Kwa hakika sasa si siri tena siku za gamba kubwa CCM Edward Ngoyaye Lowassa a.k.a Fisadi wa Richmonduli ndani ya CCM zinahesabika.
Hii ni kutokana na ukweli kwamba kifikia tar 12/02/2013 Kamati Kuu ya CCM itakuwa imeundwa na baada ya kupata pigo kubwa kwa Makamu Mwenyekiti Mzee Mangula, Katibu Mkuu Kinana na Kurudishwa kwa adui yake mkubwa Nape basi pigo la mwisho kwa EL ni uundwaji wa CC ambao kwa vyanzo vya jikoni kabisa..hakuna mtu wake hata mmoja.
Ikumbukwe vikao vitatu vya mwanzo vya uchujaji majina ya urais ni Sekretarieti chini ya Kinana na Nape, Kamati ndogo ya Maadili chini ya Mangula na Kamati Kuu chini ya JK...na kote huku hakuna kupiga kura ni mjadala tu then maamuzi..
Haya niyasemayo yalimkuta Lowassa mwaka 1995 aliondolewa kwenye kinyang'anyiro bila kura, yalimkuta pia Malecela aliondolewa bila kufilishwa kwenye kura...historia itajirudia 2015.