Yoda
JF-Expert Member
- Jul 22, 2018
- 57,243
- 90,302
Kuna watu wanamlaumu Nyerere kwamba alijilimbikizia madaraka, kujiweka kama mtawala wa kiimla na hatimaye kutuachia mfumo huo mpaka sasa ambao tunahangaika nao. Ni kweli alifanya hivyo lakini karibia mataifa yote hadi yale yaliyoendelea sana viongozi wake wa mwanzo(founders) walifanya hivyo pia.
Kuanzia Korea Kusini, Singapore, nchi za Ulaya zilizoanza kama ufalme mkamilifu(absolute monarchies) mpaka Malawi ya Kamuzu Banda, Zambia ya Kaunda, Ghana ya Nkurumah, Kenya ya Jomo Kenyatta n.k kote tawala za mwanzo zilizounda mataifa zilifanana katika Rais au Mfalme kuwa na mamlaka makubwa mno yasiyodhibitiwa(unchecked powers).
Hata hivyo mengi ya haya mataifa yameweza kurekebisha hiyo kasoro taratibu au kwa haraka hasa baada ya kupata maendeleo.
Tatizo kubwa zaidi la Africa baada ya uhuru ilikuwa ni kuletewa na watawala mfumo wa kigeni wa ujamaa. Kwa Tanzania ilikwenda mbali zaidi kwa raia kufungiwa kwenye chungu(kwa propoganda na kutofundishwa Kingereza) watu wakabaki hawajui jinsi mataifa mengine yanavyoendelea huko duniani kwa ukweli na uhalisia, sio ajabu mwaka 1992 wengi waliamini mfumo wa vyama vingi utavuruga nchi wakataka kubaki na chama kimoja.
Kama ni kuhukumiwa, Nyerere atahukumiwa kwa haki zaidi kwa haya mambo mawili ya Ujamaa na raia kufungiwa kwenye chungu.
Kuanzia Korea Kusini, Singapore, nchi za Ulaya zilizoanza kama ufalme mkamilifu(absolute monarchies) mpaka Malawi ya Kamuzu Banda, Zambia ya Kaunda, Ghana ya Nkurumah, Kenya ya Jomo Kenyatta n.k kote tawala za mwanzo zilizounda mataifa zilifanana katika Rais au Mfalme kuwa na mamlaka makubwa mno yasiyodhibitiwa(unchecked powers).
Hata hivyo mengi ya haya mataifa yameweza kurekebisha hiyo kasoro taratibu au kwa haraka hasa baada ya kupata maendeleo.
Tatizo kubwa zaidi la Africa baada ya uhuru ilikuwa ni kuletewa na watawala mfumo wa kigeni wa ujamaa. Kwa Tanzania ilikwenda mbali zaidi kwa raia kufungiwa kwenye chungu(kwa propoganda na kutofundishwa Kingereza) watu wakabaki hawajui jinsi mataifa mengine yanavyoendelea huko duniani kwa ukweli na uhalisia, sio ajabu mwaka 1992 wengi waliamini mfumo wa vyama vingi utavuruga nchi wakataka kubaki na chama kimoja.
Kama ni kuhukumiwa, Nyerere atahukumiwa kwa haki zaidi kwa haya mambo mawili ya Ujamaa na raia kufungiwa kwenye chungu.