Mwisho wa "Per Diem"? - Pinda aungwe mkono

Wakuu mambo ya kuishi bongo ndo kutumia bongo hivo

lakini the bottom line ni kwamba serikalini mshahara wanaotoa wanajua ni mdogo kumwezesha mfanyakazi kutunza familia yake na yeye mwenyewe, kulipa ada, usafiri, kodi ya nyumba etc

na serikali yenyewe ina kigeu geu. mfano ilipowauzia nyumba, kwa kuwakopesha, ilitegemea watalipa kwa hela gani kama zio mishe mishe hizi za makongamano na semina?

So kabla PM hajasema hayo, ni bora kwanza waboreshe mishara.

na ni kweli watu wa serkalini mshahara mdogo lakini maisha yao yapo juu sana kiubora kutokana na hizi nafasi nyingine....

Kaizer, sina ubishi na ukubwa au udogo wa mishahara serikalini lakini hii haihalalishi watu kufanya kazi kinyume na lililokusudiwa...ikiangalia work plan zao na hata implementation haviendani kabisa na huo mkukuta wanaowekea makongamano, vikao na elekezi! sasa hii ina tofauti gani na kuwasamehe mafisadi ikiwa watarudisha? Je tuwaache waendelee kujilipa kwa vile wanalipwa kidogo? Kwani si lilikuwa chaguo lao kufanya kazi serikalini...si soko huria jamani? Wengi wanaingia huko hivi sasa kwa vile kuna pesa nje nje...unafikiri hawajui kuna mishahara midogo? lakini na product yao unaionaje? inastahili mishahara zaidi ya hiyo wanayopata? Profit si inatokana na production? Sasa kauli km za akina Maghembe kweli zinahitaji mshahara mkubwa??
 
Kaizer, sina ubishi na ukubwa au udogo wa mishahara serikalini lakini hii haihalalishi watu kufanya kazi kinyume na lililokusudiwa...ikiangalia work plan zao na hata implementation haviendani kabisa na huo mkukuta wanaowekea makongamano, vikao na elekezi! sasa hii ina tofauti gani na kuwasamehe mafisadi ikiwa watarudisha? Je tuwaache waendelee kujilipa kwa vile wanalipwa kidogo? Kwani si lilikuwa chaguo lao kufanya kazi serikalini...si soko huria jamani? Wengi wanaingia huko hivi sasa kwa vile kuna pesa nje nje...unafikiri hawajui kuna mishahara midogo? lakini na product yao unaionaje? inastahili mishahara zaidi ya hiyo wanayopata? Profit si inatokana na production? Sasa kauli km za akina Maghembe kweli zinahitaji mshahara mkubwa??


Liz jamani umekuwa mkaaali kweli kweli...

mi nakubaliana na wewe kwa uliyosema ila nilikuwa naangalia upande wa pili wa shilingi,,

Na ninavojua ni kuwa hizo semina zinakuwa kwenye work plan zao ndo maana wanakuwaga busy wakati wa bajeti bungeni kuhakikisha bajeti zinapita...hujiulizi kwa nini wanasherekea bajeti za wizara zikipita? WANAJUA MIPANGO YAO IMEPATA BARAKA ZA KISHERIA..



Likewise, hata kwenye NGOs, kuna mmoja apo juu amesema...bajeti inapangwa na inapitishwa kuwa fedha zitatumika kwa semina...sasa itakuwaje zikanunue pembejeo? na hizi pembejeo imekuwa kama ni peremende za kuwadanganyia watu...fedha za EPA=pembejeo, za semina,=pembejeo....kweli hizo pembejeo zitawafikia ama ndo kutafuta cheap popularity?

Na kumbuka suala la kufanya kazi serikalini au popote hulazimishwi lakini mara ukiingia pale, unajikuta kuwa inabidi ufuate mfumo ulioukuta kinyume chake unakuwa sidelined...sijawahi kufanya serikalini lakinirafiki yangu alinambia ukionekana kupinga pinga kujifanya mzalendo...utapewa dawati na magazeti usome!


Hili ni suala kubwa na pana zaidi na halihitaji makaripio rahisi rahisi tu kama ya PM...unless wayaondoe kwa sheria kabisa ya bunge...
 
Ni vyema tukajikumbusha historia ya haya mambo ya bahasha za kaki kwenye mikutano na semina.

Wakati wa serekali ya awamu ya pili, nchi ilikuwa kwenye matatizo makubwa ya kiuchumi kiasi kwamba serikali ilikuwa ikishindwa kulipa hata mishahara ya watumishi wake.

Wafadhili walikuwa tayari kusaidia Tanzania katika shughuli za maendeleo lakini, wawakuwa tayari kulipa mishahara ya watumishi. Hivyo katika kutafuta njia mbadala ya kuwawezesha watumishi kuishi, serikali ilikuwa inatumia pesa za wafadhili kuwalipa watumishi kwa njia ya posho za mikutano, semina n.k ili isionekane imelipa mishahara. Hali hiyo iliendelea hivyo na baadae ikawa mazoea. Ni katika kipindi hicho pia muda wa kufanya kazi serikalini ulipunguzwa na kuwa hadi saa 9:30 jioni badala ya saa 11 jioni na kuondoa muda wa mapumziko ya chakula. Hii ilifanyika ili kuwawezesha watumishi kujishughulisha na miradi midogomidogo ya kuwaongezea kipato kama ufugaji wa kuku wa mayai na nyama n.k

Hata baada ya uchumi kuboreka haya mambo yote hayakubadilishwa.

Tatizo letu hatupendi kutumia takwimu katika kufanya maamuzi. Kabla pinda hajatoa agizo hilo angeegazi ofisi yake kufanya Takwimu kuona kwa mfano miaka 3 iliyopita tulitumia shs ngapi kwenye semina na makongamano na semina na takataka zote zinazofanana ha hayo. Then kati ya hizo zipi zilikuwa siyo za muhimu. Then kama kiasi hicho kingetumika kuongeza mishahara ya watumishi tu a satisfactory level na kuondoa mambo ya kulipana per diem kiasi gani serikali ingesave?

Kwa sasa agizo hilo halitatekelezeka kwa sababu mishahara ya watumishi wa umma ni midogo sana hivyo ili kuendelea kuishi lazima watabuni njia nyingine tu.
 
Kaizer/ MpiganajiNambaMoja sipingani nanyi sana katika swala la mishahara ile sasa hebu tujiulize hata kama tutapima wanayoyafanya kwa kutumia indicator (viashiria) watakavyokuwa wamejiwekea katika work plans zao je? watakuwa wanapima maendeleo? Je lengo la mkukuta litapimwa kupitia semina kumi walizoendesha kwa ajili ya wafanyakazi wa serikali? Au indicator itakuwa kupungua kwa vifo vya watoto walio chini ya miaka...kutokana na magonjwa yanayozuilika? Au kuongezeka kwa uzalishaji/ na uuzaji wa mazao ya biashara katika kijiji X toka asilimia ..hadi ...?

Na kwamba hili la Pinda halitekelezeki inawezekana sana ni kauli ya kisiasa na ya jazba lakini linatekelezeka kama ipo nia na watendaji wanye nia wata capitalise on his kauli. Sasa kama tukikubali halitekelezeki na kuendelea kuwapa kichwa kujipa per diem zisizo na tija then tumwach JK aendelee kutembeza bakuli la misaada ili wasitumie kodi zetu kulipana per diem na sisi hatuna maji! Huduma zinazidi kuzorota...tunalipia huduma zote mara mbili. Tunalipa kodi ingepaswa kutengeneza barabara na bado tulipe gharama za kutengeneza magari yetu kila kukicha na kulipia vijana wanaojaza mawe barabarani na mara nyingine kuchangia barabara ya mtaa.


Hii ni kodi yetu wanalipwa nayo na wanaishi kwa raha na kujisifu kwa per diem zao. Hofu yangu ni kuwa wapo wanaolipana bila tija
 
Well Haya maamuzi nayaunga mkono.
Ila nadhani semina za kuburesha ufanisi wa kazi bado ni za muhimu na si lazima zifanyikie morogoro, Bagamoyo why??? wakati lengo la semina nu kupata jambo jipya la kuboresha utendaji wa kazi.

sasa ni bora ieleweke kama semina ni ya muhimu ifanyike nadhani hamna wizara isiyokuwa na boadroom ambayo inaweza kutumika kufanyia semina kwa ajili ya wafanyakazi wake.
Kama hamna basi hata ukumbi wa zamani wa bunge unaweza ukatumika kwani kwa sasa unafanyia nini ama viti vinapigwa vumbi tu???

serikali ifanye mpango wa dhati wa kuhakikisha semina zote zitakuwa zinafanyikia dar. Hamna cha perdeam wala seating allowance.

maana muda utakaoattend semina ni muda wa kazi and already you are receiving salary. More than that you are getting free knowledge to make you more competetive in this world full of challenges.
 
Liz Senior
Nakubalianai na wewe. Ila mimi ninachotaka kuona ni hili lakupunguza matumizi yasiyo ya lazima linafanywa kisayansi na siyo kisiasa. Yaani waje na takwimu na uchambuzi. Naamini kabisa semina nyingi hazina Tija na zinaweza kabisa kuondolewa, halikadhalika Safari za nje na training zisizokwisha. Hivi unajua watu wanachukua perdiem foreign kwenda kujufunzi Microsoft word/access swaziland na nchi nyingine. Training ambazo zingeweza kufanywa hapa nchini.

Mfumo mzima wa serikali unahitaji mabadiliko makubwa (overhauling) ikiwa ni pamoja na kupunguza ukubwa wa serikali kwa maana ya wizara na Taasisi zake. Mfano TBS, TFDA, Mkemia mkuu wa serikali wote wanafanya kazi zinazofana kwa nini taasisi 3 tofauti? Ngorongoro Conservation, TANAPA wote wanafanya kazi moja kwa nini taasisi 2, na mengine mengi
 
Tatizo letu hatupendi kutumia takwimu katika kufanya maamuzi. Kabla pinda hajatoa agizo hilo angeegazi ofisi yake kufanya Takwimu kuona kwa mfano miaka 3 iliyopita tulitumia shs ngapi kwenye semina na makongamano na semina na takataka zote zinazofanana ha hayo. Then kati ya hizo zipi zilikuwa siyo za muhimu. Then kama kiasi hicho kingetumika kuongeza mishahara ya watumishi tu a satisfactory level na kuondoa mambo ya kulipana per diem kiasi gani serikali ingesave?

Kwa sasa agizo hilo halitatekelezeka kwa sababu mishahara ya watumishi wa umma ni midogo sana hivyo ili kuendelea kuishi lazima watabuni njia nyingine tu.

This way forward.
Mi nashangaa sana kuona serikali inavyobania mishahara wakati hela zipo ila basi tu kutokuwa na positive thinking.

Siku za nyuma nilisikia serikali ilikua inamoderate mishahara kwenye private sectors ili kusiwe na Gap kubwa la mishahara???? Mi naona huu ni ujinga na wivu usiokuwa wa kimaendeleo.
Nadhani Mtu akilipwa vizuri yafuatayo hutokea
1. Serikali inapata kodi kubwa ya kutosha.
2.Mpokea mshahara atakuwa na serving ya maana kisha ateweza kuanzisha miradi na hivyo kutoa ajira kwa watanzania wenzetu.

Sasa unapobania watu wasilipwe vizuri inadhihirisha ni kwa namana gani hatuoni mbele. au hatufikirii kwa makini. Nahisi viongozi wetu waliopo kwenye decision making level they have to go through critical thinking courses.
To start with they can read this
 

Attachments

  • critical thinking.pdf
    107.3 KB · Views: 36
Kuna wanaotetea kuwepo semina na makongamano, warsha n.k. Cha kujiuliza ni je? hizo seminar mpaka sasa zimezaa matunda gani?
Chukulia mfano seminar/warsha za UKIMWI,rushwa, mazingira, idadi ya watu,jinsia, afya ya mama na mtoto, uzazi wa mpango, ulemavu,kuondoa umaskini etc, mpaka leo zimeshafanyika ngapi( ni rahisi sana kujua kwani kila taasis ya serikali inaweza kutoa takwimu hii rahisi), zilitumia kiasi gani cha fedha, mapendekezo yaliyotolewa yalifanyiwa kazi kama ndiyo kwa kiwango gani na yalizaa matunda gani?
Tutaweza kulinganisha faida iliyopatikana na kujua if there was value for money.Hapo ndiyo ingewezekana kufanya uamuzi wa kuendelea nazo au kuzi scrap off.
 
Kaizer/ MpiganajiNambaMoja sipingani nanyi sana katika swala la mishahara ile sasa hebu tujiulize hata kama tutapima wanayoyafanya kwa kutumia indicator (viashiria) watakavyokuwa wamejiwekea katika work plans zao je? watakuwa wanapima maendeleo? Je lengo la mkukuta litapimwa kupitia semina kumi walizoendesha kwa ajili ya wafanyakazi wa serikali? Au indicator itakuwa kupungua kwa vifo vya watoto walio chini ya miaka...kutokana na magonjwa yanayozuilika? Au kuongezeka kwa uzalishaji/ na uuzaji wa mazao ya biashara katika kijiji X toka asilimia ..hadi ...?

Na kwamba hili la Pinda halitekelezeki inawezekana sana ni kauli ya kisiasa na ya jazba lakini linatekelezeka kama ipo nia na watendaji wanye nia wata capitalise on his kauli. Sasa kama tukikubali halitekelezeki na kuendelea kuwapa kichwa kujipa per diem zisizo na tija then tumwach JK aendelee kutembeza bakuli la misaada ili wasitumie kodi zetu kulipana per diem na sisi hatuna maji! Huduma zinazidi kuzorota...tunalipia huduma zote mara mbili. Tunalipa kodi ingepaswa kutengeneza barabara na bado tulipe gharama za kutengeneza magari yetu kila kukicha na kulipia vijana wanaojaza mawe barabarani na mara nyingine kuchangia barabara ya mtaa.


Hii ni kodi yetu wanalipwa nayo na wanaishi kwa raha na kujisifu kwa per diem zao. Hofu yangu ni kuwa wapo wanaolipana bila tija


Liz, kuhusu viashiria uko sawa kabisa lazima viwe SMART.....ila sasa tuje kwenye mchakato wa kufikia whatever objectives walizojiwekea..ndo kasheshe ipo hapo kwen implementation!

Ishu ni kuwa, wafanyakazi wengi tuseme sekta ya umma...wanaona jinsi wakubwa zao wanavokula...kama bosi akienda nje...wao wanaandaa japo kasemina walau mwezi uishe!

So mi nakubaliana na hoja kuwa ufanyike utafiti wa gharama halisi za maisha watu walipwe accordingly, then waondoe per diems....kinyume na hivo, kwa maana ya kukataza hizo semina na huku mishahara inajulikana bado haikidhi, itakuwa ni kutwanga maji kwenye kinu!
 
hata huyo boss inabidi aangaliwe anakwenda nje kufanya nini maana wengi pia wanaendea Per diem
 
hata huyo boss inabidi aangaliwe anakwenda nje kufanya nini maana wengi pia wanaendea Per diem


hahaha, sasa hapo una utani na JK ama vipi? LOL

lakini pia mahali pengine pazuri pa kuanzia, waraka wa maelekezo ya posho ufutwe,,, simple

kuna maofisa wa kawaida tu poshoyao kwa siku kuanzia 65,000, wengine hadi 100,000 kwa siku,,,halafu uliza mshahara wa kima cha chini!

je, na wabunge pia zile posho zao za nini wakati wanalipwa mshahara? wakianza wao kuzislash, nadhani utakuwa mwanzo mzuri..sijui zimefikia ngapi kwa sasa...
 
Kweli wangepunguza pia safari za nje ya nchi. DSA per day ni $ 220 per day kama mtu anasafiri kwa wiki mbili hiyo ni siku 14 x220 = $3080 bado internal travel costs, bado outfit allowance kama bado ipo....( hii ni safari moja tu kwa mtumishi mmoja)
 
Per diems zote zikipunguzwa hata watanzania watakuwa na amani ya roho. Per diems hizi zimenyang'anya watu watoto wao, wake na waume zao. Maambukizi wa Ukimwi ndo usiseme, maana mtaji wa masikini nguvu zake
Mbaya zaidi mashirika ya Umma kama UD nayo yameoza kwa per diem na allowances. Kuna siku wadosi wa chuo enzi ya Pilato walikutana kwa chini ya saa moja wakalipana per diem mpya za elfu 80. Hiyo shot kwenye bajeti ya chuo, ilibidi wakuu wafunge gavana wenyewe ila bado wataalamu wa mikutano na makonferensi wanaweza kusaini mara tatu kwa siku kwa fedha hizo hizo. Mbaya zaidi rasilimali vitu za kufundishia ni anasa kwa UD
 
Rasilimali zinazopotea in the course of kuendesha seminar hizo ni nyingi - kikubwa zaidi pia ni muda. Fikiria mfanyakazi anayetakiwa kuhudumia wananchi anakaa nje ya ofisi kwa siku saba, huko ofisini kazi zinamsubiri. Kuna nyenzo nyingine kama makaratasi, kalamu , writing pads ambazo hununuliwa kwa fujo na hazitumiki zote na pia hazirudi maofisini!
Kweli ni hasara juu ya hasara kwa mlipa kodi wa ndani na pia wa nchi wafadhili.
 
Hivi watu hawafanyi semina za ndani? Mahali ninapofanya kibarua changu kila wiki (jumatatu) tuna mkutano wa kuwakena sawa na kutathmini mambo yaliyopita n.k halafu kila mwezi tuna "communication meetings" halafu kuna mikutano ambayo watu wa HQ wanakuja kuendesha. Yote hii inafanywa hapa hapa kwenye jengo letu na hakuna cha per-diem wala posho yoyote. Kwa sababu ni sehemu ya kazi zetu.

Sasa sijui ni kwa kiasi gani au tofauti gani ya semina ipo ambayo inafanya semina za ndani zilipiwe per-diems au kutowezekana kwa semina ndani. Ungeniuliza mimi ningesema:

a. Kila ofisi lazima iwe na ukumbi wa kutosha wa mikutano ya ndani.
b. Semina na mikutano ipangwe kufanyika ndani ya wiki na muda wa kazi kwenye eneo husika (hata kwa makundi makundi)
c. Semina hizo hazina malipo yoyote yale.
d. Semina za nje ziwe zimepangwa kwenye kalenda mwaka mmoja kabla na anayeenda ajulikane na kwanini yeye aende (leo hii kwa mfano ATCL imepeleka watu kusoma SA, wakati haina ndege za kurusha!)
e. Lazima kuwe na kipaumbele na kujali matokeo ya semina hizo. Kama mtu ameenda kwenye semina ya kujifunza ziaid jinsi General Accounting Principles zinafanya kazi katika utawala wa kidemokrasia ni matarajio yetu kuwa akirudi tuone mabadiliko; kama hakuna mabadiliko semina ilikuwa ya nini? NI lazima tujifunze kupima matokeo (measuring results). Kama watu wameenda kujifunza kilimo cha kisasa halafu wakarudi na kulima kwa mtindo wa zamani, ile semina imewasaidia nini?
 
Hivi watu hawafanyi semina za ndani? Mahali ninapofanya kibarua changu kila wiki (jumatatu) tuna mkutano wa kuwakena sawa na kutathmini mambo yaliyopita n.k halafu kila mwezi tuna "communication meetings" halafu kuna mikutano ambayo watu wa HQ wanakuja kuendesha. Yote hii inafanywa hapa hapa kwenye jengo letu na hakuna cha per-diem wala posho yoyote. Kwa sababu ni sehemu ya kazi zetu.

Sasa sijui ni kwa kiasi gani au tofauti gani ya semina ipo ambayo inafanya semina za ndani zilipiwe per-diems au kutowezekana kwa semina ndani. Ungeniuliza mimi ningesema:

a. Kila ofisi lazima iwe na ukumbi wa kutosha wa mikutano ya ndani.
b. Semina na mikutano ipangwe kufanyika ndani ya wiki na muda wa kazi kwenye eneo husika (hata kwa makundi makundi)
c. Semina hizo hazina malipo yoyote yale.
d. Semina za nje ziwe zimepangwa kwenye kalenda mwaka mmoja kabla na anayeenda ajulikane na kwanini yeye aende (leo hii kwa mfano ATCL imepeleka watu kusoma SA, wakati haina ndege za kurusha!)
e. Lazima kuwe na kipaumbele na kujali matokeo ya semina hizo. Kama mtu ameenda kwenye semina ya kujifunza ziaid jinsi General Accounting Principles zinafanya kazi katika utawala wa kidemokrasia ni matarajio yetu kuwa akirudi tuone mabadiliko; kama hakuna mabadiliko semina ilikuwa ya nini? NI lazima tujifunze kupima matokeo (measuring results). Kama watu wameenda kujifunza kilimo cha kisasa halafu wakarudi na kulima kwa mtindo wa zamani, ile semina imewasaidia nini?

kaka hapo ndo penye gogoro,,
ninavofahamu maofisi mengi ya serikali na mashirika wana kumbi za mikutano, lakini hata wakikaa huko ni lazima kuna sitting allowances!

Hilo la kusafiri na kujustify ndugu yangu kwa sie wabongo mbona ni wataalam wa kujustify...ila hakuna evaluation mtu akisharudi..lakini that goes down kwenye tafiti, kwa mfano, watu wanafanya tafiti lakini matokeo yanaozea kwenye makabati huko..hasa kwenye kilimo...sasa usitegemee muujiza kwa mtu aliyeenda hapo swaziland kujifunza ms word akalamba zake dola 220 kwa siku....lol
 
Sitting allowance? well why not Breathing allowances? why not "showing to work allowance"? what on earth is sitting allowance? Hata kwa wabunge inanishangaza, ati Mbunge akihudhuria kikao cha Bunge ambacho ndiyo kazi yake anapewa sitting allowance! grrrrrrrrr
 
Sitting allowance? well why not Breathing allowances? why not "showing to work allowance"? what on earth is sitting allowance? Hata kwa wabunge inanishangaza, ati Mbunge akihudhuria kikao cha Bunge ambacho ndiyo kazi yake anapewa sitting allowance! grrrrrrrrr


hujauliza ni bei gani anapewa, niliona marupurupu ya wabunge, sijui ni hapa JF, sikumbuki. Nilichoka. Kwa mwezi nadhani wanapata kama 3.8 m (Tshs).
 
Back
Top Bottom