Azua tafrani uwanja ndege baada ya kutaka kusafiri akiwa uchi
Mwanaume mmoja amezua taharuki katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kamuzi katika mji mkuu wa Malawi Lilongwe baada ya kufika uwanjani hapo akiwa amevalia nguo ya ndani (chupi pekee) akitaka kusafiri.
Picha mbalimbali zimesambaa kwenye mitandao ya kijamii zikimuonyesha mwanaume huyo akiwa amesimama kwenye mstari kwa ajili ya ukaguzi na nyingine akihojiwa na maafisa wa usalama katika uwanja huo.
Watu wamedai kuwa ni raia kutoka nchini Afrika Kusini na alifika uwanjani hapo akitaa kurudi nchini Afrika Kusini.
Wengine walisema kuwa ni muogeleaji ambapo wakati mwingine hufanya hivyo (kutembea au kusafiri na nguo za kuogelea) ili kuchangisha fedha za kusaidia watu wenye matatizo hasa watoto.
Chanzo: South African Man “High on Weed” Tries to Fly Naked at Malawi Airport
Mwanaume mmoja amezua taharuki katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kamuzi katika mji mkuu wa Malawi Lilongwe baada ya kufika uwanjani hapo akiwa amevalia nguo ya ndani (chupi pekee) akitaka kusafiri.
Picha mbalimbali zimesambaa kwenye mitandao ya kijamii zikimuonyesha mwanaume huyo akiwa amesimama kwenye mstari kwa ajili ya ukaguzi na nyingine akihojiwa na maafisa wa usalama katika uwanja huo.
Watu wamedai kuwa ni raia kutoka nchini Afrika Kusini na alifika uwanjani hapo akitaa kurudi nchini Afrika Kusini.
Wengine walisema kuwa ni muogeleaji ambapo wakati mwingine hufanya hivyo (kutembea au kusafiri na nguo za kuogelea) ili kuchangisha fedha za kusaidia watu wenye matatizo hasa watoto.
Chanzo: South African Man “High on Weed” Tries to Fly Naked at Malawi Airport