kwasababu unaumwa ukimwi?! Niliskia mama na baba wanaongea chumbani ila hawakujua kuwa naskiliza,
Kungwi akachoka dah hadi watoto wanajua hii mbona kali sasa?!
ITAENDELEA KESHO SAA 5 ASBH
 


Haya nimeskia kilio chenu, bado nipo kwenye Team happiness wengine mnataka kuwasiliana na mie
Me napatikana whatsapp tu namba yangu +255688411043 usipige hiyo ni namba ya whatsapp tuu!

A.TEAM HAPPINESS

Hidaya amekaa zake barazani anakunywa chai saa 3 asubuhi anasikiliza redio wee baadae akanaliza chai ukapigwa mziki wa Pepekalee Hidayaaa! Akaanza kucheza huku amekaa anafurahi mwenyewe! Jina lake linaimbwa!
Mara akaingia ismail anamkuta Hidaya ameshasimama anacheza, wakaanza kucheza nae mpaka mziki umeisha wakakaa chini wanahema, mara Ismail akaona gari imepaki nje ya ofisi yake akakimbia mbio kumbe ni Patric!

Hidaya nae akaingia ndani akafunga milango yote na dirisha kubwa akaingia chumbani kwake ananasa king'amuzi.
Patric: nimekuja kuongea kuhusu ile evidence nataka niondoke nayo maana usiku nimeora kiza kinene kipo mbele yangu!
Ismail: mh! Mheshimiwa, ungeacha kwanza tuje tuivuruge huku huku usije enda nayo ukapatwa na matatizo bure!
Patric: hapana mzee acha me najua oa kuificha
Ismail: basi uje alhamisi tuichome hapo msitu wa kati, nimeificha huko
Patric: sawa hamna neno! Wakawa wanaongea mambo mengine Ismail akapewa mil 5 na Patric akaondoka

Hidaya kadaka maongezi yoote akawapigia mjini kuwa mishe imewekwa alhamisi ila sio confirmed kamili ila nitahitaji team ije inipe support huku. Mara akasikia hodii! Akazima simu haraka akaja sebulen, kufungua mlango ni Ismail, vipi kazi zimeisha?!
Ismail: ah we fungua tu bwana mlango nimepigiwa simu mjini kuna dhoruba nimechanganyikiwa
Hidaya: nini tena jaman
Ismail: mke wa Masoud ana ukimwi na inasemekana na Manoa alikuwa anatembea nae ameukwaa huku anaheeema kama kakimbizwa na simba!
Hidaya: ok kama anao ukimwi we unatetemeka nini au ulikuwa unatembea na kungwi?!
Ismail: akaona kawahiwa akadanganya, hapana mke wangu ametembea na Manoa sasa naogopa
Hidaya akapanik kwani wewe, yani, eh! Inamaana na wewe unao?!
Ismail: hata sijui kwakweli sijapima ila sijaonana na mke wangu huu mwezi wa 8
Hidaya kichwani akajipa moyo lakini bado ana wasiwasi, sasa mpenz me nawewe itabidi twende kwa dokta tukapime ukimwi unaonaje?!
Ismail akawa mduuuchuu! Akakubali shingo upande basi tutaenda jumamosi ijayo,
Hidaya akaaga anaenda kumwona mjomba wake mjini atarudi j4!
Ismail akawa amekaa tu hajaskia anachoongea akaomba apumzike kwanza ataongea baadae, Hidaya akamlaza chumbani kwake yeye akaendelea na kazi
Ismail kakaa siku nzima hajatoka ndani, anaishia seblen anakula anarudi kulala, usiku wamelala akaanza kumpapasa Hidaya! Hidaya kamchomoa hapana asee leo me siwezi kukupa umenishtua mbovu! Mpaka tukacheki afya ndio nitakupa, Ismail akachanganyikiwa mara 3 akalala zake fofofo

Kandi na Joe wamerudi toka honeymoon, kandi sasa ana mimba ya miezi 5, tumbo limesogea sogea sio kitoto! Joe anampa ma care ya kufa mtu, hata kutembea hataki anamsukuma kwa wheel chair, kandi akajiuliza ivi kwanini nilimkimbiaga Joe maskini sa hivi ningekuwa mbali kweli, ama kweli alilopanga Mungu mwanadamu asilitenganishe!

Patric akarudi Lusaka amefikia kwa Maringo, usiku wamelala Maringo anahangaika tumbo la muuma, akapelekwa hospital na Patric, kumbe saa ya kujifungua imefika, akajifungua mtoto wa kiume Maringo akafurahi, wanambeba mtoto wanakiss kiss, wakashinda hospital siku 3 wakaondoka nyumbani Patric akamwambia inahitajika mama aje sasa, me naondoka nitarudi ukimaliza uzazi la hasha ukitaka nije mtagombana na mama yako. Akamwachia dola 5000 za matumizi akamfanyia shopping akamwachia mil 3 za hospital, usafiri wake akajaza Petroli, kabla hajaondoka, wakapanga jina, mtoto akaitwa Patric Junior. Akawaaga Akaondoka! Maringo akampigia mama yake Rasmi aje, wakati Rasheeda anajiandaa kutoka Patric akaja, wakasalimiana Rasheeda akampa good news Patric akampongeza akampa mil 2 ya kuuguza akamwambia me nitakuwepo hapa ukunihitaji niambie, Rasheeda akafurahi akaondoka akijua nyuma kaacha bonge la bwana linamsubiria

Neema na Masoud wamerudi toka honeymoon, Neema mimba inakua sasa ni mwezi wa 5, Masoud akamhamisha pale kwake akaenda kumweka kwenye jumba lake la kifahari na watoto wake wote, ile nyumba yake na Pastor akaipangisha! Wanapendwaje sasa! Wanaangaliwaje vzuri sasa kuanzia food, clothing, shelter, madikodiko, Masoud full mass nondo!

Selina na Drogba wamerudi toka honeymoon, Oga na Didie wapo lusaka wanaendelea na kazi, Selina mimba ishakuaaaaaaa miezi 3 sasa! Katumbo kanasukumika kwa mbele kimtindo! Drogba anampendajje sasa, kila saa anampigia simu, kamwekea maid 2, gardner, kazi kamwachisha, akawa amekaa tu ndani analea mimba mpaka atakapomaliza uzazi atafungua biashara, Selina akajiona kama malkia wa nguvu! Sio kwa kupendwa kule, mechi kila siku, simu kila siku, kha Nigeria kaamua!

Pendo yupo na biashara yake sikunyingine mamake anakuja dukani kwake wanakaa, wanarudi wote, skunyingine anaenda job na derev, maana mimba ishakuwa miezi 6 sasa Joseph anampendaje mke wake, duka limepanuliwa likawa kibwa wateja kibaoo! Wanakuja washapazoea kazi zinakuwa nyingi inabidi kungwi amsaidie
Kungwi siku 1 akakaa kwenye akili yake ya kichina, akammpigia Drogba me nina mazungumzo na weee, Drogba akamwambia me nishaoa am happily married, kungwi akamwambia me nina ukimwi na sijui nani kaniambukiza, mh Drogba akawaza akakata simu. Kungwi akajiambia na atanitafuta kama ndio au sio muhusika. Wakiwa wamekaa miezi 3 bila kuwasiliana na Manoa akaona isiwe shida akaenda kwa sonara, akaulizia ile pete alovikwa ina thaman gan?!
Akaambiwa mil 4. Akaona nyiiingi akauza, akapewa mil 4 zake akaondoka,njiani akampigia Rasheeda kama yupo akaambiwa anamzazi analea, dah akachoka akarudi kwake. Jioni akamwambia Pendo na Joseph mimba yako bado sana na mimi nimechoka kukaa Lusaka nataka nisafiri niende nchi zingine kutalii na kufanyiwa psychology! Maana nahisi akili yangu haijachangamka! Wakamchangia mil 8 wakampeleka Dubai, wakalipia matibabu yake, na ndege kwenda na kurudi Kungei kudadeki on 1st class plane! Anakaa na wazungu anashangaa shangaa kweli mama mkwe bobaaa, Dubai mojaaa english anaiweza ye si mwalimu bwana, akafika airport akakuta mtu kashika jina lake kwenye bango, akamfuata akapelekwa mpaka hotelini, 6star hotel, akapewa line mpya ya simu, akapewa time table ya kwensa na kurudi kwenye matibabu,
mwenyewe anashangaa ulaya ndogo kapelekwa ulaya ndogo hata mumewe hajawahi mpeleka, akaona hizo ndio baraka za mwisho kabla hajaondoka duniani, akajiambia Mungu asante ningefika lini Dubai kama sio ukimwi?



ITAENDELEA SAA 9 NANUSU ALASIRI
 
B. TEAM BUBAAA

Mary akatoka hopsital kurudi home yupi anandoned Dereva kaondoka na kila kitu chake, akasikia simu inaita watoto wanatakiwa kwenda kufantwa shuleni likizo imeanza, akajikusanya akaenda kuwafuata kwa taxi!
Watoto wanafurahia kumwona mama yao hawajui chochote kuhusu divorced. Wakafika nyumbani wanahamu ya kumwona baba, baba amesafiri baadae akampigia simu Patric watoto wamerudi wanakuulizia uje ulale, alafu kesho tutawaeleza, Patric kwa kuwa yupo pekeyake kwa Rasdeeda akaona bora tu aende, wakasalimiana na watoto pale wakaingia kulala, Mary akalala kitandani Patric chini kwenye godoro, watoto hawana habari wanajua mama na baba wanapendana mambo shega!

Asbh wakaamka vizuri baba akapika chai kila kitu baada ya msosi kila mtu chumbani kwake baada ya masaa 2 watoto wakaitwa Library family meeting, wakaelezwa kila kitu watoto walilia hawaelewi nini maana ya talaka ingawa darasani wanaisoma practicality yake hawajaambiwa, wakalia wee ikabidi sa Patric alale tena pale mpaka waelewe, watoto baada ya wiki ndio wakaanza kuelewa somo, Patric akamlipa psychologist aje awahudumie kwa muda wote watakao kaa likizo na kuwaelezea hali ya mama yao Maria kuwa ana miwaya! Tobaaa watoto wakazidi kuchanganyikiwa our mom is dyiiiing?! Hooow?! Dokta akawaweka sawa wee mpaka akili ikakamata network



Maria analia haelewi atafanyaje akaomba aongezewe session ya daktari kwake ili nae apate kuelimishwa juu ya elimu ya ukimwi.

Hidaya akaenda mjini kupima miwaya akakutwa holaa! Alashukuru dah me nilijua yule mzee labda kapasua condom kudadeki! Akafurahi maana hizi kazi zetu bwana kama hautakufa kwa kuuliwa utakufa kwa ngoma. Akaenda kutoa maelezo aliosikia kwa akina Ismail kwa Boss wake!
Alhamisi ikafika akaletewa team ya watu 3, wanaume wa nguvu, akawa anasikilizia kwa Ismail kama Patric anakuja au haji
Patric akapigiwa simu na Ismail, akaulizwa anakuja kama walivyoahidiana?! Patric akasema nina mambo ya kifamilia sitaweza kuja nitakuja next week j4

Ismail akamwambia mkewe wakapime ukimwi kwasababu alikuwa na mahusiano na manoa, wakaongozana mpaka Lusaka hospital kupima, majibu kutoka Soya ana miwaya Ismail kaponaa! Ismail akajiona ameponea kwenye mdomo wa mamba, kha! Siamini wakarudi nyumbani anamlaumu sana mke wake kwa kusaliti ndoa na Mungu kamwuumbua,mkewe akawa analia tu anaguna mmh! Akahisi mumewe kahonga matokeo basi akaubaliana na hali halisi akawa anaishi kwa adabu akawa anaenda hospital ya kijiji kupata elimu juu ya VVU.
Ismail akaanza kufunguka kwa Hidaya matokeo yangu haya hapa leo buna furaha Mungu ananipenda sio kitoto, wakafurahi wote kujua hawana VVU wakapigana miti! Hidaya nae mtamu sio kitoto! Ismail kakolea mpaka akampa ahadi ya kumuoa!

Kungwi darasa likakolea dubai kudadeki, akawa anakaribia kumaliza, wiki ya mwisho akapelekwa wodi ya wagonjwa wa ukimwi ili kumfanya awe motivated kuto skip dawa za VVU! Akawashangaa wale ambao wameshachokaaa wanasuburi kufaa! Uuuwi anaogoopaaa akaambiwa ukicheza utakuwa kama hawa zingatia sana dawa na kuwaona madaktari! Ile hali nahisi ilimharibu kisaikolojia kuwa na yeye atakuwa kama vile! Mungu weee na mie nitakonda kama msumari?! Akiwa amekaa chumbani kwake anawaza! Mara analia mara anatukana mara anauchungu mahasira sheedah tupu!
Safari ya kurudi Lusaka ikawadia, ame enjoy to her fullest. Kabla hajaondoka akaenda kushop shop, akajaza sanduku 2 akalipia mzigo extra. Akashop na nguo za mjukuu wake mtarajiwa na Caroline.
Akapokelewa Lusaka vizuuuri, akafurahi mwenyewe baada ya siku 3 akagawa zawadi kwa familia yake
Drogba akaenda kupima ukimwi akakutwa hana akampigia simu kungwi, akamchaaambaaa we jimama vepee mshenzi mkubwa jini mchomoa roho wewe, unataka kunigombanisha na mke wangu unaniambia na ukimwi kufa pekeyako huko! Kungwi kikamuuma akamwambia we mtoto nikome tusitukanane ntakuendea Polisi, drogba akamwambia nenda hata Mbinguni me wala sina shida na nilichokiongea, Kungwi akamshukuru akambariki ubarikiwe we mzima haujafa haujaumbika! Akakata simu

Selina mimba ya mieizi 5 akaanza kuumwa sana, akapelekwa hospital akawa anapewa matibabu anarudishwa home, baada ya wiki mbili amelala usiku akasikia kama maji yanamtoka akapiga kelele kumbe ni damu mpaka anafika hospital mtoto keshafariki, doh Drogba aliliaje sass anamwuliza dokta kwani kuna nini hii mmba ya pili mke wangu inamtoka ana nini?! Embu mchekini kiiila kitu, wakamcheki, majibu kutoka yupo fresh kila kitu kasoro ana ukumwiii! Drogba anashangaa how?! Me nalalaga nae mbona sijapata?! Wakampima tena Drogba kuchekiwa ukimwi umejaa, akachanganyikiwa mara 3, wakamwambia ulipimia hospital gan, akaitaja wakamwambia ile hospital frmeki rudi ukalalamike, akamwacha selina akaenda kulalamika yakaja majibu yake akaambiwa anao skuile dokta alichanganya majibu yake, tobaaa Drogba aliliaaaa! Akampigua pacha wake akameeleza akaja kumtia moyo akamwambia me najua alieniua ni Kungwu naomba ukacheki Afya yako, kwenda kucheki Didie nae anaoooooo! Tobaa akachoka mara 2 akaja akamwambia Oga, Oga nae kwenda kucheki afya akakutwa kapona hanaa! Hakuamini macho yake wala nini?! Akaenda tena hospital ingine kucheki hamna. Akarudi kuwaeleza kaka zake kuwa, hana ukimwi akaanza kuwatia moyo ola rohoni anamcheka Drogba kadandia gari la selina kwa mbele!
Selina kuja kupewa matokeo ya mtoto wake na afya yake kuwa ana miwaya akapata mshtuko, presha ikampandaa sanaaaaa akashindwa kupumua ma dokta wakashindwa kum control akafa.
Drogba aliliaaaaa, hakuelewa ni mkosi gani, imagine tangu mke wake ampeleke hospital hajapata hata nafasi ya kusema hello au pole! Aliliaaaa! Lia na weyee! Tobaaa! Aliliaaa kaka zake wanambembeleza pale hataku kubembelezwa Drogba alikuwa analia na mambo matatu ati kapoteza watoto 3 mke na afya yake ni sheedah!



Patric amelala wiki nzima anaota ndoto mbaya mbaya tu, mara ananyang'anywa cheo anakuwa maskini. Mara anaenda jela mara anapigwa risasi mara anaenda Mbinguni anarudishwa motoni wiki nzima amekosa raha akaona labda nimelala nyumbani kwa Rasheeda embu nirudi hotelini nayo ivyo ivyo ndoto zinajirudia akachoka anakosa raha hajui mbele yake kuna nini akapanga kwenda kanisa la kilokole kuombewa

ITAENDELEA SAA 4 USIKU LEO
 
Back
Top Bottom