Mfufua Nyuzi
Senior Member
- Mar 11, 2024
- 193
- 240
Kijiji cha Makumbusho ni sehemu ya makumbusho inayoonesha nyumba na vifaa vilivyojengwa kihalisi kutoka kwa makabila machache ya Tanzania na liko katikati ya jiji la Dar es Salaam. Ni miongoni mwa makumbusho matano nchini, mengine yakiwa ni makumbusho ya Taifa ya Dar es Salaam, makumbusho ya Mwalimu Nyerere, makumbusho ya historia ya asili na makumbusho ya azìmio la Arusha.
Swali langu; Ni muda mrefu umepita, Je Makumbusho haya yamekuwa na tija gani kwa taifa hususan kwenye jiji la kimkakati na biashara kama Dar es Salaam?
Kwa maoni na mtazamo wangu binafsi, Kwa taifa ambalo uchumi wake bado unasua sua yale ni matumizi mabaya ya ardhi hususan kwa eneo la biashara na kimkakati kama Dar es salaam. Kwanza kabisa tayari kuna maeneo ya aina hiyo yaliyoshiba maudhui kama ya hapo Makumbusho, Mfano kuna makumbusho ya Mwalimu Nyerere, Azimio la Arusha, makumbusho ya vita ya majimaji n.k Sasa kulikuwa na haja gani ya kuweka makumbusho eneo lingine?
Kwa nchi masikini ambayo bado uchumi wake unakua lile eneo ilipaswa pajengwe aidha kiwanda kidogo cha kuchakata vifaa vya umeme au technology innovation space centre ili nchi izalishe vijana wenye ujuzi katika technology wachangie katika uchumi wa taifa. Badala yake eneo muhimu kama lile panajengwa vibanda vya vijumba vya udongo ambavyo si vitu vigeni hata kwa wageni kusema kwamba wataenda kushangaa, kwa sababu ukitoka tu nje kidogo ya Dar es salaam bado kuna watu wanaishi maisha hayo! Kwa hiyo kujenga vile vinyumba pale ni kama kuwakebehi! Kwa sababu bado kuna watu wanaishi maisha yale kutokana na umasikini.
Natambua umuhimu wa Museum, hata ukienda Uingereza pale Yorkshire kuna museum inaitwa York Museum, pia Ujerumani huko kuna museum za Nazi regimes, lakini zilijengwa baada ya mataifa hayo kukua na kuinuka kiuchumi na hata location zilipojengwa haikuathiri shughuli za uzalishaji! Pia tayari wameshatoka huko wapo hatua nyingine ndiyo maana yale yanabaki kuwa makumbusho! Ila sisi bado hatujatoka kuishi kwenye nyumba za udongo au kutumia vinu n.k sasa makumbusho ya nini?
USHAURI; Kwa kifupi Makumbusho village ibomolewe au ihamishiwe huko Kigamboni, Eneo lile pajengwe ICT/Technology Innovation hub/Centre.
Swali langu; Ni muda mrefu umepita, Je Makumbusho haya yamekuwa na tija gani kwa taifa hususan kwenye jiji la kimkakati na biashara kama Dar es Salaam?
Kwa maoni na mtazamo wangu binafsi, Kwa taifa ambalo uchumi wake bado unasua sua yale ni matumizi mabaya ya ardhi hususan kwa eneo la biashara na kimkakati kama Dar es salaam. Kwanza kabisa tayari kuna maeneo ya aina hiyo yaliyoshiba maudhui kama ya hapo Makumbusho, Mfano kuna makumbusho ya Mwalimu Nyerere, Azimio la Arusha, makumbusho ya vita ya majimaji n.k Sasa kulikuwa na haja gani ya kuweka makumbusho eneo lingine?
Kwa nchi masikini ambayo bado uchumi wake unakua lile eneo ilipaswa pajengwe aidha kiwanda kidogo cha kuchakata vifaa vya umeme au technology innovation space centre ili nchi izalishe vijana wenye ujuzi katika technology wachangie katika uchumi wa taifa. Badala yake eneo muhimu kama lile panajengwa vibanda vya vijumba vya udongo ambavyo si vitu vigeni hata kwa wageni kusema kwamba wataenda kushangaa, kwa sababu ukitoka tu nje kidogo ya Dar es salaam bado kuna watu wanaishi maisha hayo! Kwa hiyo kujenga vile vinyumba pale ni kama kuwakebehi! Kwa sababu bado kuna watu wanaishi maisha yale kutokana na umasikini.
Natambua umuhimu wa Museum, hata ukienda Uingereza pale Yorkshire kuna museum inaitwa York Museum, pia Ujerumani huko kuna museum za Nazi regimes, lakini zilijengwa baada ya mataifa hayo kukua na kuinuka kiuchumi na hata location zilipojengwa haikuathiri shughuli za uzalishaji! Pia tayari wameshatoka huko wapo hatua nyingine ndiyo maana yale yanabaki kuwa makumbusho! Ila sisi bado hatujatoka kuishi kwenye nyumba za udongo au kutumia vinu n.k sasa makumbusho ya nini?
USHAURI; Kwa kifupi Makumbusho village ibomolewe au ihamishiwe huko Kigamboni, Eneo lile pajengwe ICT/Technology Innovation hub/Centre.