Mwizi analalamika baada ya kuibiwa: mnachochea hisia ya utaifa!

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,010
1,036
VCG111122968488.jpg


VCG111436818204.jpg


“Ndugu yangu, nimekuwa nikizurura nje kwa muda mrefu...mnaweza kunipeleka nyumbani kwetu China?” Siku hizi, tamthilia fupi ya “Kutoroka kwenye Jumba la Makumbusho la Uingereza” iliyotengenezwa na mwanablogu wa China iliibua mjadala mkali ndani na nje ya nchi. Tamthilia hiyo inaelezea jinsi chungu cha kale cha jade cha China kinachoitwa Yuhu kilivyotoroka kwenye Jumba la Makumbusho la Uingereza ambako kilihifadhiwa na kurudi nyumbani. Lakini, kazi hiyo ya usanii imekuwa mwiba kwenye mioyo ya vyombo vya habari vya Uingereza kama vile BBC na Daily Telegraph, vikidai kuwa inachochea hisia ya utaifa ya Wachina wanaolalamika baada ya baadhi ya vitu vya kumbukumbu ya kihistoria kwenye Jumba hilo kuibiwa, na kudai kurejeshwa kwa vitu vya kitamaduni, lakini kamwe havikutaja ukweli kwamba vitu vya kale vya kitamaduni vya Kichina vinavyohifadhiwa kwenye Jumba la Makumbusho la Uingereza yaliporwa na Waingereza.

Kwa mujibu wa takwimu zisizokamilika kutoka Shirika la Sayansi, Elimu na Utamaduni la Umoja wa Mataifa UNESCO, takriban vitu vya kale vya kitamaduni milioni 1.67 vilivyopotea nchini China vinahifadhiwa katika majumba ya makumbusho zaidi ya 200 katika nchi 47 duniani, na jumba la makumbusho la Uingereza ni moja ya majumba yenye vitu vingi zaidi vya kale vya kitamaduni vilivyopotea nchini China. Hivi karibuni, jumba la makumbusho la Uingereza lilifanya onyesho maalum kuhusu China linaloitwa "Karne iliyofichwa ya China" - vitu vya kale vya kitamaduni zaidi ya 300 kama vile vazi la Malkia Cixi na vazi la mfalme Guangxu akiwa mtoto yalionyeshwa pamoja, kati yao kitu kilichovutia zaidi watazamaji ni nakala ya asili ya "Mkataba wa Nanjing" uliotiwa saini kati ya Uingereza na serikali ya enzi ya Qing. Chini ya nakala hiyo kumeandikwa: Mkataba wa kwanza usio na usawa uliotiwa saini kati ya China na madola. Hii inawafanya watu kujiuliza kuna vitu vingapi vya kale vya kitamaduni "vilivyoibiwa" kutoka China ambavyo vinahifadhiwa kwenye Jumba la Makumbusho la Uingereza? Vinanaweza kurudi nyumbani lini?

Hali halisi ni kuwa sio tu vitu vya kale vya kitamaduni vya Kichina, lakini pia vitu vingi vya kale vya kitamaduni vya nchi nyingine vinavyohifadhiwa katika Jumba la Makumbusho la Uingereza vilikusanywa kiharamu, kwa hivyo Jumba hilo pia limepewa jina la "Jumba la Makumbusho ya wizi". Masalia haya ya kitamaduni ni kama watoto ambao wameondoka nyumbani na kuzurura nje, yakielezea historia ya ukoloni na uvamizi wa himaya ambayo jua halitui. Miongoni mwa kile kinachoitwa "hazina" katika Makumbusho ya Uingereza, hakuna hata kitu kimoja cha Uingereza. Miongoni mwa vitu hivyo, kitu cha kale zaidi kilikuwa ni jiwe la miaka milioni 1.8 lililopatikana kwenye eneo la bonde la Olduvai la Tanzania. Mbali na jiwe hilo, inasemekana kuwa Jumba la Makumbusho la Uingereza lina jumla ya vitu laki 2 kutoka Afrika, ikiwa ni pamoja na Jiwe la Rosetta la Misri na shaba za ufalme wa zamani wa Benin. Huku kashfa ya wizi wa masalia ya kitamaduni kwenye Jumba hilo ikipamba moto, nchi za Afrika zinazidi kudai Jumba la Makumbusho la Uingereza lirudishe vitu vya sanaa katika nchi vilizotoka. Abba Isa Tijani, mkurugenzi mkuu wa Tume ya Kitaifa ya Makumbusho na Makaburi ya Nigeria alisema "Hivi ni vitu vya kitamaduni vilivyoibiwa na vinapaswa kurejeshwa mahali vilipotoka."

Kwa miaka mingi, Jumba la Makumbusho la Uingereza limekataa kurejesha vitu vya kale vya kitamaduni kwa nchi vilizotoka. Sababu ilizotoa ni kwamba ama nchi hizo hazina teknolojia ya kuhifadhi vitu hivyo, au vitu hivyo vinakabiliwa na hatari za usalama. Lakini sasa kuna watu nchini Uingereza wameweka vitu hivyo vya kitamaduni kwenye mtandao wa Internet ili kuviuza! Kashfa hiyo ya wizi sio tu imefichua ujanja wa Jumba hilo wa kukataa kurudisha vitu hivyo vya kitamaduni, lakini pia ilionyesha kiburi na upuuzi wa nchi hizo za Magharibi ambazo haziwezi kuondokana na mawazo ya kibeberu – vinavyoonyeshwa kwenye Majumba yao ya Makumbusho sio tamaduni zinazong’ara, bali ni fahari yao na matunda waliyoiba kwa njia ya ukoloni na uvamizi.

Katika mwisho wa tamthilia“Kutoroka kwenye Jumba la Makumbusho la Uingereza” Yuhu aliyefanikiwa kurudi China, alionyesha barua zilizoandikwa na vitu mbalimbali vya kale vya kitamaduni kwenye magazeti ya Uingereza kwa maandishi ya kale ya kichina, ambazo zilionyesha hisia zao nzito za kukumbuka nyumba. Inawezekana kuna safari ndefu kwa vitu hivyo vya kitamaduni kurudi nyumbani, lakini nchi zote duniani hazitasita kudai mabaki ya kitamaduni yaliyopotea nje ya nchi. Hivi majuzi, Uswisi iliirudishia China vitu vitano vya kale vya kitamadunI, na serikali ya China ilipongeza hatua hiyo. Wakati huohuo, jumba moja la makumbusho nchini Ujerumani lilitumia teknolojia ya DNA kufanikiwa kutambua kuwa mafuvu matatu yaliyochukuliwa nchini Tanzania wakati wa ukoloni, yana uhusiano na ndugu walio hai, na ni uamuzi wao kama wataamua kuyachukua mabaki hayo au la.
 
Inaonekanekana kuna mababu wachina wa miaka ya nyuma waliendekeza njaa wakaviuza, sasa vitu ivyo vimeonekana vina dhamani kubwa na kizazi cha sasa kinataka kurudi thamani hiyo nyumba.


Chonde chonde, hapa sijataja bandari.
 
Back
Top Bottom