pasco mwivi ni mwivi tu kama huyo wa jana anaulizwz unsoma nii anasema civics unategemea nibi?. Anyway mshahara wa dhambi ni mauti.
Mkuu Kasindi, pole sana kuibiwa, ila tunatofauti sana kuthamini life values, kiasi cha kuhalalisha hukumu ya kifo kwa mwizi wa kuku!.
Wakati nikiwa hapo Mabibo hostel nikikaa 3 floor zile single rooms, mtu wa opposite room yangu, aliona nilipokuwa naweka ufungio wangu, akafungua akakomba Mac Book Pro laptop, video kamera ya Sony PD 175, Nikon D.70, na vigadgets kibao (wakati nasoma UDSM, nilihamishia semi production zangu kwenye room yangu), worth more than 15M. Akaenda kuviuza kwa jamaa fulani anayenunua vitu vya wizi hapo nje ya hostel kwa laki 500,000 tuu!. Mzigo ukaingizwa sokoni hivyo hivyo ulivyo jamaa akianzia 1.5 mwisho 1!. Kuna jamaa mmoja alipoiona tuu PD 175 akanicall kuniambia kuna kamera kama yangu iko sokoni, inaiuzwa hapo Mabibo hostel pamoja na vitu vingine kibao!. Nikaja kuangalia la haula!, kamera ni yangu!. Nilichofanya kwanza ni ku bargain na jamaa, akashuka mpaka 1.M, nikatuma fungu likaletwa, nikafanikiwa kuikomboa Laptop, Video Camera na Still camera, vingine vidogo vidogo vyote alikuwa kashasukuma!. Baada ya hapo nikaenda polisi kuchukua RB, jamaa muuzaji akadakwa!, hoja ya kwanza ni kuonyesha alikovipata!. Jamaa alikuja mpaka room kwa neighbor wangu!. Naye akadakwa!. Cha kwanza nilidemand fedha zangu nilizokombolea vitu vyangu kurudishwa, vitu vyote vilivyouzwa vikombolewe, kiukweli ilinibidi kuvilipa baadhi!. Jamaa alikuwa aanze kufanya final exams zake za MA, in the next two weeks!.
Warden wa block F alikuwa jamaa mmoja mlokole ila poa sana, akamuombea msamaha, maadam vitu vyangu vyote vimekuwa recovered, jamaa angefukuzwa chuo mwaka wa 6!, aliunganisha na MA!. Huruma ikaniingia, nikakubali kufuta kesi!. Polisi nao wakanigomea huwezi kufuta criminal case, mimi ni shahidi tuu!. Polisi walishikishwa kidogo dogo, kesi ikafutwa bila kufikishwa mahakamani!. Nilisamehe kila kitu!, unconditional!.
Huku araiani nilikuja kukutana na huyo jamaa, ni jitu la Musoma, limeajiriwa Polisi Makao Makuu!, tena wakati huo waziri Masha alikuwa jamaa yangu, almanusura nimharibie kazi!, nikapiga moyo konde yaliyopita sii ndwele!.
Kama niliibiwa items worth more than 15 M nikasamehe!, laptop ndio kiwe kitu gani cha kumhukumu mtu kifo?!.
Uuuaji wowote kwangu ni unyama tuu, licha ya aliyoyafanya Osama, kitendo cha kuuawa kinyama, Saadam, Ghadafi etc, nimewaita Bush, Blair na Obama, wote ni wauaji tuu!. There is no any justification to take ones life no matter what!.
Ndio maana hata serikali yetu nimeiita ni serikali dhalimu ya mauaji kutokana na kuruhusu matumizi ya adhabu ya kifo!.
Mimi ni pro life, ambaye ninaamini life ni zawadi ya Mungu kwa binadamu, only the giver of life ndie pekee mwenye kibali to take out the life!. Uondoaji mwingine wowote wa maisha ni ushetani!. Kuushangilia ushetani ni kumtumikia shetani bila kujijua!.
Pasco.