Sorry naomba unijibu kama hutojali. Inagharimu kama kiasi gani kwa kila kitu kuanzia usafiri, accomodation etc
Mkuu kwa nini nisikujibu?? Don't you worry kabisa.
Kuhusu usafiri yaani flights inategemea unataka kusafiri na shirika gani la ndege. Kutokea Tanzania nadhani mashirika yanayokwenda huko ni Qatar airways, Turkish airways, Ethiopian airways, Emirates airways, sasa ukitaka the cheapest one kati ya hayo utachkua Ethiopian. Bei yake itagharimu kwenye $600-$700 hivi kwa mtu mmoja na hiyo ni return ticket.
Kuhusu accommodation itakugharimu $30 kwa chumba kizuri tu, japo vipo vyumba vya chini ya hapo. Kuhusu kula, ukiwa na $20 per person kwa siku wewe ni tajiri mkuu unapiga meals za maana. Kuhusu excursions almost sehemu nyingi entry fee ni bure. Utalipia kuingia sehemu chache tu na gharama sio kubwa. Most of the places hazitogharimu zaidi ya $10, unless kama utataka tour guide.
Usafiri wa ndani ya Turkey pia ni rahisi. Taxi itakayo kupeleka umbali wa km 80 itakugharimu $30 that means Tanzania taxi ni ghali sana. Kuelkea maeneo ya kitalii kwa pale Istanbul ni kwa mguu maana mengi yapo around Fatih area ambako hotels nyingi zipo.
Public transport zao kama bus na tram na train pia ni bei rahisi and are easily accessible.
Vipi mkuu umepata mwanga kiasi??